Bwawa la kufua umeme la Nyerere ni dogo mno kulinganisha na uwezo wa maji katika bonde la mto Kilombero na Rufiji. Tulipaswa kutengeneza walau 6000MW!

Bwawa la kufua umeme la Nyerere ni dogo mno kulinganisha na uwezo wa maji katika bonde la mto Kilombero na Rufiji. Tulipaswa kutengeneza walau 6000MW!

Ni ukweli Taifa hata mtu binafsi kunatakiwa kuwa na benki ya takwimu/data . Labda zipo takwimu za ni cubic meter za Maji ngapi yanayopotelea baharini za mito ya Ruvuma,Rufiji,Pangani .Kazi ya kukusanya,kuchakata,kupanga na kutunza(benki)ni lazima zifanywe na watumishi waliosomea,je ukienda pale NBS utakuta watumishi watakwimu wa kutosha?na takwimu mbalimbali.?. Huwezi kuwa na dira,mwelekeo,mpango na bajeti na maamuzi sahihi kama huna takwimu za hakika na ukweli.
CCM huwa HAIPENDI kabisa kutumia takwimu.

Ndiyo maana walitunga Sheria kali kuzika Umma kutumia takwimu.
 
Kuanzia muonekano wa bwawa la Nyerere hadi kiasi cha umeme unaotengenezwa katika bwawa hilo ambao ni megawatt 2115, kila kitu kimekuwa underplanned and underestimated (finyu). Tumepoteza nafasi adimu ya kutengeneza umeme wa kutosha kwa Taifa letu kwa miaka mingi ijayo kwa kutumia ka-sehemu kadogo tu ka uwezo wa mfumo wa maji katika bonde la mto Kilombero na Rufiji pengine kwa gharama zilezile.

Nafikiri upembuzi uliofanyika kabla ya ujenzi wa bwawa hili ulikuwa finyu sana na pia wakubwa wamekula matrilioni kupitia udanganyifu huu! Sasa tunakazana kupunguza maji kwenye bwawa kwa nguvu kubwa na kulazimika hata kuzima mashine moja tuliyokwisha kuiwasha!

UKIONA BWAWA LIMEJAA MIAKA MIWILI KABLA YA UBASHIRI WA WATAALAM MANAKE NI KWAMBA UPEMBUZI YAKINIFU HAUKUWA SAHIHI NA KUMEFANYIKA MAKADIRIO MADOGO MNO YA UWEZO KAMILI WA BWAWA LA NYERERE.

Waziri Makamba mwaka jana aliwaambia watanzania kuwa itachukua miaka miwili (hadi 2026) kwa bwawa kujaa maji ili tuweze kutengeneza umeme. Nlishangaa sana na niliandika hapa kuwa msimu huu hautaisha litajaa mpaka pomoni na ndivyo ilivyo. Na hata mpango wa Tanesco ulikuwa kuanza na mashine moja ifikapo July mwaka huu, lakini bwawa limeshajaa na kumwagika na mashine tayari iliwashwa tangu mwezi March mwaka huu! Hivi vyote ni viashiria vya misculculation kubwa.

Sijui wataalamu wetu wapo wapi na tunaliwa mno jamani! Wataalamu kutoka nje walijua fika kuwa potential ya Stigler's Gorge ni 6000MW plus lakini wametupatia vizuri mno kwa sisi kuwalipa matrilioni kwa wao kutengeneza kituo cha kuzalisha 2000MW kwa fedha ambazo pengine zingetosha kutengeneza kituo cha kuzalisha 6000MW!

KWA MARA NYINGINE TENA TUMEZALISHA GUNIA MOJA LA MAHINDI KWENYE HEKA MOJA NA TUNAWASIFU VIONGOZI WETU SANA KWA HILO!
mabwawa yotee yamejaa!sasa tusisikie kuna mgao!maaan hii serikali haishindwi!!
 
Kwanza lazima ujue flow rate ya maji ya mto. Avarage flow rate. Usiangalie maji yanayotiririka kwa wingi kipindi cha Masika tena mwaka wa Elnino. Pili unatakiwa uone unaweza kujenga bwawa lenye kimo cha kiasi gani. Maeneo ya milima unaweza jenga bwawa lenye kimo kirefu, hivyo hata kama mto ni mdogo bado unaweza zalisha umeme mwingi.
 
Kuanzia muonekano wa bwawa la Nyerere hadi kiasi cha umeme unaotengenezwa katika bwawa hilo ambao ni megawatt 2115, kila kitu kimekuwa underplanned and underestimated (finyu). Tumepoteza nafasi adimu ya kutengeneza umeme wa kutosha kwa Taifa letu kwa miaka mingi ijayo kwa kutumia ka-sehemu kadogo tu ka uwezo wa mfumo wa maji katika bonde la mto Kilombero na Rufiji pengine kwa gharama zilezile.

Nafikiri upembuzi uliofanyika kabla ya ujenzi wa bwawa hili ulikuwa finyu sana na pia wakubwa wamekula matrilioni kupitia udanganyifu huu! Sasa tunakazana kupunguza maji kwenye bwawa kwa nguvu kubwa na kulazimika hata kuzima mashine moja tuliyokwisha kuiwasha!

UKIONA BWAWA LIMEJAA MIAKA MIWILI KABLA YA UBASHIRI WA WATAALAM MANAKE NI KWAMBA UPEMBUZI YAKINIFU HAUKUWA SAHIHI NA KUMEFANYIKA MAKADIRIO MADOGO MNO YA UWEZO KAMILI WA BWAWA LA NYERERE.

Waziri Makamba mwaka jana aliwaambia watanzania kuwa itachukua miaka miwili (hadi 2026) kwa bwawa kujaa maji ili tuweze kutengeneza umeme. Nlishangaa sana na niliandika hapa kuwa msimu huu hautaisha litajaa mpaka pomoni na ndivyo ilivyo. Na hata mpango wa Tanesco ulikuwa kuanza na mashine moja ifikapo July mwaka huu, lakini bwawa limeshajaa na kumwagika na mashine tayari iliwashwa tangu mwezi March mwaka huu! Hivi vyote ni viashiria vya misculculation kubwa.

Sijui wataalamu wetu wapo wapi na tunaliwa mno jamani! Wataalamu kutoka nje walijua fika kuwa potential ya Stigler's Gorge ni 6000MW plus lakini wametupatia vizuri mno kwa sisi kuwalipa matrilioni kwa wao kutengeneza kituo cha kuzalisha 2000MW kwa fedha ambazo pengine zingetosha kutengeneza kituo cha kuzalisha 6000MW!

KWA MARA NYINGINE TENA TUMEZALISHA GUNIA MOJA LA MAHINDI KWENYE HEKA MOJA NA TUNAWASIFU VIONGOZI WETU SANA KWA HILO!
Haiwezekani siku zijazo kukafanyika mradi mwingine huko, kama Inga Dam ya DRC kuna Dam 1, 2 na sasa 3 , ina uwezo wa kuzalisha MW 100,000 kutosheleza Africa nzima lakini Kwa sasa hii ya 3 itakuwa ina zalisha MW 30,000 Tu
 
KWA MARA NYINGINE TENA TUMEZALISHA GUNIA MOJA LA MAHINDI KWENYE HEKA MOJA NA TUNAWASIFU VIONGOZI WETU SANA KWA HILO!
Ipi bora mkuu.kuzalisha gunia moja kwa heka angalau ukala ugali au kuendelea kuhemea
huku heka yako moja ikizidi kuota mbigiri?
Mi nadhani Tanesco wakijiongeza,wanaweza kuongeza uwezo wa mashine kwa kufunga mashine za kisasa zaidi
hapo mbeleni.Kwa sasa tupongeze hatua iliyofikiwa.
 
Ipi bora mkuu.kuzalisha gunia moja kwa heka angalau ukala ugali au kuendelea kuhemea
huku heka yako moja ikizidi kuota mbigiri?
Mi nadhani Tanesco wakijiongeza,wanaweza kuongeza uwezo wa mashine kwa kufunga mashine za kisasa zaidi
hapo mbeleni.Kwa sasa tupongeze hatua iliyofikiwa.
Inauma sana mambo mengi nchi yanaamuliwa na wanasiasa wasiojua ukweli wa mambo na wageni kutoka nje wanapenda mno hali hii manake wanapiga hela hadi wanafurahi. Unaona Mwendokasi Dar, tuna miundombinu lakini usafiri Dar bado ni wa shida kubwa inabidi uwe na uwezo mkubwa wa kusukumana na watu ili uweze kusafiri, tatizo ni uwezo mdogo kifikra wa viongozi wetu. Na SGR nayo itakuwa hivyo hivyo kama hatutabinafsisha mapema.
 
Inauma sana mambo mengi nchi yanaamuliwa na wanasiasa wasiojua ukweli wa mambo na wageni kutoka nje wanapenda mno hali hii manake wanapiga hela hadi wanafurahi. Unaona Mwendokasi Dar, tuna miundombinu lakini usafiri Dar bado ni wa shida kubwa inabidi uwe na uwezo mkubwa wa kusukumana na watu ili uweze kusafiri, tatizo ni uwezo mdogo kifikra wa viongozi wetu. Na SGR nayo itakuwa hivyo hivyo kama hatutabinafsisha mapema.
Suala si kubinafsisha, suala ni ipo ya kufanya kitu, mfano hao wenye kufikiria kubinafsisha wanasema hivyo kwa madhumuni yapi. Nia binafsi au Kwa ajili ya umma.
 
Back
Top Bottom