Uchaguzi 2020 CCM tutafanya makosa makubwa kama tutajaribu kuzibeza hoja za Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 CCM tutafanya makosa makubwa kama tutajaribu kuzibeza hoja za Tundu Lissu

Umesahau msemo kuwa, raisi wa nchi hii hapatikani kwa makaratasi ya kuwekwa kwenye box?. Wewe endelea kubwabwaja tu. Utanishawishi endapo utanambia kuwa chadamu mna katiba mpya na tume yenu ya uchaguzi siyo ile ya Dodoma. Fomu ya kugombea upewe Dodoma makao makuu ya CCM alafu ukabidhiwe Ikulu Dodoma makao makuu ya CCM? Ikulu yenyewe ndiyo imeanza kujengwa hata mjui inajengwaje ... Endeleeni kuota mchana.
Wananchi wakiamua mzee hamna wa kuwazuia
 
wacha nkuulize swali moja jepesi, unajua kwanini lazima ukope hata kama sio kwa ajili ya matumizi? ukishindwa hili swali basi we ni mbumbumbu
Usilete maskhara kwenye Mambo ya msingi, hili ni taifa kubwa linalopaswa kujengwa kwenye misingi ya haki, usawa,utu na uadilifu mkubwa!

Usifaninishe na familia yako wala ya bibi na babu yako, kwani lini tuliambiwa kuwa pesa tumekopa na tunafanya mambo haya, zaidi zaidi tunaambiwa makusanyo yameongezeka na tunatekeleza miradi mikubwa kwa pesa zetu cash,(mfano kununua ndege)

Sasa Kama huwezi kushtuka deni la taifa kupaa kwa 40 Trilioni ndani ya miaka 5 pekee, wewe utakuwa mfu kifikra!

Kasome mkopo wa Trilioni 2.7 za ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar-es-salaam, ITAKUSAIDIA!
 
Ni hizo tu ulizozisikia kutoka kwa Tundu Lissu? Ngoja nikukumbushe...

1. Kwa miaka 5 tu serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi ya Trilioni 40, (kama Ni kweli zimekwenda wapi?) Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa sababu tumeambiwa mara zote kuwa makusanyo yameongezeka na miradi yetu inatumia fedha za ndani

2. Ujenzi wa Hydroelectric power kule rufiji sio jambo jipya, (japo ni zuri) kwani kuna wengine walishajenga mabwawa kama hayo na yanafanya kazi mfano, Kidatu, Mtera n.k

3. Ujenzi wa reli si Jambo jipya (japo ni zuri), kwani reli zilijengwa na watangulizi wengine, mf.TAZARA NA RELI YA KATI na waliondoka baada ya muda wao kuisha, kwa hiyo hoja kwamba yeye aongezewe muda kwa sababu hizo ni dhaifu sana

4. Kukanyagwa kwa sheria mbali mbali, ikiwemo kuwadhulumu wafanyakazi haki zao za kimsingi kama kuwaongezea mishahara, kuwapandisha madaraja (vyeo) uhamisho, kusinyaa kwa ajira n.k haya yote ameyakanyaga bila huruma,kinyume Cha sheria!

Hayo ni baadhi tu ya mengine mengi ambayo Tundu Lissu ameyazungumzia na yanapaswa kujibiwa kwa hoja, unaweza kutusaidia kujibu kwa niaba ya chama chako?

Umemaliza mkuu, labda niongezee hapo, kwa kauelewa kangu kadogo najaribu kuwaza izo Trilioni 40 ni fedha nyingi sana, basi hata nusu yake ingeelekezwa kwenye kuboresha huduma za kijamii zinazomgusa mwananchi moja kwa moja, ingekuwa jambo la mbolea sana kwa upande wa Mh' Pombe.
Mfano:

>Upatikanaji wa maji safi vijijini,

>Elimu bora kwenye shule za serikali (Maabara kwenye kila shule+Waalimu wenye weledi),

>Huduma bora ya afya (madawa+Huduma bora za vipimo"vifaa vya kisasa"-Hapa nazungumzia hospitali zetu za rufaa mikoani sio lazima mgonjwa kutoka Arusha Mt' Meru Hospital kupelekwa kcmc au muhimbili), bila kusahau vituo vidogo vya afya.

Ni dhahiri wame"MISUSE" hayo mapesa na wajanja wamepiga za kwao huku walipa kodi wanapiga mihayo na kuvuja jasho juani huku wao kwenye ma-V8 yao wanakula ac na kujilipa mamilioni na hawalipi kodi. Inaumiza sana hii kitu, na huu unafiki hautaisha Tanzania bila kuwatoa hawa jamaa wamejisahau sana kwa kuishi kimazoea.

Angalau wapinzani asilimia kubwa wapo majimbo ya mijini hata wanachangamoto ndogo ndogo, sasa hawa wa ccm ukiangalia majimbo yao (Maisha ya Mbunge na Mwananchi anayemwongoza ni sawa na MBINGU NA ARDHI) kichekesho akiwa bungeni kazi yake ni kusifu na kuabudu, anajisahaulisha makusudi matatizo ya waliomtuma pale bungeni. TUAMKE WATANZANIA, HATUJALOGWA ILA TUNA HURUMA ZA KIJINGA.

#NIYEYE
 
Kwa hakika Kuna mambo ni surprise aisee,nimeshangaa Sana kwamba eti kwa miaka 5 tu, tumekopa zaidi ya Trilioni 40!(Kama hii ni kweli) hii nchi tutakuwa tumerogwa haki ya Mungu, hivi kweli tunakopa pesa nyingi kiasi hicho zinakwenda wapi? Ndiyo haya madaraja, barabara, ndege na vivuko?

Kama ndiyo ina maana kila kitu tunafanya kwa kukopa? Makusanyo yetu yaliyoongezeka yanakwenda wapi?

Kama kweli haya yametokea, (kukopa zaidi ya trilioni 40 kwa miaka 5 tu) itakuwa ni UHUJUMU UCHUMI WA KIWANGO CHA JUU ZAIDI HAPA NCHINI!
Miundombinu unayoiona tunajenga kwa pesa zetu za ndani, alisikika Magufuli kwenye mikutano yake akiongea.
 
Viongozi wako Ile siku ya Uhuru walivyoenda jijini mwanza kwaajili ya kuomba maridhiano walikodi maji ya bahari ya Hindi kwenda Mwanza?

Halafu watu tukisema Upinzani wa Tz umejaa wanafiki wa Taifa hili mnatunanga.
Walianza hivi hivi kwenye kuchukua form, nyuzi kibao dodoma kuzizima, lissu kufunika kwa wasindikizaji.
Ilipofika siku yenyewe aibu, wakaanza kulalamikia media, sijui media ndio zilizuia watu wasijitokeze.
 
Viongozi wako Ile siku ya Uhuru walivyoenda jijini mwanza kwaajili ya kuomba maridhiano walikodi maji ya bahari ya Hindi kwenda Mwanza?

Halafu watu tukisema Upinzani wa Tz umejaa wanafiki wa Taifa hili mnatunanga.

Kwani walikodi ya ATCL?
 
Kwani walikodi ya ATCL?
Hujaelewa swali Mkuu mimi sijauliza walienda na kampuni gani Bali nimeuliza walienda na usafiri gani?

Je walienda na usafiri wa maji mnayoyataka au walienda na usafiri wa ndege msioutaka?
 
Walianza hivi hivi kwenye kuchukua form, nyuzi kibao dodoma kuzizima, lissu kufunika kwa wasindikizaji.
Ilipofika siku yenyewe aibu, wakaanza kulalamikia media, sijui media ndio zilizuia watu wasijitokeze.
Hawa CDM wakati mwingine wanahitaji Akili kidogo ili uwaelewe ukiwa na Akili timamu Huwezi kuwaelewa wanataka Nini, msimamo wao Ni upi na Sera zao za kudumu Ni zipi.
 
Msinge wafanyia roho mbaya fastjet unadhani nani angepanda humo
Inshu hapa nikwanini walipanda kitu ambacho hawataki kinunuliwe nchini si Kama siyo wanafiki kweli wangepanda Basi au wakaenda kwa usafiri wa maji wanaoyataka.

Upuuzi na ujinga wa kupinga pinga Kila kitu ndo unaufanya upinzani wa Afrika kuonekana wa hovyo kabisa.
 
Tundu Lissu tayari ameshaonyesha wazi kuwa ni mwiba mchungu kwa CCM kuelekea kwenye kampeni, kwa muda mfupi aliopanda kwenye majukwaa yasio rasmi kwa ajili ya kampeni ameoneka kuwa Ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja zitakazo wabadilisha wengi mawazo hata kwa WanaCCM wenyewe.

Huyu Tundu ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, kujenga , na kutetea hoja kuliko watu wanavyo fikiria.

Na kwa vile Watanzania wa leo wengi hawana tena ushabiki wa vyama kama zamani, ni rahisi sana kuoambanua kile anacho kusema Lissu na yale yaliyotokea miaka mitano iliyo pita Kisha wakachukua hatua ambazo zitaweza kuishangaza hata CCM ambao wanadhani wanaweza kuhodhi utawala milele.

Ni ukweli ulio wazi tu kwamba kwa vyama vyote vya siasa watu wao watakaopanda kwenye majukwaa ya kampeni wasipojipanga vizuri Tundu atawagaragaza vibaya sana kwa hoja.

Kuna hoja dhaifu inayotolewa na makada wengi wa CCM kwamba urais hauwezi kutolewa kwa mtu kama huruma kwa sababu tu eti alipata shambulio la kupigwa risasi; huo ni udhaifu wa kujenga hoja na hilo litweza kuamsha hisia na kuwakumbusha wengi juu ya kipindi kigumu walichopitia Watanzania hapo nyuma.

La msingi kwa CCM msimbeze Lissu na kujaribu kupambana naye, bali mjipange kupambana na hoja zake ambazo kwa hakika zitakuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda kibichi.

Mbona mwaka 2015 alikuwa majukwaani lakini hamkuchua nchi pamoja na kuwapo lowasa?
 
Tundu Lissu tayari ameshaonyesha wazi kuwa ni mwiba mchungu kwa CCM kuelekea kwenye kampeni, kwa muda mfupi aliopanda kwenye majukwaa yasio rasmi kwa ajili ya kampeni ameoneka kuwa Ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja zitakazo wabadilisha wengi mawazo hata kwa WanaCCM wenyewe.

Huyu Tundu ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, kujenga , na kutetea hoja kuliko watu wanavyo fikiria.

Na kwa vile Watanzania wa leo wengi hawana tena ushabiki wa vyama kama zamani, ni rahisi sana kuoambanua kile anacho kusema Lissu na yale yaliyotokea miaka mitano iliyo pita Kisha wakachukua hatua ambazo zitaweza kuishangaza hata CCM ambao wanadhani wanaweza kuhodhi utawala milele.

Ni ukweli ulio wazi tu kwamba kwa vyama vyote vya siasa watu wao watakaopanda kwenye majukwaa ya kampeni wasipojipanga vizuri Tundu atawagaragaza vibaya sana kwa hoja.

Kuna hoja dhaifu inayotolewa na makada wengi wa CCM kwamba urais hauwezi kutolewa kwa mtu kama huruma kwa sababu tu eti alipata shambulio la kupigwa risasi; huo ni udhaifu wa kujenga hoja na hilo litweza kuamsha hisia na kuwakumbusha wengi juu ya kipindi kigumu walichopitia Watanzania hapo nyuma.

La msingi kwa CCM msimbeze Lissu na kujaribu kupambana naye, bali mjipange kupambana na hoja zake ambazo kwa hakika zitakuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda kibichi.
Ana uwezo kujieleza kisheria, kwa kisiasa hamna kitu
 
Ni hizo tu ulizozisikia kutoka kwa Tundu Lissu? Ngoja nikukumbushe...

1. Kwa miaka 5 tu serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi ya Trilioni 40, (kama Ni kweli zimekwenda wapi?) Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa sababu tumeambiwa mara zote kuwa makusanyo yameongezeka na miradi yetu inatumia fedha za ndani

2. Ujenzi wa Hydroelectric power kule rufiji sio jambo jipya, (japo ni zuri) kwani kuna wengine walishajenga mabwawa kama hayo na yanafanya kazi mfano, Kidatu, Mtera n.k

3. Ujenzi wa reli si Jambo jipya (japo ni zuri), kwani reli zilijengwa na watangulizi wengine, mf.TAZARA NA RELI YA KATI na waliondoka baada ya muda wao kuisha, kwa hiyo hoja kwamba yeye aongezewe muda kwa sababu hizo ni dhaifu sana

4. Kukanyagwa kwa sheria mbali mbali, ikiwemo kuwadhulumu wafanyakazi haki zao za kimsingi kama kuwaongezea mishahara, kuwapandisha madaraja (vyeo) uhamisho, kusinyaa kwa ajira n.k haya yote ameyakanyaga bila huruma,kinyume Cha sheria!

Hayo ni baadhi tu ya mengine mengi ambayo Tundu Lissu ameyazungumzia na yanapaswa kujibiwa kwa hoja, unaweza kutusaidia kujibu kwa niaba ya chama chako?
Umeanza Vizuri kabisa Ila umemaliza kipuuzi Sana Baada ya kumaliza hoja zako kwa kuhusisha Mambo ya uchumia chama.

To be honestly Mimi Sina chama hivyo Basi siwezi kukujibu Maana Mimi siyo mwanachama na wewe unataka kujibiwa na mwanachama.

Mimi Ni raia mpiga kura tu Namkubuli Sana Mbowe, namkubali Sana Magufuli na simukubali kabisa Tundu lissu.
 
Hujaelewa swali Mkuu mimi sijauliza walienda na kampuni gani Bali nimeuliza walienda na usafiri gani?

Je walienda na usafiri wa maji mnayoyataka au walienda na usafiri wa ndege msioutaka?

Kwahiyo ulitaka waende na meli Dar-mwanza.
 
Alisema enough is enough!
Waendelee na propaganda yeye anajenga na kutetea hoja.
 
CCM hawana ubavu wa kujibu hoja za Lissu, Wamefumbwa na mazoea ya kubebwa na tume pamoja na vyombo vya dola! Mwaka huu watashangaa! Yale mambo ya kuanza kuambiana mtaisoma namba au mtapata tabu sana wakati sote tuna haki ya kufaidi rasimali za taifa letu, ule uhuni uliopitiliza! Tena safi waendelee kuimba kiwimbo chao hichoicho cha kura za huruma ili siku atakaposhinda asubuhi wapate aibu ya mwaka!
 
Back
Top Bottom