CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

Chama kikongwe kama CCM kinapaswa kusimama ktk misingi yake ya awali, ile ambayo waasisi wake walienenda kupitia kwayo. CCM ambayo ilikuwa ni vikao vya chama vyenye vyenye maamuzi ya uhakika, na pia ni sehemu muhimu sana ktk kuambiana ukweli, kuonyana, kurekebishana na hata kuwekana sawa pale endapo kulionekana kuwa na dalili hasi za mgawanyiko miongoni mwa makada wenye nguvu kiasi cha kutishia kukigawa chama.

Sasa tunaiona siasa mpya ambayo inaendeshwa na hisia za Mwenyekiti Taifa. Endapo kada akakosa kibali mbele ya macho yake, pasipo kujali mchango wake ndani historia ya chama, atadukuliwa mazungumzo yake ya faragha, afuatiliwa kwa ukaribu nyendo na maongezi yake. Yote yatafanyika ili kuhalalisha kukosa kwake utiifu kwa chama.

Mh. Membe tambua ya kuwa wewe bado ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa sana nchi na pia mwenye kuiheshimika, na umeishi maisha ya kisiasa kwa muda mrefu. Sasa umeingia ktk ukurasa mpya wa maisha haya. Bado una uwezo, ama kufanya uamuzi wa kustaafu siasa za kiushindani ili kukwepa adha, maudhi na maisha mengine ya mahangaiko ambayo mahasimu wako ni lazima watakuwa wamejiandaa kukupitisha ktk tanuru la moto, ili kuzidi kukitia madoa ya fedheha mbele ya jamii.

La kama si hivyo, bado una uwezo wa kuendelea na mapambano ya kisiasa, ili kufungua ukurasa mpya wa siasa ndani ya nchi yetu, ndani ya CCM hata nje yake pia ktk vyama vya upinzani. Unao uwezo mkubwa wa kuwa kiunganishi cha wapenda mabadiliko ya kweli ktk siasa za nchi yetu. Unao uwezo wa kukabiliana na siasa chafu na michezo dhalimu na ya dhuluma ktk kupindisha maamuzi ya kweli ya umma kupitia upigaji wa kura ktk chaguzi mbalimbali zifanyikazo hapa nchini, kama huu tunaoutegemea mwaka huu wa 2020.

Jipe, muda wa kutosha na tena kwa kushauriana na watu makini, kabla ya kutoa msimamo wako mpya. Nakutakia kila la heri.

Naamini, watu wengi bado wapo nyuma yako, na pia wanakuunga mkono. Umevuliwa uanachama si kwa sababu ya kukosa utiifu kwa chama chako, ambacho umekitumikia kwa uaminifu, umakini na uweledi mkubwa, isipokuwa kwa vikao vya uamuzi kuweza kukidhi hisia za Mwenyekiti Taifa dhidi yako.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAJUA SANA! MIMI NAULIZA TU, JE WAMEKIKOSEA CHAMA AU WAMEMKOSEA MWENYEKITI WA CHAMA? SASA KAMA MWENYEKITI WA CHAMA NDIO KAKOSEWA HIVI VIKAO VYA NINI? SI HUYU ALIYEKOSEWA NDIO AAMUE CHA KUWAFANYA? SASA ANAWAKUSANYA WENGINE WAAMUE NINI WAKATI ALIYEKOSEWA NI MMOJA?
Labda aliwashitaki kwenye chama na chama ndio kimeamua, ingawaje kimaadili angempisha makamu mwenyekiti kuongoza kikao cha hukumu endapo yeye ndie mlalamikaji.
 
mbenge, Mbona mnahamisha magoli? Haya maamuzi yamechukuliwa na Magufuli pekee yake?

Mtu aliitwa kwanza kuhojiwa, na baada ya mahojiano ndio kamati ikaona imtoe chamani, sasa unataka nini tena? Je, angefukuzwa bila kusikilizwa kabisa?

Alafu si mlikuwa mnasema Membe ni kachero mzoefu hagusiki.? Kiko wapi sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mamadogo.lakini hakuna mwana CCM aliyefurahishwa na maamuzi ya kidikteta Kama haya ya kufukuza watu hovyo hatujui kesho atakuwa nani.
Dada naona umekomaa kweli kweli.
Nikwambie tu kwamba bora ukajipinde kuanzisha thread za kudai tume huru ila haya unayofanya hapa hayakusaidii kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wekeni wazi sababu za kumfukuza membe uanachama ni zipi?
Mbona mnahamisha magoli? Haya maamuzi yamechukuliwa na Magufuli pekee yake?

Mtu aliitwa kwanza kuhojiwa, na baada ya mahojiano ndio kamati ikaona imtoe chamani, sasa unataka nini tena? Je, angefukuzwa bila kusikilizwa kabisa?

Alafu si mlikuwa mnasema Membe ni kachero mzoefu hagusiki.? Kiko wapi sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana Jr kwa hizi nchi zetu kupimana ubavu na aliye kwenye kiti cha urais ni kujitakia maangamizi. JK alishakuwa pale na anajua nguvu ya rais. Hata kama haridhishwi lakini hana la kufanya. Ni nani alikuwa na mikakati na ushawishi kama Lowassa? Nadhani hujasahau mziki wake. Hapa ndiyo imetoka hivyo. Membe nje ya CCM ni mwepesi kama ubua.

Sana sana atapiga piga kelele kwa maumivu anayougulia lakini yakishapoa atapotea kwenye duru za siasa (hasa baada ya uchaguzi). Siyo ajabu akaja kuomba msamaha siku zijazo (baada ya kupigika) na kurudishwa chamani kama kina Sofia Simba. Mtu aliyezoea kula na kunywa kwa kutumia mgongo wa uheshimiwa ku-survive kwenye haya maisha yaliyojaa kila aina ya madhila siyo rahisi. Atachoka mapema sana na kunyoosha mikono.

Hizi kelele anazopiga piga sasa hivi anatumia ''pumzi'' ya akiba aliyokuwa ameihifadhi. Ikikata na mashabiki na marafiki wakinza kumkimbia atanyooka tu.
 
Membe sio wa kunyamaza atasonga mbele hadi aone mwisho wa barabara
Mtu aliyezoea kula na kunywa kwa kutumia mgongo wa uheshimiwa ku-survive kwenye haya maisha yaliyojaa kila aina ya madhila siyo rahisi. Atachoka mapema sana na kunyoosha mikono. Hizi kelele anazopiga piga sasa hivi anatumia ''pumzi'' ya akiba aliyokuwa ameihifadhi. Ikikata na mashabiki na marafiki wakinza kumkimbia atanyooka tu.
 
Labda aliwashitaki kwenye chama na chama ndio kimeamua, ingawaje kimaadili angempisha makamu mwenyekiti kuongoza kikao cha hukumu endapo yeye ndie mlalamikaji.
MLALAMIKAJI ANAONGOZA KIKAO CHA KUAMUA KUHUSU WALALAMIKAJI. HAPO INAKAAJE? HAKI ITATENDEKA? HAJI MANARA ANAKUWA REFARII KWENYE MECHI YA YANGA NA SIMBA, MWEEEEE
 
Hili Wana CCM mkilifumbia macho mmekwisha
Walishachelewa, eti yamekalia muhula atatoka akimaliza. Hii kasi ya kununua wapinzani ni kuuwa ccm masalia wabakie CCM tumbo wao mbele ya pesa wataona sawa tu atawale milele maadamu wanashiba.mtu kama pinda unategemea nn zaidi ya kusema ndio.

Wanalumumba wanaochekelea leo mwenzao kunyolewa kesho watanyolewa wao mwenye chake atakapowafurusha. Aliyesema atawabatiza kwa moto leo kabatizwa yeye.
 
Back
Top Bottom