Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia

Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia

Francis12

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2016
Posts
7,533
Reaction score
22,281
Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia.

Malisa GJ

Mosi, Huu uchungu anaouonesha Ndugai sio wa Halima na wenzake kupigwa, ni uchungu wa kupoteza yale matrilioni ya wafadhili. Ameshaona dalili zote kwamba hata akiwalinda akina Mzee Halima na wenzake waendelee kuwa wabunge, wafadhili wanaweza kugomea kutoa yale matrilioni.

Pili, Halima na wenzake hawakupigwa kwa ajili ya Mbowe. Walipigwa kwa sababu ya kutetea haki zao. Walipotolewa Segerea askari magereza waliwapiga kama vibaka kwa sababu tu walienda kupokelewa na wafuasi wao. Mashinji alipokelewa na msafara wa wafuasi wa CCM lakini hakupigwa. Double standards. Kama kweli Ndugai ana uchungu angewakemea wale askari waliofanya unyama ule sio Mbowe.

Tatu, Mzee Halima na wenzake hawajafukuzwa bila kusikilizwa. Walipewa haki ya kusikilizwa (audi alteram partem) lakini wakakataa kuitumia. Waliitwa kwa maandishi kwenye kamati kuu ili wasikilizwe wakagoma. Sasa Bwana Ndugai alitaka chama kifanyeje? Hata mahakamani mtuhumiwa akikataa kujitetea bila sababu za msingi, mahakama hulazimika kuamua kwa kusikikiza upande mmoja.

Nne, Maamuzi ya Chadema hayakufanywa na Mbowe. Yalifanywa na Kamati kuu ambayo ina wajumbe zaidi ya 40. Ni ujinga kuamini wajumbe wote hawakua na sauti isipokua Mbowe peke yake. Ndugai elewa kwamba Mbowe sio kamati kuu ya Chadema.

Tano, kumbe Ndugai anajua Halima na mwenzake walipigwa hadi wakazimia pamoja na kuvunjwa mikono na askari magereza? Unyama huu aliwahi kuulaani popote? Aliwahi kumuita Kamishna Mkuu wa Magereza kwenye kamati za bunge ajieleze kwanini Askari wake walifanya unyama ule tena kwa wabunge wanawake? Au aliona ni sawa tu kwa sababu walikua Chadema. Leo wamefurushwa ndio anasikia uchungu.

Huu utaratibu wa mtu kuonewa lakini unakaa kimya kwa sababu sio wa chama chako sio ubinadamu kabisa. Ningemuona Ndugai ana hoja kama angekemea tukio lilipotokea. Sasa Halima ameshapona na kusahau ndio Ndugai anasikia uchungu leo? Haina tofauti na mkeo kulia kwa uchungu na kukuomba msamaha kwa sababu ya vita vya majimaji eti babu yake alishirikiana na wakoloni kuwapiga wazawa. Wendawazimu!
 
Kaandika Bibi Happy
MBOWE NI NANI?
Kwa hiyo Mbowe ni Kamati kuu ya CHADEMA? Au Mbowe aishurutishe kamati kuu?

Ngoja kwanza, Kwamba Mdee alivunjika akiwa anazungumza na Mbowe? Au Bulaya ALIPIGWA na Mbowe hadi akazimia? Au Matiko alilazwa kisa alifumwa na Mbowe? Yaani MBOWE ni nani jamani hata hakamatiki akipiga hawa wanawake?

Kwamba Nusrat aliwekwa mahabusu na Mbowe sio? Kwamba Mbowe alimweka huko ili afie magereza? Wow! Kwamba Mbowe ANAMILIKI magereza, mahakama na wanasheria wote? Wow!

Sasa mkuu, mbona sijaelewa? Kwamba wabunge hawa wapewe nafasi kwa kuwa MBOWE amewanyanyasa? Kwamba ofisi ya BUNGE inawatambua kwa kuwa ndiyo ILIYOAMUA wapewe nafasi hizo?

Kama kweli wabunge hawa HAWAKUJITEUA na walitokana na uteuzi RASMI toka CHADEMA, je, haimaanishi kwamba CHADEMA ILIWAJALI? Kwa nini CHADEMA iwape nafasi halafu IWAFUKUZE uwanachama?

Je, kauli zako hizi zinathibitisha kuwa hawa wabunge HAWAKUTEULIWA na CHADEMA?
Nani aliyemtoa NUSRAT mahabusu? Kama ni CHADEMA ILIMTOA ILI AKAAPE, kwa nini huoni hili ni jambo jema? Kama CHADEMA walimtoa huko mahabusu, unataka kusema CHADEMA ndio wana nguvu ya kumtoa mahabusu yeyote wanayetaka? Hii inaleta picha gani kwa huu mhimili mkuu wa serikali?

Kwamba ALIYEMTOA Nusrat ili akaapishwe, alikuwa ANAMWEPUSHA na unyanyasaji ambao MBOWE aliufanya?

Basi, ni NANI huyo ALIYEMTOA AKAAPE ILI ASIFIE MAGEREZA kama alivyotaka Mbowe ?

Bado najiuliza, MBOWE NI NANI KATIKA NCHI HII? Spika anamlalamikia tu, hata hamfanyi kitu.

Aliyeelewa anieleweshe...
Its so confusing.
 
Hivi sijui. kwanini CCM mara zote huwa hawajibu hoja badala yake humshambulia mtu na kuacha hoja za msingi. Sasa ukisikiliza majibu ya Ndugai utaamini kuwa ni mtu mwenye sifa ya kuwa spika wa bunge? Mbona ni kama mjinga fulani asiyekuwa na elimu yoyote kichwani?
 
Mimi hizo sababu zako zote natofautiana ila la msingi ni kwamba Ndugai atajidhalilisha kama ataruhusu wabunge wasiokuwa na chama bungeni.

Wanachohitajika kufanya CHADEMA ni kulifahamisha bunge rasmi kuhusu kuwatimua chama hao wabunge wao.

Tena CHADEMA waweke wazi kwa wananchi kuhusu hatua hiyo kisha tuone kama ndugai hatawatimua kina halima bungeni.

Isije kua janja na hila za mbowe na mnyima kuvunga na kufanya propagandakwa kumbe taarifa rasmi kwa ndugai hawajatoa wala hawatatoa.
 
Chadema haina Wabunge wa Viti maalumu Ila kama Kuna Watu wataendelea Kuwa Wabunge hao siyo tatizo maana watakuwa wabunge wa Spika Ndugai kwa upande wetu tulisha maliza kazi kupitia maamuzi ya Kamati Kuu tarehe 27

Mengine ni makelele tuu
 
Hivi sijui.kwanini CCM mara zote huwa hawajibu hoja badala yake humshambulia mtu na kuacha hoja za msingi. Sasa ukisikiliza majibu ya Ndugai utaamini kuwa ni mtu mwenye sifa ya kuwa spika wa bunge? Mbona ni kama mjinga fulani asiyekuwa na elimu yoyote kichwani?
Nchi imekosa dira madhubuti,inaongozwa kwa matamko na siyo sheria tena,kufukuzwa kwa wabunge wa COVID-19 kunamhusu nini?Ndugai anachotakiwa kufuata ni sheria zinasemaje kama Mbunge akifukuzwa uanachama na siyo hizi porojo!.
 
Ni kweli bro msaada unahitajika lakini kwa taarifa za wataalam wa matibabu ya lile gonjwa sugu ni kwamba ikifikia "stage" ARV zikishazidiwa nguvu (stage ya moto inaitwa) mgonjwa anaanza kubwabwaja kila kimjiacho kinywani na mara nyingi anakuwa ni mtu wa hasira kali an visilani...tumsamehe tu kwani tayari watanzania wengi tunajitambua na kikubwa zaidi tunaelewa ila za watawala wa sasa
 
Hivi sijui.kwanini CCM mara zote huwa hawajibu hoja badala yake humshambulia mtu na kuacha hoja za msingi. Sasa ukisikiliza majibu ya Ndugai utaamini kuwa ni mtu mwenye sifa ya kuwa spika wa bunge? Mbona ni kama mjinga fulani asiyekuwa na elimu yoyote kichwani?
Kama ulikuwa unaamini bunge lina speaker basi umechelewa mkuu.
Jengo lile halina kiongozi /speaker tangu 2015 going forward-labda tutakuwa na speaker tena 2025 going forward.
Jamaa ni kilaza hata mtoto wa std 3 anamzidi busara na reasoning capacity.
 
Chadema ni imani. Chama kipo kwenye mioyo ya watu. Chadema imevuka hatua zote za kuuwawa na wafilisti wenye mamlaka. Viongozi watafungwa, wanachama watafungwa na kupotezwa. Lakini chama kitasimama imara. Chadema imevuka vikwazo vyote vigumu. Chadema ni mabadilko na uhuru wa kweli

Ndugai mmoja ni sawa na headless chicken
 
Back
Top Bottom