Chadema kinahitaji kujindaa kwelikweli na kama kweli chama hiki kina dhamira ya kweli ya kushika dola, basi kina wajibu wa kuachana na siasa za matukio na kujikita katika kujenga hoja zenye tija ili kujijengea imani kwa wapiga kura.
1. Unaishi Tanzania gani wewe? Unaongelea CHADEMA kujenga imani kwa wapiga kura/wananchi? Kuna chama kingine ambacho ni tumaini la kuaminiwa na wananchi nje ya CHADEMA?
2. Katika siasa, matukio ya makosa ya chama kinachoongoza serikali/dola ndiyo mtaji mkuu na muhimu wa kisiasa wa chama/vyama pinzani kwa wananchi au wapiga kura. Kama ulikuwa hujui, katika siasa hakuna msamiati wa "acha siasa za matukio" kwa sababu makosa ya chama tawala ya kisheria, kisera na kimipango ndiyo hutengeneza matukio ambayo hutumiwa na vyama vinavyotaka kuwa - replace kwa kujijenga kwa wananchi kwa kuwaonesha mbadala...
Hiki ndicho wasichokitaka CCM kukiona na ndiyo chanzo cha migogoro tunayoishuhudia sasa kati ya wapinzani hususani CHADEMA na CCM kwa mgongo wa polisi, TISS na DPP...
Suala la mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kuwa na kesi ya ugaidi inayoendelea mahakamani lisiwe sababu ya Chadema kama chama ambacho kina miaka 29 sasa kwenye ulingo wa siasa za vyama vingi kukosa mwelelekeo na kuonekana hakina mikakati.
Wamekuambia hawana mikakati au wamekosa uelekeo kwa ya kesi ya mwenyekiti wao mahakamani? Hebu soma maelezo yangu ya ziada hapo juu....
Huu ndo ulikuwa wakati wa makamu mwenyekiti Tundu Lissu kuwa mastari wa mbele kukiongoza chama hicho na pengine kupewa nafasi ya uenyekiti wa chama hicho ili akiandane uzuri chama kwa uchaguzi ujao.
Mnadhani mnaweza kuvuruga chama hiki kwa kumbambikia kesi M/kiti ili mje na hoja hii? Hata hivyo, ktk wakati huu m/kiti Freeman Mbowe akiwa mahabusu, chama bado kipo kwenye mikono salama ya Makamu M/kiti (Tanganyika) Tundu Lissu na yule wa Zanzibar. Kuna kilichoharibika hapo?
Ni maoni yangu binafsi kuwa Tundu Lissu kwa sasa amejifunza kuwa mwanasiasa badala ya mwanaharakati na kwa uwezo wake, ujasiri wake na kauli zake ambazo atakuwa sasa amefahamu namna ya kuzipanga uzuri, anafaa kabisa kuwa mwenyekiti wa Chadema.
Come on, this shit can't work..!!
Unajaribu kuchochea mgogoro, right?
In case you didn't know. Ni kwamba, chama kina M/kiti Freeman Mbowe na Tundu Lissu ni Vice Chairperson...!
Ni wakti sasa kwa Tundu Lissu kurudi nyumbani Tanzania na kuanza kazi ambayo nadhani bado hajaimaliza.
Kwa sharti moja tu. Wasiojulikana wajulikane. Thank God kwamba, mmoja Ole Lengai Sabaya amejulikana + mwendazake John P. Magufuli
Vyombo vyote vya ulinzi na usalama havina budi sasa kujifunza kutoka Zambia na Malawio kuwa kuna wakati wananchi wanaamua kuwa chama kilichopo madarakani kimefikia tamati na wanataka chaama mbadala.
Hapa umetumia akili vizuri kuandika. That's correct. Vyomba vya ulinzi na usalama i.e polisi, TISS, DPP na JWTZ waache kujiguza chama cha siasa kuisaidia CCM...!!
Serikali ina wajibu wa kuhakikisha maisha ya Tundu Lissu yanalindwa na wale wote wasio na nia njema kwake na anasimama kwa uhuru katika jukwaa la kisiasa.
That's correct too. Umenena vyema...!
Tundu Lissu akiwa mwenyekiti wa Chadema taifa atakipanga chama atakavyoona yeye inafaa, kuteua timu yake ambayo ina watu makini na kutengeneza sera na ilani mpya ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa 2025.
Not now. Chama kina M/kiti anaitwa Freeman Aikael Mbowe. Hizi assumptions zako kaa nazo mpaka next party election...
Kama raisi wa Malawi Chikwera na mgombea wa sasa wa uraisi Zambia bwana Hakainde Hichilema waliweza, sioni tatizo Chadema washindwe uchaguzi wa 2025.
Ndiyo maana tunapigania Katiba mpya ya wananchi ambayo itatuhakikishia Tume Huru ya Uchaguzi. Tukijenga mazingira huru ya namna hii, ndipo utakapoona kwa ukamilifu wake jinsi wananchi/wapiga kura walivyo na imani na CHADEMA. !!!
Mgombea wa chama cha upinzani akipata kura za kutosha na watu wakijitokeza kwa wingi kama walivyofanya Zambia kiasi cha tume ya Uchaguzi ya Zambia kutia akili kuwa Hichilema anashinda kwa kura za kutosha.
Mara zote hapa Tanzania kuanzia 2005, 2010, 2015 na mwaka jana 2020 wananchi walijitokeza kwa wingi sana tu na kuipa ushindi CHADEMA lakini CCM wakapora kwa nguvu. Moja ya adhabu ya dhambi hii kubwa kabisa ya CCM ni kifo cha aliyeongoza uporaji huu mwendazake John P. Magufuli...!!