Bunge la Ulaya: Hii ni bahati mbaya au ni malengo maalum?

Bunge la Ulaya: Hii ni bahati mbaya au ni malengo maalum?

Na watu wa mkuu atakayekuja hiyo sentensi inazungumzia hao watu na wala haizungumzii huyo mkuu, ila inawakilisha kwamba hao ni watu wa mkuu

Watauangamiza mji na patakatifu hapo inaongelewa wingi wa watu watakaouangamiza huo mji na sio mkuu mwenyewe

Mkuu mwenyewe ni nani sasa!? fungu la 27 linaelezea

Daniel 9:27 Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.

kwa hiyo mambo yote yanaanzia hapo sasa kwenye hilo fungu la Daniel 9:27, hilo ndio mpinga kristo anaelezewa, ndio maana hata Yesu aliposema mkiona Chukizo la Uharibifu lililonenwa na nabii Daniel alikuwa akirejea hilo fungu la Daniel

Ni kweli pia roho ya mpinga kristo inafanya kazi, lakini mnyama Masihi wa uongo ambae Wayahudi watamkubali kwasababu walimkataa Yesu ni huyo mmoja na wala sio wengi kwa hiyo huyo ndio tunayemzungumzia, hiyo Daniel 9:27 bado sioni kama imetimia...

hiyo kuharibu hapo mahali patakatifu na mji imo ndani ya majuma 69, kwa hiyo juma la 70 hapo bado halijatimia...
Mkuu,unawezaje kupata watu "wa fulani" bila kuwa na huyo fulani?

Mfano huwezi kusema watu wa Kikwete bila ya kuwa na Kikwete ...!
 
Ok mkuu,hebu kaweke halafu tuone kama tunaweza kujifunza kitu kwa pamoja

Sasa mkuu,mnyama wa nne wa kwenye Danieli 7 ni nani?

Ni revival Roman au ni ancient Roman Emperor?

Okay sawa mkuu nitaziweka zile hesabu kule, mnyama wa nne wa kwenye Daniel 7 ni ancient Roman Empire... wale wafalme kumi yaani zile pembe kumi ndio zinaweza zikaform Revived Roman Empire, hizo pembe kumi kwa mtazamo wangu naona zinaenda corresponding kwa zile nyayo kumi za vidole kwenye ile sanamu katika sura ya 2 ya Daniel...

Halafu rejea na ile concept ya kwenye Ufunuo niliyokupa nikielezea fungu la Ufunuo 17:8
 
Sasa Mkuu wa chuo ulichosema kimetimia 70AD ni nini kwenye Unabii.. mbna kama wasema na mkuu wa watu atakayekuja kwamba bado hajaja

Halafu wasema tena kwamba Walioharibu Mahali Patakatifu walitimiza 70AD.. wakati stori ya kuharibiwa si kwamba imekatwa katwa ila Watu hao lazima waje na mkuu wao...

Hebu hapa kidogo tujadili

Naenda kule jukwaa la dini kupiga hayo mahesabu ya majuma 69 kwenye uzi wa Papa sio mpinga kristo...

Hayo yote yalitimizwa katika majuma yale 69, ila juma moja ambalo ndio limebaki, kumbuka hiyo sura ya 9 ilihusu mji wa Yerusalem na watu wake yaani Wayahudi...

Hapo anaposema kwamba mkuu atakayekuja inaweza ikawa inamaanisha pia watu wa Mataifa, Daniel 9:27 ina deal na ile miaka saba ya dhiki pamoja na dhiki kuu miaka mitatu na nusu sawa na siku 1260...

kwa hiyo huyo mkuu atakayekuja ndiye mpinga kristo, na mkuu atakayekuja anaweza akatokana na hao mataifa waliouharibu mji, kwa hiyo hao waliouharibu mji ni watu wa Mataifa tofauti na Wayahudi...
 
Mkuu,unawezaje kupata watu "wa fulani" bila kuwa na huyo fulani?

Mfano huwezi kusema watu wa Kikwete bila ya kuwa na Kikwete ...!
Lakini pia unaweza ukasema watu wa Kikwete watafanya hivi, lakini sio kwamba Kikwete atakuwa anafanya nao kwa pamoja... inamaana Kikwete pia anaweza pia asiwepo ila wakawepo watu wake...

Tukirudi katika concept mkuu anaweza akatokana na hao Mataifa, kwa hiyo kwa lugha nyingine naweza kusema watu wa Mataifa tofauti na Wayahudi...

Kwa hiyo yupo huyo mkuu ambaye ana mamlaka aliyopewa na Joka, anaweza akawa mkuu wa Tito pia...
 
Okay sawa mkuu nitaziweka zile hesabu kule, mnyama wa nne wa kwenye Daniel 7 ni ancient Roman Empire... wale wafalme kumi yaani zile pembe kumi ndio zinaweza zikaform Revived Roman Empire, hizo pembe kumi kwa mtazamo wangu naona zinaenda corresponding kwa zile nyayo kumi za vidole kwenye ile sanamu katika sura ya 2 ya Daniel...

Halafu rejea na ile concept ya kwenye Ufunuo niliyokupa nikielezea fungu la Ufunuo 17:8

Ok,ngoja nisubiri hizo hesabu halafu nione kama nitapata jambo hapo ....!!
 
Lakini pia unaweza ukasema watu wa Kikwete watafanya hivi, lakini sio kwamba Kikwete atakuwa anafanya nao kwa pamoja... inamaana Kikwete pia anaweza pia asiwepo ila wakawepo watu wake...
Hili ni gumu sana mkuu kwasababu ukishasema watu wa Kikwete tayari kikwete anaexist,hivyo haiwezekani wawe watu wa kisichokuwepo
Tukirudi katika concept mkuu anaweza akatokana na hao Mataifa, kwa hiyo kwa lugha nyingine naweza kusema watu wa Mataifa tofauti na Wayahudi...

Kwa hiyo yupo huyo mkuu ambaye ana mamlaka aliyopewa na Joka, anaweza akawa mkuu wa Tito pia...
Bado hapo inatakiwa huyo mkuu awepo ili ilete maana mkuu

Hapawezi kuwepo watu wa fulani halafu huyo fulani awe hayupo

Mkuu hili nashindwa kulikubali ...!!
 
Hata nikiamua kunyamaza nashindwa kwa maswali yako ya kitoto.!

Uwezekano huo upo.
Yesu alipokufa, waliobaki waliitwa Watu wa yesu.

Moses alipoondoka Watu wake waliitwa WATU WA MUSA.

Sio lzm mtu awepo ndio watu wake waitwe kwa Jina lake.

Point iko wazi

Kwa muktadha huu ni sawa ....

Nilichokuwa nakataa hapa ni kupata watu wa fulani halafu huyo fulani akawa hajawahi kuwepo

Unaweza kupata watu wa "fulani" kama huyu fulani aliwahi kuwepo halafu akaondoka lakini sio huyo fulani awe hajawahi kuwepo!
 
Hili ni gumu sana mkuu kwasababu ukishasema watu wa Kikwete tayari kikwete anaexist,hivyo haiwezekani wawe watu wa kisichokuwepo

Bado hapo inatakiwa huyo mkuu awepo ili ilete maana mkuu

Hapawezi kuwepo watu wa fulani halafu huyo fulani awe hayupo

Mkuu hili nashindwa kulikubali ...!!
na watu wa mkuu atakayekuja watu wa mkuu atakayekuja...

Hapo sentensi inamaana nyingi, huyo mkuu atakayekuja hajulikani ni nani, lakini pia haimaanishi mkuu atakayekuja ni Tito kwasababu tumeona kwasababu kabla ya Tito walipita Wafalme wengine na hatujui huyo mpinga kristo atakuwa ni nani, ukirejea Ufunuo 17:8 kuna concept ya mnyama yu tayari kupanda kutoka kuzimu

pia kuna concept ya alikuwepo, je huyo mkuu ni nani!? halafu hayo matukio yote yapo katika time frame, ndio maana majuma yote 70 hayakupelekwa moja kwa moja , kwa hiyo kumbuka nimesema kuna gap kati ya juma la 69 na 70

Nafikiri pia hapo juu jamaa atakuwa ametoa maana nzuri ya hiyo concept...
 
Umeniona wapi wewe! Au we ni mmoja ktk wale wapika chips wa KFC!

Basi nahamia Subway! Usije niwekea sumu bure kwenye kuku.
Mara zote unapenda mambo ya udini tu!na bora uhame nitakuwekea sumu kweli pambaf zako
 
na watu wa mkuu atakayekuja watu wa mkuu atakayekuja...

Hapo sentensi inamaana nyingi, huyo mkuu atakayekuja hajulikani ni nani, lakini pia haimaanishi mkuu atakayekuja ni Tito kwasababu tumeona kwasababu kabla ya Tito walipita Wafalme wengine na hatujui huyo mpinga kristo atakuwa ni nani, ukirejea Ufunuo 17:8 kuna concept ya mnyama yu tayari kupanda kutoka kuzimu

pia kuna concept ya alikuwepo, je huyo mkuu ni nani!? halafu hayo matukio yote yapo katika time frame, ndio maana majuma yote 70 hayakupelekwa moja kwa moja , kwa hiyo kumbuka nimesema kuna gap kati ya juma la 69 na 70

Nafikiri pia hapo juu jamaa atakuwa ametoa maana nzuri ya hiyo concept...

Tatizo linakuja pale Warumi walipolivunja hekalu na kuonekana wametimiza unabii ....!!
 
mbona hata jengo letu la bunge pale Dodoma nalo limefanana kweli na mnara wa babeli
 
Na watu wa mkuu atakayekuja hiyo sentensi inazungumzia hao watu na wala haizungumzii huyo mkuu, ila inawakilisha kwamba hao ni watu wa mkuu

Mi nadhani hapa hujapaelewa vizuri.. inakuwaje watu wanakuja kuangamiza mji bila kuwa na Kiongozi wao.. ?

Mfano

Jeshi haliwezi kuvamia sehemu bila kuwa na amri kutoka kwa Raisi. Na Raisi ndo anayezungumziwa hapo kwamba ndiye mkuu

Watauangamiza mji na patakatifu hapo inaongelewa wingi wa watu watakaouangamiza huo mji na sio mkuu mwenyewe

Hapa nakubaliana na wewe kwamba ni watu ndio watakao uharibu mji ila hao watu hawawezi kuuharibu mji kama hawajapata Amri kutoka kwa Huyo mkuu ambaye amezungumzwa hapo juu

Mkuu mwenyewe ni nani sasa!? fungu la 27 linaelezea

Daniel 9:27 Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.

kwa hiyo mambo yote yanaanzia hapo sasa kwenye hilo fungu la Daniel 9:27, hilo ndio mpinga kristo anaelezewa, ndio maana hata Yesu aliposema mkiona Chukizo la Uharibifu lililonenwa na nabii Daniel alikuwa akirejea hilo fungu la Daniel

Kama unakumbuka ulisema kuwa Antious alikamilisha kusimamisha Sanamu zake mule ndani ya hekalu na ukasema kuwa ndio chukizo haribifu lenyewe..

Ila hapa Tena naona nachanganyikiwa kwa weww tena kusema kuwa Mpinga Kristo anakuja na bado hayajatimia

Ni kweli pia roho ya mpinga kristo inafanya kazi, lakini mnyama Masihi wa uongo ambae Wayahudi watamkubali kwasababu walimkataa Yesu ni huyo mmoja na wala sio wengi kwa hiyo huyo ndio tunayemzungumzia, hiyo Daniel 9:27 bado sioni kama imetimia...



hiyo kuharibu hapo mahali patakatifu na mji imo ndani ya majuma 69, kwa hiyo juma la 70 hapo bado halijatimia...

Yaani hapa ndo panatia moto akilini.. kwahiyo kama kuharibiwa kwa mahali Patakatifu palitimia kwenye majuma 69... palifanyikaje bila Huyo mkuu kuwepo kama iliyosema

●Daniel 9:26 biblia ya SUV inasema hivi
..........Na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji na mahali Patakatifu

●Daniel 9:26 BHND inasema hivi
...... mji na mahali patakatifu kabisa vitaaribiwa Na Jeshi la mtawala atakayekuja kushambulia...

●Daniel 9:26 biblia ya BHN inasema hivi

......mji na mahali patakatifu kabisa vitaaribiwa Na jeshi la mtawala atakayekuja...


Sasa Wewe wasema mkuu hapo hayupo ila ni watu wake ila yeye bado hajaja... ila baadae tena wasema kwamba ni kweli jambo hilo lilitoea mwaka 70AD kwamba Mahali Patakatifu paliharibiwa na Jeshi la Rumi na Titus sasa inamaa mkuu hapo ni Yule aliyeliongoza Jeshi

Confused
 
Hata nikiamua kunyamaza nashindwa kwa maswali yako ya kitoto.!

Uwezekano huo upo.
Yesu alipokufa, waliobaki waliitwa Watu wa yesu.

Moses alipoondoka Watu wake waliitwa WATU WA MUSA.

Sio lzm mtu awepo ndio watu wake waitwe kwa Jina lake.

Point iko wazi

Daniel Imeandikwa hivi

"Na watu wa mkuu atakayekuja wataangamiza mahali Patakatifu "

MKUU NDO ATAKUJA NA WATU WAKE

Tunaambiwa na Mkuu wa chuo kuwa mahali hapo paliharibiwa mwaka 70AD.. na watu wa huyo Mkuu

Sasa ndo nauliza hao watu wameharibuje bila amri ya huyo mkuu wao
 
Last edited by a moderator:
na watu wa mkuu atakayekuja watu wa mkuu atakayekuja...

Hapo sentensi inamaana nyingi, huyo mkuu atakayekuja hajulikani ni nani, lakini pia haimaanishi mkuu atakayekuja ni Tito kwasababu tumeona kwasababu kabla ya Tito walipita Wafalme wengine na hatujui huyo mpinga kristo atakuwa ni nani, ukirejea Ufunuo 17:8 kuna concept ya mnyama yu tayari kupanda kutoka kuzimu

pia kuna concept ya alikuwepo, je huyo mkuu ni nani!? halafu hayo matukio yote yapo katika time frame, ndio maana majuma yote 70 hayakupelekwa moja kwa moja , kwa hiyo kumbuka nimesema kuna gap kati ya juma la 69 na 70

Nafikiri pia hapo juu jamaa atakuwa ametoa maana nzuri ya hiyo concept...

Ngoja mkuu nikupe challenge moja
● Kama huyo mkuu atakayekuja hajulikani bado kwahiyo kilichotokea 70AD kitamuhusishaje sasa huyo mkuu ambaye unahisi atatokea baadae

Mfano huyo mkuu atokee leo.. inakuwaje wale walioharibu mahali Patakatifu 70AD wakawa ni watu wa huyu Aliyejitokeza leo?
 
Tatizo linakuja pale Warumi walipolivunja hekalu na kuonekana wametimiza unabii ....!!

Yes hapo ndo tatizo.. maana Mkuu wa chuo alisema kuwa 70AD Unabii ulikamilika wa kuharibiwa mahali Patakatifu. .ila bila huyo mkuu kujulikana..

Na wakati Daniel anapewa huu unabii mambo yalikuwa bado hayajatimia Inamaana yalitimia baadae wakati wa Kukataliwa kwa YESU kristo. . Ila Mkuu wa chuo anasema tena kwamba yametimia ila ni Nusu bila Mkuu mwenyewe kujulikana ni nani

Yaani hapo tu ndo nachanganyikiwa na kujiuliza swali Hili
● Kama watu wa huyo mkuu ndo walioharibu mwaka 70AD na tayari wameshakufa wote. Inakuwaje huyo mkuu aje atokeze baadae na awe na hao watu tena. Yaani tuseme huyo mkuu ajitokeze leo 2014.. atakuwaje na watu wale wake wa 70AD?
 
Last edited by a moderator:
Hata nikiamua kunyamaza nashindwa kwa maswali yako ya kitoto.!

Uwezekano huo upo.
Yesu alipokufa, waliobaki waliitwa Watu wa yesu.

Moses alipoondoka Watu wake waliitwa WATU WA MUSA.

Sio lzm mtu awepo ndio watu wake waitwe kwa Jina lake.

Point iko wazi
Hapa unachanganya BEFORE and AFTER

●Yesu watu wake walikuja baada ya yeye kuondoka

● Musa naye alikuwa pamoja nao na akawaacha.

Yaani ni sawa na USEME WAKRISTO kabla Yesu kristo hajaja...Jambo ambalo haliwezekani

ILA DANIEL inatuambia kwamba na WATU wa mkuu ATAKAYEKUJA walikuja na kuharibu mahali Patakatifu

HAPO Tayari mkuu ana watu na ndo anawaongoza kwenda kuharibu mahali Patakatifu. .. NI SAWA NA JESHI LENYE AMRI JESHI WAKE
 
Back
Top Bottom