Wananchi wakiamua mzee hamna wa kuwazuiaUmesahau msemo kuwa, raisi wa nchi hii hapatikani kwa makaratasi ya kuwekwa kwenye box?. Wewe endelea kubwabwaja tu. Utanishawishi endapo utanambia kuwa chadamu mna katiba mpya na tume yenu ya uchaguzi siyo ile ya Dodoma. Fomu ya kugombea upewe Dodoma makao makuu ya CCM alafu ukabidhiwe Ikulu Dodoma makao makuu ya CCM? Ikulu yenyewe ndiyo imeanza kujengwa hata mjui inajengwaje ... Endeleeni kuota mchana.
Usilete maskhara kwenye Mambo ya msingi, hili ni taifa kubwa linalopaswa kujengwa kwenye misingi ya haki, usawa,utu na uadilifu mkubwa!wacha nkuulize swali moja jepesi, unajua kwanini lazima ukope hata kama sio kwa ajili ya matumizi? ukishindwa hili swali basi we ni mbumbumbu
Ni hizo tu ulizozisikia kutoka kwa Tundu Lissu? Ngoja nikukumbushe...
1. Kwa miaka 5 tu serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi ya Trilioni 40, (kama Ni kweli zimekwenda wapi?) Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa sababu tumeambiwa mara zote kuwa makusanyo yameongezeka na miradi yetu inatumia fedha za ndani
2. Ujenzi wa Hydroelectric power kule rufiji sio jambo jipya, (japo ni zuri) kwani kuna wengine walishajenga mabwawa kama hayo na yanafanya kazi mfano, Kidatu, Mtera n.k
3. Ujenzi wa reli si Jambo jipya (japo ni zuri), kwani reli zilijengwa na watangulizi wengine, mf.TAZARA NA RELI YA KATI na waliondoka baada ya muda wao kuisha, kwa hiyo hoja kwamba yeye aongezewe muda kwa sababu hizo ni dhaifu sana
4. Kukanyagwa kwa sheria mbali mbali, ikiwemo kuwadhulumu wafanyakazi haki zao za kimsingi kama kuwaongezea mishahara, kuwapandisha madaraja (vyeo) uhamisho, kusinyaa kwa ajira n.k haya yote ameyakanyaga bila huruma,kinyume Cha sheria!
Hayo ni baadhi tu ya mengine mengi ambayo Tundu Lissu ameyazungumzia na yanapaswa kujibiwa kwa hoja, unaweza kutusaidia kujibu kwa niaba ya chama chako?
Miundombinu unayoiona tunajenga kwa pesa zetu za ndani, alisikika Magufuli kwenye mikutano yake akiongea.Kwa hakika Kuna mambo ni surprise aisee,nimeshangaa Sana kwamba eti kwa miaka 5 tu, tumekopa zaidi ya Trilioni 40!(Kama hii ni kweli) hii nchi tutakuwa tumerogwa haki ya Mungu, hivi kweli tunakopa pesa nyingi kiasi hicho zinakwenda wapi? Ndiyo haya madaraja, barabara, ndege na vivuko?
Kama ndiyo ina maana kila kitu tunafanya kwa kukopa? Makusanyo yetu yaliyoongezeka yanakwenda wapi?
Kama kweli haya yametokea, (kukopa zaidi ya trilioni 40 kwa miaka 5 tu) itakuwa ni UHUJUMU UCHUMI WA KIWANGO CHA JUU ZAIDI HAPA NCHINI!
Walianza hivi hivi kwenye kuchukua form, nyuzi kibao dodoma kuzizima, lissu kufunika kwa wasindikizaji.Viongozi wako Ile siku ya Uhuru walivyoenda jijini mwanza kwaajili ya kuomba maridhiano walikodi maji ya bahari ya Hindi kwenda Mwanza?
Halafu watu tukisema Upinzani wa Tz umejaa wanafiki wa Taifa hili mnatunanga.
Viongozi wako Ile siku ya Uhuru walivyoenda jijini mwanza kwaajili ya kuomba maridhiano walikodi maji ya bahari ya Hindi kwenda Mwanza?
Halafu watu tukisema Upinzani wa Tz umejaa wanafiki wa Taifa hili mnatunanga.
Hujaelewa swali Mkuu mimi sijauliza walienda na kampuni gani Bali nimeuliza walienda na usafiri gani?Kwani walikodi ya ATCL?
Hawa CDM wakati mwingine wanahitaji Akili kidogo ili uwaelewe ukiwa na Akili timamu Huwezi kuwaelewa wanataka Nini, msimamo wao Ni upi na Sera zao za kudumu Ni zipi.Walianza hivi hivi kwenye kuchukua form, nyuzi kibao dodoma kuzizima, lissu kufunika kwa wasindikizaji.
Ilipofika siku yenyewe aibu, wakaanza kulalamikia media, sijui media ndio zilizuia watu wasijitokeze.
Inshu hapa nikwanini walipanda kitu ambacho hawataki kinunuliwe nchini si Kama siyo wanafiki kweli wangepanda Basi au wakaenda kwa usafiri wa maji wanaoyataka.Msinge wafanyia roho mbaya fastjet unadhani nani angepanda humo
Mitano mingine atakopa 40 tenaUnalizingumziaje swala la kukopa 40 tr ndani ya miaka mitano? Achana kwanza na swala la kukwapua 1.5 tr
Tundu Lissu tayari ameshaonyesha wazi kuwa ni mwiba mchungu kwa CCM kuelekea kwenye kampeni, kwa muda mfupi aliopanda kwenye majukwaa yasio rasmi kwa ajili ya kampeni ameoneka kuwa Ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja zitakazo wabadilisha wengi mawazo hata kwa WanaCCM wenyewe.
Huyu Tundu ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, kujenga , na kutetea hoja kuliko watu wanavyo fikiria.
Na kwa vile Watanzania wa leo wengi hawana tena ushabiki wa vyama kama zamani, ni rahisi sana kuoambanua kile anacho kusema Lissu na yale yaliyotokea miaka mitano iliyo pita Kisha wakachukua hatua ambazo zitaweza kuishangaza hata CCM ambao wanadhani wanaweza kuhodhi utawala milele.
Ni ukweli ulio wazi tu kwamba kwa vyama vyote vya siasa watu wao watakaopanda kwenye majukwaa ya kampeni wasipojipanga vizuri Tundu atawagaragaza vibaya sana kwa hoja.
Kuna hoja dhaifu inayotolewa na makada wengi wa CCM kwamba urais hauwezi kutolewa kwa mtu kama huruma kwa sababu tu eti alipata shambulio la kupigwa risasi; huo ni udhaifu wa kujenga hoja na hilo litweza kuamsha hisia na kuwakumbusha wengi juu ya kipindi kigumu walichopitia Watanzania hapo nyuma.
La msingi kwa CCM msimbeze Lissu na kujaribu kupambana naye, bali mjipange kupambana na hoja zake ambazo kwa hakika zitakuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda kibichi.
Hoja hapa siyo kuzungumuzia ushoga Mara kwa Mara hoja Ni kusapoti ushoga.Toka arudi amegusia tena suala la ushoga?
Ana uwezo kujieleza kisheria, kwa kisiasa hamna kituTundu Lissu tayari ameshaonyesha wazi kuwa ni mwiba mchungu kwa CCM kuelekea kwenye kampeni, kwa muda mfupi aliopanda kwenye majukwaa yasio rasmi kwa ajili ya kampeni ameoneka kuwa Ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja zitakazo wabadilisha wengi mawazo hata kwa WanaCCM wenyewe.
Huyu Tundu ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, kujenga , na kutetea hoja kuliko watu wanavyo fikiria.
Na kwa vile Watanzania wa leo wengi hawana tena ushabiki wa vyama kama zamani, ni rahisi sana kuoambanua kile anacho kusema Lissu na yale yaliyotokea miaka mitano iliyo pita Kisha wakachukua hatua ambazo zitaweza kuishangaza hata CCM ambao wanadhani wanaweza kuhodhi utawala milele.
Ni ukweli ulio wazi tu kwamba kwa vyama vyote vya siasa watu wao watakaopanda kwenye majukwaa ya kampeni wasipojipanga vizuri Tundu atawagaragaza vibaya sana kwa hoja.
Kuna hoja dhaifu inayotolewa na makada wengi wa CCM kwamba urais hauwezi kutolewa kwa mtu kama huruma kwa sababu tu eti alipata shambulio la kupigwa risasi; huo ni udhaifu wa kujenga hoja na hilo litweza kuamsha hisia na kuwakumbusha wengi juu ya kipindi kigumu walichopitia Watanzania hapo nyuma.
La msingi kwa CCM msimbeze Lissu na kujaribu kupambana naye, bali mjipange kupambana na hoja zake ambazo kwa hakika zitakuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda kibichi.
Umeanza Vizuri kabisa Ila umemaliza kipuuzi Sana Baada ya kumaliza hoja zako kwa kuhusisha Mambo ya uchumia chama.Ni hizo tu ulizozisikia kutoka kwa Tundu Lissu? Ngoja nikukumbushe...
1. Kwa miaka 5 tu serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi ya Trilioni 40, (kama Ni kweli zimekwenda wapi?) Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa sababu tumeambiwa mara zote kuwa makusanyo yameongezeka na miradi yetu inatumia fedha za ndani
2. Ujenzi wa Hydroelectric power kule rufiji sio jambo jipya, (japo ni zuri) kwani kuna wengine walishajenga mabwawa kama hayo na yanafanya kazi mfano, Kidatu, Mtera n.k
3. Ujenzi wa reli si Jambo jipya (japo ni zuri), kwani reli zilijengwa na watangulizi wengine, mf.TAZARA NA RELI YA KATI na waliondoka baada ya muda wao kuisha, kwa hiyo hoja kwamba yeye aongezewe muda kwa sababu hizo ni dhaifu sana
4. Kukanyagwa kwa sheria mbali mbali, ikiwemo kuwadhulumu wafanyakazi haki zao za kimsingi kama kuwaongezea mishahara, kuwapandisha madaraja (vyeo) uhamisho, kusinyaa kwa ajira n.k haya yote ameyakanyaga bila huruma,kinyume Cha sheria!
Hayo ni baadhi tu ya mengine mengi ambayo Tundu Lissu ameyazungumzia na yanapaswa kujibiwa kwa hoja, unaweza kutusaidia kujibu kwa niaba ya chama chako?
Hujaelewa swali Mkuu mimi sijauliza walienda na kampuni gani Bali nimeuliza walienda na usafiri gani?
Je walienda na usafiri wa maji mnayoyataka au walienda na usafiri wa ndege msioutaka?
Nafikiri haya yalikuwa mapepo ya ccm pamoja na akina Alumni.Bia Yetu sijui yuko wapi siku hizi?