Pre GE2025 CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025

Pre GE2025 CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mtabiri tambi tambi anasema milio itaanza mwishon mwa mwez huu na mwanzon mwa mwez Feb..
Mamaee january
 
Watu watofautishe Dr Nchimbi na Dr Nchemba Jamanii. Leo Songea huko ni kugalauka mpaka pakuche.

**Jokate Mwegelo ajipange
 
Sjui nataka kusema Nini ila ya jiwe maybe yakajirudia one term prez ?

Anyway wazee wa mikakati wanamuingiza kingi mbaya sana

M.A.P IN ADVANCE

Mbichi Alianza ongelewa Toka yupo Kwa kina VINNI
20250106_201444.jpg
 
===
Wana jamii forum hii ndio habari kuu mpya toka mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa kuwa Mhe Dkt Emmanuel Nchimbi ndio Mgombea mwezi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu Ujao Oct 2025.

Uteuzi na mabadiliko haya yataanza rasmi baada ya mwezi July Bunge litakapovunjwa hivyo Dkt Philip Esdori Mpango na Dkt Emmanuel Nchimbi wataendelea kuwa katika nafasi zao mpaka wakati wa Uchaguzi Mkuu huku Dkt Philip Esdori Mpango yeye atasalia mpaka siku ya kuapishwa kwa Rais na Makamu wa Rais.
===

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameridhia kwa kauli moja kumpitisha Katibu Mkuu wa CCM Taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza (Makamu wa Rais) kwa Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni mgombea urais, Samia Suluhu Hassan alimpendekeza Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 2025 baada ya Makamu Wa Rais, Dkt. Philip Mpango kuomba kupumzika.

Soma: Breaking News: - Uchaguzi 2025 - Dr. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu wa Rais, Rais Samia aridhia ombi hilo

Dkt. Nchimbi aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Januari 15, 2024 katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho kilichofanyikia Unguja, visiwani Zanzibar.

Dkt. Nchimbi alichukua nafasi iliyoachwa wazi na Daniel Chongolo aliyejiuzulu Novemba 29, 2023.

Rais Samia amempendekeza Dk Nchimbi leo Jumapili, Januari 19, 2025 katika mkutano mkuu maalumu jijini Dodoma.

Hakika hili ni jembe haswa! Wapinzani kazi wanayo huku Rais Samia huku Dk Nchimbi
 
Mambo yanakwenda kwa kasi ndani ya chama dola kongwe CCM kuelekea 2025
 
𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐌𝐀𝐀𝐋𝐔𝐌 𝐖𝐀 𝐂𝐂𝐌 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐖𝐀𝐑𝐈𝐃𝐇𝐈𝐀 𝐃𝐊𝐓. 𝐍𝐂𝐇𝐈𝐌𝐁𝐈 𝐊𝐔𝐖𝐀 𝐌𝐆𝐎𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐌𝐖𝐄𝐍𝐙𝐀 𝐖𝐀 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameridhia kwa kauli moja kumpitisha Katibu Mkuu wa CCM Taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza (Makamu wa Rais) kwa Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025.
 

Attachments

  • VID-20250120-WA0014.mp4
    22.5 MB
Nyerere, Mkapa, Magufuli, Mpango na Nchimbi ni baadhi yao.

Julius Nyerere, rais wa kwanza wa Tanzania, ambaye alipenda kuwa padre, alisoma katika Shule ya White Fathers Missionary school huko Musoma na baadaye kufundisha St. Mary High School. Wakati akisoma, alijihusisha sana na Kanisa na baadaye aliziandika Injili zote 4 kwa mfumo wa mashairi.

Benjamini Mkapa rais wa tatu wa Tanzania, alisoma katika Seminari ya Kigonsera, Ndanda akipenda kuwa padre, lakini aliona aende kwenye masomo mengine ya mambo ya kidunia.

John Magufuli rais wa tano wa Tanzania, alisoma katika Seminari ya Katoke, Biharamulo Kagera, lakini aliondoka kabla ya kumaliza kutokana na changamoto mbalimbali zilizomkumba akiwa shuleni.

Philip Mpango, makamu wa rais wa JMT, naye alikuwa akisoma katika Seminari ya Ujiji na Itaga, Tabora na pia alifikia uamuzi wa kutoendelea na masomo ya upadre.

Na sasa, mgombea mwenza wa CCM Emmanuel Nchimbi ni ex-seminarian katika Seminari Ndogo ya Mitume wa Yesu, Uru mkoani Kilimanjaro.

Wapo viongozi wengi sana nchini waliosoma seminari za Kanisa Katoliki na wametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi. Hongera kwa Kanisa Katoliki na mtandao wa shule za seminari kwa kuwa viwanda vya kuzalisha viongozi wakubwa katika Taifa letu.
 
Julius Nyerere, rais wa kwanza wa Tanzania, ambaye alipenda kuwa padre, alisoma katika Shule ya White Fathers Missionary school huko Musoma na baadaye kufundisha St. Mary High School. Wakati akisoma, alijihusisha sana na Kanisa na baadaye aliziandika Injili zote 4 kwa mfumo wa mashairi.

Benjamini Mkapa rais wa tatu wa Tanzania, alisoma katika Seminari ya Kigonsera akipenda kuwa padre, lakini aliona aende kwenye masomo mengine ya mambo ya kidunia.

John Magufuli rais wa tano wa Tanzania, alisoma katika Seminari ya Katoke, Biharamulo Kagera, lakini aliondoka kabla ya kumaliza kutokana na changamoto mbalimbali zilizomkumba akiwa shuleni.

Philip Mpango, makamu wa rais wa JMT, naye alikuwa akisoma katika Seminari ya Ujiji na Itaga, Tabora na pia alifikia uamuzi wa kutoendelea na masomo ya upadre.

Na sasa, mgombea mwenza wa CCM Emmanuel Nchimbi ni ex-seminarian katika Seminari Ndogo ya Mitume wa Yesu, Uru mkoani Kilimanjaro.

Wapo viongozi wengi sana nchini waliosoma seminari za Kanisa Katoliki na wametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi. Hongera kwa Kanisa Katoliki na mtandao wa shule za seminari kwa kuwa viwanda vya kuzalisha viongozi wakubwa katika Taifa letu.
Sikua nafahamu hili, So Nchimbi ni mpango maalumu wa Kanisa Katoliki au Ni Coincidence????
 
Back
Top Bottom