KERO CCM na Serikali yake wameharibu sana Miji ya Tanzania, na imebakia kuwa magulio, miji imejaa Frame hadi kwenye makazi ya watu. Miji ni michafu sana

KERO CCM na Serikali yake wameharibu sana Miji ya Tanzania, na imebakia kuwa magulio, miji imejaa Frame hadi kwenye makazi ya watu. Miji ni michafu sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kama pale Rangi 3 dah nchi imejaa wachuuzi kinoma kudanganya kua kuna nafuu ya maisha wakati miaka na miaka mtu yule yule ana biashara ile ile mtajo ule ule maisha yale yale na yanazidi kudidimia. Imagine mtu anafanya biashara kwa miaka 10 ila siku moja akilala nyumbani basi chungu hakiwekwi jikoni.
 
Naunga mkono hoja.maana.serikali iko chini ya.ccm. Imeshindwa kupanga.miji na.kusimamia mipango miji.

Road reserve zimemezwa na fremu. car.wash. siku ikipiga tsunami ndio tutaelewa maana ya kuwa na mipango miji.
Ajabu ukienda kenya nchi yao wamejitahidi sana kuipanga vizuri kuachia breathing areas. Open spaces.and parks.

Ingewezekana barabara zote zipanuliwe mapema na waliozidi wabomolewe mapema zipatikane service roads. Kama njia ya. Mwenge mpaka bagamoyo service.road zichimbwe mapema. Njia ya.kwenda goba.ipanuliwe mapema njia ya madale goba ipewe service roads. Mwai kibaki ipanuliwe mapema wanovunjiwa wavunjiwe mapema
 
Miaka michache iliyopita Mkurugenzi wa Jiji la la Arusha na Meya wake walipendekeza makaburi ya majengo yafukuliwe vijengwe vibanda upande mmoja na mwingine wajigawie madiwani na matajari wa Mirerani.
Tuliokuwa na wapendwa wetu wamelala hapo tukisaidiwa na gazeti la Rai tukapiga kelele na kuuvunja mpango huo.
Wanachojali mafisiemu ni kura za machings na matumbo yao tuu ,na mipango miji ni sawa na Kiyunani kwao, hawaelewi kitu.
Hilo ndo limetokea kwa stendi ya Bukoba mjini kati kukwama hadi sasa...wanataka kujenga vibanda kuzunguka stendi wakati hela hawana na watachafua mji...sasa stendi imekwama na ilibidi ikamilike toka mwezi wa nne... Daladala zinapaki popote tu
 
Uchumi wa Fremu
Fremu katika makazi
Fremu hospital
Fremu stendi
Fremu makanisani
Fremu karibu na kambi,
Fremu...
ulitakaje kwani, watu wanapanga kwenye hayo mafrem tiharahei wanaokota besa ngoda
 
Serikali Haina mpango na Wananchi.... Nikienda Babati nikawa napita mitaani nahesabu fremu nacheka mwenyewe.
Serikali ije na mkakati wa kufuta consumers society iliyonayo itengeneze manufacturing society.... Tujifunze Toka hasa Pakistan, Wana viwanda vidogo sana vingi, vipo majumbani TU na wanatengeneza vioo, wanayeyusha chuma kutengeneza vitu vingine, sabuni, magodoro n.k..... Nyumbani TU.....

Hii fremu economy ni disaster na unakuta mpaka maprofessor na wanasiasa wanamiliki fremu na wanaona ni kitu Cha maana kabisa ... Useless
 
Ni dalili pia ya.umaskini economically watu wanakosa.kazi wanadandia kwenye fremu
 
CCM inahusikaje hapo? CCM ndio unatumia wanachama wake kuingiza Serikali?
Hivi uko serious kweli? Serikali imetokana na chama gani? Inaendeshwa na kusimamiwa na chama gani? Kwa ufupi, hakuna chochote katika nchi hii ambacho unaweza kukitenganisha na CCM?
 
Naishangaa mpaka sasa bado kipo madarakani!

INAWEZEKANA WENGII WA WATANZANIA NI VICHAA NDIO MAANA WANAENDELEA KUKIWEKA MADARAKANI!
Shida iliyopo ni kwamba wapo watu wengi ambao hawawezi kuona uhusiano kati ya CCM na umaskini na shida nyingine walizonazo.
 
Back
Top Bottom