CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

Tunasema Siku zote, hivi vyama Ni Mali ya watu badala ya taasisi, membe kafukuzwa uwanachama kwa sababu ya kutaka kumpinga jpm ndani ya ccm kugombea urais sio kingine.
 
CCM ni taasisi ambayo haiyumbishwi na mtu au watu,kuwepo/kutokuwepo kwa membe and his colleagues hakukifanyi chama kuyumba,membe and the alike ni kama jani kwenye nyumbani,je likindondoka nyumba itavuja?,CCM ina mifumo imara sio kama CHADEMA ambayo inamuabudu only one person

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sasa CCM inaabudu MTU, tena jpm..huo ndo ukweli.
 
Hapo CCM wamekosea kweli, hao watu walitakiwa wawekwe ndani (mahabusu) kwa kipindi kisichojulikana mpaka hapo rais atakapoapishwa, haiwezekani watu wanatukana mkuu wa nchi eti adhabu ni kuwafukuza chama.😎 😎 😎 😎
 
Kufuatia kwa kufukuzwa chamani Bernard Membe kwa makosa mbali mbali ya kanuni ya chama kama ilivoyoelezwa na msemaji wa chama ndugu Hamfrey polepole,hivi kwa mfano hapo mbeleni tena kama miezi kadhaa akaomba kujiunga tena na chama hicho hicho kama mwanachama mpya aombe kuwa kajirekebisha ,hivi sheria/ kanuni ya chama inasemaje ,je?atakubaliwa kwa masharti au huwa inakuwaje ufafanuzi tafadhali.
 
Upo sahihi na mtaji wa chama cha siasa ni watu
Mbona mashinji katoka Chadema kahamia CCM kwahiyo huo nao tuite mtego ? Na wengine wengi mpaka vyeo mmewapa kwenye siasa kawaida sana hiyo. Kama akitaka kuhamia upinzani wala sioni tatizo wamkubalie tuu.

In God we Trust
 
Ni mchezo kama game zingine tu na huu wa safari ni rahis kabisa.
 
Walichokifanya Ni divide and rule,Membe katimuliwa,Kinana karipio na Makamba kusamehewa.
Ili hata Kama walikuwa na mipango yao ivurugike.

Hapo itakuwa ngumu kuungana tena japo binafsi Makamba nilikuwa najua aweza kuomba msamaha.

Wanaamini Membe hatakuwa na nguvu tena hata wakimuondoa,ila wamepata hofu kubwa juu ya makatibu wasitaafu
 
Leo imetoka taarifa ambayo imewashtua watu wengi ya kufukuzwa kwa mwanachama nguli wa ccm mh bernard camilius member kutoka kwenye chama chake cha ccm akituhumiwa kwa makosa ya maadili..hili jamabo nililitegemea hasa tukielekea kwenye uchaguzi wa october.kwangu mimi nimenusa hataribya mtego uliotegwa na ccm kwa chadema kama wasipojinasua wakaingia kichwa kichwa wameliwa mazima na watabaki historia

Kama chadema wataamua kurudia kosa la 2015 na kumchukua member hakika atapata umaarufu mkubwa then atawaletea kiasi fulani cha mtaji wa kisiasa hata sehemu ya kusini ambaye yeye ndo prominent politicina ,na maeneo mengine ambako kuna ccm asili inayooneka kutengwa kwa siku za karibuni.lakini madhara yake ya takuwa makubwa sana huko mbeleni

Kama member ataamua kwenda ACT litakuwa pigo kubwa kwa chadema lakini ahuheni kwa ccm,ACT kitakuwa chama kikubwa cha upinzani ambacho kitaleta ushindani mkubwa kwa chadema na kuzigawa kura upinzani,lakini ni bora chadema kubaki na wanacham wake loyal ambao na amini watakuwa na impact kiasi kuliko kutema bigiji kwa karanga za kuonjeshwa!ushauri wangu

Chadema wakae mbali na membe kam ukoma kama kweli wanataka ku sustain after october 2020 tuko kwenye kipindi kigumu cha siasa ambacho ccm wamechokwa kila idara ila watatumia kila mbinu hata kama ni kimfukuza uwanachama Raisi mstaafu ili upinzani uingie kwenyw mtego ni bora kutumia silaha ulizozizoe kuliko kukodi silaha ambayo itakuletea madhara!

Sent using Jamii Forums mobile app
Bahati mbaya sana CCM ya Magufuli hakuna mtu mwenye umaarufu; wote wanategema umaarufu wa Chama. Anayeondoka ataondoka yeye na familia yake na pengine hata familia yake wanaweza wamkatalie
 
Back
Top Bottom