CCM na Serikali jibuni hoja za Humphrey Polepole, msimzime kidola

CCM na Serikali jibuni hoja za Humphrey Polepole, msimzime kidola

Katiba imetamka neno term, na hii term ndio alikuwepo Magufuli kama kiongozi na Samia kama msaidizi, huwezi kuifuta hii term kwasababu tu Magufuli alifariki wakati msaidizi wake bado anaiendeleza, ndio maana nae husema "kazi iendelee" kazi ipi hiyo? ya awamu ya tano.
Neno term kwenye katiba lina maana ya kipindi au vipindi. Kila rais aweza kuwa na terms 2 au vipindi viwili na si zaidi. neno term halikumaanisha awamu kama uavotaka kutuaminisha hapa. Habari ya kazi iendelee ni kaslogan tu ambako hakana maana yoyote kakisemwa au kasiposemwa
 
Ingiza hili kwenye akili yako nyembamba. amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ya JMT mheshimiwa SSH aliingia madarakani kwa mujibu wa katiba ya JMT iliyopitishwa na bunge la JMT na kuapishwa kuwa Rais wa JMT. aliapishwa hivyo baada ya kuwa makamu wa Rais wa JMT katika serikali iliyoongozwa na jpm aliyefariki.

Kwa kuzingatia katiba ya JMT rais SSH ni rais halali wa JMT kwa utaratibu halali wa JMT. kwa kuwa hakuna mahali popote panapotoa muongozi wa kutaja uongozi wa rais fulani kuita uongozi kwa jina lolote ikiwemo mambo ya awamu, anayejua habari ya uongozi fulani ni wa awamu gani anayejua namba bora ya kutaja ni rais aliyeko madarakani. rais aliye madarakani ndie anayejua maslahi sahihi ya taifa hili na aweza kubadili maamuzi ya mtangulizi wake yeyote kwa maslahi mapana ya taifa na sio kwa kupata shinikizo kutoka popote. zoeeni tu hilo
Kwani kuna mtu amesema Samia siyo Rais halali?

Halafu suala la awamu na mihula ya kila awamu lipo kwenye Civics form one.

Shida mna shule ndogo sana vijana, njaa zitawaua.

Uhuni siyo deal. #kataawahuni
 
Kwani kuna mtu amesema Samia siyo Rais halali?

Halafu suala la awamu na mihula ya kila awamu lipo kwenye Civics form one.

Shida mna shule ndogo sana vijana, njaa zitawaua.

Uhuni siyo deal. #kataawahuni
civics form one ndio katiba ya JMT inayoelekeza mamba haya ya msingi? marais wanaongozwa na civics form one?
 
Huyo rais samia anapojitambulisha kama rais wa awamu ya Sita,iyo tafsiri ya awamu ameitoa wapi?
kajisikia tu kuiitwa awamu ya sita ambayo hakatazwi na wala hajatukana. kusema kasi mpya nguvu mpya au hapa kazi tu au kazi iendelee au awamu ya nne ni maneno anayoweza kuyatumia yeyote ikiwemo rais aliya madarakani kuhamasisha utendaji wa serikali anayoongoza hakuna kanuni maalum kwenye hili
 
Na tunapenda iwe hivyo, amalizie hii minne, halafu aanze 10 ya kwake kisha atamalizia na mitano ya shukrani.
Kweli akili za celebrity forum haziwezi kufit sehemu zote.

Ni vizuri mkawa mnasubiria hoja mserereko mlizozoea kabla ya kuandika mada zilizowapita uwezo kiakili.
 
CCM NA SERIKALI JIBUNI HOJA ZA POLEPOLE, MSIMZIME KIDOLA.

Na Yericko Nyerere

Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon. Hivi ndivyo wahenga husema, Kinga ya kirais aliyokuwa nayo Humphrey Polepole katika ule utawala dharimu imeisha, ni kinga hiyohiyo ndio alikuwa nayo Paul Makonda, Sabaya, Chalamila, Mnyeti, Odunga na wahuni wengine wengi.

Tulishaisikia na kuona milio ya maumivu ya Sabaya, huku Paul Makonda akianza kuwambwa kisawasawa na kuandaliwa makazi mapya Segerea. Naam miliyo ya maumivu ya Polepole tumeanza kuisikia vizuri sana, Bahati mbaya kwetu sisi milio hiyo sio migeni, Tulishalia sana, Tulishazika ndugu zetu wengu, Tulishafungwa jela sana na tulishafanyiwa madhila mengi, Polepole akiwa ni moja ya magenge makuu ya uhalifu huo nchini. Lakini tulishavuka viwango hivyo vya mateso, na Sasa tuna wajibu wa kumtetea yoyote anayeonewa.

Serikali inawajibu wa kujibu hoja za Polepole badala ya kutumia vyombo vyake vya dola kumnyamazisha, Hoja za Polepole ni nzito na zina maslahi kwa umma wa Watanzania, zijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo. Uhuru wa Polepole usipokwe kwa njia zilezile tulizopitishwa sisi. Yale madhila yaishie kwetu, tuzuie yasiendelee kwa wengine. Polepole ajibibiwe.

Hoja ya Polepole kwamba hii ni Awamu ya Tano itakayokamilika 2025 na sio ya Sita ni hoja ya muhimu sana kwa umma, Kwasababu kwa muda mrefu serikali hii iliyojichagua kinguvu 2020 kukamilisha awamu ya tano ya miaka 10, imekuwa ikijitambulisha kwamba ni serikali ya awamu ya sita. Jambo ambalo kimantiki si kweli. Ni wajibu wa serikali itoke imjibu Polepole, badala yake inamjibu kwa kutumia machineries zilezile ilizotumia kwetu.

CCM na Serikali yake kwa miaka mingi ikishindwa kujibu hoja kinzani, imekuwa ikiagiza Vyombo vya "dola" kama Polisi, TRA, TCRA, Uhamiaji, TAKUKURU, MAHAKAMA nk, kuzima hoja za wapinzani, na kwa miaka mitano iliyopita vimetumika kwakiwango cha kutisha kuumiza Watanzania wengi sana hususani Wanachadema wengi hadi leo wako waliokufa (Alfonce Mawazo), wako walipotea (Ben Saanane na Azory), wako vilema (Lissu), wako walioko jela (Mbowe), na wako waliofilisiwa (Mbowe na wengine), wako wanaohangaika mahakamani kila siku (Wanachadema kila kona ya Tanzania. Msingi wa haya yote ni ccm na serikali yao kushindwa kujibu hoja zao.

Hatuna shida na Polepole kusulubiwa kwa mechanism zilezile zilizotusurubu sisi, Msulubuni Polepole kama Polepole kwa makosa mengine hata yake ya kijinga ya Vieitii, sio kwa hizi hoja zake, hoja zake jibuni kwa hoja, Hoja zake ni hoja zetu pia, Hoja zake zina maslahi kwa umma. Tunakemea na kuzitaka mamlaka zirudi kwenye mstari, Leo Polepole analilia uhuru wa kutoa maoni ambao yeye akiwa madarakani aliupora kwa wengine, Noo tunaka Polepole awe huru tena huru kabisa.

Ni Polepole huyu huyu na CCM yao walichota pesa ya Umma na wakaongoza genge la kupora uhuru wa Watu kuwa wanachama wa chama chochote wakipendacho, wakawatishia na kuwapatia pesa na ahadi lukiki za kimadaraka ili wahame vyama vyao walivyovipenda, ni Polepole huyu huyu alikuwa na lugha chafu sana kwa wanaccm wenzake waliokuwa na maoni tofauti ndani ya Chama kumbuka matusi yake ya nguoni kwa Paul Makonda alipoanza kuonyesha nia ya kugombea ubunge Kigamboni.

Hayo yote hayawezi kuwa sababu tuache kusikiliza na kujadili hoja zake, Tumpuuze Polepole, lakini tuzichukue hoja zake tuzichambue, tuzitake mamlaka ya dola na chama chake wazijibu hoja zake. Tutakuwa wajinga kama hatutaitaka serikali ijibu hoja za Polepole na badala yake tukaacha Polepole asulubiwa kama tulivyofanyiwa sisi, Kitendo cha kuitaka serikali ijibu na ikijibu, tutatukuwa tumefanikiwa kufunga njia ya mateso kwa Watanzania wengine kesho.

Tunaposimama kudai Katiba mpya tuna maana pana zaidi na moja ya mambo muhimu ni kama haya katiba itazuia vyombo vya dola kutumika kisiasa, Leo Mwenyekiti wetu amebambikiwa kesi ya Ugaidi kisa anadai katiba mpya, Hilo haliwezi kuwa mwisho wa madai ya umma kuhusu katiba mpya. Mwachieni Mbowe, jibuni hoja zake.

View attachment 2041229
View attachment 2041233
Nilishawahi kusema kuwa ndani ya CCM huwa wanaupinzani wa asili. Ukiona upinzani unang'ra nje ya CCM ujue watu waliomo ndani wanafanana na wananufaika kwa kadri ya fursa wanayopata. Upinzani uliomo humo unasababishwa na vita dhidi ya haki,ufisadi, kiburi, kujiona bora, dharau, fursa za dhuluma ya kumiliki mali na mamlaka hicho ndicho kinachoendelea kwa sasa na hapo huenda tukapoteza mtu wa mhimu kwenye taifa kutokana na vita zao zisizozingatia maslahi ya wananchi na taifa.
 
kajisikia tu kuiitwa awamu ya sita ambayo hakatazwi na wala hajatukana. kusema kasi mpya nguvu mpya au hapa kazi tu au kazi iendelee au awamu ya nne ni maneno anayoweza kuyatumia yeyote ikiwemo rais aliya madarakani kuhamasisha utendaji wa serikali anayoongoza hakuna kanuni maalum kwenye hili
Sikuwa najua kuwa nchi inaongozwa kwa kujisikia tu, mpaka leo niliposoma hii hoja yako😅.
 
Sikuwa najua kuwa nchi inaongozwa kwa kujisikia tu, mpaka leo niliposoma hii hoja yako😅.
of course kila jambo analolifanya mtu ni kwa kujisikia kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu zilizopo kwenye taifa au kwa lugha iliyozoeleka ni kwa kuamua kwa utaratibu huo huo. mtu anaweza kujisikia kufanya lolote ili mradi havunji sheria na katiba ya JMT
 
Nimemsikiliza Polepole mara kadhaa,anazo hoja zenye mashiko.
Tunatakiwa kushambulia hoja na sio mtu.Hoja za Polepole ni wanasiasa wachache sana wanaweza kuzijibu.Polepole anajua kujenga hoja.Nape anaongea mipasho,vijembe,mijisifu na kuzomea, hakuna cha zaidi.Tofauti ya Polepole na Nape kisiasa,ni sawa kuifananisha mbingu na ardhi! Polepole (mbingu),Nape(Ardhi).
CDM acheni kuingilia maugomvi ya CCM yatawaondoa kwenye ramani .
Endeleeni kukijenga chama,kuandikisha wanachama kidigitali na kupaza sauti nchini na duniani kote kuhusu uonevu anaofanyiwa Mwenyekiti pamoja na wanachama wengine waliowekwa korokoroni!
 
of course kila jambo analolifanya mtu ni kwa kujisikia kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu zilizopo kwenye taifa au kwa lugha iliyozoeleka ni kwa kuamua kwa utaratibu huo huo. mtu anaweza kujisikia kufanya lolote ili mradi havunji sheria na katiba ya JMT

Wewe jamaa utakuwa umechanganyikiwa nakuhakikishia haiwezekani kuwa na mfumo huo
Labfa ndio huu utumbo uliokoment.
Haiwezekani kusema kuna mfumo mtu unafanya kazi kwa kujisikia huku ukifuata sheria,kanuni na taratibu.
Ukishasema sheria,kanuni na taratibu hapo suala la kujisikia halipo
 
Wewe jamaa utakuwa umechanganyikiwa nakuhakikishia haiwezekani kuwa na mfumo huo
Labfa ndio huu utumbo uliokoment.
Haiwezekani kusema kuna mfumo mtu unafanya kazi kwa kujisikia huku ukifuata sheria,kanuni na taratibu.
Ukishasema sheria,kanuni na taratibu hapo suala la kujisikia halipo
ni kwa sababu tu akili yako imekukatalia kukubali kuwa pale unapoinua mkono wako kufanya jambo ni kuwa umefanya maamuzi ya kufanya hilo jambo ukijua matokeo yake na ndio kujisikia huko. akili nyepesi zenye kutenda kwa haziwezi kuconceptualize mambo kama haya. we sema tu kuwa nimechanganyikiwa kwa sababu hivyo ndivyo unavyojisikia
 
ni kwa sababu tu akili yako imekukatalia kukubali kuwa pale unapoinua mkono wako kufanya jambo ni kuwa umefanya maamuzi ya kufanya hilo jambo ukijua matokeo yake na ndio kujisikia huko. akili nyepesi zenye kutenda kwa haziwezi kuconceptualize mambo kama haya. we sema tu kuwa nimechanganyikiwa kwa sababu hivyo ndivyo unavyojisikia
Kutakuwaje na Sheria na kanuni Kisha mtu afanye kwa namna anavyojisikia? Vipi asipojisikia kufanya kitu fulani ilihali sheria inamtaka?

Acheni kuleta hoja mlendamlenda kama mmekatwa vichwa.
 
CCM NA SERIKALI JIBUNI HOJA ZA POLEPOLE, MSIMZIME KIDOLA.

Na Yericko Nyerere

Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon. Hivi ndivyo wahenga husema, Kinga ya kirais aliyokuwa nayo Humphrey Polepole katika ule utawala dharimu imeisha, ni kinga hiyohiyo ndio alikuwa nayo Paul Makonda, Sabaya, Chalamila, Mnyeti, Odunga na wahuni wengine wengi.

Tulishaisikia na kuona milio ya maumivu ya Sabaya, huku Paul Makonda akianza kuwambwa kisawasawa na kuandaliwa makazi mapya Segerea. Naam miliyo ya maumivu ya Polepole tumeanza kuisikia vizuri sana, Bahati mbaya kwetu sisi milio hiyo sio migeni, Tulishalia sana, Tulishazika ndugu zetu wengu, Tulishafungwa jela sana na tulishafanyiwa madhila mengi, Polepole akiwa ni moja ya magenge makuu ya uhalifu huo nchini. Lakini tulishavuka viwango hivyo vya mateso, na Sasa tuna wajibu wa kumtetea yoyote anayeonewa.

Serikali inawajibu wa kujibu hoja za Polepole badala ya kutumia vyombo vyake vya dola kumnyamazisha, Hoja za Polepole ni nzito na zina maslahi kwa umma wa Watanzania, zijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo. Uhuru wa Polepole usipokwe kwa njia zilezile tulizopitishwa sisi. Yale madhila yaishie kwetu, tuzuie yasiendelee kwa wengine. Polepole ajibibiwe.

Hoja ya Polepole kwamba hii ni Awamu ya Tano itakayokamilika 2025 na sio ya Sita ni hoja ya muhimu sana kwa umma, Kwasababu kwa muda mrefu serikali hii iliyojichagua kinguvu 2020 kukamilisha awamu ya tano ya miaka 10, imekuwa ikijitambulisha kwamba ni serikali ya awamu ya sita. Jambo ambalo kimantiki si kweli. Ni wajibu wa serikali itoke imjibu Polepole, badala yake inamjibu kwa kutumia machineries zilezile ilizotumia kwetu.

CCM na Serikali yake kwa miaka mingi ikishindwa kujibu hoja kinzani, imekuwa ikiagiza Vyombo vya "dola" kama Polisi, TRA, TCRA, Uhamiaji, TAKUKURU, MAHAKAMA nk, kuzima hoja za wapinzani, na kwa miaka mitano iliyopita vimetumika kwakiwango cha kutisha kuumiza Watanzania wengi sana hususani Wanachadema wengi hadi leo wako waliokufa (Alfonce Mawazo), wako walipotea (Ben Saanane na Azory), wako vilema (Lissu), wako walioko jela (Mbowe), na wako waliofilisiwa (Mbowe na wengine), wako wanaohangaika mahakamani kila siku (Wanachadema kila kona ya Tanzania. Msingi wa haya yote ni ccm na serikali yao kushindwa kujibu hoja zao.

Hatuna shida na Polepole kusulubiwa kwa mechanism zilezile zilizotusurubu sisi, Msulubuni Polepole kama Polepole kwa makosa mengine hata yake ya kijinga ya Vieitii, sio kwa hizi hoja zake, hoja zake jibuni kwa hoja, Hoja zake ni hoja zetu pia, Hoja zake zina maslahi kwa umma. Tunakemea na kuzitaka mamlaka zirudi kwenye mstari, Leo Polepole analilia uhuru wa kutoa maoni ambao yeye akiwa madarakani aliupora kwa wengine, Noo tunaka Polepole awe huru tena huru kabisa.

Ni Polepole huyu huyu na CCM yao walichota pesa ya Umma na wakaongoza genge la kupora uhuru wa Watu kuwa wanachama wa chama chochote wakipendacho, wakawatishia na kuwapatia pesa na ahadi lukiki za kimadaraka ili wahame vyama vyao walivyovipenda, ni Polepole huyu huyu alikuwa na lugha chafu sana kwa wanaccm wenzake waliokuwa na maoni tofauti ndani ya Chama kumbuka matusi yake ya nguoni kwa Paul Makonda alipoanza kuonyesha nia ya kugombea ubunge Kigamboni.

Hayo yote hayawezi kuwa sababu tuache kusikiliza na kujadili hoja zake, Tumpuuze Polepole, lakini tuzichukue hoja zake tuzichambue, tuzitake mamlaka ya dola na chama chake wazijibu hoja zake. Tutakuwa wajinga kama hatutaitaka serikali ijibu hoja za Polepole na badala yake tukaacha Polepole asulubiwa kama tulivyofanyiwa sisi, Kitendo cha kuitaka serikali ijibu na ikijibu, tutatukuwa tumefanikiwa kufunga njia ya mateso kwa Watanzania wengine kesho.

Tunaposimama kudai Katiba mpya tuna maana pana zaidi na moja ya mambo muhimu ni kama haya katiba itazuia vyombo vya dola kutumika kisiasa, Leo Mwenyekiti wetu amebambikiwa kesi ya Ugaidi kisa anadai katiba mpya, Hilo haliwezi kuwa mwisho wa madai ya umma kuhusu katiba mpya. Mwachieni Mbowe, jibuni hoja zake.

View attachment 2041229
View attachment 2041233
Chochea kuni .
 
Kutakuwaje na Sheria na kanuni Kisha mtu afanye kwa namna anavyojisikia? Vipi asipojisikia kufanya kitu fulani ilihali sheria inamtaka?

Acheni kuleta hoja mlendamlenda kama mmekatwa vichwa.
ndo maana nakwambia kichwa chako kibovu kinakukatalia tu hili jambo. je akijisikia kutenda kulingana na sheria? au je akijisikia kutenda kinyume na sheria? kwani kote si huwa kuna matokeo yake. we hujawahi kusikia rais wa chad alimuondoa CAG wake kwa kujisikia tu. we hujawahi kusikia kuwa rais wa JMT aweza kujisikia kuwaachilia au kutowaachilia wafungwa wenye sifa fulani hata kama wana sifa fulani fulani za kusamehewa vifungo. hujawahi kusikia rais akijisikia anaweza kumteua mtu anayemtaka kuwa mbunge wa bunge wa JMT. akili yako yaonekana imefungwa ndani ya boxi ambalo limeshaachwa wazi lakini hujui ufanye nini
 
Back
Top Bottom