Brigadier Ahmed Takadiri Kitete: Shujaa aliyepiganisha vita toka Kagera mpaka Koboko alikozaliwa Idi Amin

Hawa ndio wanajua maana ya uzalendo sio kina Mrisho Mpoto kujichekesha kwa rais halafu wanajiita wazalendo
 
Mkuu natambua hii ni comment ni ya April lakini unaweza kutupa details kuhusu hii 'vita ya wajomba'
 
Mkuu natambua hii ni comment ni ya April lakini unaweza kutupa details kuhusu hii 'vita ya wajomba'
Baada ya Mreno kuondoka ilitokea vita ya RENAMO na FRELIMO. Hivi ni vyama vya ukombozi vya nchi moja.
Mfano wake ni MPLA na UNITA ya Savimbi kule Angola.

Maana yake ni moja, ni ndugu wanapigana, si Mreno si Kaburu.
 
Huyu shujaa wetu KITETE ana mtoto wa kiume anaitwa TAKADIRI ambaye naye kwasasa ni mwanajeshi?
 

Nadhani unawajibu vizuri. Lakini nadhani kinachosumbua watu ni kutojua kuwa ndani ya jeshi kuna division of labor. CoS anafanya mambo ya administration....anaangalia mambo ya kuajiri watu, mambo ya procurement na mengine. Hivyo hawezi kuwa anayeongoza tactics kwenye uwanja wa mapambano.
 
SUNDAY MONITOR, TANZANIA - UGANDA (KAGERA) WAR:

Maj Gen Abdallah Twalipo was TPDF’s Chief of Defence Forces but the responsibility to respond to Amin’s invasion fell on Brig Gen Tumainieli Kiwelu who had to reorganise the army from different parts of the country.

By then, TPDF had only one army division with four infantry brigades in different parts of the country.

Brigade 101st, nicknamed Nyuki (Bee) was based in Zanzibar, 302nd in Dar es Salaam, 202nd Faru in Tabora and 401 Tembo in Songea.

The youth who had participated in national service training were transformed into a reserve force; trained militias were prepared for battle, police and prisons personnel were mobilised, while the ordinary civilians offered food and livestock, private companies surrendered their vehicles to transport troops and hardware.

At the same time the Uganda exiles living in Tanzania also united to form the Uganda National Liberation Army, which included groups such as Fronasa of Yoweri Museveni, Save Uganda Movement of Akena p’Ojok, Ateker Ejalu and William Omaria and Kikosi Maalum (Special Unit) led by Lt Col David Oyite Ojok and Col Tito Okello. They established a joint training camp of close to 1,200 recruits at Tarime near Musoma on the shores of Lake Victoria.

From Brig Gen Kiwule’s reorganisation, a 20th division was created with different brigades like Brigade 206th under Brig Gen Silas Mayunga – later taken over by Brig Gen Roland Makunda, 207th under Brig Gen Butler Walden and 208th under Brig Gen Mwita Marwa.

As the war progressed more brigades were formed, including 201st under Brig Gen Imran Kombe, 205th under Brig Gen Herman Lupogo – later taken over by Brig Gen Muhidin Kimario, Brigade Minziro under Brig Gen Takadiri Kitete and Brigade Kagera under Brig Gen Ramadhan Haji.

The overall commander of the operation was Brig Gen David Msuguri who was promoted to the rank of Maj Gen as Brig Gen Kiwelu went back to the headquarters as Chief of Staff. Within weeks, the TPDF had mobilised its numbers from 40,000 to 100,000.
 

..mchangiaji uliyemjibu alikuwa na nia ya kupotosha.

..na katika uzi huu ametoa madai bila kuwa na vyanzo vinavyaominika kutetea madai yake.

..wakati mwingine amepingana hata na waandishi wa Jwtz walioandika kitabu kinachohusu vita vya Kagera.
 

Tunaomba mrejesho mkuu.
kwa talanta uliyo barikiwa taifa linakutegemea.
jitahidi utuandalie documentary
 
Afande maneno Alisha fariki siku nyingi amekaaa tegeta nimekaa kambini na mwanae wa kike aliolewa na major

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Ninachojilaumu ni kuwa sikujiwekea kumbukumbu vizuri wakati ule kwa maana ya kuja kuziandika baadaye. Nilikuwa nimemaliza form 6 na nilikuwa na elimu ya kutosha kuweka kumbukumbu hizo. Nilifanya kwanye COMM unit ya brigade kwa zaidi ya miezi sita nikiwa napokea taarifa nyingi sana za vitani na kuzipeleka kiwa makamanda wahusika ndani ya brigade. Hata hivyo wakati huo nilikuwa nimepikwa kuwa msiri sana na niliamini kuwa habari hizo ni classified na hazikutakiwa kutoka nje ya maeneo ya kijeshi; kwa hiyo sikuondoka na notisi zozote za binafsi. Baada ya kushindwa kujiunga na air-force ambayo ndilo lililokuwa chaguo langu wakati huo, nikarudishwa uraiani, na kutupwa kule Anti-corruption Squad kama reporter tu, siyo afisa, lakini vile vile ikiwa ni kwa kuamini kuwa nilikuwa trained kuwa msiri. Hata hivyo baadaye nilipenda kuendelea na elimu ya juu na hivyo kuondoka kwenye system hiyo yenye habari classified. Leo hii najiuliza iawpo ningejiwekea notisi zakutosha ningeweza kuandika kitabu kizuri sana. Lakini ndiyo hivyo, wakati ule nilikuwa mtu msiri wa mambo ya kitaifa kweli kweli, yaani huwezi kuamini!!
 
Si wewe tu, kwakweli ni watu wengi tu walipatwa na hali hiyo. Nadhani siasa za wakati ule ambapo Watanzania walikuwa 'wamefungwa' zilichangia sana kutudumaza katika kuona mambo kwa mtazamo tofauti

Unakumbuka kuwa na 'passport' ya kusafiria ilikuwa 'issue' sasa nyaraka za jeshi kwakweli zilitisha sana

Katika mambo ninayotofautiana sana na Mwalim Nyerere moja ni hili la kuwafunga macho Watanzania kwa miaka kadhaa . Kipindi cha 1970-1985 ilikuwa ngumu sana kupata taarifa za dunia hata kusafiri ilionekana kama 'privilege' na siyo haki ya mtu.

Lakini pia JWTZ ifike mahali wabadilike. Habari za miaka 40 iliyopita zinaweza kuwa declassified na watu wenye kumbukumbu wakaunganisha dots na kuandika. Sioni kwanini vita ya Uganda ibaki kuwa classified
 
Supersonic Kitete ni moja wa makamanda walioandaa mpango madhubuti wa kivita wa kumuondoa kwanza Nduli na majeshi yake nje ya mipaka ya nchi yetu , na kazi hii iliwachukua masaa 24 tu . nilipata kumuuliza juu ya hili na alinijibu kwamba ilikuwa lazima adui atolewe kwanza nje ya mipaka yetu ndo vita iendelee. kwa maelezo yake mpango huu ulitengenezwa na yeye pamoja na Tumaineli kiwelu
CONTINUE TO REST IN PEACE SUPERSONIC KITETE
 
Tusiwasahau mashujaa wengine kama Jenerali Yusuf Himid wa Zanzibar aliyekuwa Mkuu wa Brigedi ya Tabora wakati tunavamiwa, na kikosi cha KMKM kilivyoonja mauti msitari wa mbele mwazoni kabisa. Hii inadhihirisha mshikamano wa Watanzania, khasa baada ya OIC kutuma askari wa Libya, PLO na Pakistan kuingia vitani kwa upande wa mwislamu "mwenzao" Idi Amin. Baadaye walijuta wakajirudi.
 
Mambo gani makubwa aliyoyafanya?? Kuuwa waislamu wenzie askari wa libya, Raia wa uganda wasio waislamu na waislamu/Civilians. Hayo ndio yakukumbukwa!!
 

..kweli kabisa.

..tulikuwa na askari wetu ambao walijitahidi kuzuia majeshi ya Amini yasivamie nchi yetu.

..na Brigade commander wao alikuwa Yussuf Himid, na nadhani battalion commander aliyekuwepo mpakani alikuwa Lt.Col.Maurice Singano.

..mchango wa vikosi vya Tanzania ambavyo vilikuwa vya kwanza kukabiliana na uvamizi wa majeshi ya Amin lazima utambuliwe.
 


Kushoto: Brigedia Tumainieli Kiwelu kamanda mkuu wa operation chakaza.
Kulia: Kanali Ahmed Kitete mkuu wa mipango ya kivita operation chakaza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…