CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

Hii ndio chama ya mapinduzi hata haingalii cheo historia wala sura magufuli akileta zake anagongwa za uso muulize maalimu seif anajua!
Malim seif kipindi yupo ccm magufulu ndio kwanza anasoma shule ya msingi na pole pole hajazaliwa bashiru yy ndio kwanza ananyonya kwahiyo hao waliopo hakuna hata mmoja anaemkumbuka maalim kipindi yuko ccm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wawafukuze tu.. Hii ni CCM mpya..
CCM mpya!
tapatalk_1582623324418.jpeg
 
Membe katuchafulie kwa mabeberu tukose misaada.
Wamemwaga mboga wewe mwaga ugali, bora tukose wote
 
Samurai ukimusikiliza Sumaye baada ya kutoka Chadema nako ni mchang'anyiko pia sasa Wa Tz twende wapi au ni wapi penye unafuu?

CDM haikuwahi kutawala hii nchi, CCM inamwaka zaidi ya 50 inatawala hii nchi na kuna madhara makubwa sana ambayo mpaka sasa lazima tuilaumu CCM. Madhara kama Elimu duni iliyoawaacha mamilioni yawatanzania kuendelea kuwa masikini na wajinga, Huduma mbovu za Afya na miundombinu, makazi duni kwa mamilioni ya watanzania yanasosababishwa na gharama kubwa za ujenzi wa nyumba, nk.

Uwepo wa CCM zaidi ya miaka 50 umesababisha CCM na wanaCCM kuamini Tanzania ni yao na kila Mtanzania akizaliwa tu tayari ni mwanaCCM na si kuamini kwamba CCM ni chama cha siasa kama vyama vingine ambacho kinategemea maamuzi ya wananchi ili kiwe madarakani. Hali hii umeifanya CCM kujiwekea mizizi na kuhodhi kila kitu kiasi cha kuaminisha jamii bila CCM hakuna Tanzania kitu ambacho si kweli maana Zambia, DRC,SA, ANGOLA nk zipo na hakuna CCM huko hivyo hata Tanzania inawezekana bila CCM.

Ni wakati wananchi tukasimama upande wetu kama watanzania bila kujali dini, Rangi, kabila nk tukaitoa CCM kwanza ili tujenge heshima yetu kama Watanzania bila kujali chama gani kinatuongoa maana maauzi yapo mikononi kwetu. Huyo atakayetuongoza ndani ya miaka mitano tukiona muenendo ni mbaya sio lazima ifike miaka mitano bali ndani ya miaka minne mitatu tunaweza kupiga chini akakaa mwingine ili hawa wanasiasa watuheshimu Watanzania..
 
Hapo mimi mgeni(huu uwanaharakati na uwanasiasa wangu wa kuungaunga kwa matukio ndo unanipa changamoto) hebu nijuze kwanini hawezi kugombea?

Sheria iliyopitishwa na wana Lumumba ni kwamba mtu haruhusiwi kugombea mpaka awe ametimiza walau miaka miwili ndani ya chama.
 
Back
Top Bottom