CCM inabidi itumie nguvu kubwa kuhakikisha matokeo makubwa uwekezaji wa bandari

CCM inabidi itumie nguvu kubwa kuhakikisha matokeo makubwa uwekezaji wa bandari

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Mwanafilosofia na mwanahistoria Niccolo Machiavelli kutoka nchini Italia aliwahi kusema " the end will justify the means" ambapo tukipeleka Kwa tafsiri isiyo rasmi alimaanisha " hata jambo baya likiwa na matokeo mazuri basi jambo hilo "morally" linakuwa ni zuri".

Kinachoangaliwa na kutazamiwa kama ubora wa jambo lolote ni matokeo ya jambo husika. Matokeo ndio yatatoa ukweli wa uzuri au ubaya wa jambo husika.

Kulingana na nukuu ya kauli ya Machiavelli, CCM itumie kauli katika utekelezaji wa mkakati wa uwekezaji katika bandari hususani kipindi hiki ambacho kuna mitazamo tofauti kuhusu uwekezaji huo.

Kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kwenda na uwekezaji wa bandari kulingana na tathmini kuonesha uwekezaji kwenye bandari una faida na Kwa kuwa faida hizo hata zikisemwa Sasa Kwa baadhi inakuwa ni ngumu kuziona mpaka waone matokeo basi ni vema CCM ikajikita kwenye kufanikisha matokeo ya uwekezaji huo.

Matokeo yanatakiwa kufanikishwa ni zile faida zote tunazoambiwa Sasa zitatokana na uwekezaji huo. Ni matokeo ndio yataonesha nia na dhamira njema iliyonayo CCM kwenye uwekezaji wa bandari.

Hili ni ombi Kwa CCM hakikisheni matokeo ya uwekezaji huo yanafikiwa ili wanaopinga leo wasipate sababu ya kuongea baadaye kama malengo yasipofikiwa.

Suala hili la uwekezaji wa bandari halitakwisha mpaka pale matokeo yatakapoonekana. Matokeo chanya ni "asset" Kwa CCM ila matokeo mabovu ni "liability" na kufanya watu waje kuamini Kila anayepinga uwekezaji yupo sahihi.
 
Shida zenu ni tamaa za vyeo tu. Ubinafsi tu umewajaa.
 
Swala la bandari siku hizi haliongelewi kwa kuunga unga maneno ndo maana waropokaji wamekata Moto. Uongeaji wa sasa ni kwa kutumia vifungu vya sheria za nchi, hukumu zilizopita, katiba ya Tanzania na UAE, na kama huvijui unakaa kimya waliosaini waendelee kunyolewa.
 
Suala hili la uwekezaji wa bandari halitakwisha mpaka pale matokeo yatakapoonekana. Matokeo chanya ni "asset" Kwa CCM ila matokeo mabovu ni "liability" na kufanya watu waje kuamini Kila anayepinga uwekezaji yupo sahihi.
Naunga mkono hoja
P
 
Swala la bandari siku hizi haliongelewi kwa kuunga unga maneno ndo maana waropokaji wamekata Moto. Uongeaji wa sasa ni kwa kutumia vifungu vya sheria za nchi, hukumu zilizopita, katiba ya Tanzania na UAE, na kama huvijui unakaa kimya waliosaini waendelee kunyolewa.
Sio ajabu pumzi yenu kwenye siasa ni ndogo
 
Mwanafilosofia na mwanahistoria Niccolo Machiavelli kutoka nchini Italia aliwahi kusema " the end will justify the means" ambapo tukipeleka Kwa tafsiri isiyo rasmi alimaanisha " hata jambo baya likiwa na matokeo mazuri basi jambo hilo "morally" linakuwa ni zuri".

Kinachoangaliwa na kutazamiwa kama ubora wa jambo lolote ni matokeo ya jambo husika. Matokeo ndio yatatoa ukweli wa uzuri au ubaya wa jambo husika.

Kulingana na nukuu ya kauli ya Machiavelli, CCM itumie kauli katika utekelezaji wa mkakati wa uwekezaji katika bandari hususani kipindi hiki ambacho kuna mitazamo tofauti kuhusu uwekezaji huo.

Kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kwenda na uwekezaji wa bandari kulingana na tathmini kuonesha uwekezaji kwenye bandari una faida na Kwa kuwa faida hizo hata zikisemwa Sasa Kwa baadhi inakuwa ni ngumu kuziona mpaka waone matokeo basi ni vema CCM ikajikita kwenye kufanikisha matokeo ya uwekezaji huo.

Matokeo yanatakiwa kufanikishwa ni zile faida zote tunazoambiwa Sasa zitatokana na uwekezaji huo. Ni matokeo ndio yataonesha nia na dhamira njema iliyonayo CCM kwenye uwekezaji wa bandari.

Hili ni ombi Kwa CCM hakikisheni matokeo ya uwekezaji huo yanafikiwa ili wanaopinga leo wasipate sababu ya kuongea baadaye kama malengo yasipofikiwa.

Suala hili la uwekezaji wa bandari halitakwisha mpaka pale matokeo yatakapoonekana. Matokeo chanya ni "asset" Kwa CCM ila matokeo mabovu ni "liability" na kufanya watu waje kuamini Kila anayepinga uwekezaji yupo sahihi.
Ilani ya Uchaguzi 2020 haikuelekeza Ugawaji bandari zote bila UKOMO,

Pia hakuna utafiti wowote ulifanyika zaidi ya kuamua tu ghafula walipokuwa matembezi Dubei.

SHERIA za tenda zimekiukwa.

Endeleeni kupuuzwa wazee, maana safari ya kuzimu, Huwa imepamba na AHADI na hadaa za Kila namna.

Tusubiri.
 
Mwanafilosofia na mwanahistoria Niccolo Machiavelli kutoka nchini Italia aliwahi kusema " the end will justify the means" ambapo tukipeleka Kwa tafsiri isiyo rasmi alimaanisha " hata jambo baya likiwa na matokeo mazuri basi jambo hilo "morally" linakuwa ni zuri".

Kinachoangaliwa na kutazamiwa kama ubora wa jambo lolote ni matokeo ya jambo husika. Matokeo ndio yatatoa ukweli wa uzuri au ubaya wa jambo husika.

Kulingana na nukuu ya kauli ya Machiavelli, CCM itumie kauli katika utekelezaji wa mkakati wa uwekezaji katika bandari hususani kipindi hiki ambacho kuna mitazamo tofauti kuhusu uwekezaji huo.

Kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kwenda na uwekezaji wa bandari kulingana na tathmini kuonesha uwekezaji kwenye bandari una faida na Kwa kuwa faida hizo hata zikisemwa Sasa Kwa baadhi inakuwa ni ngumu kuziona mpaka waone matokeo basi ni vema CCM ikajikita kwenye kufanikisha matokeo ya uwekezaji huo.

Matokeo yanatakiwa kufanikishwa ni zile faida zote tunazoambiwa Sasa zitatokana na uwekezaji huo. Ni matokeo ndio yataonesha nia na dhamira njema iliyonayo CCM kwenye uwekezaji wa bandari.

Hili ni ombi Kwa CCM hakikisheni matokeo ya uwekezaji huo yanafikiwa ili wanaopinga leo wasipate sababu ya kuongea baadaye kama malengo yasipofikiwa.

Suala hili la uwekezaji wa bandari halitakwisha mpaka pale matokeo yatakapoonekana. Matokeo chanya ni "asset" Kwa CCM ila matokeo mabovu ni "liability" na kufanya watu waje kuamini Kila anayepinga uwekezaji yupo sahihi.
Hivi mtu akiuza gari au nyumba huwa ni matokeo gani anasubiri tena ?
 
Hivi mtu akiuza gari au nyumba huwa ni matokeo gani anasubiri tena ?
Unakuwaje na umiliki na kitu kisichohamishika? Jaribuni kuja na tungo nyingine hii imekosa wasikilizaji.

Unapouza gari au nyumba lengo ni kupata pesa za either kukuza mtaji au kupata mtaji wa biashara au uwekezaji.

Tuje kwenye mfano wako bila shaka unahusanisha na sakata la bandari, tuseme ni kweli bandari imeuzwa, binafsi naona uuzaji huo una faida Kwa sababu unakwenda kuongeza mapato.

Hapa ndio napata mashaka na wote wanaopinga uwekezaji wa bandari hususani kwenye uelewa wao wa mambo.

Kwanza tukubaliane, mtu anapouza Mali yake anakosa uhalali wowote juu ya Mali hiyo lakini kwenye suala la bandari Bado Tanzania itakuwa na uhalali wa umiliki wa bandari hivyo hapa dhana ya kuuzwa bandari inakosa mantiki.

Pili, sheria ya ardhi inasema ardhi ni Mali ya Serikali chini ya usimamizi wa Rais hivyo Kwa vyovyote vile uendelezaji wa bandari utasimamiwa na sheria ya ardhi. Mtu anapewa ardhi aiendeleze tu na sio kuwa na umiliki. Sasa kama DP World watakosa umiliki wa ardhi Kwa hapa tuseme ni bandari watakuwaje wameuziwa.

Tatu, umiliki wa Mali husika ni pale ambapo Mali hiyo itakuwa inahamishika. Bandari sio Mali inayohamishika.

Kwa hiyo hoja ya kusema bandari imeuzwa inakosa mantiki Kwa hoja hizo
 
Back
Top Bottom