Bukoba: Mwalimu atakiwa kurejesha Mshahara aliolipwa kwa kufanya Udanganyifu kwa Mwajiri

Bukoba: Mwalimu atakiwa kurejesha Mshahara aliolipwa kwa kufanya Udanganyifu kwa Mwajiri

Ukisoma comment za wachangiaji waliowengi katika huu uzi utaona ni namna gani nchi yetu imejaa wezi.
Kwa hali hii namuunga mkono mama yetu kuuza bandari hata ikibidi atuuze hata sisi watanzania.
 
Maelezo yanaonesha, alikuwa na ruhusa ya kusoma shahada.

Lakini alipomaliza shahada, akaandika kwa mwajiri kuwa hajamaliza hiyo shahada yake kwahiyo anahitaji muda zaidi (ili atumie huo muda kusoma, Masters).

Sasa inavyoonekana Kuna elements zenye Chuki, roho mbaya na kuchomeana zimehusika hapa.
Sijaelewa hiyo mishahara anairejesha kwa Nini!??
 
Nchi ngumu hii.
Sitetei huu ujinga wa mwalimu. Nchi yetu kesi za dagaa unaangushia adhabu ya kubeba jiwe la tani 5 lakini kesi ya nyangumi adhabu zao ni barua tu. Huna kazi kaa pembeni hatimae nywiiii. Hakuna kinachoendelea.
 
Novemba 22, 2023 katika Mahakama ya Bukoba imeamriwa kesi ya Jamhuri dhidi LYDIA KOKUSHOBOKA KAOO, ambaye ni alikuwa mwalimu wa Shule ya Msingi Kashai- Manispaa ya Bukoba.

Imemtia hatiani kwa makosa mawili la kwanza matumizi ya nyaraka kumdanganya mwajiri kwa kuandika barua kwa mwajiri kujifanya hajamaliza masomo ya shahada ya kwanza ndani ya muda aliopewa na mwajiri wake ili aweze kuendelea na shahada ya pili.

Kosa la pili ni kuisababishia Serikali hasara kwa kuendelea kulipwa mishahara kwa kipindi cha udanganyifu asichokuwepo kazini.

Mshtakiwa ametiwa hatiani na kupewa adhabu ya kifungo cha miaka 3 or fine ya 1 milioni kwa kosa la kwanza. Na kifungo cha miaka 3 bila fine kwa kosa la pili.

Pia imeamuliwa jumla ya sh. 22,252,134.73/= iliyopokelewa kama mishahara azirudishe kwa mwajiri wake.
Mtuhumiwa hana hata upenyo wa kutokea. Akilipa faini, atafungwa. Asipolipa faini bado atafungwa tu. Kibaya zaidi anatakiwa arudishe hayo mamilioni ya fedha wakati tayari atakuwa gerezani. Ama kweli tamaa nyingi, mbele kiza kitupu.
 
Hahaha watanzania tunashida sana, Umeandika vizuri kuonyesha umeelewa udanganyifu alioufanya. Sasa hizo chuki,roho mbaya na kuchomeana zimetoka wapi?

Rudi mwanzo, Je alidanganya ama Hakudanganya. Kam alidanganya muajiri anakosa gani hapo? Au mahakama inakosa gani kutoa hukumu? Muajiri anajukumu la kufuatilia watumishi wake wakiwa masomoni, kama mtumishi amepewa ruhusa ya miaka mitatu kwenda masomoni. Miaka mitatu imeisha unadhani ni nani mwenye jukumu la kufuatilia kama mtumishi kamaliza au hajamaliza masomo? Muajiri anatakiwa apewe report, awe ka fail na anarudia mwaka, au ana suppliment, still muajiri anapaswa kupewa report hiyo. Ikiwa muajiri hato pata hiyo taarifa kwa maandishi, ni wajibu wa muajiri kuwasiliana na chuo anachosoma mwajiriwa na apewe taarifa ya nini ni nini au kipi na inawekwa kwenye personnel record za mwajiriwa/mtumishi.

Hili lazima lifanyike kwasababu huyo mwajiriwa/mtumishi analipwa mshahara, na unaweza kuta na ada ananlipiwa kulingana na mkataba waliokuwa nao. Na kama muajiri hafuatilii watumishi wake huyo muajiri ni mwendawazimu.
Sio kila kitu mnachomewa, au kufitiniwa kuna vitu viko straight foward, hakuna mchawi.

Mwajiri kafuatilia kapata report yeye kaandika barua ya kudanganya. Muajiri akamshitaki, yeye mtumishi alipaswa aombe msamaha hatua za awali za kesi, na amuombe radhi muajiri wake kwa kueleza ukweli ngesamehewa. lakini kakubali kuumeza ukweli na kwenda na ukweli mahakamani kesi/shauri limeendeshwa mpaka hukumu imetolewa, wewe unasema kachomewa.

Mahakama zikitenda haki hamtaki, zisipotenda haki hamtaki, hata hamueleweki.
Umeandika Gazeti, bila sababu za msingi.
 
Si ajabu alimchoma mwalimu mwenzake,ndo maana tunashauriwa kuwa wasiri maana watu wamejawa na wivu.
Alafu nashangaa jambo dogo kama hili limefikaje mahakamani,yaani kuna watu nu wa kuendea kwa mganga tu
 
Sijui ni njaa mchana huu mbona sielewi,yaani hii mifumo yetu mbona ya kishamba hivi,loopholes kibao,hapo wamwache msomi wetu wawajibishwe wenye mamlaka,Kwa wenzetu hapo wangeshajiuzulu mbuzi kadhaa ila huku hawagusiki.
 
Back
Top Bottom