Buriani Mzee Ruksa: Ni Deng Xiaoping Wetu wa Mageuzi ya Kiuchumi, Demokrasia, Haki za Binadamu na Uhuru wa Habari. Asante kwa Ruksa Zako, Pumzika!

Hapakuwa na saloon za kunyoa nywele miaka ile, tulikuwa na kinyozi wetu pale kwenye mti wa mwembe kabla hujavuka barabara na kuingia ferry kupanda pantoni siku hizi wanapaki bodaboda ukiwa unapandisha kuelekea jengo la wizara ya ardhi, anakunyoa na kiwembe tu lakini utadhani katumia machine za kisasa.

Duka la keki lilikuwa moja tu gloria bakery pale karibu na mnara wa askari ukiwa unaelekea Saint Joseph, wazee walinunua keki siku moja kabla ya krismasi.
 
Maisha yalikuwa yanatisha sana

Leo viatu vya plastic vimejaa kariakoo hata kama vinaisha mapema lakini vimesaidia watu wengi

Leo kariakoo zimejaa nguo feki za kusukuma siku hata kama zinachakaa mapema zinasaidia

Nchi imetoka mbali sana ,Mnaenda kutafuta mafuta ya taa ,Leo mafuta ya taa yatakuwa yamebaki vijiji vichache sana

Usiku ni mwendo wa tochi tu ukiwa unatembea barabarani,Maana nyumba nyingi hakuna umeme

Radio ni moja tu ya kusikiliza,Taarifa ya habari wazee wanakuwa makini kusikiliza na wako punctual sana na muda
 
Kulikuwa na nguo za kupika, kulikuwa na zile raba asante Salim.

Ukivaa raba za Kenya shuleni unaonekana wa maana mbele ya marafiki zako.

Leo hii umeme unakaribia kuifikia Tanzania nzima, maendeleo makubwa sana.
 
Kwa shida nilizozipata wakati wa Nyerere hata ukiuza dawa ya mbu unaitwa mlanguzi!!!

Leo mtu anambie Nyerere alikuwa mzuri huwa nashangaa sana na ndio maana wakati mwengine nashindwa kuchangia chochote kwa kujua wengi wanaobisha ni watoto wa juzi madhila tuliopitia hawayajui
 
Jamaa mpuuzi, anaamin kwenye thamani ya sh ila sio ubora wa maisha, naonaga bongo watu wengi wana huu upuuzi
 
Kuna kipindi alipwaya mpaka Nyerere aliamua kumsaidia.

Alishindwa kabisa kucontrol bunge , serikali ilikua inaanguka.

Anyways nitamkumbuka kwa kuuza Loliondo kwa waarabu.

Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
Tofautisha kupwaya na demokrasia Mmasai wa CDm. Aliwaacha waongeze, na Nyerere alitaka amuendeshe vyote alivimaliza kwa style Ile Ile ya Jakaya. Nyerere alipigwa pini na azimio lake likafa na wale wehu wakina Njelu Kasaka wakapotezwa katika siasa.

Tatizo lenu cdm mnataka kuendeshwa pita kama aliyofanya chuma JPM
 
Mmojawapo ni huyu Stroke ..toto la miaka ya 2000 linachojua ni ChaDema,Mbowe na kunakili ujinga na matusi ya Lema au mdude Mdude_Nyagali mtandaoni.

Hovyo sana hili toto. Hata Maghayo anakuwaga ana afadhali
 
Kuna kipindi alipwaya mpaka Nyerere aliamua kumsaidia.

Alishindwa kabisa kucontrol bunge , serikali ilikua inaanguka.

Anyways nitamkumbuka kwa kuuza Loliondo kwa waarabu.

Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
Hivyo ndivyo namna ulivyoona umkumbuke Mzee? Wewe ni NARCISSISTIC PERSON fanya mpango umuone Therapist.
 
Kuna kipindi alipwaya mpaka Nyerere aliamua kumsaidia.

Alishindwa kabisa kucontrol bunge , serikali ilikua inaanguka.

Anyways nitamkumbuka kwa kuuza Loliondo kwa waarabu.

Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
Kwenye nchi ya watu waliostaarabika siyo sifa nzuri kwa rais wa nchi kuingilia shughuli za bunge.
Bunge liliachwa lifanye kazi yake.
Na hoja kubwa wakati huo ilikuwa ni aina ya Muungano.
Jiulize tangu wakati ule mpaka sasa takriban miaka 30 imepita, je hoja ya Muungano wa serikali tatu imefutika mioyoni mwa watanzania?
Kila siku watu wanajadili Muungano hapa hapa Jamiiforums.
 
Nikikumbuka dhiki ya 1980 -1985, baada ya Vita vya Kagera na mazungumzo na IMF kuvunjika, ilikuwa si ya kitoto.

Tulikosa vitu basic kama sabuni na dawa ya kupigia mswaki, chakula kununua kwa kidaftari duka la kaya, kwa kulikimbiza gari la ugawaji, ukitaka kununua sukari, unalazimishwa kununua unga wa muhogo. Nguo midabwada.

Mwinyi alikuja kuimaliza.
 
Kuna kipindi alipwaya mpaka Nyerere aliamua kumsaidia.

Alishindwa kabisa kucontrol bunge , serikali ilikua inaanguka.

Anyways nitamkumbuka kwa kuuza Loliondo kwa waarabu.

Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
Mimi huwa kuna mambo wanamsifia mzee Ruksa lakini mimi huwa naona ni kama kujikomba au kutofikiria kwa kina.
1. Ni kweli aliruhusu biashara huria, lakini nina uhakika ni kutokana na mabadiliko ya dunia, na hata kama Nyerere angeendelea kuongoza, angefanya hivyo hivyo. Anyways, kwa hili nampa maksi 75%.
2. Vyama vingi na demokrasia. Hili hakuwa na jinsi kwa sababu yalikuwa ni mabadiliko ya dunia nzima, na hata zile serikali za kufashisti zilijikuta zikiingia kwenye huo mfumo. Na mbaya zaidi, alileta mabadiliko ya bandia kwa sababu hakupenda kubadilisha mfumo wa utawala uendane na hali halisi. Hili nampa maksi 40%
3. Uhuru wa vyombo vya habari. Hili nalo alifeli kwa sababu aliachia uholela wa habari na siyo ubora wa habari. Matokeo yake mpaka leo hali ni mbaya sana kwa kuwa sekta ya habari imekuwa ni sekta ya kitapeli ambayo watu ''wajanja wajanja'' wanaingia ili kutafuta kula yao.
4. Na mwisho niseme kuwa mwalimu Nyerere alisaidia sana kurekebisha mambo yalipokuwa yanaenda mrama kipindi cha utawala wa Mwinyi. uzuri wa Mwinyi ni kuwa alikuwa mnyenyekevu na alikubali kusahihishwa pale alipoteleza.
 
Nadhani unafikiri ki rivasi rivasi mambo yaliharibika sana sana chini ya Nyerere Nchi ilikuwa UCHI hakuna kipindi kilikuwa na DHIKI kuliko kipindi cha Nyerere.

Majeshi yetu yenyewe yalikuwa yanavaa Viraka.
Nyerere hakuwahi shindwa.

Mabeberu waliamua kumdhalilisha tu maana aliwashinda kwa mengi.

Akili ndogo hamuwezi elewa.

Mashirika yote aliyoyaanzisha Nyerere viongozi wetu wajinga wameyaua.

Mashirika na viwanda vyote wapumbavu wameviua.
 
Kwa kupitia huu Uzi ndiyo napata picha halisi kwa nini Bw. Malcolm aliandika uzi kuwa kwa nini Nyerere aliwapitisha watanzania hii njia (dhiki za awamu ya Nyerere kwa watanzania).
 
Kwa kupitia huu Uzi ndiyo napata picha halisi kwa nini Bw. Malcolm aliandika uzi kuwa kwa nini Nyerere aliwapitisha watanzania hii njia (dhiki za awamu ya Nyerere kwa watanzania).
Nairobi palionekana kama Ulaya, mtu akitoka Nairobi anarudi na sabuni, dawa za kupigia mswaki na bidhaa nyingine za basic needs.

Mwinyi aliondoa habari hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…