Tetesi: CCM wanapita vyuoni kuorodhesha UVCCM waliokosa mkopo

Watu mnajua kupandikiza chuki
 
Mwisho wa siku mtasema kwamba CCM imetoea maagizo kuhakikisha wanafunzi wote walio wanachama wa CCM hawatakiwi kupata supp..
 
wewe endelea kujitoa ufahamu mengi yanakuja
Idea,drowing au write -up ,product banadamu yeyote kwenye ufahamu jambo lake lolote lazima lipitie njia hizo tatu na njia hzo zinamahitaji yake ya matumizi ya ubongo kuanzia Akili,Ufahamu,Nguvu sasa watanzania tunapenda sana product ambayo inatumia nguvu tu na so kabla ya uchaguzi na wakat wanatangaza jina lake tayali drowing na write - up ziliandikwa sana juu ya tabia yake so kwa vile watanzania ni wavivu kusoma na matumizi ya ubongo ni madogo kuliko matumizi ya nguvu ndo mkaenda kuchagua so mm nimeshajiandaa na lolote linalokuja so cwezi kupata shida nilishajiandaa toka anatangazwa tatizo lipo kwenu tu
 
Ujiulizi hapo kwanini? Hao uvccm waandikishe majina wao kama nani?
 

Nawapa pole sana wanafunzi watakaokoseshwa mkopo kwa umangimeza wa UVCCM. Hilo la kuandikisha makada wa ccm vyuoni kwa ajili ya kupta mikopo halina nia njema kam ani kweli inagawa siamini kama ni kweli. Linakusudiwa kuwanyima haki hiyo ya mikopo kwa wanafunzi ambao wazee wao ama wao wenyewe si wafuasi wa CCM. Kwa znz hili sio geni, miaka ya nyuma ilikuwa wanafunzi ambao wazee wao waliodhaniwa kuwa ni wafuasi wa cuf walinyimwa scholarships na fursa nyengine za udhamini kwa sababu tu ya kuegemea itikadi fulani ya kisiasa. Walioathirika zaidi na ndugu zangu kutoka Pemba na badhi ya wanafunzi wa unguja mimi nikiwa ni mmoja wao. Walikoseshwa scholarships mchana kweupe bila ya huruma. Haya yalitokea wakati wa utawala wa Salamin Amour Juma. Kwa Zanzibar ilikuwa unapopata scholarship lazima upitie ofisi ya usalama ( wenyewe wanaita GSO) ukakaguliwe na kuchunguzwa kila sehemu, unajaza fomu yenye masuala fyoko kama vile umezaliwa wapi, umesoma shule gani, umeoa wapi, wifi zako , shemeji zako nani , unapendelea michezo gani n aviwanaja vipi unakwenda, unakaa wapi na masuala mengine kedekede unayoulizwa kwenye hiyo fomu ya GSO ambayo ilikuwa ikiratibiwa na usalama wa taifa. mwisho wa siku unasikia tu kuwa hutopata scholarship na huambiwi sababu ya kukoseshwa. kama hali hii imehamia T/ Bara, ni masikitiko makubwa hususan kwa wanafunzi wanaotoka ktk kaya masikini na ambao wazee wao hawana uwezo wa kuwasomesha watoto wao ngazi ya chuo kikuu. Ni huzuni kubwa na ninawapa pole wale wote watakaoathirika.
 
Ili mradi kumbe hayo mambo ya kuandikshana yapo,basi mleta uzi yuko sahihi.Uvccm wanaandikisha waliokosa mkopo wao kama nani?
 
kwanini waandikwe na watu wa chama? usipokuwa na chama chochote maana yake hupewi mkopo? bodi imewapata tenda hiyo ccm? msipige kelele njooni mjibu haya maswali
 
Nothing but Discrimination! Tena ndani ya nchi yako! Bila kuzingatia kuwa Kodi zinalipwa na wote,ila Huduma zinatolewa kiubaguzi! Iko siku tu!
 
TETESI.... au huelewi maana ya TETESI?
 
Well let them do what they think is right for them. But we do believe God the almight is supreme
 
Mkuuu usiangaike na lumumba wanawaza kwa kutumia tumbo

Hapa tunaongelea watoto kukosa mkopo Na ubaguzi wanaofanyiwa we ling'ombe unakuja kuleta Mambo ya mbowe,inaonesha ni jinsi gani ulivo mtupu kichwani,wanetu wamekosa mikopo huku wanavigezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…