Bunge lapitisha Muswada unaotaka wake wa Marais na Maspika wastaafu kulipwa kiinua mgongo

Bunge lapitisha Muswada unaotaka wake wa Marais na Maspika wastaafu kulipwa kiinua mgongo

Bunge limepitisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 4 wa mwaka 2023 ambapo moja ya marekebisho katika sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa kisiasa inapendekezwa Wenza (Mke/Mume) wa Marais Wastaafu, Wenza wa Makamu wa Rais Wastaafu na Wenza wa Mawaziri Wakuu Wastaafu walipwe kiinua mgongo kwa kipindi cha uongozi wa Wenza
wao.

Akiwasilisha marekebisho hayo leo Oktober 31,2023 wakati wa kikao cha Bunge Mjini Dodoma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema kuwa vifungu vipya vya 9A, 12A na 14A vinapendekezwa kuongezwa katika Sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa Kisiasa, Sura ya 225.

Sambamba na marekebisho hayo, vifungu vya 11, 13 na 15 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa malipo ya fadhila kwa Wenza wa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu endapo watafariki wakiwa madarakani au baada ya kumaliza muda wao na kufariki kabla ya kulipwa mafao au stahiki zao.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kifungu cha 18 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa wenza wa Spika Mstaafu aliyefariki kupokea mafao ya pensheni ya kila mwezi.

Muswada huo uliopitishwa utawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kuutazama muswada huo na akiuridhia atasaini ili iwe sheria.
#MillardAyoBUNGENI
Nani atawapa kiinua mgongo wake za walimu, wanajeshi wetu JWTZ, polisi, madaktari na wauguzi, na watumishi chungu nzima?

Imagine Mke wa Rais awamu ya 4,Ana haja ya kiinua mgongo kweli? 😀😀, yeye analipwa mafao ya mke wa Rais na mafao ya mbunge? Naambiwa alikuwa mwalimu, je amefikiria kuhusu kiinua mgongo cha mke wa mwalimu?

CCM mbele kwa mbele 😀😀😀Karibuni mnisakame
 
Ni kwanini wamewaacha watoto wa marais wastaafu? Napendekeza watoto, mashemeji, wakwe, mabinamu, wajomba na mashakazi wa marais wastaafu nao waanze kulipwa kiinua mgongo, tusibague.

Nchi maskini ambayo hata kuendesha bandari imewashinda ila watu wanawaza kujaza matumbo yao tu. Pesa ni nzuri lakini tukumbuke kwamba hazijawahi kutosha. Mishahara mikubwa,marupurupu mengi lakini bado ufisadi hauishi, hamjifunzi?

Ukiambiwa waliopitisha hiyo sheria baadhi yao kwenye majimbo yao kuna watoto wanasoma huku wamekaa chini na hawana madarasa ya kutosha huwezi kuamini.
 
Nani atawapa kiinua mgongo wake za walimu, wanajeshi wetu JWTZ, polisi, madaktari na wauguzi, na watumishi chungu nzima?

Imagine Mke wa Rais awamu ya 4,Ana haja ya kiinua mgongo kweli? 😀😀, yeye analipwa mafao ya mke wa Rais na mafao ya mbunge? Naambiwa alikuwa mwalimu, je amefikiria kuhusu kiinua mgongo cha mke wa mwalimu?

CCM mbele kwa mbele 😀😀😀Karibuni mnisakame
Pesa haijawahi kitosha mkuu, hata wewe huwezi kutosheka pesa. Lakini kuna wakati mtu inampasa kuona aibu, mtu sasa unakuwa na tamaa hadi unatia aibu. Wananchi watakushangaa!
 
Bunge limepitisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 4 wa mwaka 2023 ambapo moja ya marekebisho katika sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa kisiasa inapendekezwa Wenza (Mke/Mume) wa Marais Wastaafu, Wenza wa Makamu wa Rais Wastaafu na Wenza wa Mawaziri Wakuu Wastaafu walipwe kiinua mgongo kwa kipindi cha uongozi wa Wenza
wao.

Akiwasilisha marekebisho hayo leo Oktober 31,2023 wakati wa kikao cha Bunge Mjini Dodoma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema kuwa vifungu vipya vya 9A, 12A na 14A vinapendekezwa kuongezwa katika Sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa Kisiasa, Sura ya 225.

Sambamba na marekebisho hayo, vifungu vya 11, 13 na 15 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa malipo ya fadhila kwa Wenza wa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu endapo watafariki wakiwa madarakani au baada ya kumaliza muda wao na kufariki kabla ya kulipwa mafao au stahiki zao.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kifungu cha 18 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa wenza wa Spika Mstaafu aliyefariki kupokea mafao ya pensheni ya kila mwezi.

Muswada huo uliopitishwa utawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kuutazama muswada huo na akiuridhia atasaini ili iwe sheria.
#MillardAyoBUNGENI
Bunge Kwa Sasa linatumia muda uliobaki kupitisha vitu vya ovyo Kwa sababu ni la chama kimoja, ila wakumbuke Yana mwisho
 
Kuna kamsemo vijana wa hovyo hua wanasema kwamba "Tanzania ni channel ya vituko kuzimu" nakubaliana kabisa na haka kamsemo, wanalipwa kiinua mgongo kwa kazi gani waliyo ifanyia serikali 🤔🤔🤔 hata aibu hawaoni kwa upumbavu kama huu 🤔🤔 wanafunzi kwenye vijiji vingi tuu wanakaa chini na kusomea chini ya miti kwa kukosa madarasa na madawati, lakini watu wanakaa na kuamua kupitisha wizi kama huo 🤔🤔

Kuna wabunge wengine wamepitisha huo wizi na majimboni kwao maji ya kunywa tuu ni mgogoro

kama kuna vitu vinatia hasara hii nchi basi ni lile jengo la Dodoma na waliomo ndani yake, pamoja na chama cha mboga mboga yani ni msiba wa taifa 🤦🤦🤦
 
Leo Mwanasheria mkuu wa Serikali ametoa taarifa kwenye vyombo vya habari na kusema kwamba wenza wawastaafu sasa ni wakati wa kulipwa kiinua mgongo kwakuwa wenza wao wanakuwa wamelitumikia taifa kwa uzalendo mkubwa.

Hata hivyo waliowengi wameshindwa kuelewa kama ni kwa wafanyakazi wote wa serikali kuanzia ngazi za chini au sheria hiyo itahusu wafanyakazi kama raisi, makamu wa raisi, spika, na waziri mkuu pamoja na majaji

Maoni yangu ni kwamba kama sheria hii imepitishwa tunawajibu wa kupinga sheria hiyo na ikafutwa kabisa kwan kodi za wananchi inaonesha imefikia mahali ambapo zinatumika kwa faida ya watu wenye vyeo vikubwa serikalini , viongozi tulionao hawataki kujali matatizo ya wananchi wanajitengenezea sheria za ulaji ambazo hazipo kumsaidia mtu wa chini.

Nawatakia usiku mwema
 
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116] bunge letu
FB_IMG_1698784969544.jpg
 
Leo mwanasheria mkuu wa serikali ametoa taarifa kwenye vyombo vya habari na kusema kwamba wenza wawastaafu sasa ni wakati wa kulipwa kiinua mgongo kwakuwa wenza wao wanakuwa wamelitumikia taifa kwa uzalendo mkubwa.

Hata hivyo waliowengi wameshindwa kuelewa kama ni kwa wafanyakazi wote wa serikali kuanzia ngazi za chini au sheria hiyo itahusu wafanyakazi kama raisi, makamu wa raisi, spika, na waziri mkuu pamoja na majaji

Maoni yangu ni kwamba kama sheria hii imepitishwa tunawajibu wa kupinga sheria hiyo na ikafutwa kabisa kwan kodi za wananchi inaonesha imefikia mahali ambapo zinatumika kwa faida ya watu wenye vyeo vikubwa serikalini , viongozi tulionao hawataki kujali matatizo ya wananchi wanajitengenezea sheria za ulaji ambazo hazipo kumsaidia mtu wa chini.

Nawatakia usiku mwema
Tija ya hao wenza kulipwa ni nini haswa?
 
Iz ni moja ya sababu kwanin Mataifa ya Africa yana rasilimali nyingi lkn hayaendelei. sababu ni iz wenye nacho ndo wanazidi kujirimbikizia mahari na asiye nacho anabaki alivyo ama anazidi kushuka chini zaidi kiuchumi. Fikiria hao pesa watakazokuwa wanalipwa ni nyingi sana. Kiasi kwamba sehemu kubwa sana bado wanachi wa kawaida hawana huduma muhimu kama hospital, madarasa, maji, barabara n.k.. Na kama haitoshi wako watumishi wana mishahaa kiduchu sana hao hawafikiriwi kunyenyuliwa bali wenye nacho ndo wanajifikiria wao kuzidi kupaa tu. serikali utasikia haiajiri kwasababu haina pesa za kutosha vijana wengi ni wahitimu wako mtaani kazi hawana, wakubwa wao wanachowaza ni matumbo yao tu. Dah! inauma sana na tutafika tumechoka sana na c kufika hatutofika kwa stahili hii cc walala hoi, bali tutalala mauti tukiwa tumechoka sana!.
 
Back
Top Bottom