CCM walienda kufanya "show off" na uvunjifu wa Katiba Yao wenyewe, haukua mkutano!

Hapo ningekuwa nakutafsiria kama mtoto mdogo asiyejua kusoma.

Mimi pia si mwanachama wa CCM.

Katiba ya CCM ipo mtandaoni, access ya mtandao uliyo nayo wewe ndiyo hiyo hiyo ninayo mimi, sasa kwa nini unataka nikusomee na kukutafsiria?
Alimaanisha kwa kuwa katiba husika unayo basi, ungeweka hicho kifungu ama uipandishe katiba nzima pamoja na wasilisho lako. Hayo mengine meengii hayakustahili!
Hii ni 2025 wazee. Turahisishe mambo yawe mepesi!
 
Alimaanisha kwa kuwa katiba husika unayo basi, ungeweka hicho kifungu ama uipandishe katiba nzima pamoja na wasilisho lako. Hayo mengine meengii hayakustahili!
Hii ni 2025 wazee. Turahisishe mambo yawe mepesi!
Mbona nishajibu kuwa katiba ipo mtandao huu huu tunaotumia wote hata mimi sina ya kitabu, na vifungu nishaviweka.

Tatizo liko wapi?

Hujui kusoma kwa ufahamu?

Hamjui ku Google?
 
Sasa nini faida ya Mtu kuwa Mzee ??!
Je Wazee wa namna hiyo wenye tamaa kuna umuhimu wa kuwafuata na kutaka ushauri wao ??!
Je na Nyerere alikuwa na Tamaa hizo ??!
CCM wanakuangalia kama Una manufaa kwao wanakuweka, unataka hutaki. Mzee Wasira alitakiwa afuate nyayo za Mzee Kinana
 
Tunashanga judge mtungi yupo wapi? Sheria inataka mgombea anatakiwa apate Saini za wanachama kila mkoa kabla mgombea hajatangazea na chama ila mwaka huu imezimwa

Huyo Mtungi yupo hapo kukabili upinzani kulinda masirahi ya CCM. Akitia neno tu, wanamuondoa. Kwanza usikute pia ana kadi ya CCM.
 
Huyo Mtungi yupo hapo kukabili upinzani kulinda masirahi ya CCM. Akitia neno tu, wanamuondoa. Kwanza usikute pia ana kadi ya CCM.
Aibuuu Sana na nasikia amri anapewa na makada wa CCM very junior. Hawa ndio wanafanya Elimu ionekane ya kipumbavu
 
CCM ni mabingwa wa demokrasia feki.
Bila umafia, na magumashi CCM haiwezi kusavaivu.
Bahati mbaya ndio wapo madarakani na hawatoki.
 
Ile ilikuwa fashion show mwanzo mwisho..ni mwendo wa kuonyesha ufahari,mavazi na starehe..Wananchi wengi hawakupendezwa ukizingatia hali wengi ya uchumi ni mbaya.
 
Ile ilikuwa fashion show mwanzo mwisho..ni mwendo wa kuonyesha ufahari,mavazi na starehe..Wananchi wengi hawakupendezwa ukizingatia hali wengi ya uchumi ni mbaya.
Hapa TUNDUMA kuna Shule ya msingi wanakaa chini watoto
 
..kama na barua ya mtu kuomba kupumzika ilishaandikwa kwa maana kwamba hana nia ya kuwa mgombea mwenza, halikuwa jambo la kushtukiza..walishapanga na kuarifiana kila kitu kabla ya mkusanyiko wao huo..!
 
..kama na barua ya mtu kuomba kupumzika ilishaandikwa kwa maana kwamba hana nia ya kuwa mgombea mwenza, halikuwa jambo la kushtukiza..walishapanga na kuarifiana kila kitu kabla ya mkusanyiko wao huo..!
Yawezekana au wengine Wanasemaga Labda 🙄!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…