CCM msituletee tena viongozi kama Awamu ya Tano

CCM msituletee tena viongozi kama Awamu ya Tano

Me binafsi nilishaacha kujibizana na watu jamii ya mtoa mada kwa sababu niligundua mambo haya;

Mosi kuna kundi kutoka CCM linalofanya kila njia kumpondea kumtukana nk JPM humu mitandaoni,na hii inasababishwa na kwamba mwamba kweli kafa lakini bado kuna kundi kubwa linampigania,kipindi Magu yupo waliamini hili kundi linamtetea ili kujipendekeza na kujikomba tu kwa kiongozi wa juu kama ilivyo ada katika nchi hii,sasa roho zinawauma sana Leo hii kuona Mwamba bado anatetewa na kukubalika sana pamoja na kwamba ametangulia mbele za haki,na kibaya zaidi viongozi/watu wao waliobaki Leo hii hawakubaliki kabisaa hata nusu ya Magu tu



Kundi la pili ni hawa wafuasi wa CDM ,hawa bhana walishajiaminisha kwamba wao ndio wao chama chao ni Taasisi kubwa na nguvu ya umma kweli ipo nyuma yao,sasa alichowafanya yule mwamba hakitawatoka akilini mwao mpaka kifo,walipigwa mapigo matakatifu wakapoteana vibaya mpaka leo wengine Belgium wengine Canada na wengine wapo tu kitaaa hawaelewi kitu,yaani chama ndio kimeshapotea na hakiwezi kurudi kama kilivyokuwa kabla ya uchaguzi wa 2015,wao wenyewe wanaufahamu ukweli huu ingawa hawataki kuukubali,ndio maana roho zinawauma sana,hawa jamaa ni kuwaonea huruma tu na si vinginevyo maana machungu waliyonayo hayamithiliki kabisaa, watabaki kumtukana Magu mpaka kiama



Haya Makundi yote mawili huwa hawana hoja zozote za msingi juu ya Magu zaidi ya pumba na matusi tu,story zao kila siku ni zile zile,sasa basi dawa ni kuwadharau na kuwapotezea tu waacheni wajifariji humu mitandaoni ingawa ukweli wanaujua vizuri mioyoni mwao!!
Na wale wenye vyeti fyeki ndo usiseme maana waliamini wangeishi kwa ujanja unja moaka wastaafu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wee kichwani hauna kitu unaulelwew mdogo sana .Auditing quarrel Huwezi kuwa termed kama wizi mpaka hizo hoja zitakapokosa majibu ya hoja husika hebu tusubiri hii awamu ya huyu mama

Sent using Jamii Forums mobile app
Sweet Mataga tears.
200 (9).gif
 
Aina ya uongozi kama ule wa Awamu ya Tano ulikuwa balaa kwa mustakabali wa umoja wa nchi yetu.

Sina haja ya kurudia madhambi mabaya ya Awamu ya Tano maana kila mtu yalimgusa.

Kiini cha hayo matatizo ni kinyang'anyiro cha urais wa 2015 ambapo walijitokeza wagombea zaidi ya 40.

Naona hili linajirudia mbio za Uspika.

CCM waliboronga vibaya mwaka 2015, na matokeo tuliyaona.

Sasa hivi CCM iwe makini na waache umavikundi, mitandao, na "gangs" za kimasilahi binafsi.
JPM hayuko lakini bado unamuota, umeshindwa kujiongoza mpaka ulalamikie walio umauti ?
 
CCM waliboronga vibaya mwaka 2015, na matokeo tuliyaona.

Sasa hivi CCM iwe makini na waache umavikundi, mitandao, na "gangs" za kimasilahi binafsi.
kuboronga ni jadi yao. Mara chache sana wanapatia!
Ndivyo walivyo.
Walishajipindua kutoka jembe na nyundo hadi kuwa chama cha magang masters!
 
Usije sahau kuwa Magufuli tulimchagua sisi wenyewe kwa roho njema na safi.
Tulichokipata hakifai kuhadithia, hatukujua tumepata mtu mwenye visasi, roho mbaya, mkatili, mtu anayejiona yeye ndio kilakitu nchini.
Na bahati mbaya Katiba ilimpa hayo madaraka na kayatumia vibaya.
CCM wasirudie makosa.
Ccm wasirudie makosa kwa vipi ?? Una maana wakubali kuandikwa katiba mpya ambayo haitampa madaraka makubwa kupita kiasi mkuu wa nchi ??! Au wasirudie makosa kwa katiba hii hii iliyopo ??!!
 
Aina ya uongozi kama ule wa Awamu ya Tano ulikuwa balaa kwa mustakabali wa umoja wa nchi yetu.

Sina haja ya kurudia madhambi mabaya ya Awamu ya Tano maana kila mtu yalimgusa.

Kiini cha hayo matatizo ni kinyang'anyiro cha urais wa 2015 ambapo walijitokeza wagombea zaidi ya 40.

Naona hili linajirudia mbio za Uspika.

CCM waliboronga vibaya mwaka 2015, na matokeo tuliyaona.

Sasa hivi CCM iwe makini na waache umavikundi, mitandao, na "gangs" za kimasilahi binafsi.

Kuna Waziri nilimsikia akisema vjana niwavivu na mnachagua kazi!!!! Kimsingi magufuli Alitakiwa a endelee kuwepo ata wewe usingepata huu muda wakumjadili
 
Ajabu sana mkuu hebu soma comments humu ujionee mwenyewe watu wanao jiita ma GT wanacho kijadili.

Eti hadi Leo hii mtu anadai kuwa Magufuli kafa kwasababu hakuwa na utumishi ulio tukuka.

Anasema angekuwa na utumishi ulio tukuka angekuwa hai mpaka Leo.

Inamaana ma GT watu wenye akili kubwa humu wanaamini kuwa mtu akiwa kiongozi tu basi huwa hafi hadi amalize uongozi na akifa tu anakufa kwasababu yeye ni mtenda dhambi. Kwahiyo viongozi wote walio kufia madarakani duniani kote walikuwa watu wabaya sana ndio maana wakafa!!

Hongera sana ma GT wote Kwa mawazo yenu chanya.
Wapuuzi kama hao huwa ndo wananipaga ban
 
Ccm wasirudie makosa kwa vipi ?? Una maana wakubali kuandikwa katiba mpya ambayo haitampa madaraka makubwa kupita kiasi mkuu wa nchi ??! Au wasirudie makosa kwa katiba hii hii iliyopo ??!!
Katika hii mada dadavua upendavyo.
Ukiona sungura kula.
 
Back
Top Bottom