CCM, Serikali Mbili Zilizoboreshwa, na Hatima Ya Muungano

CCM, Serikali Mbili Zilizoboreshwa, na Hatima Ya Muungano

Unahamisha mjadala kwa makusudi kabisa lakini sio ajabu kwani ulianza hivyo miaka miwili iliyopita na uzi wangu kuhusu kiini macho cha muungano. Maswali yako yote hayo nilishatoa majibu. Kwa sasa ngoja nijikite zaidi kwenye hoja juu ya mapendekezo ya rasimu ya ccm, nikilenga hasa kujadili, je serikali mbili zitaboreshwa muungano? Wewe ni muumini wa serikali moja, so in a way you are an outlier. Nitazirudia hoja zako hapo juu kama marudio tu ya hoja zangu kwako. Nikichelewa sana nikumbushe tena.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Nitakukumbusha, nimekujibu maswali uliyouliza sikuwa na nia ya kuuhamisha mjadala. Ila kuhusu asilimia 80 nitataka jibu lake, kwa sababu nimekupa majibu ila wew hujanipa majibu.

Umeeleza kwa kirefu, lakini kuna uwalakini.
 
Nitakukumbusha, nimekujibu maswali uliyouliza sikuwa na nia ya kuuhamisha mjadala. Ila kuhusu asilimia 80 nitataka jibu lake, kwa sababu nimekupa majibu ila wew hujanipa majibu.

Umeeleza kwa kirefu, lakini kuna uwalakini.

Mkuu Kobello,

Ebu tuanze na 80pct. Tueleze mantiki yake ipo wapi ili tuwe na terms of reference kabla hatujaingia kwenye mjadala wake. Eleza yote uliyonayo juu ya hii magic number "80".


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
1.

4.State ninayoishi, iwapo Feds wangerun kila kitu sioni kwanini pasikalike. The Feds here are freaking organized to the point that they know im on JF right now. They can do it easily as long as people give them the right to. Labda unataka kutuonyesha kuwa Federation is beeter that unitary government. Hii kitu ipo very subjected my friend.
Congo is Federated and France is Unitary ..... u tell me who's doing better! lol.

Kuhusu suala la feds kuwa all over your "cyber space" haijibu hoja. Kama wewe haujui kwanini umechagua kuishi state "A" and not "B", wenzako walio wengi wanajua kwanini. Hata sisi tulioishi huko kwa muda before 9/11, pia tulijua kwanini state A was a better place for us than the rest kwa muda fulani, then later, state "X". This is because we were "voting with our feet". Tafiti maana ya maneno haya.

Kuhusu ufaransa kuwa unitary but its stable, basi haujui nini kinaendelea in europe at present. Niishie hapa on this one, ntalirudia baadae. Congo ni mfano "bogus", hakuna constitutionalism in the DRC. Let's reserve these trial issues fr later, tujadili takwimu za tume.




Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Alinda, nikiri kwamba sikulifikiria hili. Nadhani majibu uliyotoa ndio uhalisia wenyewe.
Nashukuru kwa angalizo hili muhimu.



Nadhani chini ya mfumo wa sasa ambao ccm lazima wataendelea kuupigia chapuo ni kwamba - mshindi atakuwa ni yule mwenye simple majority katika jumla ya kura za zanzibar na Tanzania bara. Kwa maana hii, mshindi wa urais atakuwa yule atakayepata hata 50.01 percent ya kura zote, bila ya kutenganisha kura zilizopigwa Zanzibar na zile zilizopigwa Tanzania Bara.

Nadhani wenye uelewa zaidi wa mambo haya watatusaidia kutuelimisha humu.


Vinginevyo kama ulivyosema, mkorogo ni mkubwa sana.
Nguruvi3, mag3, FJM, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, Ezekiel Maige, MwanaDiwani, Yericko Nyerere,


JokaKuu, Ritz, Pasco, Ben Saanane


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Ni kweli hii nayo habri nyingine. Kuna uwezekano mkubwa wa rais wa Muungano kupata kura chache sana zanzibar na hivyo kuonekana hakubaliki zanzibar. hili litakuwaje? Ikumbukwe kwamba zanzibar sio mkoa ni nchi kamili mshirika wa muungano. Hivyo ni lazima ionekane kwamba rais wa JMT anakubalika pande zote!
 
1. Zanzibar wasingesema wao ni “nchini kamili” ndani ya Muungano.”
Mkuu Mchambuzi, walichofanya Zanzibar ni haki na halali yao!, Zanzibar ni nchi kamili ndani ya JMT, ndio maana tumeuita muungano wetu ni muungano wa aina yake!.

2. Baraza la wawakilishi lisingepitisha azimio la kutaka mfumo wa serikali tatu.
Kificho alikanusha na hapa nilimsikia mimi mwenyewe kwa masikio yangu!. [h=3]Jaji Warioba Ni Muongo?!- BLW Halikupendekeza Serikali Tatu!, [/h]
3. BLW lisingeamuru sheria zote zinazotungwa na bunge la jamhuri ya muungano, kwanza zipate Baraka ya Baraza la Wawakilishi kabla hazijatumika Zanzibar.
Hili ni takwa la kikatiba na kisheria kwa mujibu wa Hati za Muungano, kuwa Bunge la JMT lina uwezo wa kutunga sheria zinazohusu mambo ya muungano tuu!. Bunge la JMT halina mamlaka ya kutunga sheria kwa mambo ambayo sio ya muungano!, chombo chenye mamlaka ya kutunga sheria kuhusu mambo ya Zanzibar, yasiyo ya muungano ni BLW!. Inapotokea bunge la JMT likatunga sheria ya jambo ambalo sio la muungano, lazima sheria hiyo ipitishwe na BLW ili kuwa legal mandate ya kutumika Zanzibar!.

4. Zanzibar isingemega vitu vya pamoja vya muungano - isingedai mamlaka kamili juu ya - mafuta na gesi asilia, elimu ya juu, posta mawasiliano, biashara za nje, ushuru wa bidhaa, takwimu, utafiti, ushirikiano wa kimataifa, leseni za viwanda, bandari, usafiri wa anga, polisi na usalama wa taifa.
Zanzibar haikumega bali imerejesha what was his rightiful things zilizoporwa na JMT bila Zanzibar kuwa consulted na kuridhia!. Kiukweli ni sisi bara ndio miaka yote tumekuwa waporaji wakuu wa haki za Zanzibar, kufikia kiwango cha wengi kudhani, kila inachokifanya bara ndio haki, sasa Zanzibar wanapodai haki zao, na kuzirejesha, tunataka kuzing'ang'ania!. Muungani ulikuwa na mambo 11!, hati ziliweka utaratibu bayana wa kuyaongeza au kuyapunguza, JMT haikufuata na badala yake ilipora hadi yamefika 27!.

5. Zanzibar isingedai kupewa bendera yake, wimbo wa taifa, vikosi vyake vya ulinzi na usalama, benki kuu yake, sarafu, mabalozi wake wa nje, na uraia wake.
What is bendera for?, hata mimi pale ofisi yangu ya PPR nina bendera mezani kwangu!, what is wimbo wake wa taifa?!, watu tuna nyimbo za tangu shule, makabila, familia, makanisani etc!, its not a big deal!, kama unawazungumzia hao wagambo wa JKU na KMKM, hata mimi kwangu ni amiri jeshi wa jeshi langu lenye askari mmoja!, saluti yake ni kunifungulia geti!, kama ni saluti tuu au vigora, huwa najipigia kigora cha honi getini kwangu!. Sarafu haikuwemo kwenye yale mambo 11!, hivyo tumepora!, whote hivyo ni nothing kama ka nchi kenyewe ni ka nchi ndani ya nchi!.

6. Tusingesikia viongozi wa BLW wakilalamika kwamba umaskini wa Zanzibar unatokana na mfumo wa muungano wa serikali mbili.
Haya ni malalamiko ya mbaazi tuu, zikikosa maua!.

Serikali Mbili zilizoboreshwa zitavunja muungano, na CCM wajiandae kutafunwa na dhambi ya kupinga mapendekezo ya tume ya katiba iliyoongozwa na Jaji Warioba. Tusemezane.
Mkuu Mchambuzi, hili ndilo kubwa, nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%, na hili nimelisemea hapa,
[h=3]Chonde Chonde JK: Msimamo wa CCM wa Serikali Mbili, Ndio Utakaovunja Muungano!. [/h]
Ila mimi mimi msimamo wangu ni serikali moja!. Kwa zana nilizoziona jana!, hawa jamaa zetu, wenzetu na jirani zetu wakikataa taifa moja, serikali moja chini ya rais mmoja na amiri jeshi mkuu, then, tuwahamishe kwa nguvu hao watu milioni moja!, tuvisawazishe tuu visiwa vile tujue moja!.
[h=3]Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then ...[/h]
Pasco.
 
Mkuu Mchambuzi, walichofanya Zanzibar ni haki na halali yao!, Zanzibar ni nchi kamili ndani ya JMT, ndio maana tumeuita muungano wetu ni muungano wa aina yake!.


Kificho alikanusha na hapa nilimsikia mimi mwenyewe kwa masikio yangu!. [h=3]Jaji Warioba Ni Muongo?!- BLW Halikupendekeza Serikali Tatu!, [/h]
Hili ni takwa la kikatiba na kisheria kwa mujibu wa Hati za Muungano, kuwa Bunge la JMT lina uwezo wa kutunga sheria zinazohusu mambo ya muungano tuu!. Bunge la JMT halina mamlaka ya kutunga sheria kwa mambo ambayo sio ya muungano!, chombo chenye mamlaka ya kutunga sheria kuhusu mambo ya Zanzibar, yasiyo ya muungano ni BLW!. Inapotokea bunge la JMT likatunga sheria ya jambo ambalo sio la muungano, lazima sheria hiyo ipitishwe na BLW ili kuwa legal mandate ya kutumika Zanzibar!.

Zanzibar haikumega bali imerejesha what was his rightiful things zilizoporwa na JMT bila Zanzibar kuwa consulted na kuridhia!. Kiukweli ni sisi bara ndio miaka yote tumekuwa waporaji wakuu wa haki za Zanzibar, kufikia kiwango cha wengi kudhani, kila inachokifanya bara ndio haki, sasa Zanzibar wanapodai haki zao, na kuzirejesha, tunataka kuzing'ang'ania!. Muungani ulikuwa na mambo 11!, hati ziliweka utaratibu bayana wa kuyaongeza au kuyapunguza, JMT haikufuata na badala yake ilipora hadi yamefika 27!.

What is bendera for?, hata mimi pale ofisi yangu ya PPR nina bendera mezani kwangu!, what is wimbo wake wa taifa?!, watu tuna nyimbo za tangu shule, makabila, familia, makanisani etc!, its not a big deal!, kama unawazungumzia hao wagambo wa JKU na KMKM, hata mimi kwangu ni amiri jeshi wa jeshi langu lenye askari mmoja!, saluti yake ni kunifungulia geti!, kama ni saluti tuu au vigora, huwa najipigia kigora cha honi getini kwangu!. Sarafu haikuwemo kwenye yale mambo 11!, hivyo tumepora!, whote hivyo ni nothing kama ka nchi kenyewe ni ka nchi ndani ya nchi!.

Haya ni malalamiko ya mbaazi tuu, zikikosa maua!.


Mkuu Mchambuzi, hili ndilo kubwa, nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%, na hili nimelisemea hapa,
[h=3]Chonde Chonde JK: Msimamo wa CCM wa Serikali Mbili, Ndio Utakaovunja Muungano!. [/h]
Ila mimi mimi msimamo wangu ni serikali moja!. Kwa zana nilizoziona jana!, hawa jamaa zetu, wenzetu na jirani zetu wakikataa taifa moja, serikali moja chini ya rais mmoja na amiri jeshi mkuu, then, tuwahamishe kwa nguvu hao watu milioni moja!, tuvisawazishe tuu visiwa vile tujue moja!.
[h=3]Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then ...[/h]
Pasco.

Mkuu pasco, kwanini mshirika mmoja wa muungano awe na haki za kikatiba lakini sio mshirika mwingine? Kwanini katiba ya mshirika mmoja iwe ni ile ya pamoja (Tanganyika/Muungano), halafu hapo hapo mshirika mwenza anakuwa na katiba yake tofauti? Chini ya mfumo mmoja wa chama haikuwa tatizo sana kwa vile legitimacy ya utawala wa ccm haikutokana na katiba bali azimio la arusha, mafanikio ya Tanu kutetea wanyonge, na uadilifu na uzalendo wa mwalimu, so mambo yakaenda ingawa not as smooth (rejea sakata la jumbe, G55). Times have changed, hizoo sources of legitimacy za ccm are long gone, kwa sababu ya ccm yenyewe. Uhalali wa kutawala sasa na katiba ya nchi, itokanayo na maoni ya wananchi wenyewe. Wamenena kupitia rasimu.

Hoja kuhusu znz kuwa na bendera, amiri jeshi mkuu, na pia vitisho kwa znz juu ya nguvu za kijeshi za bara, I will pass on that as "commentary".

Swali la msingi ni je - kati ya rasimu ya tume na rasimu mbadala ya ccm, ipi itaboresha na kudumisha muungano?

Hoja ya serikali moja ni sawa na kusema "hautaki muungano".


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Kobello,

Ebu tuanze na 80pct. Tueleze mantiki yake ipo wapi ili tuwe na terms of reference kabla hatujaingia kwenye mjadala wake. Eleza yote uliyonayo juu ya hii magic number "80".


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Watanzania waliotoa maoni yao kwa Tume kwa mdomo na maandishi walikuwa 351,664. Kati yao ni wananchi 47,820 au sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano hivyo wakauzungumzia. Wananchi 303,844 au sawa na asilimia 86.4 hawakuzungumzia muunganokabisa.

Kwanini hao ambao hawakuzungumzsia muungano maoni yao yasishirikishwe?? Mbona nilijieleza vizuri tu?
 
Kuhusu suala la feds kuwa all over your "cyber space" haijibu hoja. Kama wewe haujui kwanini umechagua kuishi state "A" and not "B", wenzako walio wengi wanajua kwanini. Hata sisi tulioishi huko kwa muda before 9/11, pia tulijua kwanini state A was a better place for us than the rest kwa muda fulani, then later, state "X". This is because we were "voting with our feet". Tafiti maana ya maneno haya.

Kuhusu ufaransa kuwa unitary but its stable, basi haujui nini kinaendelea in europe at present. Niishie hapa on this one, ntalirudia baadae. Congo ni mfano "bogus", hakuna constitutionalism in the DRC. Let's reserve these trial issues fr later, tujadili takwimu za tume.




Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Huo ni mfano wa kuonyesha jinsi walivyokuwa organized. Usi-twist maneno ili nionekane nimeandika kichekesho, huo ni msisitizo wa kuonyesha jamaa wana uwezo wa kufanya hivyo bila misukosuko, ili mradi ridhaa tu.
Sidhani kama kuna umuhimu wa mimi kutafiti "voting with our feet" ... hiyo ni termonology uliyoipenda tu ila najua unachomaanisha. Anyways, sijui hata kwanini uliniuliza swali hili ila tuyaache haya kwa sasa, turudi kwenye 80%.
 
Watanzania waliotoa maoni yao kwa Tume kwa mdomo na maandishi walikuwa 351,664. Kati yao ni wananchi 47,820 au sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano hivyo wakauzungumzia. Wananchi 303,844 au sawa na asilimia 86.4 hawakuzungumzia muunganokabisa.

Kwanini hao ambao hawakuzungumzsia muungano maoni yao yasishirikishwe?? Mbona nilijieleza vizuri tu?
Mkuu Kobello sidhani kama hapo kwenye blue ndio tafsiri sahihi ya takwimu za timu. Sio kweli waliozungumzia jambo flani ndo limewakera. Kila mtu alikua anachangia kwa utashi wake na eneo alilohitaji kulizungumzia.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kobello sidhani kama hapo kwenye blue ndio tafsiri sahihi ya takwimu za timu. Sio kweli waliozungumzia jambo flani ndo limewakera. Kila mtu alikua anachangia kwa utashi wake na eneo alilohitaji kulizungumzia.
Sawa,
Je ambao hawakuzungumzia muungano unawaweka kundi gani? Au huwahesabu kabisa?
 
Wana jamvi,

Chini ya Serikali mbili zitakazoboreshwa na CCM, yafuatayo hayatabadilika:

1. Zanzibar kuwa ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano. Hii ni kinyume cha katiba ya muungano (1977) ambayo CCM inasema inataka "iboresha".

2. Zanzibar imechukua madaraka ya muungano ikiwa ni pamoja na kuelekeza sheria zote zinazopitishwa na bunge la jamhuri ya muungano kwanza zipelekwe kwenye baraza la wawakilishi.

Now we have a double edged sword situation: upande wa kwanza - kwa Zanzibar ilipofika, haiwezi tena kurudi ilipotoka (pre - 2010 constitution); na upande wa pili, kuiacha Zanzibar kama ilivyo (post – 2010), chini ya kinachoitwa ni maboresho ya serikali mbli, maana yake ni kwamba Zanzibar sasa itakuwa juu ya Katiba ya jamhuri ya muungano.

Awali tulijadili juu ya mapendekezo ya CCM ya kuanzisha kwa Bunge la Tanzania Bara. Moja ya sababu za msingi za CCM kuja na pendekezo hili ni pamoja na kwamba – tumefikia mahali sasa tutakuwa na wabunge kutoka nchi jirani ya Zanziar kuja kutunga na kupitisha sheria kwa masuala ambayo sio ya muungano, na yasiyo wahusu. Huku hakuna tofauti na kukubali umuhimu wa serikali tatu.
Inawezekana CCM imetambua kwamba, muda sio mrefu, haitaingia akilini mwa wananchi wa Tanzania Bara pale watakapogundua kwamba - sheria zinazotungwa na wabunge wa Muungano, kumbe pia washiriki wa utunzi huo ni watu ambao sheria hizo haziwagusi na wala haziwahusu kwa namna yoyote ile. Kwa maana nyingine, wabunge wa Zanzibar wanashiriki katika utungaji sheria zisizohusu muungano (zenye impact kwa Tanzania Bara). Sasa iwapo CCM inaona tatizo hili, hivyo kulianzishia bunge lake,bunge hili litafanyaje kazi bila ya kuwa na serikali yake? This is a timing bomb for CCM.

Wakiwa "off record", viongozi wengi wa CCM wanakiri kwamba Katiba ya Zanzibar na ya Muungano imejaa migongano mingi sana ambayo suluhisho lake haliwezi kuletwa na serikali mbili zilizoboreshwa bali serikali tatu. Pamoja na kuona ukweli huu, wakiwa bungeni Dodoma, "wanaufyata". Wanaogoa kupoteza vyeo, wakidhania vyeo hivi ni ajira na fursa za kuendesha maisha yao wakati kimsingi, ubunge ni dhamana tu, hakuna lingine lolote.

Tukiendelea na hoja yetu juu ya mgongano baina ya katiba ya Muungano na Katiba ya Zanzibar:

Ibara ya (1) ya mkataba wa muungano (1964) ilianisha wazi kwamba Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar zitaungana na kuwa NCHI MOJA yenye MAMLAKA MOJA YA KIDOLA. Vile vile, ibara ya (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano (1977) inatamka kwamba Jamhuri ya Muungano ni NCHI MOJA. Wajumbe wa NEC wakikaa ndani kama chama, wanajadili kwa uwazi kabisa kwamba kwa katiba ya Zanzibar kutamka kwamba Zanzibar ni nchi, huku ni kukinzana na Katina ya JMT (1977) inayosema kwamba Jamhuri ya Muungani ni NCHI MOJA NA DOLA MOJA.

Wajumbe wa NEC (CCM), wakiwa ndani ya vikao vyao, wanakiri wazi kwamba – ibara ya (147) ya Katiba ya JMT imekataza mtu yeyote au shirika au kikundi chochote kuunda jeshi katika jamhuri ya muungano wa Tanzania, isipokuwa serikali (cc Pasco). Pamoja na mamlaka hayo kujulikana kwa mujibu wa sheria ndani ya Katiba ya Muungano, bado Zanzibar imejiundia majeshi yake ya ulinzi. In private, viongozi wengi wa CCM wanakiri wazi kabisa kwamba hii ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Tukiangalia kwa undani juu ya mgongano wa utungaji wa sheria, Zanzibar pia imenyofoa mamlaka ya muungano katika suala hilo (cc Pasco). In private, Viongozi wengi wa CCM wanakiri wazi kwamba ibara ya 64(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatoa mamlaka kwa Bunge la Muungano kutunga sheria ambazo zinaweza kutumika hadi Zanzibar. Lakini Katiba ya Zanzibar kupitia ibara ya 132(1), inaweka masharti ya kutumika sheria iliyotungwa na bunge la muungano na kutamka kwamba sheria hiyo iwe ni kwa ajili ya mambo ya muungano pekee, na sio vinginevyo. Katika ufafanuzi wake, ibara ya 132 (2) ya Katiba ya Zanzibar inafafanua kwamba sheria hiyo lazima ipelekwe kwenye baraza la wawakilishi na waziri anayehusika.

Pia upo mgongano unaohusu mahakama ya rufani ya Jamhuri ya Muungano. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, hii ni mahakama yenye uwezo wa kuamua rufaa zote nchini – Tanzania Bara na Zanzibar. Lakini tukiangalia kwa upande wa Zanzibar - masuala yote yanayohusiana na dini ya kislamu ambayo yanahusika na mahakama ya kadhi Zanzibar, na mambo mengine yote yaliyoainishwa katika katiba ya Zanzibar pamoja na sheria nyingine yeyote iliyotungwa na baraza la wawakilishi yanazuiwa kupelekwa kwenye mahakama ya rufaa na katiba ya sasa ya Zanzibar.

Pia upo mgongano juu ya mamlaka baina ya Rais wa Muungano na Yule wa Zanzibar. Tukiangalia ibara ya 2(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, ibara hii inampa rais wa muungano mamlaka ya kugawa mikoa nchini. Wakati huo huo, Katiba ya Zanzibar pia imetoa mamlaka kama hayo kwa Rais wa Zanzibar.

Vilevile, ibara ya 34 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano (1977), inaweka wazi masuala ambayo serikali ya muungano itakuwa na mamlaka nayo huku pia ikifafanua masuala ambayo serikali ya muungano ina mamlaka nayo. Lakini cha kushangaza, serikali ya muungano haikuweka wazi mipaka yake ni ipi; haikuweka ni wakati gani itasimamia mambo ya muungano, na wakati gani itasimamia mambo yasiyo ya muungano (yani ya Tanzania Bara). Hiki ndio kiini cha hoja kwamba Tanganyika imevaa koti la muungano, na kwamba Tanganyika inatumia mamlaka haya kujinufaisha yenyewe kwa gharama za Zanzibar.

Mengi ya matatizo haya ni mambo ya KISHERIA NA KIKATIBA. Suluhisho lake haliji kwa kukumbushana kwa maneno mazuri na matamu juu ya historia ya muungano wetu, au jinsi gani waasisi walivyojitolea kutuunganisha, au jinsi gani pande mbili za muungano zinavyoishi kwa pamoja. Badala yake, Suluhisho la haya yote lazima liwe ni la KISHERIA NA KIKATIBA.Basi! Iwapo kweli tuna nia ya dhati ya kulinda muungano, nasi ufumbuzi wa mattaizo haya ni kuzinduliwa kwa Serikali ya Tanganyika ili sasa kila upande wa muungano uwe na mamlaka kamili ya kujiendeshea mambo yake nje ya muungano, na kuchangia katika yale machache tu ya muungano kama rasimu ya katiba inavyopendekeza.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
 
Huo ni mfano wa kuonyesha jinsi walivyokuwa organized. Usi-twist maneno ili nionekane nimeandika kichekesho, huo ni msisitizo wa kuonyesha jamaa wana uwezo wa kufanya hivyo bila misukosuko, ili mradi ridhaa tu.
Sidhani kama kuna umuhimu wa mimi kutafiti "voting with our feet" ... hiyo ni termonology uliyoipenda tu ila najua unachomaanisha
. Anyways, sijui hata kwanini uliniuliza swali hili ila tuyaache haya kwa sasa, turudi kwenye 80%.

kama kuchekesha tayari umesha chekesha mkuu. ntakurudia punde na suala la takwimu za tume.
 
Sawa,
Je ambao hawakuzungumzia muungano unawaweka kundi gani? Au huwahesabu kabisa?

Mimi nawachukulia ni watu huru ambao hawakusukumwa au kuguswa kulizungumzia hilo. Ukitaka tuitimishe kwamba wao wameona muundo huu huko sawa na si kero kwao ndo maana hawakuuzungumzia utakua unadanganya nafsi na akili yako mkuu Kobello kwa tafsiri hiyo. Kwa tafsiri yako hiyo na tukiingia kuchambua kipengele kimoja kimoja italeta tafsiri ambayo hadi wewe mkuu utaikataa kwa mfano kwenye jedwali 16a katika Randama ya rasimu ya katiba (ukurasa wa 58) waliozungumzia haki za wanawake ni watu 5755 sawa na 5.4 ya waliochangia katika haki za binadamu kwa maana hiyo utatafsiri kwamba ni tupo katika kiwango kizuri cha usawa wa kijinsia ndo maana waliozungumzia hilo ni wachache. La pili ni hili linalotikisa Afrika la mahusiano ya kimwili ya jinsi moja ambalo limezungumziwa na watu 10,261. kwa hiyo inamaanisha waliobaki wameafiki mahusiano ndo maana hawajalizunguzia? Je hitimisho lako kwa muundo wa muungano litafanana na hayo mawili hapo? Mwisho naomba tafsiri ya takwimu kwa hayo baadhi hapo juu.
ttt.jpg
 
Last edited by a moderator:
Watanzania waliotoa maoni yao kwa Tume kwa mdomo na maandishi walikuwa 351,664. Kati yao ni wananchi 47,820 au sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano hivyo wakauzungumzia. Wananchi 303,844 au sawa na asilimia 86.4 hawakuzungumzia muunganokabisa.

Kwanini hao ambao hawakuzungumzsia muungano maoni yao yasishirikishwe?? Mbona nilijieleza vizuri tu?

Kwa vile umekubali to deal with the same datas et, tuanza mjadala juu ya hili:

Watanzania waliotoa maoni kuhusu haki za wanawake walikuwa ni takribani watanzania elfu tano (5,000). Wananchi elfu tano kati ya hao 351,664 ni sawa na 1.4%, ambao ndio waliokerwa na ukiukwaji wa haki za wanawake nchini, hivyo wakazizungumzia. Wananchi karibia 346, 000 au sawa na karibia 98% hawakuzungumzia kuhusu haki za wanawake kabisa!

kwanini hao ambao hawakuzungumzia haki za wanawake maoni yake yasishirikishwe kwa maana ya kwamba ukimyaa wao maana yake wanaona hali iliyopo ni sawa tu? Kwanini maoni ya 1.4% yapewe uzito na msiyajengee hoja ya 80%, lakini maoni ya 13.6% mnayajengea hoja ya 80%? kumbuka, we are dealing with the same dataset.
 
Mimi nawachukulia ni watu huru ambao hawakusukumwa au kuguswa kulizungumzia hilo. Ukitaka tuitimishe kwamba wao wameona muundo huu huko sawa na si kero kwao ndo maana hawakuuzungumzia utakua unadanganya nafsi na akili yako mkuu Kobello kwa tafsiri hiyo. Kwa tafsiri yako hiyo na tukiingia kuchambua kipengele kimoja kimoja italeta tafsiri ambayo hadi wewe mkuu utaikataa kwa mfano kwenye jedwali 16a katika Randama ya rasimu ya katiba (ukurasa wa 58) waliozungumzia haki za wanawake ni watu 5755 sawa na 5.4 ya waliochangia katika haki za binadamu kwa maana hiyo utatafsiri kwamba ni tupo katika kiwango kizuri cha usawa wa kijinsia ndo maana waliozungumzia hilo ni wachache. La pili ni hili linalotikisa Afrika la mahusiano ya kimwili ya jinsi moja ambalo limezungumziwa na watu 10,261. kwa hiyo inamaanisha waliobaki wameafiki mahusiano ndo maana hawajalizunguzia? Je hitimisho lako kwa muundo wa muungano litafanana na hayo mawili hapo? Mwisho naomba tafsiri ya takwimu kwa hayo baadhi hapo juu.
View attachment 154334
Afadhali wewe umeeleza jinsi unavyoona.
Katiba iliyop inatoa haki kwa hayo yote, kwa hiyo hata kama watu laki tatu na nusu wangepinga haki na usawa wa binadamu, suala la haki za binadamu siyo suala la kidemokrasia.
Hata hivyo, wananchi ambao walikaa kimya kuhusu hilo, walimaanisha kuwa kutokana na hali ilivyo, suala la haki za binadamu kwa Tanzania haliwakeri na li8meanishwa vizuri kwenye katiba. Usifananishe incidences za hapa na pale za uvunjwaji wa haki za binadamu na sheria zilizopo.
Sheria za Tanzania haziruhusu ushoga, kwa hiyo kukaa kwao kimya ni kuridhika na status quo.
cc. Mchambuzi
 
Last edited by a moderator:
Afadhali wewe umeeleza jinsi unavyoona.
Katiba iliyop inatoa haki kwa hayo yote, kwa hiyo hata kama watu laki tatu na nusu wangepinga haki na usawa wa binadamu, suala la haki za binadamu siyo suala la kidemokrasia.
Hata hivyo, wananchi ambao walikaa kimya kuhusu hilo, walimaanisha kuwa kutokana na hali ilivyo, suala la haki za binadamu kwa Tanzania haliwakeri na li8meanishwa vizuri kwenye katiba. Usifananishe incidences za hapa na pale za uvunjwaji wa haki za binadamu na sheria zilizopo.
Sheria za Tanzania haziruhusu ushoga, kwa hiyo kukaa kwao kimya ni kuridhika na status quo.

Asante kwa jibu linalo pwaya kupita maelezo. Nilijua tu kwa swali hilo, ambalo nimekujibu kwa logic ile ile uliyo present, utakimbia logic, utakimbia mathematics of probability na badala yake utakuja kwenye blah blah ambazo hazina any parameters, any analytical framework but just subjective views. I wanted us to focus on numbers because they don't lie, they don't have time for politics. Politics and manipulation by playful words ni suala la baadae.

Ngoja nijipange na mimi kisiasa and subjectively, nikiwa tayari ntakuja kujibu hoja yako ambayo nadhani wengi wanaona jinsi gani imefeli.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Asante kwa jibu linalo pwaya kupita maelezo. Nilijua tu kwa swali hilo, ambalo nimekujibu kwa logic ile ile uliyo present, utakimbia logic, utakimbia mathematics of probability na badala yake utakuja kwenye blah blah ambazo hazina any parameters, any analytical framework but just subjective views. I wanted us to focus on numbers because they don't lie, they don't have time for politics. Politics and manipulation by playful words ni suala la baadae.

Ngoja nijipange na mimi kisiasa and subjectively, nikiwa tayari ntakuja kujibu hoja yako ambayo nadhani wengi wanaona jinsi gani imefeli.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Umeamua tu kutoelewa. And I can even see the tone is changing. Nielezee kimahesabu kama unavyodai, hiyo asilimia 86 ina-represent nini?
Kimahesabu.
 
Mkuu pasco,
  1. kwanini mshirika mmoja wa muungano awe na haki za kikatiba lakini sio mshirika mwingine?
  2. Kwanini katiba ya mshirika mmoja iwe ni ile ya pamoja (Tanganyika/Muungano), halafu hapo hapo mshirika mwenza anakuwa na katiba yake tofauti?
  3. Swali la msingi ni je - kati ya rasimu ya tume na rasimu mbadala ya ccm, ipi itaboresha na kudumisha muungano?

Hoja ya serikali moja ni sawa na kusema "hautaki muungano".

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mkuu Mchambuzi,

1. Kabla ya muungano ndipo kulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Uguja, baada ya muungano, nchi hizi mbili ziliungana zikawa moja Tanzania, hakuna tena nchi ya Tanganyika, wala hakuna tena nchi ya Zanzibar, zote zilikufa, hivyo hakuna mshirika yoyote!. Ila Tanzani hii kwa ridhaa yake, yenyewe, ilikubali kumpa mamlaka ya ndani sehemu ya nchi hiyo, iitwayo Zanzibar!, mpaka leo, mpaka kesho, Nchi ya Tanzania ni moja tuu, hakuna nchi ya Zanzibar, bali Zanzibar kiukweli ni semu ya Tanzania!. Hivi wewe na mkeo, watu wote wanawajua mu mke na mume, mkatofautiana kidogo na mkeo, akaamua kujipa talaka, akaiandika na kuibandika kabatini kwenu, kila ukifungua mlango wa kabati, unaiona hiyo talaka, utakwenda kulalamika nje eti mke wangu kanipa talaka?. Ili si ni talaka ya kujifurahisha tuu huyo mkeo, mbele ya macho ya umma, wewe na mkeo ni mtu na mkewe!.
2.Hivyo ndivyo ilivyo katiba ya Zanzibar, hata wakijiita nchi, wakapiga na tarumbeta na kupaaza saiuti ati sisi nchi, Tanzania tuliona tangu matayarisho, marekebisho na hadi kuipitisha, tumejinyamazia kimya, kwa sababu huko kote ni kujifurahisha!, hata wewe, kama ni kweli unampenda mkeo, na kuna vitu anavihitaji sana ili kujifurahishia, wimbo, bendera, migambo, saluti, na hiyo katiba ya mwisho chumbani, kwa nini usimwachie afurahi?!. Katiba kweli ya nchi ni ile ya JMT tuu!, ile ya Zanzibar sio katiba ya nchi, bali ni katiba ya nchi jina tuu ambalo ni sehemu ya JMT!. Kwa vile hakuna mshirika bali sehemu ya JMT, Katiba ya JMT ndio katiba moja tuu, ile ya kijaluba cha mkeo, itakukosesaje usingizi!.

3.So far rasimu bado ni moja tuu, ile ya serikali tatu, ila maoni ya walio wengi ndio wanaotaka serikali mbili, muungano utadumishwa kwa serikali moja!.

Mtu akiisha achana na baba yake na mama yake na kuandamana na mkewe, watu hawa huma mwili mmoja!.

Pasco.
 
Kuna hatari moja kubwa ambayo CCM hawaioni kwa rasimu yao. Wabunge wa bunge la bara(a.k.a Tanganyika) watakapokaa wenyewe, watajiuliza maswali.
Nani anawasikiliza, bunge lao liendeshwe kwa utaratibu gani na maoni yao yafanyiwe kazi na nani.

Wztabaini kuwa wao ni Watanganyika kwanza kabla ya Tanzania.
Watakapokwenda kukutana na wa znz ndani ya bunge la Tanzania, watakuwa wamejihisi ni mayatima wasiyo na mlezi.

Nguvu zao zitakuwa kubwa sana kwasababu watawaangalia wznz kama wale, nao kama sisi. Tatizo ni kuwa chuki itajengeka kimya kimya na kutakuwa na kukwamishana kiaina.

Mfano mzuri ni ule wa Passport za kuingia znz.
Huko nyuma Watanganyika walilazimika kubeba passport kuingia znz.

Hilo lilizua chuki kwanini wao wasije na passport. Malalamiko yakawa makubwa na siku yalipoibuka bungeni ilikuwa ni azimio moja, waje na passport kama hawaondoi hali hiyo.

Kwa nyakati hizo akina Nyerere walikuwa na busara. Walijua huo ndio mwanzo wa kuligawa taifa kuelekea kifo cha muungano. Wakaingilia kati na kusema znz ifute, na ikawa.

Chuki ya passport ikabaki kama kovu, tunaita 'antigen' kwa maana kuwa Tanganyika ilishakuwa exposed na hivyo kuanza kujenga immunity dhidi ya znz.

Lilipokuja suala la OIC Watanganyika waka react haraka sana kwasababu tayari walishakuwa sensitive na znz.

Ili kuondoa tatizo hilo la 'sensitivity' tume tya Warioba ikasema Tanganyika ijitambue na znz ijitambue. Hapo hakuna sensitivity yoyote na wala hakuna atakayejenga immune dhidi ya mwingine. Kwamba jambo hilo lirasimishwe.

Lakini pia wabunge wa znz watakuwa sensitive kuwa wenzao waliobaki kujadili mambo yasiyo ya muungano pengine wana njama dhidi yao.

Kwa kuzingatia uchache wa 'watalii hao wa visiwani' na upungufu wa mambo ya kuzungumzia ndani ya bunge la JMT, nao watakuwa na hisia za kuonewa hata penye haki.

Again, ili kuondoa inferiority complex inayoweza kuwapa wabunge wa nchi jirani ya znz wawapo Dodoma kwa utalii, tume ya Warioba ikasema kila upande uwe na bunge lake, ukaweka wazi mambo 7 tu ya kuzungumzia.

In other words. tume ya Warioba imeweka agenda ya kuwakutanisha wznz na Watanganyika.

Hii rasimu CCM mafichoni, haielezi mambo gani ya muungano na yapi si ya muungano.
Hilo tu ni dalili njema ya failure ya rasimu hata kabla ya kujadiliwa.

Na kushindwa kwake ni pale wabunge wa Tanganyika watakApojitambua kuwa Tanganyika yao ndiyo imebeba mzigo wote lakini hawana mahala pa kuzunguzia fadhila na udhia wa mzigo wa muungano. Hawana serikali wala chombo kingine cha kisheria.

Ili bunge la Tanganyika lifanye kazi kwa sheria lazima kutakuwa na mwanasheria mkuu.
Huyo atatoka wapi? Atatoka katika muungano? Na kama ni huko koti linalotakiwa livuliwe Tanganyika litawezekana?

Nimalizie kwa kusema kuwa, rasimu ya mafichoni ya CCM haisemi mambo yapi ya muungano na yapi yasiyo kwasababu kuu moja.
Kutenga mambo hayo ni kuhalalisha uwepo wa Tanganyika na serikali yake, jambo wasilolitaka.

Labda CCM warudie katika drawing board watueleze, S3 zinaepukika vipi kwa hoja tunazoulizia?
Huu ni uchambuzi mzuri, wa kwako na wa wengine humu, ambao nitausemea kwa pamoja. Mna mapungufu. Kwanza, CCM hawana rasimu nyingine. Nimepitia mapendekezo yao yote tangu wakati wa rasimu ya kwanza (wameshakuwa na version 4), nao wanatafuta majibu tu kama sisi. Ukiacha muundo wa serikali, hawapingi mapendekezo ya Tume katika mambo muhimu km kufumua Tume ya Uchaguzi, kupanua haki za binadamu, kuwa na mgombea binafsi, kuondoa madaraka ya Rais kuteua viongozi wakuu peke yake, kuwa na vyombo huru vya uwajibikaji, nk. Pili, CCM hawana hodhi ya mawazo ya serikali 2; wako wengine wengi ila hawaongei majukwaani au majamvini. Tatu, Rais wa Tanzania hawezi kuwa wa kwanza ki-itifaki katika sherehe za mapinduzi. Iko hivyo toka 1964. Nne, kumkataa Rais wa Z'bar kuwa Makamo wa Rais wa Jamhuri kwenye mfumo wa vyama vingi lilijadilkwa toka 1992 hadi 1995 lilipopitishwa na Bunge (kwa theluthi mbili za pande zote mbili) kwa sababu Rais wa Zanzibar huchaguliwa na watu wachache mno. Ndiyo maana akakubalika mgombea mwenza, maana anagombea nchi nzima akiwa na mwenza wake ambaye ni mgombea Urais. Hili linawapa Wanzibari viongozi wengi zaidi wa juu kuliko zamani. Tano, kutangaza Zanzibar kuwa ni nchi haikutupendeza wengi, lakini si lazima iwe na maana kuwa ni nchi ya nje ya Muungano. Yaweza kuwa nchi ndani ya nchi nyingine, na kwa mataifa ya nje ikatambulika ile nchi kubwa tu. Sita, sina jibu kwa wazo la kuiita Z'bar nchi ya jirani!
 
Afadhali wewe umeeleza jinsi unavyoona.
Katiba iliyop inatoa haki kwa hayo yote, kwa hiyo hata kama watu laki tatu na nusu wangepinga haki na usawa wa binadamu, suala la haki za binadamu siyo suala la kidemokrasia.
Masuala ya kidemokrasia nia yapi, yalianishwa natume au walikatazwa kuchangia kwa kuwa sio ya kidemokrasia. Kama muundo wa muungano ni swala la kidemokrasia mbona hakukuwa na kura za kuchagua muunndo upi wa muungano utakao wafaa wananchi?
Hata hivyo, wananchi ambao walikaa kimya kuhusu hilo, walimaanisha kuwa kutokana na hali ilivyo, suala la haki za binadamu kwa Tanzania haliwakeri na li8meanishwa vizuri kwenye katiba.

Kwa hiyo unaamini kuna usawa wa kijinsia kwenye sasa? Vipi kuhusu huduma za maji waliolizungumzia walikua watu 962 nao walikua kimya kwa kuwa wameridhika au? Afya, umeme na huduma za elimu vipi?

Usifananishe incidences za hapa na pale za uvunjwaji wa haki za binadamu na sheria zilizopo.
Sheria za Tanzania haziruhusu ushoga, kwa hiyo kukaa kwao kimya ni kuridhika na status quo.
cc. Mchambuzi
Hapa mimi nilichukulia kwa tafsiri yako mkuu Kobello kwamba ambao awakuzungumzia wameridhika (kwa kupinga au kukubali ndo maana wapo kimya). Kwa hiyo kama unakubaliana na hapo juu kilichobaki ni kuzungumzia waliochangaia hoja na sio ambao hawakuchangia (nikiwa na maana kwamba tujadili wale ambao wamezungumzia muumdo wa muungano kama ni s1, s2 au s3).
tt2.jpg
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom