CCM, Serikali Mbili Zilizoboreshwa, na Hatima Ya Muungano

CCM, Serikali Mbili Zilizoboreshwa, na Hatima Ya Muungano

Haya ni mapendekezo ya chama juu ya rasimu ya katiba. Hivyo ndivyo ccm inapanga kuboresha mfumo wa serikali mbili. Nyaraka hiyo iliwasilishwa na Asha Migiro kwenye kikao cha NEC kuelekea Bunge La Katiba. Aliwasilisha haya kwa nafasi yake kama Katibu NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Je, was it a coincidence for her to be appointed Waziri Wa Sheria na Katiba? Tutajua mengi zaidi Bunge la Katiba liki "resume" baadae mwezi wa nane, 2014.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Sidhani kama mapendekezo haya yataweza kutekelezeka.
Ni sawa na report ya Mukama na January Makamba kuhusu uchaguzi wa 2010 inayoelezea low voter turn out. haikufanywa kitaalam, na haikukubaliwa na CCM.
Sidhani kama CCM itajaribu hata kupendekeza hii rasimu/maoni mbele ya chombo chochote. Ni sawa na kutaka serikali tatu which is worse than the status quo.
 
Duh sasa CCM naona wanatuletea mkorogo..
Mkuu Mchambuzi nina swali... Je ikitokea rais wa Muungano akafariki/au kuugua kwa muda mrefu ni nani atakahimu nafasi yake? Je ni makamo wa rais (Rais wa Zanzibar ambaye hakuchaguliwa na watanganyika (Bara) au ni Waziri mkuu ambaye hakuchaguliwa na wazanzibar (Maana nafasi ya rais wa Muugano ni muhimu kukahimiwa na kiongozi aliyechaguliwa pande zote za Muugano.

Swali la pili itakuwaje kama mgombea urais wa Muungano (tusema CCM) (Tanzania Bara) akapochaguliwa kwa kura nyingi bara. lakini kwa Zanzibar akapata kura chache saaaaana au hata hasipate kura kabisa na Mgombea urais wa Cuf apate kura za kutosha kutoka Zanzibar lakini kura pungufu Bara. Swali je nani atakuwa Rais wa Muungano maan rais wa Muugano inatakiwa akubaliwe sehemu zote.
Alinda ahasante, intriguing questions.
Nichangie kidogo

Kwa katiba iliyopo makamu wa rasi ni mgombea mwenza kwa maana alishirikiana na Mgombe kutafuta kura. Kwa msingi huo ana mamlaka katika JMT.

Tatizo lililopo ni kuwa hana mamlaka yoyote kule znz kwasababu katiba ya znz haimtambui kama ambavyo Katiba ya JMT isivyomtambua makamu wa rais wawili wa znz bali waziri kiongozi.


Ukisoma katiba ya znz ya 2010 sijaona mahali Rais wa JMT ametajwa.
Kilichotajwa ni serikali ya muungano.


Hapo napo kuna utata kama Rais wa JMT ana hadhi yoyote awapo znz.
Pengine ndiyo maana itifaki inamweka nyuma ya Rais wa znz.


Kwa muundo wa S2 maboresho, Rais akitoka Tanganyika makamu atatoka znz, Rais wa ZNZ.
Kimsingi Rais huyo hakuchaguliwa na watu na mamlaka yake bara yanakuwa na uhalali wa kisheria bila kuwa na uhalali wa kisiasa.

Hilo litaleta taabu unless kiwepo kifungu kinachomlazimu aitishe uchaguzi.
Kuanzia hapo itakuwa ni vurugu tupu.

Hatuna experience ya kupoteza kiongozi madarakani na pengine linafanya issue iwe trivial hata kama ina impact kwa taifa.

Kuhusu suala la Rais wa bara na znz kuwa wa Upinzani, hilo lina utata mkubwa sana.
Njama zilizofanyika huko nyuma kuhakikisha kuwa rais anashinda kwa simple majority hata ya 50.01 kama alivyosema Mchambuzi.

Hii maana yake ni kuwa CCM watatumia kila aina ya mbinu kuhakikisha znz wanapata simple majority ambalo ni jambo rahisi kwa hujuma na kwa uhalali.

Kwa hujuma ni kutumia tume ya uchaguzi, vyombo vya dola na mbinu luluki walizo nazo ikiwa ni pamoja na 'suppression'

Ni kwa msingi huo CCM hawataki katiba mpya itakayotoa au kuweka tume huru za uchaguzi

Njia halali ni kuhakikisha kuwa Unguja, ngome yao na ambayo hadi sasa wanaungwa mkono sana inashinda. Kushinda Unguja tu kutawapa simple majority.

Kumbuka kuwa ushindi wa chaguzi zetu si idadi ya viti ni idadi ya kura.
Hata kama wapinzani kama CUF watashinda viti uwezekano wa kupata simple majority ni mdogo.


Hatari wasiyoiona CCM ni moja, kwamba wameshajenga mbegu ya uzanzibar zaidi kuliko uchama.

Kuwatisha Dodoma hakuwezi kuwa sawa na nguvu ya umma.
Ili CCM ifanikiwe ni lazima yawepo mabadiliko ya katiba ya znz.

Hilo litawaunganisha wznz zaidi kuliko kuwatenga kama walivyo Dodoma.
Uwezekano wa kuwa na mkanganyiko wa Rais wa bara ni chama X na znz ni chama Z ni mkubwa.


CCM wanaona mfumo wanaotengeneza ni mzuri, wasichojua ni kuwa uzuri wake ni wa 'perfume' baada ya muda utachuja. Ni mfumo wa mnyama mzuri sana anayeonekana lakini hana mifupa.

Ikifika wakati ambapo kuwa confusions and political wrangling muungano utafikia hatima.
Utafikia hatima kwasababu haujengwi kwa misingi ya watu, unajengwa kwa misingi ya chama na kulindwa na FFU.

Miaka 50 FFU hawajaweza kuzuia majeraha ya muungano, kidonda bado kibichi kama tunavyoshuhudia. Ndani ya crisis kidonda kitatoa funza na fupa litavunjika.
 
MUUNDO WA BUNGE

Katika maboresho yake ya serikali mbili, CCM inapendekeza kuwepo Kwa MABUNGE MATATU (chini ya serikali mbili), kwa kuongeza Bunge la tatu litakaloitwa "Baraza La Wawakilishi la Tanzania Bara". Jukumu la chombo hiki litakuwa ni kusimamia masuala ya Tanzania Bara pekee, tofauti na sasa ambapo masuala haya yanasimamiwa na Bunge la Muungano ambalo, wabunge kutoka nchini jirani ya Zanzibar pia ni sehemu ya bunge hili la Muungano. CCM inapendekeza kwamba – wakati Bunge la Muungano litakapo kuwa linajadili mambo ya muungano, wabunge wote – kutoka Tanzania Bara na nchi jirani ya Zanzibar, watashiriki katika majadiliano. Lakini pale mijadala juu ya masuala ya Tanzania bara pekee itakapoanza, wabunge kutoka Zanzibar hawataruhusiwa kushiriki katika mijadala hiyo. Kwa maana nyingine, mijadala juu ya "Tanzania Bara" itakapoanza ndnai ya Bunge, hii itawapa Wabunge kutoka nchi jirani ya Zanzibar, fursa ya - nikiazima maneno ya Nguruvi3, "KUTALII".

Lipo suala lingine muhimu katika kile CCM inachokiita "maboresho ya serikali mbili". Bunge la Muungano litakuwa na Spika na Naibu Spika. Spika atatokea sehemu moja ya muungano, na naibu wake atatokea sehemu ya pili ya muungano. CCM inapendekeza kwamba wakati wa vikao vinavyohusu mambo ya Tanzania bara, Spika au Naibu Spika atakayetokea Tanzania Bara ndiye atakaye endesha kikao hicho.

MGOGORO UTAKAOJITOKEZA

Utaratibu huu wa kuanzisha Baraza la Wawakilishi la Tanzania Bara ambalo litasimamia masuala ya Tanzania bara, hautatekelezeka chini ya mfumo wa Serikali Mbili zitakazo boreshwa na CCM. Hii ni kwa sababu, kitendo cha kuwazuia wabunge kutoka wa Zanzibar kushiriki mijadala isiyohusu masuala ya muungano ni kutengeneza mgogoro mwingine mkubwa. Hii ni kwa sababu:
  • Chini ya mfumo wa serikali mbili ulioboreshwa, HAKUNA MAMBO YA TANZANIA BARA PEKEE YAKE. Badala yake, Yapo MAMBO YA ZANZIBAR, NA MAMBO YA MUUNGANO. Basi!.

Chini ya serikali mbili, wananchi wa Tanzania Bara wasahau kuwa na chombo kitakacho wawakilisha kwa dhati – yani Bunge. Hii ni kwa sababu, chini ya kitakachoitwa "Bunge la Tanzania Bara/Baraza la wawakilishi la Tanzania Bara", maamuzi ya bunge hili yanayohusu mambo ya Tanzania Bara hayatakuwa na Serikali ya kuyasimamia au kuyatekeleza. Badala yake, utekelezaji wake utayeyuka ndani ya serikali ya muungano na kupoteza fedha nyingi sana za walipa kodi. Hali hii itazua migogoro mikubwa ndani ya muungano kwa sababu uwepo wa "Bunge la Tanzania Bara" bila ya "Serikali Ya Tanzania Bara", maana yake ni kwamba hakuna mtu au chombo chochote ambacho kitawajibika/wajibishwa moja kwa moja iwapo yale yanayopitishwa au yanayoamulia na bunge la Tanzania Bara, hayatatekelezwa!

CCM kuwaanzishia wananchi wa TANZANIA BARA lao kwa maana ya - "Bunge la Tanzania Bara" bila ya kuwaanzishia Serikali ya Kufanya kazi na Bunge hili kutawafungua akili na macho wananchi wa Tanzania bara juu ya nini ambacho watetezi wa serikali tatu walikuwa wanakijengea hoja. Hali hii itapelekea wananchi wengi wa "Tanzania Bara" kuanza kudai serikali yao ya Tanganyika (ukipenda, ita Tanzania Bara). Hii ni kwa sababu, hata kupitia elimu zao za sekondari, elimu ambayo sasa imeanza kutambulika kama ni Elimu Ya Msingi kwa kwa wananchi wote, elimu waliyopata na ambayo inaendelea hata leo ni kwamba - Duniani kote, BUNGE ni moja ya mihimili mikuu mitatu ya dola, mihimili mingine miwili ikiwa ni SERIKALI NA MAHAKAMA. Wananchi wa Tanzania Bara wataanza kuhoji - kwanini tuna Bunge la Tanzania Bara lisilokuwa na Serikali yake? Maamuzi wa bunge hili kwa maana ya sera mbalimbali za maendeleo zinasimamiwa na nani? Hapo ndio wataanza kuelewa Profesa Lipumba alikuwa anamaanisha nini aliposema bungeni kwamba – kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika la DFID la Uingereza, 35% ya fedha zinazotengwa katika bajeti ya muungano kila mwaka wa fedha, hazifanyi kitu chochote cha maana kwa wananchi. Kwa maana nyingine, fedha hizi hazileti ufanisi wowote katika uchumi kutokana na mfumo mbovu wa utawala
Kuna hatari moja kubwa ambayo CCM hawaioni kwa rasimu yao. Wabunge wa bunge la bara(a.k.a Tanganyika) watakapokaa wenyewe, watajiuliza maswali.
Nani anawasikiliza, bunge lao liendeshwe kwa utaratibu gani na maoni yao yafanyiwe kazi na nani.

Wztabaini kuwa wao ni Watanganyika kwanza kabla ya Tanzania.
Watakapokwenda kukutana na wa znz ndani ya bunge la Tanzania, watakuwa wamejihisi ni mayatima wasiyo na mlezi.

Nguvu zao zitakuwa kubwa sana kwasababu watawaangalia wznz kama wale, nao kama sisi. Tatizo ni kuwa chuki itajengeka kimya kimya na kutakuwa na kukwamishana kiaina.

Mfano mzuri ni ule wa Passport za kuingia znz.
Huko nyuma Watanganyika walilazimika kubeba passport kuingia znz.

Hilo lilizua chuki kwanini wao wasije na passport. Malalamiko yakawa makubwa na siku yalipoibuka bungeni ilikuwa ni azimio moja, waje na passport kama hawaondoi hali hiyo.

Kwa nyakati hizo akina Nyerere walikuwa na busara. Walijua huo ndio mwanzo wa kuligawa taifa kuelekea kifo cha muungano. Wakaingilia kati na kusema znz ifute, na ikawa.

Chuki ya passport ikabaki kama kovu, tunaita 'antigen' kwa maana kuwa Tanganyika ilishakuwa exposed na hivyo kuanza kujenga immunity dhidi ya znz.

Lilipokuja suala la OIC Watanganyika waka react haraka sana kwasababu tayari walishakuwa sensitive na znz.

Ili kuondoa tatizo hilo la 'sensitivity' tume tya Warioba ikasema Tanganyika ijitambue na znz ijitambue. Hapo hakuna sensitivity yoyote na wala hakuna atakayejenga immune dhidi ya mwingine. Kwamba jambo hilo lirasimishwe.

Lakini pia wabunge wa znz watakuwa sensitive kuwa wenzao waliobaki kujadili mambo yasiyo ya muungano pengine wana njama dhidi yao.

Kwa kuzingatia uchache wa 'watalii hao wa visiwani' na upungufu wa mambo ya kuzungumzia ndani ya bunge la JMT, nao watakuwa na hisia za kuonewa hata penye haki.

Again, ili kuondoa inferiority complex inayoweza kuwapa wabunge wa nchi jirani ya znz wawapo Dodoma kwa utalii, tume ya Warioba ikasema kila upande uwe na bunge lake, ukaweka wazi mambo 7 tu ya kuzungumzia.

In other words. tume ya Warioba imeweka agenda ya kuwakutanisha wznz na Watanganyika.

Hii rasimu CCM mafichoni, haielezi mambo gani ya muungano na yapi si ya muungano.
Hilo tu ni dalili njema ya failure ya rasimu hata kabla ya kujadiliwa.

Na kushindwa kwake ni pale wabunge wa Tanganyika watakApojitambua kuwa Tanganyika yao ndiyo imebeba mzigo wote lakini hawana mahala pa kuzunguzia fadhila na udhia wa mzigo wa muungano. Hawana serikali wala chombo kingine cha kisheria.

Ili bunge la Tanganyika lifanye kazi kwa sheria lazima kutakuwa na mwanasheria mkuu.
Huyo atatoka wapi? Atatoka katika muungano? Na kama ni huko koti linalotakiwa livuliwe Tanganyika litawezekana?

Nimalizie kwa kusema kuwa, rasimu ya mafichoni ya CCM haisemi mambo yapi ya muungano na yapi yasiyo kwasababu kuu moja.
Kutenga mambo hayo ni kuhalalisha uwepo wa Tanganyika na serikali yake, jambo wasilolitaka.

Labda CCM warudie katika drawing board watueleze, S3 zinaepukika vipi kwa hoja tunazoulizia?
 
Mkuu Mchambuzi Umechambua kisawasawa..

Big "Like" :thumbup:
 
Last edited by a moderator:
Kama serikali ya CCM imepanga haya na ndiyo msimamo wao sasa kulikuwa na haja gani taifa kuingia gharama na matumizi mabaya ya pesa zetu, mfano kiasi cha Sh8.2 bilioni zimetumika kafanya ukatabati wa bunge, bado gharama za tume ya katiba na malipo ya posho za wajumbe.
 
...

Hatuna experience ya kupoteza kiongozi madarakani na pengine linafanya issue iwe trivial hata kama ina impact kwa taifa.

...

Mkuu, mwaka 2001 tulimpoteza Makamu wa Rais, Dr. Omari Juma na hivi majuzi nusura janga kama hilo lijirudie pale JNIA kwenye ajali ya helkopta (Mwenyezi Mungu apishe mbali lakini ni mambo yanayowezekana sana maadam sote tu wanadamu). Hapo ndipo hoja ya Alinda inapokuwa na mashiko kwa wanaoona mbali.
 
Mchambuzi hatuwezi kulazimisha muungano mimi naona ni kama tunahonga bila kujua sababu. Je kuna faida gani ya Muungano kwa Mtanzania wa kawaidi ambaye ni mkulima mikoani au hata mtu yeyote wa bara kuna faida gani ya muungano kwa sasa naomba mtu anieleze kwasababu sijasikia bado faida za muungano na huu si muungano ni kwasababu upande mmoja tu Zanzibar watu wake wana haki kote. Hivyo muungano ukivunjika sioni hasara kwa sisi wa bara hasa ukuzingatia Wanzanzibar wengi hawautaki muungano

Ni kweli kabisa
Hapa chochote tunachofanya ni rushwa ya kuwabembeleza waukubali muungano lakini kinacho onekana ni kwamba hawana haja nao.
Mara nyingi najiuliza juu ya dhana ya kumezwa maana yake nini sipati jibu labda kama kuna watu wanajua maana ya Nyerere alipokataa serikali moja akiogopa znz kumezwa.
Kwa ufahamu wangu hiyo dhana imejengea uoga wa znz usio na msingi kwa sababu maana ya kuungana ni kuzika historia ya nchi hizo 2 na kuanzisha historia nyingine ,shida inaanza pale mmoja anataka kuwepo na anataka kuungana.Huwezi kupata yote waswahili husema karamu mbili zilimshinda fisi.
Kwa hali iliyofikia sasa naona sio ccm bali JK anataka kufunika kombe kama alivyosema yaje yajidhihirishe mbele(maana tayari) kuwa muungano haupo.Lakini namshauri afadhali 3 kuliko hizo 2 (zinazoitwa zilizoboreshwa) zitatupeleka angalao miaka mingine mbele .
Sababu yake ya kututishia jeshi naona ni kosa la ulimi tu, kwa sababu hilo linahusu hila za wachache ambazo bahati mbaya hazipo kwa sasa kama hizo zingekuwepo sababu za kupindua hata sasa zipo na sio kwamba mfumo tulio nao ndio kinga,inawezekana anajaribu kujisahaulisha kuwa nchi hii imeponea chupuchupu mara kadhaa kupinduliwa na wanajeshi lakini imeshapinduliwa na wana siasa (wa znz ) sasa kwa kuanzisha nchi ndani ya nchi.
 
Pomoja uwasilishaji wa mchambuzi ni vema tukawasikia na ccm wenyewe na hiyo rasimu yao kama kweli ipo na ndio waliyojadili/itakayojadiliwa otherwise mchambuzi analeta propaganda tuuu. Na kama hivyo ndivyo naungana na wanaolaumu ukawa kutoka kwenye bml coz wangeyapinga haya kwa nguvu zote, tungewasikia na kuwaunga mkono
 
Kaka yangu Mchambuzi kwanza naomba nikupe haki yako ya msingi,unastahili pongezi kwa kuja na hoja nzito kama hii,I wish Watanzania wote tunaoingia humu tukalichukulia hili serious na kulijadili bila kujali itikadi zetu.

Ninauhakika hata usalama wa uanachama wako uko matatani lakini umeweza kueleza ukweli ili uwe huru,hongera.

Kama haya uliyoyaleta ndiyo msimamo wa CCM then sioni kama wanatofauti na kuwa na serikali tatu,ila sababu ya kupoteza vyeo kwenye taasisi yetu basi tutafanya hata kisichowezekana na kupinga hata kama ukweli ndiyo utakaotusaidia.

Kama Muungano wenyewe ndio huu wautakao CCM basi wajiandae hilo Jeshi wanalolitamka kuchukua nchi,ninauhakika kwa Katiba hii wanayotaka kuileta basi wajue ndiyo wanawakaribisha wanajeshi zaidi kuliko hata zile serikali tatu walizoleta Tume ya Warioba.Na kama mawazo ya wengi muungano huo hautafika hata miaka mitano kabla haujapigwa na TB ya Utanganyika ambao utakuwa mkubwa zaidi kuliko sasa,kumbuka kizazi cha vijana siku hadi siku kinakuwa na ni kizazi kinachojadili,kutafiti na kutaka hoja kwa hoja na si hoja kwa matusi.

Kaka yangu hapa ninategemea akina Lissu,Zitto,na Jussa kadhaa kuzaliwa ndani ya CCM na nje ya CCM.Kwa kweli sijui uwoga wa viongozi wetu ni upi,sababu muungano tunaoutaka ni wa wananchi na si wa viongozi wa siasa,leo nalipia umme unit moja Tzs350 wakati Zanzibar unit moja hiyo hiyo ni pungufu ya Tzs.200 sasa .

Cha msingi bado vijana mlioCCM ndiyo mliobeba dhamana kubwa ya Taifa letu pale mtakapoungana na kuwaambia wazee huko wanakotaka kutupeleka siko.

Ninahofu na huu muungano kuvunjika zaidi ukiwa kwenye serikali mbili kuliko ukiwa kwenye serikali tatu.

Naweza kusema nafuu kuwa na kiongozi aliyeishia darasa la saba lakini akawa na BUSARA kuliko mwenye madegree mengi halafu akakosa BUSARA na hata kuisikiliza sauti ya busara.
 
Dogo1, Tetty, Kobello, Nguruvi3, Ritz

Mapendekezo ya CCM kuhusu rasimu ya pili ya Katiba pamoja na mchanganuo wa kero zilizopo ndani ya muungano na tiba zake yaliwasilishwa na Asha Migiro kwenye kikao cha NEC mwishoni mwa mwezi February, 2014. Wanaopinga hili waje hapa kutueleza vinginevyo.
Nguruvi3, hoja kuhusu wabunge wa Bara kuhisi yatima - mapendekezo ya CCM katika maboresho ya serikali mbili ni pamoja na uundwaji upya wa majimbo ya uchaguzi - ambayo yanaitwa "majimbo ya jamhuri ya muungano". Kwa upande wa znz, majimbo ya uchaguzi ya BLW yataendelea kuwa hayo hayo kama majimbo ya uchaguzi ya bunge la jamhuri ya muungano. Je, mabadiliko haya yataleta tofauti gani na hali ya sasa? Je tutakuwa na bunge la Tanzania bara na likafanya kazi kama bunge la wananchi wa Tanzania Bara? Bunge hili litafanyaje kazi bila ya serikali? Wananchi wa Bara wanashindwa kuelewa kwamba - hata kwenye halmashauri zao Songea, Mpanda, Rungwe, Karagwe, Biharamulo, Nzega, Newala, Hai, na kwingineko, kote huku pia kunakuwa na serikali. Madiwani husika hawawezi fanya kazi bila ya serikali. Hatuwezi kuwa na bunge la Tanzania Bara bila ya bunge hili kuwa na serikali yake - mawaziri na rais au waziri mkuu, vinginevyo ni kujenga migogoro na uhasama usio na sababu, na ni kupoteza fedha za walipa kodi kwani hakuna accountability.

Zipo taarifa kutoka ndani ya tume zinazosema kwamba baadhi ya viongozi wa ccm walipendekeza serikali mbili huku wakija na maboresho ambayo yatavunja muungano. Yet, ni hawa hawa ambao wanaona maboresho yao ni bora kwa muungano kuliko serikali tatu, na wanamshutumu warioba anavunja muungano. Rekodi zipo ndani ya tume kwamba viongozi kadhaa walipendekeza serikali mbili huku katiba ikifanyiwa mabadiliko - just to accommodate znz. Kwa mfano, walitaka:

1. Znz iwe na kiti chake UN. Hili moja kwa moja linavunja muungano.

2. Znz iwe na sarafu, jeshi, usalama wa taifa, polisi, rais wake kutambulika kama amiri jeshi mkuu. Haya yote yanavunja muungano.

Makada hawa wanaona mapendekezo yao ni bora kuliko serikali tatu. Na ni hawa ndio wamesaidia ile ripoti ya Asha Rose Migiro ije na mapendekezo tuliyojadili.

MAKOSA YA TUME: CCM INATAFUTA TU PA KUJIFICHA

Tukirudi nyuma kidogo, mjadala wa muundo wa muungano uliingizwa kwenye sheria ya muswada wa sheria ya kuundwa kwa tume ya katiba kwa sababu mbili:

Kwanza - mabadiliko ya katiba znz (2010) yalileta athari ya moja kwa moja juu ya muundo wa muungano. Kwa mfano, znz ikatambulika kama nchi yenye mipaka yake, wimbo wa taifa, bendera yake na vikosi vyake vya ulinzi na usalama. Kufuatia mabadiliko haya, ndio maana ikaja serikali ya umoja wa kitaifa. Hili halipo kwenye katiba ya JMT (1977) ambayo CCM inataka "iboresha".

Pili, mjadala juu ya muundo wa muungano haukuja na matakwa ya watawala. Tuliwasikia Jaji Werema, Celina Kombani (akiwa waziri wa sheria na katiba) wakisema hatuna haja ya katiba mpya. Lakini hali ikabadilika pale wazanzibari walipogoma mbele ya Samuel Sitta na kuchoma waraka ule moto kwa kudai suala la muundo wa muungano lazima lijadiliwe.

Sasa Jaji warioba analaumiwa kwa lipi? Tume yake imekoosea wapi? Kwa kweli kwa hili, CCM na viongozi wake wanaionea tu tume, wanatafuta mahali pa kusukumia lawama, basi. Na ipo siku wananchi amba leo hawaoni hili, watakuja ona ukweli upo wapi, kwani historia ndio inaandikwa...


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Dogo1, Tetty, Kobello, Nguruvi3, Ritz

Mapendekezo ya CCM kuhusu rasimu ya pili ya Katiba pamoja na mchanganuo wa kero zilizopo ndani ya muungano na tiba zake yaliwasilishwa na Asha Migiro kwenye kikao cha NEC mwishoni mwa mwezi February, 2014. Wanaopinga hili waje hapa kutueleza vinginevyo.......

...... Sasa Jaji warioba analaumiwa kwa lipi? Tume yake imekoosea wapi? Kwa kweli kwa hili, CCM na viongozi wake wanaionea tu tume, wanatafuta mahali pa kusukumia lawama, basi. Na ipo siku wananchi amba leo hawaoni hili, watakuja ona ukweli upo wapi, kwani historia ndio inaandikwa...


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
CCM, CDM, CUF na taasisi nyingine ndani ya vikao vyao kuna mambo mengi yaliyopendekezwa na tume zao za ndani kuhusu masuala mengi tu. Hii haimaanishi kuwa hayo ndiyo maoni yao ya mwisho, bali it's just a bluprint that can be fine-tuned before being executed. Na isitumiwe kama ndiyo sheria ya mwisho bali ni muelekeo tu unaoweza kubadilishwa. Hata rasimu ya pili ya tume ya warioba bado ina mambo mengi tu yasiyoweza kutekelezeka.

Kuhusu kosa la Warioba, ni lazima ukubali kuwa,"NOT TO DECIDE, IS TO DECIDE".

asilimia 80 ya waliotoa maoni hawakuzungumzia suala la muungano, je hii inamaanisha nini?

1.They are okay with the status quo.
2. They don't care about the form of union be it federal,unitary or confederal.

Huwezi kusema kuwa asilimia 80 isijaliwe, bali tujali wale tu waliotoa maoni kuhusu muungano. That will be wrong.
Kwa hiyo ndiyo maana CCM inasema kuwa kuna kundi kubwa ambalo halitaona tabu kama muungano utabaki kuwa wa serikali mbili.
 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote,kwa sababu moja kubwa walioko kwenye madaraka wanaogopa kuwepo kwa serikali tatu kwa sababu ya kuwajibika mbele ya umma wa watanzania tofauti na katiba ya sasa.

Nina sema hivyo kwa sababu moja kubwa haiingii kwenye akili ya kawaida ya binadamu pale Rais anapotetea MBUNGE abaki tu bungeni sababu umri wake una ruhusu,hivi hao waliokaa madarakani/bungeni kwa miaka arobaini au zaidi wameliletea taifa na majimbo yao maendeleo yapi ambayo mtanzania wa kawaida atayaona.Tumeona Majimbo mengi au yote ni masikini mno na haya yote yapo chini ya wabunge wa chama tawala na siyo kwa miaka miwili au mitatu bali kwa miaka mingi mengine toka uhuru yaani miaka hamsini yapo chini ya chama tawala na ni bado masikini,je hili nalo wananchi kulisema ni wajinga?AU tumeonekana watanzania hatuna elimu na ujuzi wa kujua nini tunataka bali kiongoi tu ndiye anayeweza kutuamulia nini tunahitaji na kwa wakati gani?

Sababu nyingine wanaogopa pale haki itakapochukua mkondo wake wengi wataishia kushtakiwa au kufunguliwa mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi walizoshika,ubadhirifu,rushwa,ufisadi na uuzaji holela wa raslimali za Taifa.

Na nyingine wengi wao wanataka kugombea URAIS sasa ni namna gani kukubalika kwenye chama basi wanatumia nafasi zao bila kujali Taifa letu linamisuguano kwa kiasi gani.

Sidhani kama kuendelea kuipa Zanzibar haki zote za kuwa NCHI kamili ndiyo kutaweza kuudumisha muungano ninadhani kutauua haraka zaidi kuliko kuudumisha.

Wanasema Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.Walizoea kuipa Zanzibar kila wakitakacho wasitegemee siku wakipata sarafu yao,bank kuu yao na kupata kiti kwenye UN ndiyo muungano utakuwepo,tutakuwa tunalipia gharama nyingi zaidi kwenye muungano huu na mwisho wa siku ukavunjika kwa msuguano mkubwa zaidi.

Sielewi,lakini nina uhakika vijana mlio ndani ya chungu (CCM) ndiyo wenye uwezo wakuinusuru nchi kwa sasa,sababu wapinzani wanadharaulika na kuonekana hawafai mbele ya jamii.Na sichelei kusema hili litawezekana tu kama kutakuwa na UZALENDO kwa vijana zaidi ya itikadi.

Na mwisho naweza kukubaliana na betlehem njia ya kuinusuru Tanzania ni kuwa na umoja wa vijana wa Tanzania usioangalia itikadi ya mtu ili kuleta Taifa pamoja.
 
Kuhusu kosa la Warioba, ni lazima ukubali kuwa,"NOT TO DECIDE, IS TO DECIDE".

asilimia 80 ya waliotoa maoni hawakuzungumzia suala la muungano, je hii inamaanisha nini?

1.They are okay with the status quo.
2. They don't care about the form of union be it federal,unitary or confederal.

Huwezi kusema kuwa asilimia 80 isijaliwe, bali tujali wale tu waliotoa maoni kuhusu muungano. That will be wrong.
Kwa hiyo ndiyo maana CCM inasema kuwa kuna kundi kubwa ambalo halitaona tabu kama muungano utabaki kuwa wa serikali mbili.

Zipo rekodi ndani ya tume jinsi gani watu wengi walikuwa wanataka kutoa mapendekezo ya muundo wa muungano lakini tume ikawa inawazuia kwa hoja kwamba wenzenu hapa wameshaliadili, toeni maoni kwa mambo mengine mapya au ambayo hayajaguswa na wengi. Muda ukifika, tutaziona tu hizi video clips.

Vinginevyo huko nyuma nilikueleza jinsi gani based on mathematics of probability, takwimu za tume zipo sawa. Ukipata muda rejea kule kwani haukunijibu.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
mm nilitamani sana kuwaona akina s2 kuja kujenga hoja jinsi gani s2 itavyoboresha muungano. na kuonyesha jinsi gani hayo matatizo ulioyaeleza kua si ttz wala si tishio la kuvunjika muungano.

kina Nape, bwana mwigulu na wengine njooni tujifunze elimu dunia
 
Zipo rekodi ndani ya tume jinsi gani watu wengi walikuwa wanataka kutoa mapendekezo ya muundo wa muungano lakini tume ikawa inawazuia kwa hoja kwamba wenzenu hapa wameshaliadili, toeni maoni kwa mambo mengine mapya au ambayo hayajaguswa na wengi. Muda ukifika, tutaziona tu hizi video clips.

Vinginevyo huko nyuma nilikueleza jinsi gani based on mathematics of probability, takwimu za tume zipo sawa. Ukipata muda rejea kule kwani haukunijibu.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Sasa mkuu, hilo ni kosa la tume ambayo unasema haina makosa au serikali au CCM?
Maana unasema huoni kosa la tume wakati huohuo unaishutumu kwa kuwabana watoa mawazo .... sasa tukuelewe vipi? Kwamba labda kulikuwa na watu wengi waliotaka kuunga mkiono serikali moja wakazuiwa au?

Ili tusiende mbali sana, mimi nimeangalia post nyingi sana kuhusu muundo wa serikali za muungano na sijaona mtu yeyoite aliyekuja na kutuelezea uhalali wa kutokuhusisha asilimia 80 ya wasiotoa maoni kuhusu muungano, labda ungenipa link ila nitajaribu kuitafuta.
All in all, kuna propaganda nyingi mno humu JF ambazo msingi wake kwa kweli hata siuelewi na mara nyingi nikitaka kuuliza undani wake, majibu huwa mafupi na sometimes ni kama mtu unalazimishwa ukubaliane na maelezo ya watu fulani hata kama basis ya maelezo hayo haieleweki.

Kwa mfano, sijasikia bungeni CCM wakija na hoja ya bunge la Tanzania bara/tanganyika, sijasikia kuhusu zanzibar kupewa kiti UN,
Sijasikia rais Kikwete akisema jeshi litachukua nchi kama kutakuwa na serikali tatu, ila labda kuna goals zinazotakiwa kuwa reached and im standing on the way. Sijasikia wala kuona mahali popote takwimu za tume ya Warioba zikiwajumuisha watanzania ambao hawakutoa maoni yao kuhusu muundo wa muungano na maelezo kwanini wasijumuishwe.
 
Sasa mkuu, hilo ni kosa la tume ambayo unasema haina makosa au serikali au CCM?
Maana unasema huoni kosa la tume wakati huohuo unaishutumu kwa kuwabana watoa mawazo .... sasa tukuelewe vipi? Kwamba labda kulikuwa na watu wengi waliotaka kuunga mkiono serikali moja wakazuiwa au?

Sioni kwanini makada wa ccm wanasema warioba kaja na mawazo yake juu ya muundo wa muungano, na kwamba maoni hayo yatavunja muungano. Awali nimeku "cc" juu ya jinsi gani suala la muundo wa muungano liliingia katika muswada husika, tena way before tume haijaanza kazi kukusanya maoni.

Pia nimejadili kwanini nadhani mapendekezo ya ccm juu ya rasimu ya pili ya katiba ni hatari zaidi kwa muungano kuliko mapendekezo ya tume. Ilitakiwa uje na counter arguments on that.

Kuhusu suala la tume kuzuia maoni ya wananchi, ilikuwa yale ya serikali tatu ambayo yalikuwa yanajirudia rudia. Nia ilikuwa sio kukandamiza wananchi bali kutoa fursa kwa wengine kutoa maoni juu ya maeneo menginr ya katiba. Lakini kwa vile ushahidi upo, compilation ikifanyika, ushahidi utawekwa wazi. Najua wewe ni mfuasi wa serikali moja, tusubiri muda ukifika tutaona ushahidi.

Ila angalizo tu: state unayoishi, iwapo kila kitu kikiendeshwa na federal government/central government, pangekalika hapo?

Ili tusiende mbali sana, mimi nimeangalia post nyingi sana kuhusu muundo wa serikali za muungano na sijaona mtu yeyoite aliyekuja na kutuelezea uhalali wa kutokuhusisha asilimia 80 ya wasiotoa maoni kuhusu muungano, labda ungenipa link ila nitajaribu kuitafuta.
All in all, kuna propaganda nyingi mno humu JF ambazo msingi wake kwa kweli hata siuelewi na mara nyingi nikitaka kuuliza undani wake, majibu huwa mafupi na sometimes ni kama mtu unalazimishwa ukubaliane na maelezo ya watu fulani hata kama basis ya maelezo hayo haieleweki.

This is commentary, na sioni cha kujibu hapa zaidi ya kuheshimu maoni yako. Vinginevyo as an intellectual, you have to know of your role katika jamii yetu hii ambayo wengi hawajaliwa uelewa. Unaisha taifa la waelewa walio wengi, ilitarajiwa uwaongoze wenzako nchini. Ni hilo tu ndio tunalofanya wenzako. Sasa kama hatueleweki, nia yetu sio kutafuta majority. Hata kwa mungu, "one is majority".

Kwa mfano, sijasikia bungeni CCM wakija na hoja ya bunge la Tanzania bara/tanganyika, sijasikia kuhusu zanzibar kupewa kiti UN,
Sijasikia rais Kikwete akisema jeshi litachukua nchi kama kutakuwa na serikali tatu, ila labda kuna goals zinazotakiwa kuwa reached and im standing on the way.
Nimeshaeleza source yangu juu ya hili ni nini. Subiri uone mchakato utakavyo hitimishwa bungeni then tutarudi kukumbushana juu ya suala hili.

Sijasikia wala kuona mahali popote takwimu za tume ya Warioba zikiwajumuisha watanzania ambao hawakutoa maoni yao kuhusu muundo wa muungano na maelezo kwanini wasijumuishwe.

Nimeshajadiliana na wewe hili hapa and elsewhere. Cha ajabu ni kwamba huwa haunirudi na hoja mbadala, lakini once you show up, unauliza swali lile lile.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kama serikali ya CCM imepanga haya na ndiyo msimamo wao sasa kulikuwa na haja gani taifa kuingia gharama na matumizi mabaya ya pesa zetu, mfano kiasi cha Sh8.2 bilioni zimetumika kafanya ukatabati wa bunge, bado gharama za tume ya katiba na malipo ya posho za wajumbe.
CCM walipanga kuingilia mchakato wakati wa kukusanya maoni, kuiingilia tume ili mambo yote yawe'safi' kuanzia mwanzo. Waligonga mwamba na matokeo yake ndio haya

Ninachotaka nikuhakikishie ni kuwa siyo CCM wote, ni kundi la CCM lenye nguvu sana kifedha, kiushawishi na kimadaraka.
Hili limewachukua mateka wana CCM. Kuna wana CCM wananung'unika sana. Wabunge wa CCM wengi wao ni mateka ya kundi hilo. Hivyo ni kundi si CCM yote, lkundi hilo lina nguvu.

Limechukua mateka wabunge wa CCM bara, wale wa znz walipofika bandarini wakachaukuliwa mateka'kuufyata'

CCM hiyo hiyo inalalamikia gharama za UKAWA, imesahau kuwa kuna gharama za mchakato mzima ambazo ni mabilioni ya fedha, leo CCM hao hao hawataki matokeo wanataka kuingiza rasimu yao ya porini.
 
CCM imeshajipalia mkaa usioisha milele.Obvious should be so considered. Uongo uongo wa kipuuzi hautawasaidia hata hao wabunge njaa wanaoamini watakosa Ubunge. Kwani Ubunge ni taaluma?Wakasome wapate taaluma na sio vijineneo vusivyokuwa na mashiko.
 
Sioni kwanini makada wa ccm wanasema warioba kaja na mawazo yake juu ya muundo wa muungano, na kwamba maoni hayo yatavunja muungano. Awali nimeku "cc" juu ya jinsi gani suala la muundo wa muungano liliingia katika muswada husika, tena way before tume haijaanza kazi kukusanya maoni.

Pia nimejadili kwanini nadhani mapendekezo ya ccm juu ya rasimu ya pili ya katiba ni hatari zaidi kwa muungano kuliko mapendekezo ya tume. Ilitakiwa uje na counter arguments on that.

Kuhusu suala la tume kuzuia maoni ya wananchi, ilikuwa yale ya serikali tatu ambayo yalikuwa yanajirudia rudia. Nia ilikuwa sio kukandamiza wananchi bali kutoa fursa kwa wengine kutoa maoni juu ya maeneo menginr ya katiba. Lakini kwa vile ushahidi upo, compilation ikifanyika, ushahidi utawekwa wazi. Najua wewe ni mfuasi wa serikali moja, tusubiri muda ukifika tutaona ushahidi.

Ila angalizo tu: state unayoishi, iwapo kila kitu kikiendeshwa na federal government/central government, pangekalika hapo?



This is commentary, na sioni cha kujibu hapa zaidi ya kuheshimu maoni yako. Vinginevyo as an intellectual, you have to know of your role katika jamii yetu hii ambayo wengi hawajaliwa uelewa. Unaisha taifa la waelewa walio wengi, ilitarajiwa uwaongoze wenzako nchini. Ni hilo tu ndio tunalofanya wenzako. Sasa kama hatueleweki, nia yetu sio kutafuta majority. Hata kwa mungu, "one is majority".
1. Kuhusu kwanini makada wengi wa CCM wanasema Warioba kaja na mawazo yake, nadhani kama ungetuelezea kwa kifupi hapahapa, sasa hivi kwanini tume imesema asilimia 80 ya waliotoa maoni yao hawakuzungumzia muungano na kundi hili tulipe category gani? ... Je walitaka status quo au liwalo na liwe (which includes status quo)? Hapo ndiyo CCM wanapopata hoja kwa ku-base kwenye asilimia 86 ya watanzania ambao hawatojali iwapo status quo itendelea, versus 14 percent wanaotaka changes.
Ndiyo maana nikakuuliza maoni yako kuhusu hawa 80% na wewe ukani-brush off. Just say it right here, tuwaweke wapi?

2. Kuhusu majibu yako kuwa wengi waliozuiwa walitaka serikali tatu, kwanini tume isiwaorodheshe hao katika ile asilimia 14? Huoni kuwa hapo ni wewe unayeituhumu tume kuja na wrong numbers, only kwa sababu upo the other side?? Yaani ndugu yangu unataka kuniambia huoni jinsi unavyoituhumu tume ya Warioba kimaandishi kabisa, na kusema una videotape inayoonyesha jinsi walivyochakachua? CCM wamebase on produced numbers, wewe umebase on what?

3.Is it? Kama ni commentary why don't you comment ili tuone unapoiweka hiyo asilimia 80, just put it in short. It ain't gonna cost you but a few mins. I just wanna see where you stand on this 80% stuff.

4.State ninayoishi, iwapo Feds wangerun kila kitu sioni kwanini pasikalike. The Feds here are freaking organized to the point that they know im on JF right now. They can do it easily as long as people give them the right to. Labda unataka kutuonyesha kuwa Federation is beeter that unitary government. Hii kitu ipo very subjected my friend.
Congo is Federated and France is Unitary ..... u tell me who's doing better! lol.
 
1. Kuhusu kwanini makada wengi wa CCM wanasema Warioba kaja na mawazo yake, nadhani kama ungetuelezea kwa kifupi hapahapa, sasa hivi kwanini tume imesema asilimia 80 ya waliotoa maoni yao hawakuzungumzia muungano na kundi hili tulipe category gani? ... Je walitaka status quo au liwalo na liwe (which includes status quo)? Hapo ndiyo CCM wanapopata hoja kwa ku-base kwenye asilimia 86 ya watanzania ambao hawatojali iwapo status quo itendelea, versus 14 percent wanaotaka changes.
Ndiyo maana nikakuuliza maoni yako kuhusu hawa 80% na wewe ukani-brush off. Just say it right here, tuwaweke wapi?

2. Kuhusu majibu yako kuwa wengi waliozuiwa walitaka serikali tatu, kwanini tume isiwaorodheshe hao katika ile asilimia 14? Huoni kuwa hapo ni wewe unayeituhumu tume kuja na wrong numbers, only kwa sababu upo the other side?? Yaani ndugu yangu unataka kuniambia huoni jinsi unavyoituhumu tume ya Warioba kimaandishi kabisa, na kusema una videotape inayoonyesha jinsi walivyochakachua? CCM wamebase on produced numbers, wewe umebase on what?

3.Is it? Kama ni commentary why don't you comment ili tuone unapoiweka hiyo asilimia 80, just put it in short. It ain't gonna cost you but a few mins. I just wanna see where you stand on this 80% stuff.

4.State ninayoishi, iwapo Feds wangerun kila kitu sioni kwanini pasikalike. The Feds here are freaking organized to the point that they know im on JF right now. They can do it easily as long as people give them the right to. Labda unataka kutuonyesha kuwa Federation is beeter that unitary government. Hii kitu ipo very subjected my friend.
Congo is Federated and France is Unitary ..... u tell me who's doing better! lol.

Unahamisha mjadala kwa makusudi kabisa lakini sio ajabu kwani ulianza hivyo miaka miwili iliyopita na uzi wangu kuhusu kiini macho cha muungano. Maswali yako yote hayo nilishatoa majibu. Kwa sasa ngoja nijikite zaidi kwenye hoja juu ya mapendekezo ya rasimu ya ccm, nikilenga hasa kujadili, je serikali mbili zitaboreshwa muungano? Wewe ni muumini wa serikali moja, so in a way you are an outlier. Nitazirudia hoja zako hapo juu kama marudio tu ya hoja zangu kwako. Nikichelewa sana nikumbushe tena.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom