CAG Prof. Assad astaafu, Charles Kichere ateuliwa kuwa CAG mpya

CAG Prof. Assad astaafu, Charles Kichere ateuliwa kuwa CAG mpya

In facts he dont know what happen....
 

Attachments

  • 77148205_3454338214578053_1431037782532292608_n.jpg
    77148205_3454338214578053_1431037782532292608_n.jpg
    21.6 KB · Views: 1
Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Prof.Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo. Lakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"
_
Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.

Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?

Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.

Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.

Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo kwa mujibu wa KATIBA alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano". I stand to be corrected.!View attachment 1252811
Embu cheki Sheria ya Ofisi ya CAG inasemaje....usijekuta imetoa masharti mengine
 
Rais ameteua CAG mnyonge, kwa ajili ya Serikali ya wanyonge. Hatari sana.
Hakuna CAG wa wanyonge. Kinachotakiwa ni uadilifu. Hata ukitoka kwenye familia maskini, kama wewe ni mwizi utakuwa mwizi tu. Kumbuka hata katika wanyonge kuna waliyo afadhali. Watanzania wengi wanatoka familia za kinyonge kiuchumi. Lakini Nyerere hakutoka familia ya kinyonge kiuchumi. Baba yake alikuwa chifu na kuchumi alikuwa afadhali. Lakini yeye alikuwa raisi wa wanyonge.

Ukiangalia TZ maraisi wengi walitoka kwenye familia zenye hali mbaya kuuchumi, lakini tunajuwa kilichotokea. Kwa hiyo mtu anaweza akatoka kwenye utajiri lakini akawa na moyo wa kuwatetea wanyonge. Anaweza akatokana na wanyonge kiuchumi na akawa mfakamiaji wa mali za walipa kodi, tena anakula bila kunawa.

Kwa hiyo mimi naona Assad alikuwa pia wa wanyonge lakini kulikuwa na mikwaruzano ya kibinadamu, ambayo kiukweli ilikuwa vigumu kuongezewa muda. Hata Assad nadhani aliyaona hayo na hakutaka kuwa chanzo cha migogoro ya mihimili mitatu. Bunge (spika) tayari alikuwa haelewani na CAG lakini hao wawili wanatakiwa kufanya kazi pamoja. Mimi ninamsifu CAG kuyaona hayo na kuamuwa kuondoka. Maana angeomba kuongezewa angemweka raisi pabaya, maana kulikuwa na uwezekano wa kutomuongezea muda maana tayari alikuwa na mkwaruzano na Bunge (spika).
 
Only in Tanzania. Miezi michache tu alimtumbua toka TRA hadi kuwa RAS.
Alisema dhahiri kashindwa kazi TRA. Sasa ataweza kuwa CAG na elimu yake yenye mashaka?
Ndio maana tunasema huyu MtuPori huwa haeleweki au tuseme anaropoka bila kupima maneno. Leo unamshusha cheo mtu kuwa utendaji wake hauridhishi, baada ya muda mfupi unampa madaraka makubwa zaidi hata ya Yale uliyokuwa umemvua.
Shida sana kuwa na mtu wa aina hiyo
 
Hakuna CAG wa wanyonge. Kinachotakiwa ni uadilifu. Hata ukitoka kwenye familia maskini, kama wewe ni mwizi utakuwa mwizi tu. Kumbuka hata katika wanyonge kuna waliyo afadhali. Watanzania wengi wanatoka familia za kinyonge kiuchumi. Lakini Nyerere hakutoka familia ya kinyonge kiuchumi. Baba yake alikuwa chifu na kuchumi alikuwa afadhali. Lakini yeye alikuwa raisi wa wanyonge.

Ukiangalia TZ maraisi wengi walitoka kwenye familia zenye hali mbaya kuuchumi, lakini tunajuwa kilichotokea. Kwa hiyo mtu anaweza akatoka kwenye utajiri lakini akawa na moyo wa kuwatetea wanyonge. Anaweza akatokana na wanyonge kiuchumi na akawa mfakamiaji wa mali za walipa kodi, tena anakula bila kunawa.

Kwa hiyo mimi naona Assad alikuwa pia wa wanyonge lakini kulikuwa na mikwaruzano ya kibinadamu, ambayo kiukweli ilikuwa vigumu kuongezewa muda. Hata Assad nadhani aliyaona hayo na hakutaka kuwa chanzo cha migogoro ya mihimili mitatu. Bunge (spika) tayari alikuwa haelewani na CAG lakini hao wawili wanatakiwa kufanya kazi pamoja. Mimi ninamsifu CAG kuyaona hayo na kuamuwa kuondoka. Maana angeomba kuongezewa angemweka raisi pabaya, maana kulikuwa na uwezekano wa kutomuongezea muda maana tayari alikuwa na mkwaruzano na Bunge (spika).
Mkuu mbona unachanganya mambo? CAG ameomba kuondoka lini? Huyu amestaafishwa bila hata ya yeye mwenyewe kupewa taarifa, fuatiliana maoni yake baada ya hizi taarifa za CAG mpya.
 
Huyu ametenguliwa ndiyo maana hapo kwenye andiko la mtoa mada amemnukuu mwenyewe Prof Assad kuwa hana taarifa yoyote na huo utenguzi wake kwakuwa yupo nje kikazi.sasa cha kujiuliza mtu kama Pro Assad inakuwaje asielewe kwamba muda wake kukaa ofisini umeisha halafu yeye asafiri tena safari ya kikazi.yeye anachoamini muda wa kustaafu yaani miaka bado haijafika.
 
Kwa kuwa CAG Ni independent office yake ifanye tu hivo kuepuka kuwa unable kujua Nani kakwapua na mwisho kuwa office ya kusema tu hazionekani!
Hicho kitengo cha ujasusi watu wake watatoka sayari gani? Na watakuwa wanafanya kazi chini ya nani? Bajeti yao je? Na recruitment atafanya nani?
 
wasalaam, kuna habari zinasambaa kwa kasi sehemu mbalimbali nchini kwamba CAG mpya mh kichere ni dhaifu kutoka na historia yake ya utendaji huko nyuma. Habari zinasema kwamba bwana kichere ni mtu wa ndio mzee na kuanzia sasa ukaguzi wa hesabu za serekali utafanywa na serikali yenyewe kwa maelekezo kutoka pale nyumba nyeupe.

Tusubiri muda ni rafiki huenda ni majungu tu labda watu wanazusha. Maendeleo yana vyama usipochagua ccm hakuna kuletewa maendeleo.
Ova.
 
Back
Top Bottom