CCM imeruka maji ikakanyaga tope. Sophia na Shaka ni "light materials" majukwaani!

CCM imeruka maji ikakanyaga tope. Sophia na Shaka ni "light materials" majukwaani!

Acha kujichanganya na kujidanganya mwenyewe,ach kuota ndoto ukiwa umekaa kwenye daladala.

Napenda kukuambia kuwa CCM bado Ni chama imara Sana,madhubuti,shupavu , chenye mvuto wa kipekee na chama kiongozi hapa nchini na mfano wa kuigwa Barani Afrika,CCM ndio chama pekee chenye Sera na ajenda za kugusa wananchi ,Ni chama chenye dira na muelekeo unaoeleweka,Ni chama chenye misingi imara, Ni chama chenye mizizi mpaka mashinani iliyo imara na imara,

Hakuna chama chenye uwezo wa kuitikisa CCM kisera ,kiajenda,kiitikadi na kihoja,CCM imesheni na kuwa na vitu vyote hivyo,uchapa kazi wa CCm na serikali Yake umeifanya CCM kukaa katika mioyo ya watanzania,kuungwa mkono na kutetewa na watanzania, CCM ndio Tumaini la watanzania katika kuwaletea maendeleo,Ndio chama kilicho na uchungu na maisha yao, ndio chama kinachojuwa Mahitaji ya watanzania,ndio chama kinachoongoza mapambano ya kumtetea mnyonge bila kuchoka,Ni sauti kwa wasio na sauti na nguvu kwa wasio na nguvu kwa wasio na nguvu, ni mdomo wa watanzania na ulimi wa wenye shida.

Mama Sophia Mjema Ni mama Wa shoka na imara,Ni shupavu na madhubuti,Ni Hodari na Jasiri Sana,Atawasha Moto majukwaani mpaka upinzani utakimbia kimvuli chake,Atayatetemesha majukwaa mpaka upinzani utakimbia kishindo chake,atateka anga la Siasa za Tanzania mpaka upinzani utapotelea gizani hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa upinzani wa nchi hii Ni wa usaka tonge na mkusanyiko wa watu wasio na muelekeo Wala dira inayoeleweka
Luka umesahau kuweka namba za simu
 
Inawezekana laana za "wabaya"sasa zimeanza kufanya kazi yake ndani ya CCM hii.kama mmefikia kujiita Chawa wa Taifa!

Halafu mnaamini Kwamba Sophia atakuwa bora majukwaani,katika kipindi ambacho Siasa za majukwaani zinaenda kuanza rasmi.

Na kwamba atamzidi Shaka aliyekuwepo? Ambaye hata yeye alikuwa ni mwepesi kama cream ya uso! Muda utaongea soon!

Tatizo ni kwamba CCM mnaishi kwa kukariri! Juzi sio jana, na jana sio leo. Na pia leo haitakuwa hivi mpaka 2025 au 2030!

Watu sasa hawaangalii majina ya wanasiasa. Bali watu wanamsikiliza mtoa hoja na sera makini, na inayogusa kile wanachokiishi huku site!

Maana tumejua rasmi kwamba,wengi wa wanasiasa ndani ya CCM. Mpo hapo kwa maslahi yenu na makundi yenu ya kimfumo.

Msidhani ni wakati ule wananchi walipokuwa wakishabikia vyama kama timu za mpira!

Kwamba yeyote atakayewekwa,ilimradi amesajiliwa na timu,basi atashangiliwa pia na wananchi, La hasha!

Mambo yamebadilika sana,tumejifunza mengi sana! Mnapobadilishana vyeo kama magari, mnapobadilishana bila kutafakari ni nani anaweza nini?

Na anaweza kwa kiasi gani kulisimamia jukwaa na kuongea na wananchi kwa kujua nini hasa wanakihitaji!

Mnapobadili viongozi, kwa kuangalia wanaowafaa nyinyi, kwa maslahi yenu.
Badala ya kuchagua kwa kuangalia wanaowafaa wananchi, kwa maslahi yao na maendeleo ya taifa letu!

Inaweza kuwa ndio anguko lenu linaanza kujitokeza.

Sio kwa hali hii,ambapo tunaona ufisadi ukirudi na kuitafuna CCM, kama ilivyokuwa kabla ya 2015.

Kama hamuamini,tumieni mfano wa kilichotokea juzi huko Mwanza,kati ya Mkurugenzi wa jiji, na kamati ya ulinzi na usalama mkoa.

Tangu siasa za 2015 huko upinzani na pia CCM,hadi 2020! Na kuja mpaka tulipo sasa!

Wananchi wamejifunza mengi sana kutoka matendo ya nyinyi viongozi wa kisiasa nchi hii.

Wameujua ukweli na uhalisia wenu kimatendo na nafsi zenu!

Tumewajua wauaji, tumewajua wezi,tumewajua wanasiasa CCM wanafiki na pia tumewajua wanasiasa wazuri,ambao wanabaniwa na vyama vyao.

Kwa sababu ya ukweli na uzalendo wao.

Kwa hiyo msitarajie wananchi kukurupukia mikutano,ambayo itakosa sera madhubuti ili kugusa utatuzi wa kero zao za kimaisha ya kila siku.

"Wananchi wanalia na mfumuko wa bei,pamoja na Tozo lukuki zinazowafilisi kila uchao huko mitaani."

"Wananchi wanalia na huduma mbovu za kijamii, kuanzia hospitalini mpaka Polisi na ofisi zote nyeti za Umma"

Wakati nyinyi mnagawiana magari ya kifahari ya milioni 500 kwa milioni 600. maofisini,mikoani hadi wilayani.

Wananchi nao wanataabika kuanzia mikoani hadi vijijini. Kwa mfumuko wa bei,ambao hauhusiani hata na vita ya Ukraine na Russia.

Nyama ya Ng'ombe,Mchele,Unga wa Mahindi ni mifano tosha wa hilo.

Tunawasubiri majukwaani na tutawapimia huko. Na pia majibu mtayapata huko huko.

Ilimradi msikae kwa kutegemea maguvu ya Dola mlioishikilia kwa sasa!
Kuweni fair na muache wananchi wawe huru kuamua mbichi na mbivu.
Jumapili njema!

Alamsikhi.
10101.
View attachment 2481544
Ni kweli kabisa hii ni laana kamili ...samia mwanamke na huyo sofia mwanamke tena kwa kimbembe cha 2025 labda ccm wamweke majaliwa kuwa mgombea urais au polepole vinginevyo ....watajuta kwa kunya akili na kubakisha kinyesi kichwani
 
Ni hivi: CCM hata siku moja haizingatii sifa kwenye kuteua. Ingekuwa inazingatia sifa, huyo Shaka asingekuwa hata mwenyekiti wa kijiji. Hii ni kwa sababu wanajua dola ni yao. Wanajua machinery ya kuandaa, kusimamia na kutoa matokeo ya uchaguzi ni wao wanai-control.
Shaka huyu alipigwa chini na JPM kwa kadhfa ya rushwa kule Morogoro halkustahili kupewa nafasi tena ya uongozi ila uzanzibari wake ndiyo ulimbeba
 
Ni kweli kabisa hii ni laana kamili ...samia mwanamke na huyo sofia mwanamke tena kwa kimbembe cha 2025 labda ccm wamweke majaliwa kuwa mgombea urais au polepole vinginevyo ....watajuta kwa kunya akili na kubakisha kinyesi kichwani
CCM IS A TEAMWORK!
Stop lie yourself.
 
Huna hata aibu unaposena tozo,kwa hiyo unataka huduma bure bila kuchangia, unafikiri nchi zilizoendelea kiuchumi zilifika hapo kwa kushushiwa maendeleo kutoka angani,unafikiri wananchi wake walibweteka Kama unavyotaka wewe? Watanzania wanamuunga mkono Rais wetu Ndio maana wanataka kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe kwa kuchangia kulingana na vipato vyao
TOZO za kununulia ma v8 wakuu wa MIKOA na warugenzi wewe ndio umekosa aibu pesa zetu CCM inafanyia anasa (WANAJITAJILISHA) WEWE enderea kusaga matako hapo lumumba Huku ukiamini CCM italeta maendereo miaka 61 ya UHURU
 
Back
Top Bottom