Huyu ni mmoja kati ya makamanda walioongoza vita vya Kagera lakini siyo maarufu ktk vyombo vyetu vya habari, lakini ukisoma VITABU mbalimbali vinavyohusu VITA VYA KAGERA utagundua kwamba alikuwa na mchango mkubwa toka mwanzo mpaka mwisho wa vita, yaani toka Mutukula/Kagera mpaka Koboko kijiji alikozaliwa Iddi Amin Dada.
Baada ya majeshi ya Uganda kuvamia ardhi ya Tanzania na kuikalia, Tumainieli Kiwelu [meja jenerali wakati huo] ambaye alikuwa Chief of Staff JWTZ alipewa jukumu la kuandaa majeshi yetu na kuongoza mapigano ya kukomboa ardhi yetu.
Ahmed Takadiri Kitete [kanali wakati huo] ametambulishwa ktk kitabu cha " Vita vya Kagera -- 'kagera hadi arua' "kama mkuu wa mipango ya uamrishaji kivita ktk operesheni ya kuyaondoa majeshi ya Uganda ktk ardhi ya Tanzania.
Ahmed Kitete alipandishwa cheo na kuteuliwa kuongoza Brigade ya Minziro ambayo ilipigana maeneo ya Bushenyi, Kasese, Fort Portal, Hoima, Masindi, Karuma Falls, Pakwach, Bondo, Arua, Yumbe, na Moyo mpakani na Sudan [sasa hivi South Sudan].
Brigade ya Minziro ndiyo iliyohitimisha vita vya Uganda na Brigadier.Kitete ndiye kamanda wa Tanzania aliyefika mpaka kijiji cha Koboko alipozaliwa alipozaliwa Iddi Amin Dada.
Makamanda wote wakuu waliopiganisha vita vya Kagera walikuwa na majina yao ya kimapigano au nom de guerre, kwa mfano Major General Kimario alijulikana kama "kamanda mbogo."Major General Imran Kombe alijulikana kama "kamanda ngono" kwasababu aliongoza mapigano kuvuka mto ngono. Colonel Tumbi ambaye alikuwa mkuu wa vikosi vya mizinga aliitwa "kamanda radi." Ahmed Takadiri Kitete alipewa jina la " kamanda supersonic. "
Baada ya vita vya Kagera Ahmed Kitete alikuwa mkuu wa operesheni na mafunzo wa Jwtz. Kwa bahati mbaya alifariki kwa ajali ya gari jijini D'salaam.
Nakaribisha michango ya wengine wenye taarifa za Ahmed Takadiri Kitete shujaa na kamanda mahiri wa jeshi la wananchi Watanzania.
Kushoto Brigedia Tumainieli Kiwelu kamanda mkuu wa operesheni chakaza ya kuondoa majeshi ya Uganda ktk ardhi ya Tanzania. Kulia Kanali Ahmed Kitete mkuu wa mipango ya kivita ktk operesheni chakaza.
cc Echolima, Manyerere Jackton , gobore, Mohamed Said, Nguruvi3, gobore, The only, Ukwaju
Baada ya majeshi ya Uganda kuvamia ardhi ya Tanzania na kuikalia, Tumainieli Kiwelu [meja jenerali wakati huo] ambaye alikuwa Chief of Staff JWTZ alipewa jukumu la kuandaa majeshi yetu na kuongoza mapigano ya kukomboa ardhi yetu.
Ahmed Takadiri Kitete [kanali wakati huo] ametambulishwa ktk kitabu cha " Vita vya Kagera -- 'kagera hadi arua' "kama mkuu wa mipango ya uamrishaji kivita ktk operesheni ya kuyaondoa majeshi ya Uganda ktk ardhi ya Tanzania.
Ahmed Kitete alipandishwa cheo na kuteuliwa kuongoza Brigade ya Minziro ambayo ilipigana maeneo ya Bushenyi, Kasese, Fort Portal, Hoima, Masindi, Karuma Falls, Pakwach, Bondo, Arua, Yumbe, na Moyo mpakani na Sudan [sasa hivi South Sudan].
Brigade ya Minziro ndiyo iliyohitimisha vita vya Uganda na Brigadier.Kitete ndiye kamanda wa Tanzania aliyefika mpaka kijiji cha Koboko alipozaliwa alipozaliwa Iddi Amin Dada.
Makamanda wote wakuu waliopiganisha vita vya Kagera walikuwa na majina yao ya kimapigano au nom de guerre, kwa mfano Major General Kimario alijulikana kama "kamanda mbogo."Major General Imran Kombe alijulikana kama "kamanda ngono" kwasababu aliongoza mapigano kuvuka mto ngono. Colonel Tumbi ambaye alikuwa mkuu wa vikosi vya mizinga aliitwa "kamanda radi." Ahmed Takadiri Kitete alipewa jina la " kamanda supersonic. "
Baada ya vita vya Kagera Ahmed Kitete alikuwa mkuu wa operesheni na mafunzo wa Jwtz. Kwa bahati mbaya alifariki kwa ajali ya gari jijini D'salaam.
Nakaribisha michango ya wengine wenye taarifa za Ahmed Takadiri Kitete shujaa na kamanda mahiri wa jeshi la wananchi Watanzania.
Kushoto Brigedia Tumainieli Kiwelu kamanda mkuu wa operesheni chakaza ya kuondoa majeshi ya Uganda ktk ardhi ya Tanzania. Kulia Kanali Ahmed Kitete mkuu wa mipango ya kivita ktk operesheni chakaza.
cc Echolima, Manyerere Jackton , gobore, Mohamed Said, Nguruvi3, gobore, The only, Ukwaju