By 2015 Kigoma kuwa kama Dubai, Mwanza kuwa kama California

By 2015 Kigoma kuwa kama Dubai, Mwanza kuwa kama California

Safari hii atakuwa na wakati mgumu sana kujinadi. Ndo maana anawadanganya ataifanya Tanzania kuwa kama Ulaya.
Ulaya kwanza wanyonge ndo huishi kwenye nyumba za serikali ila hapa Tanzania ni kinyume chake.
Ulaya mtu akiachishwa kazi anaendelea kulipwa kwa miezi kadhaa wakati akitafuta kazi nyingine.
Ulaya maji yapo kila sehemu na hayakatiki siku 365/365.
Umeme kila nyumba na haukatiki kwa siku 365/365.
Na mengine kibaooooo.
Ulaya yenyewe anayoiongelea analijua au ameiona kwenye TV?
 
Yaani anajua anaongea na watu kawashina upeo wa akili. Believe me kuna watu watampigia kura just because wanaamini ataifaya Tanzania kuwa kama Uholanzi.
Napata tabu sana. Kuona watanzania wenzangu bado akili zao zimeganda. Mpk leo hawajui kama walitaabika Jana sababu ya ahadi za anaetoa ahadi leo! [emoji15][emoji15]
 
mkuu Mbona China, Singapole, Malaysia zilibadilika ndani ya muda mfupi tu licha ya kufulia kwa muda mrefu.

Usimbeze wala usimfananishe na asiye yeye, Kikubwa ni kumuuliza " How" ya hicho alichokisema
Uchina ni taifa lenye miaka zaidi ya 6000 na katika vipindi hivyo limekuwa na milima na mabonde. Mpaka kufika karne ya 15 ndiyo lilikuwa taifa tajiri na lenye teknolojia kubwa zaidi duniani: Wakomunisti unaowaona walipochukua nchi mwaka 1949 ilikuwa ni taifa masikini lakini lenye miondombinu ya kuliwezesha kuendelea kwa haraka. Usisahau kwamba Uchina ilianza kukua kiuchumi miaka ya 1979 baada ya Deng-Xiaoping kufungua milango na kuruhusu mataifa ya nje kama Japani, Uingereza na Marekani wawekeze kwa wingi Uchina. Hivyo Today's China is just rebounding lilishwahi kuwa taifa tajiri zaidi duniani likufuatiwa na India.

Deng-Xiaoping aliwaonya sana Wachina kuachana na ujinga wa kuwatukana watu ambao wangeweza kuusaidia Uchumi wao. Aliachana na propaganda za kipumbavu za Kikomunisti za wakina Mao-Zedong na Zhou-Enlai na akauvaa uhalisia kwamba bila mataifa ya Magharibi Uchina isingeweza kurudi katika hali yake ya utajiri mkubwa ambao ilikuwa nao miaka 200 iliyopita. Ndipo akaja na sera maarufu kabisa ya "BIDE AND HIDE" na kuanza kuruhusu wawekezaji kutoka nje.

Raisi wetu akiwa na genge lake la wale TISS wenye akili za Vita Baridi (The Soldiers of the bygone regime) wameamua kuirudisha nchi yetu kwenye siasa za kijamaa zilizokuwa zimejaa propaganda mufilisi za Vita Baridi. Hawa watu wanaomshauri mkuu wa nchi ni watu waliopungukiwa hekima na maarifa, They are Morally Depraved and Spiritually Bankrupt. Hivi kuna taifa ambalo linaweza kuendelea kiuchumi hapa duniani bila kushirikiana na mabepari ??? Umoja wa Kisovieti ulijaribu kufanya hivi lakini pumzi iliwakatikia miaka ya 70 hadi kupelekea kuanguaka.

Unapotolea mfano wa nchi kama Singapore unazidi kutudhihirishia ule msemo kwamba "In Tanzania intellectuals are an endangered specie". Hivi kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kulinganisha Singapore ya Lee Kuan Yew na Tanzania ya Magufuli kweli ??? Basi ni lazima atakuwa mwendawazimu aliyepungukiwa na akili. Singapore imefika hapo ilipo kwa kucheza karata yake vizuri katika kushirikiana na mataifa hasimu kama Uchina na Marekani ambayo yanatumia sana mfereji wa Malacca. Hakufungamana na upande wowote ule katika siasa za kimataifa na kipaumbele chake kikubwa kilikuwa ni ELIMU (Maendeleo ya watu) siyo maendeleo ya vitu. Ndiyo maana leo hii Singapore inatoa wasomi nguli kama Dr. Kishore Mahbubani ambao Alma Mater zao ni Harvard University. Ninyi mna wakina nani hata kujivunia kimataifa ???

ACHA UPUMBAVU........
 
Labda ana mpango wa kuelekeza mapato yote ya nchi maeneo hayo, Maana yeye ndio mwenye uamuzi wa mwisho Katika nchi lakini halitawezekana, Kwa sababu tunakwenda kufanya mageuzi katika uchaguzi wa mwaka huu.
 
Mkuu Mbona China, Singapole, Malaysia zilibadilika ndani ya muda mfupi tu licha ya kufulia kwa muda mrefu.

Usimbeze wala usimfananishe na asiye yeye, Kikubwa ni kumuuliza " How" ya hicho alichokisema

Zilibadilikq kwa muda mkuu sio miaka mi5 tu

Hatua zinaonekana lakini itahitaji muda wa kati/muda mrefu kufikia kiwango kizuri(Sio kiwango cha Ujerumani lakini)
 
hahaha
You can Bring God to stop Corona mkuu.

Dah ila kwenye swala la Corona JPM kiboko. Yaani alivyodeal nalo anajua mwenyewe tu 😄😄😄😄 na kila mtu kabaki anashangaa matokeo chanya yalivyokua. Sio nchi za nje sio sisi wenyewe hata hatuelewi Corona imepeperukia wapi walahy. Katuchanganya changanya weee mpaka Corie nae akajikuta kachanganyikiwa haelewi atufanye nini ikabidi awe mpole tu asepe zake
 
Labda ana mpango wa kuelekeza mapato yote ya nchi maeneo hayo, Maana yeye ndio mwenye uamuzi wa mwisho Katika nchi lakini halitawezekana, Kwa sababu tunakwenda kufanya mageuzi katika uchaguzi wa mwaka huu.
Acheni mambo ya ajabu ninyi watu, GDP ya California ni dola za Kimarekani Trilioni 3.2 ambazo ni sawa na Trillioni 7000 za Kitanzania, hata ukiunganisha nchi zote za Afrika hazifikii GDP ya California. Hao Dubai wenyewe kufika hapo walipo waliachana na propaganda za kipumbavu za kijamaa na kidini na wakaamua kukubali teknolojia na pesa za Makafiri wa Kikristo kutoka Marekani na Ulaya ambao waliwekeza kwenye mafuta yao. Sasa ninyi wawekezaji mnachukia hizo pesa za kupeleka Chato na Kigoma mtazitoa wapi ???

NB: Our President is playing a child's game called Make-Believe.......
 
Kwaiyo we unadhani nani atakujengea nchi si bora hata magufuli kaanzisha hiyo sgr wengine wangetumia hizo kwa kusafiri ughaibuni jifunze kushukuru.
116350776_3206264756079584_1537352306806413178_o.jpg
 
.... Ndiyo maana leo hii Singapore inatoa wasomi nguli kama Dr. Kishore Mahbubani ambao Alma Mater zao ni Harvard University. Ninyi mna wakina nani hata kujivunia kimataifa ???
Tunaye Mzee Andrew Chenge. Msomi nguli wa sheria kutokea huko Harvard.
====
Kwenye jukwaa hili huwa nabadilika kidogo mkuu. Utanisamehe. Hata hivyo, Mkuu, punguza ukali wa maneno ili hoja yako iweze kueleweka bila ukakasi.

Tuendelee na mjadala.
 
Dah ila kwenye swala la Corona JPM kiboko. Yaani alivyodeal nalo anajua mwenyewe tu 😄😄😄😄 na kila mtu kabaki anashangaa matokeo chanya yalivyokua. Sio nchi za nje sio sisi wenyewe hata hatuelewi Corona imepeperukia wapi walahy. Katuchanganya changanya weee mpaka Corie nae akajikuta kachanganyikiwa haelewi atufanye nini ikabidi awe mpole tu asepe zake
Corona ipo. Alichosaidia kuondoa ni panic. Nami ninampongeza kwa hilo.
Ila kutuambia Tanzania kuwa kama Ulaya ni anatudanganya kabisa. Tumeshaona miaka yake mitano.
 
Uchina ni taifa lenye miaka zaidi ya 6000 na katika vipindi hivyo limekuwa na milima na mabonde. Mpaka kufika karne ya 15 ndiyo lilikuwa taifa tajiri na lenye teknolojia kubwa zaidi duniani: Wakomunisti unaowaona walipochukua nchi mwaka 1949 ilikuwa ni taifa masikini lakini lenye miondombinu ya kuliwezesha kuendelea kwa haraka. Usisahau kwamba Uchina ilianza kukua kiuchumi miaka ya 1979 baada ya Deng-Xiaoping kufungua milango na kuruhusu mataifa ya nje kama Japani, Uingereza na Marekani wawekeze kwa wingi Uchina. Hivyo Today's China is just rebounding lilishwahi kuwa taifa tajiri zaidi duniani likufuatiwa na India.

Deng-Xiaoping aliwaonya sana Wachina kuachana na ujinga wa kuwatukana watu ambao wangeweza kuusaidia Uchumi wao. Aliachana na propaganda za kipumbavu za Kikomunisti za wakina Mao-Zedong na Zhou-Enlai na akauvaa uhalisia kwamba bila mataifa ya Magharibi Uchina isingeweza kurudi katika hali yake ya utajiri mkubwa ambao ilikuwa nao miaka 200 iliyopita. Ndipo akaja na sera maarufu kabisa ya "BIDE AND HIDE" na kuanza kuruhusu wawekezaji kutoka nje.

Raisi wetu akiwa na genge lake la wale TISS wenye akili za Vita Baridi (The Soldiers of the bygone regime) wameamua kuirudisha nchi yetu kwenye siasa za kijamaa zilizokuwa zimejaa propaganda mufilisi za Vita Baridi. Hawa watu wanaomshauri mkuu wa nchi ni watu waliopungukiwa hekima na maarifa, They are Morally Depraved and Spiritually Bankrupt. Hivi kuna taifa ambalo linaweza kuendelea kiuchumi hapa duniani bila kushirikiana na mabepari ??? Umoja wa Kisovieti ulijaribu kufanya hivi lakini pumzi iliwakatikia mwaka 1970 hadi kupelekea kuanguaka.

Unapotolea mfano wa nchi kama Singapore unazidi kutudhihirishia ule msemo kwamba "In Tanzania intellectuals are an endangered specie". Hivi kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kulinganisha Singapore ya Lee Kuan Yew na Tanzania ya Magufuli kweli ??? Basi ni lazima atakuwa mwendawazimu aliyepungukiwa na akili. Singapore imefika hapo ilipo kwa kucheza karata yake vizuri katika kushirikiana na mataifa hasimu kama Uchina na Marekani ambayo yanatumia sana mfereji wa Malacca. Hakufungamana na upande wowote ule katika siasa za kimataifa na kipaumbele chake kikubwa kilikuwa ni ELIMU (Maendeleo ya watu) siyo maendeleo ya vitu. Ndiyo maana leo hii Singapore inatoa wasomi nguli kama Dr. Kishore Mahbubani ambao Alma Mater zao ni Harvard University. Ninyi mna wakina nani hata kujivunia kimataifa ???

ACHA UPUMBAVU........
Miundombinu iliyoshindwa kumsaidia Mao kwa Muda mfupi ilimsadia Deng Xioping (Quantum economic leap) bila kujali historia ya miaka 6000 iliyopita. Hata sisi inawezekana. Hija yangu imejikita katika china,Singapore (Lee kuan Yew) na Malaysia miaka ya 70 mpaka mwanzoni mwa 90.


Ukisema eti kwa sababu wao waliwahi kuwa matajili huko nyuma unaleta propaganda hata Misri imewahi kuwa superpower zaidi ya karne nyingi tu, ugiliki, Mali empire lakini umiaka wao mingi wa tajiri hauonyeshi hiki tunachokiona kwenye mifano niliyotoa.

La Kuacha upumbavu silizungumzii mkuu
 
Tunaye Mzee Andrew Chenge. Msomi nguli wa sheria kutokea huko Harvard.
====
Kwenye jukwaa hili huwa nabadilika kidogo mkuu. Utanisamehe. Hata hivyo, Mkuu, punguza ukali wa maneno ili hoja yako iweze kueleweka bila ukakasi.

Tuendelee na mjadala.
Tulikuwa naye Professor Justinian Rweyemamu Msomi nguli kutoka Harvard University na moja ya waandishi wa The Brandt Report: A Share of World's Resources ya mwaka 1980. Ripoti ambayo mpaka leo inatumiwa na wachumi wakubwa duniani katika kulinganisha maendeleo baina ya nchi Masikini na Tajiri. Huyo Chenge ni msomi wa kujivunia kwa lipi ???
 
Safari hii atakuwa na wakati mgumu sana kujinadi. Ndo maana anawadanganya ataifanya Tanzania kuwa kama Ulaya.
Ulaya kwanza wanyonge ndo huishi kwenye nyumba za serikali ila hapa Tanzania ni kinyume chake.
Ulaya mtu akiachishwa kazi anaendelea kulipwa kwa miezi kadhaa wakati akitafuta kazi nyingine.
Ulaya maji yapo kila sehemu na hayakatiki siku 365/365.
Umeme kila nyumba na haukatiki kwa siku 365/365.
Na mengine kibaooooo.
Hapo kwenye maji na umeme inawezekana kabisa
 
Back
Top Bottom