Bwana wangu anaendesha bodaboda, nifanyaje?

Bwana wangu anaendesha bodaboda, nifanyaje?

Ina maana sisi sio wanaume au? Vipi huyo mwenzako hakuwaona pia ambao sio bodaboda?
Me nadhani njoo soma huu Uzi
Ukitoka hapo kafanye KAZI
 
Hawajuagi nini wanataka hao
Wewe unaejua njoo soma huu Uzi
 
Kwani baba yake binti anayo hayo .....?
 
Jamani, si bachela huyo?🤣

Au Bachelor ina maana gani Money Minie?😀😀
 
Dear Money Penny

YAH: BWANA WANGU ANAENDESHA BODABODA
Mimi NI binti ambae sikuwahi kuwa kwenye mahusiano nikiwa chuoni.

Nilikuwa busy na masomo na ibada za casfeta.

Mapenzi yangu yalikuwa Kwa Yesu.

Baada ya kumaliza masomo sikupata KAZI, nikasota benchi Kwa Miaka 5, wenzangu nilisoma NAO walishaolewa na kuzaa na KAZI wanazo.

Nimevumilia lakini dadangu akaniambia tafuta bwana angalau uzae UMRI unaenda.

Siku Niko kwenye fellowship nikakutana na Kaka mmoja mlokole mwenzangu, nae NI graduate lakini Hana ajira
Amenunua bodaboda Kwa mkopo WA kampuni ya "WATU" pale Tegeta ndio anafanya nayo biashara apate kipato

Lakini ni mwaminifu, ananipenda mno na KAOKOKA,

Hatujawahi zini, Ila naogopa Sana kuolewa nae, maana kipato chake NI bodaboda Tu naona aibu mpaka aje kununua gari haya maisha yatakuwaje?

Kweli money penny bwana wangu anaendesha bodaboda lakini naona aibu kumtambulisha kwetu, ananipenda Sana nifanyaje??

Wako
Eliza."

Jamaa. Eliza anaomba msaada huku

View attachment 2724672



Yawezekana sijakuelewa vizuri, ila
Kwani wewe unataka kuolewa na mtu au unataka kuolewa na mali?

Jambo la muhimu katika maisha ni umpate mtu sahihi, mali zinatafutwa tu.

Unaweza kuolewa na mtu mwenye kila kitu, lakini si mtu sahihi, na ukajutia kuolewa naye.

Huyu mtu unayemsema mimi naona tayaru amejitahidi hadi kuwa na bodaboda japo ya mkopo, muda si mrefu atamiliki yakwake. Je wewe mpaka sasa unamiliki nini?
 
Cr wa familia huyu ndio kaongea ukweli
Wengine mnatupaka blueband ili tukaumwe pumu
Big NO kubadilika ni hulka ya mtu alafu pia lengo la muhusika litachangia kama ana lengo la kumtumia na kupita akipata hela lazima ataenda na hata kabla ya kupata hela anaweza badlika pia ila kama ana lengo la kuwa nae regardless atakuwa nae BTW haya mambo hayanaga formula bora tu nitafute hela nikimpata wakuwa nae asijesema nilivyopata hela nkabadilika akute nshabadilika 😀
 
Huyu ndio kaongea ukweli WA wanaume wote cocochanel
Wengine wooooote mnatupaka blueband tukaumwe pumu in the name of dharau

Maisha ya wanaoamua hayo wayaishi.. mwanamke lazima asimamie asitegemee pesa ya mwanaume ili aishi hata chupa ya maji ya kunywa njiani anunuliwe au kubaki na kiu..
 
Sikiliza moyo wako unataka nn ushauri wa watu utakupotezea mda

Km unataka maisha mazuri na kwa mwenendo wa mmeo unao uona maisha mazuri itakua ni ndoto fanya maamuzi sahihi

Afu pia usipende kujipa moyo kwamba ipo sku maisha yatakua mazuri maisha na dunia haiko ivyo kuna watu watakwambia mvumilie ipo sku mambo yatakua poa izo ni imagination hazina uwakika
 
Dear Money Penny

YAH: BWANA WANGU ANAENDESHA BODABODA
Mimi NI binti ambae sikuwahi kuwa kwenye mahusiano nikiwa chuoni.

Nilikuwa busy na masomo na ibada za casfeta.

Mapenzi yangu yalikuwa Kwa Yesu.

Baada ya kumaliza masomo sikupata KAZI, nikasota benchi Kwa Miaka 5, wenzangu nilisoma NAO walishaolewa na kuzaa na KAZI wanazo.

Nimevumilia lakini dadangu akaniambia tafuta bwana angalau uzae UMRI unaenda.

Siku Niko kwenye fellowship nikakutana na Kaka mmoja mlokole mwenzangu, nae NI graduate lakini Hana ajira
Amenunua bodaboda Kwa mkopo WA kampuni ya "WATU" pale Tegeta ndio anafanya nayo biashara apate kipato

Lakini ni mwaminifu, ananipenda mno na KAOKOKA,

Hatujawahi zini, Ila naogopa Sana kuolewa nae, maana kipato chake NI bodaboda Tu naona aibu mpaka aje kununua gari haya maisha yatakuwaje?

Kweli money penny bwana wangu anaendesha bodaboda lakini naona aibu kumtambulisha kwetu, ananipenda Sana nifanyaje??

Wako
Eliza."

Jamaa. Eliza anaomba msaada huku

View attachment 2724672
Hiyo boda boda ni ofisi yake.
Namaanisha ni chanzo chake cha mapato.
Unapohitaji gari unalihitaji kwa shughuli gani?
Alinunue kwa ajili ya kusafiri kwenda wapi?
Usidhani kuwa wote wasio na nagari kuwa hawana uwezo wa kuyanunua.
Kila.kinachotafutwa/kinachonunuliwa kinakuwa na sababu.
Tuna matajiri wana maghorofa na magari ya usafirishaji lakini hawajanunua nagari yao ya kutembelea.
Wahindi wengi kama si wote wamo kwenye nyumba za Msajili au Shirika la Nyumba.
Unaamini hawana uwezo wa kujenga.
Unaolewa na mume.
Huolewi na bodaboda wala gari.

TUMAINI LETU NI KWA BWANA.
 
Back
Top Bottom