Shirikisho la Soka Afrika CAF limeufungia Uwanja wa Benjamin Mkapa

Shirikisho la Soka Afrika CAF limeufungia Uwanja wa Benjamin Mkapa

Ubaya Ubwela

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2024
Posts
1,353
Reaction score
3,060
Inasemekana Shirikisho la Soka Afrika CAF limeufungia uwanja wa Benjamin Mkapa kwa muda kutokana na ubovu wa eneo la kuchezea (pitch). Ripoti inaonyesha pitch mbovu na inazidi kuzorota. Wameitaka TFF kuchagua kiwanja kingine kwajili ya Robo fainali ya Shirikisho ya Simba hapo tarehe 9 April

Huu uwanja toka msimu unaanza hautumiki kwa mechi za ndani walidai kua wanaufanyia marekebisho, hii ncho yetu Siasa nyingi sana,

Gl0RgdOXsAA1HiY.jpeg


Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeufungia kwa muda Uwanja wa Benjamin Mkapра, Dar es Salaam kutokana na eneo la kuchezea (pitch) kuendelea kupungua ubora wake.

CAF imeelekeza eneo hilo liboreshwe haraka kufikia viwango vinavyotakiwa ili kuepuka Uwanja huo kufungiwa kwa muda mrefu.

Mechi ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF (CAF CC) kati ya Simba na Al Masry ya Misri imepangwa kuchezwa kwenye uwanja huo Aprili 9, 2025.

Ili kuondoa usumbufu, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetakiwa kutuma jina la uwanja mbadala utakaotumiwa na Simba kufikia Machi 14, 2025.

CAF itafanya ukaguzi wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Machi 20, 2025 ili kuona maboresho yaliyofanyika kabla ya kuamua kuuruhusu utumike au kuendelea kuufungia. Mbali ya mechi hizo za CAF CC, Uwanja wa Benjamin Mkapa umepangwa kutumika kwa ajili ya Fanali za CHAN zitakazofanyika Agosti 2025.

Pia soma: Msigwa Atoa Ufafanuzi Taarifa ya CAF Kuufungia Uwanja wa Mkapa, Kuhusu Derby Asema Waulizeni TFF
View attachment 3267578
 
Simba na yanga limeanza kuwa tatizo, watu hawafanyi kazi Sasa ni Simba na yanga.
We ndio unawalisha? Ebu acheni kulaumu watu kwa kufeli kwenu nyie CHADEMA. Jitafakarini wenyewe ndani ya chama na sio kulaumu watu.

Pia nakushauri kitu mkuu, usijipe umuhimu usionao kwa maisha ya watu. Wacha watu wafanye kile wapendacho.
 
We ndio unawalisha? Ebu acheni kulaumu watu kwa kufeli kwenu nyie CHADEMA. Jitafakarini wenyewe ndani ya chama na sio kulaumu watu.

Pia nakushauri kitu mkuu, usijipe umuhimu usionao kwa maisha ya watu. Wacha watu wafanye kile wapendacho.
Kila kitu chadema.
Mkiambiwa ukweli mnarukia chadema.
Waswahili hata kuhudumia wake zao wamefeli ,kisa Simba na yanga
 
Hivi malipo ya matumizi ya uwanja na mapato hulipwa tff au kwa control number za serikali ya hela huenda wapi? Mfano yanga au simba wakiuza soldout zao.
 
Inasemekana Shirikisho la Soka Afrika CAF limeufungia uwanja wa Benjamin Mkapa kwa muda kutokana na ubovu wa eneo la kuchezea (pitch). Ripoti inaonyesha pitch mbovu na inazidi kuzorota. Wameitaka TFF kuchagua kiwanja kingine kwajili ya Robo fainali ya Shirikisho ya Simba hapo tarehe 9 April

Huu uwanja toka msimu unaanza hautumiki kwa mechi za ndani walidai kua wanaufanyia marekebisho, hii ncho yetu Siasa nyingi sana,
pesa ya walipa kodi ishapgwa na maccm maana walidai watabadili mpk viti aaahaaha
 
Back
Top Bottom