Burkina Faso: Cptn. Ibrahima Traore apunguza mishahara ya wanasiasa

Burkina Faso: Cptn. Ibrahima Traore apunguza mishahara ya wanasiasa

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814

View: https://youtu.be/GxN6WSDDIF8?si=6EyFTUpKptlgFoEm

Huko ni Burkina Faso.
Kutokana na fedha alizoziokoa, Capt. Ibrahima amenunua matrekta 5,000 na kuyagawa kwenye vijiji vya Burkina Faso. Ameweka lengo la kutonunua chakula kutoka nje katika miaka mitano ijayo, pia kutengeneza asilimia 60% ya nguo zote nchini (Tujilishe na tujivishe wenyewe).

Na kwa vile nchi hiyo inakabiliwa na uasi uliopangwa na Ufaransa kwa sababu ya kuchukua rasilmali za nchi hiyo (kumbuka Congo), Cap. Ibrahim aliwafukuza wanajeshi wote wa Ufaransa nchini mwake na sasa vita vya kukomboa maeneo yanayoshikiliwa na waasi, wanapigana Waburkinabe wenyewe.

Baada ya majeshi ya Ufaransa kusua sua kwa miaka mingi wakidai waasi wana silaha kali, sasa jeshi la Burkinabe limeanza kurudisha ardhi yake.

Leo hii amekomboa eneo muhimu lenye machimbo makubwa ya dhahabu lililokuwa linashikiliwa na waasi.

Amefanikiwa kufanya hivyo baada ya kununua vyombo vya kisasa vya kijeshi, vifaru na magari ya deraya, zikiwemo drone 20 kutoka China, Iran...na drone zinazosifiwa zaidi kutoka Uturuki za Akinci ambazo zina uwezo wa kugundua na kuwaangamiza waasi hata saa nane za usiku, hata wakiwa wamejificha chini ardhini, kwa kutumia miali ya laser ya kuangaza (infra red).

Sidhani kama Bongo tuna zana hizo, ingawaje tuna uchumi almost maradufu ya BF. Ni uaminfu, uzalendo, akili na upangaji (vitu ambavyo hatuna).

Nikisoma hivi nalia kwa uchungu na hasira. Acha nisiendelee nisije nikatukana! Kweli matatizo yetu makubwa ni uongozi mbovu. Huyu kijana wa miaka 34 ameigeua nchi kabisa katika miaka miwili tu.

Dhahabu yote ya BF inachimbuliwa, kusafishwa na kuuzwa na Waburkinabe wenyewe. Hata baadhi ya mashine za kufanya hivyo zimebuniwa na kutengenezwa na Waburkinabe wenyewe! Amekwisha nunua mashine za kupanda, kuvuna, kuondoa mbegu na kusuka pamba...katika miaka hiyo.

Ukosefu wa kazi umepungua kwa asilimia 4 katika miaka hiyo miwili tu. Na sasa amepunguza mshahara wake na Mawaziri kulipia maendeleo.

Bado anatembelea Isuzu 2018!
 
Demokrasia sometime ni upumbavu wa kuwapumbaza watu.
Nakubali. Lakini kutoka jeshi letu hawezi kuja mtu kama Traore au Kagame. Mijitu iliyokulia wizi itawaona raia ni adui zao! Afadhali tudeme hivyo hivyo na the so-called democracy. Akija mjeshi ataona maendeleo ni kuuwa tu.
Quality education hakuna!
 
Kwani idd Amin alianzaje mwanzoni mwa utawala wake si watu walikuwa wanasema ameletwa na Mungu ila baadae iliishaje...
mara nyingi utawala wa kupinduana kijeshi kama hivyo hauna mwisho mwema. Sifa kubwa ni kukataa kutoka madarakani na kuona nchi ni kama mali yako si mnamuona m7 wa ug.
 

View: https://youtu.be/GxN6WSDDIF8?si=6EyFTUpKptlgFoEm

Huko ni Burkina Faso.
Kutokana na fedha alizoziokoa, Capt. Ibrahima amenunua matrekta 5,000 na kuyagawa kwenye vijiji vya Burkina Faso. Ameweka lengo la kutonunua chakula kutoka nje katika miaka mitano ijayo, pia kutengeneza asilimia 60% ya nguo zote nchini (Tujilishe na tujivishe wenyewe).
Na kwa vile nchi hiyo inakabiliwa na uasi uliopangwa na Ufaransa kwa sababu ya kuchukua rasilmali za nchi hiyo (kumbuka Congo), Cap. Ibrahim aliwafukuza wanajeshi wote wa Ufaransa nchini mwake na sasa vita vya kukomboa maeneo yanayoshikiliwa na waasi, wanapigana Waburkinabe wenyewe. Baada ya majeshi ya Ufaransa kusua sua kwa miaka mingi wakidai waasi wana silaha kali, sasa jeshi la Burkinabe limeanza kurudisha ardhi yake. Leo hii amekomboa eneo muhimu lenye machimbo makubwa ya dhahabu lililokuwa linashikiliwa na waasi. Amefanikiwa kufanya hivyo baada ya kununua vyombo vya kisasa vya kijeshi, vifaru na magari ya deraya, zikiwemo drone 20 kutoka China, Iran...na drone zinazosifiwa zaidi kutoka Uturuki za Akinci ambazo zina uwezo wa kugundua na kuwaangamiza waasi hata saa nane za usiku, hata wakiwa wamejificha chini ardhini, kwa kutumia miali ya laser ya kuangaza (infra red). Sidhani kama Bongo tuna zana hizo, ingawaje tuna uchumi almost maradufu ya BF. Ni uaminfu, uzalendo, akili na upangaji (vitu ambavyo hatuna). Nikisoma hivi nalia kwa uchungu na hasira. Acha nisiendelee nisije nikatukana! Kweli matatizo yetu makubwa ni uongozi mbovu. Huyu kijana wa miaka 34 ameigeua nchi kabisa katika miaka miwili tu. Dhahabu yote ya BF inachimbuliwa, kusafishwa na kuuzwa na Waburkinabe wenyewe. Hata baadhi ya mashine za kufanya hivyo zimebuniwa na kutengenezwa na Waburkinabe wenyewe! Amekwisha nunua mashine za kupanda, kuvuna, kuondoa mbegu na kusuka pamba...katika miaka hiyo. Ukosefu wa kazi umepungua kwa asilimia 4 katika miaka hiyo miwili tu. Na sasa amepunguza mshahara wake na Mawaziri kulipia maendeleo. Bado anatembelea Isuzu 2018!

Hata mugabe alianza kwa mbwembwe hizihizi lakini kili hocuata wanachi wanalia mpaka leo. Closed economy does not work anywhere.

Sana sana kitakachofuata hapo ni kuua kila anayemkosoa kwa strategy hizi mbovu anazotumia
 
Back
Top Bottom