Elections 2010 CCM yatoa tamko kuhusu kitendo cha wabunge wa CHADEMA

Elections 2010 CCM yatoa tamko kuhusu kitendo cha wabunge wa CHADEMA

Genge la wahuni hutafuta uhalali kwa kuwazushia uovu wenye haki. Awali ya yote Si tu kwamba sitambui uhalali wa rais JK, bali hata waziri wake mkuu si halali. CCM wooote jibuni hoja hii na mnipe kipengele cha kisheria kinachomhalalisha Mizengo K. P. Pinda kuwa mbunge. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuna aina tatu tu za wabunge wa bunge la jamhuri 1. wabunge wa kuchaguliwa 2. Wabunge wa viti maalum 3. Wabunge wa kuteuliwa na rais ambao kwa mujibu wa katiba ni 10. Na mtu mmoja ambaye si mbunge lakini anapata wadhifa wa ubunge kwa mamlaka aliyopewa a.k.a mwanasheria mkuu wa serikali. Sasa mnieleze mbunge aliyepita bila kupingwa anaangukia kwenye kifungu gani cha katiba????
Kwa kuwa mmezoea kupindisha sheria, hata kudharau kura halali kwa mujibu wa sheria na kufanya ufedhuli wa kupinda matokeo mnaona ni jambo linalostahili.
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati
Sijamaanisha simjui ila kwa HOJA USIKA yeye ni nani mpaka aingilie madaraka ya Bunge alafu aedeeeeeeee bila uonga kuingilia mambo ya chama kingine cha siasa ambaco yeye siyo mwanachama wala kiongozi. Ndo maana nikauliza maana nimemuona kama chizi...
 
Cha ajabu ni kwamba walishaapa kuilinda katiba ambayo ndiyo iliyomweka Rais wasiyemtambua madarakani.

Mimi nafikiri ndio wanaitetea katiba kwani wananchi wana haki ya kumchangua rais wao. Kitendo cha mtu au kikundi cha watu ku over ride matakwa ya wananchi kwa kuitumia NEC ni kinyume cha katiba. NEC haijapewa madaraka yoyote na katiba kumchagua rais!!!!!
 
Tusijidanganye. CCM know what they are talking about.
Itakuwa vigumu kwa wabunge wa Chadema kufanya kazi bungeni iwapo chama chao hakiitambui serikali inayotawala.
Cha ajabu ni kwamba walishaapa kuilinda katiba ambayo ndiyo iliyomweka Rais wasiyemtambua madarakani.
Motion inayopelekwa na CCM itapita na wabunge watafukuzwa bungeni. Take my word.

Mnaojiita wasomi, weledi, bla bla ... hamlioni hilo?

Liko wazi hata kwa sisi wa kawaida.

Hawajaapa kwa Raisi, na pili hawajibiki kwa raisi. ingekuwa wamegomea uwepo wa spika kwa kuchaguliwa kwake ndo tugejiuliza IWEJE WAAPE KWA SPIKA ALAFU WAMGOMEE??

Mambo kama hayo unayosema kamuulize Pinda na Walema walioapa kwa raisi kama wasipomtambua rais.

CCM inataka watanzania wawe na akili kama yako wooote ndo watawale.

Mbunge hawajibiki kwa raisi.

Taasisi ya Raisi iko chini serikali kama muhimili sio BUNGE ambalo ni muhimili mwingine ulio na kiongozi wake.

Tafakali usije ukazeeka kama Makamb, bora uzeeke kama Mrhm Kolimba
 
Usichoelewa ni kwamba, CHADEMA hawamtambui Kikwete kwa sababu hakupewa madaraka yale kwa mujibu wa Katiba. Wao wameapa kuilinda katiba, na kwa kuwa katiba hiyo ilivunjwa wakati wa kumsimika Kikwete, basi hawamtambui Kikwete kama rais. Iwapo Kikwete angesimikwa kwa kufuata Katiba kuwa watu walipiga kura, zikahesabiwa sawasawa na kujumlishwa bila makosa, basi tatizo hili lisingekuwapo.

Jibu zuri sana. Chadema wanapigania kuheshimiwa kwa Katiba. Katiba yetu haisemi kuwa Kikwete ni Raisi wa Tanzania bali inataka Raisi atokane na matakwa ya Watanzania. Chadema wanasema kuwa Kikwete si Raisi aliyetokana na matakwa ya Watanzania bali ya wizi wa kura. Hivyo kumkubali Kikwete ni kuvunja Katiba ya nchi ambayo ibara ya 26 inataka wailinde na kuitetea.
 
Hivi chiligati cv yake ikoje?
Yaani anafikiri kuna la kuwazui wabunge wa chadema wasiingie bungeni wkt walichaguliwa bila mchakachuo?
Aache ndoto za mchana kama ni uwaziri anautaka ataupata tu bila nguvu.
Chadema watakuwepo na mambo ndo kwaaanza yameanza.
 
Huu ni upuuzi mwingine ulioandikwa na gazeti la porojo za kila siku

Wananchi wailaani, waionya Chadema
Imeandikwa na Waandishi Wetu; Tarehe: 19th November 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 167; Jumla ya maoni: 0

Habari Zaidi: Wananchi wailaani, waionya Chadema

KITENDO cha wabunge wa Chadema kutoka ukumbi wa Bunge wakati Rais Jakaya Kikwete alipoanza kuhutubia Dodoma juzi, kimelaaniwa na kuelezwa kuwa utovu wa nidhamu, kukosa busara, uchochezi, kutokomaa kidemokrasia na chuki dhidi ya Serikali iliyoko madarakani.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili jana kuhusu kitendo hicho, walilaani na kuwaonya wabunge hao kutorudia tukio kama hilo kwa vile hawakuwatendea haki wananchi waliowachagua na badala yake wamewadhalilisha na kujidhalilisha pia, chama chao na kujipunguzia heshima kisiasa.

Spika wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Pius Msekwa, Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa na Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema (TLP) ni miongoni mwa waliolaani kitendo hicho.

Kiongozi hao walisema kwa nyakati tofauti kuwa kitendo hicho kimedhihirisha jinsi wabunge hao wanavyofanya mambo kwa kukurupuka na jazba, hatua inayowafanya wasahau kuwa wametumwa na wapiga kura wao, wawawakilishe katika chombo hicho ambacho sasa wanakisusa.

Pamoja na kulaani, Msekwa alisema kitendo hicho kimekiuka taratibu za Bunge na wananchi wanapaswa kukikemea na kukilaani kwa nguvu zote, wakati Bunge likitafakari namna sahihi ya kulimaliza, ikiwa ni pamoja na kutumia taratibu rasmi, zinazoweza kuamuliwa na Spika aliyeko madarakani, Anne Makinda kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Bunge.

Kwa mujibu wa Msekwa, Chadema wamepotea, kwa sababu wanatenda makosa huku wakijua madhara yake kwa chama chao, kwa jamii na kwa Serikali na licha ya Bunge kuwa na utaratibu wa kushughulikia suala kama hilo la utovu wa nidhamu, jamii nayo ina nafasi ya kulikomesha.

Msekwa alisema, "mwaka 1995 CUF walifanya mambo kama hayo lakini hawa (Chadema) wamekosea zaidi, kwa sababu wanamkataa Rais aliyewekwa madarakani kwa amani na kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi, ilhali wamekula kiapo cha uti."

Kwa maelezo yake, Chadema wanafikiri hiyo ndiyo njia sahihi ya kumaliza matatizo yao au namna pekee ya kumfedhehesha, kumkomoa na kumdhalilisha Rais Kikwete, huku wakisahau kuwa Kikwete si wanayemwakilisha bungeni, bali wapiga kura wao.

"Wakubali wakatae, Kikwete ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wanalazimika kumheshimu. Kugomea Bunge ili kuonesha kutomtambua kwao, hakusaidii na zaidi kumeonesha kuwa hawana nidhamu, busara na wanahitaji muda zaidi ili wakue kisiasa … wametenda makosa hawa na wanahitaji kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za Bunge."

Tendwa alisema kitendo hicho si cha kiungwana wala ujasiri, bali ni fedheha na kimeidhalilisha Chadema na wabunge wake.

Tendwa alisema wabunge hao wangetumia njia nyingine za kistaarabu, kuonesha hisia zao au kupingana na mambo wasiyopenda na si kususa na kutoka bungeni wakati Rais akihutubia.

Alisema kwa vile wabunge hao wamekiuka sheria na kanuni za Bunge, hakuna sheria nyingine inayoweza kuwaadhibu zaidi ya zile za Bunge kwa vile wamefanya hayo wakiwa ndani ya Bunge.

"Umefika wakati viongozi wa vyama vya siasa, lazima waoneshe ukomavu wao kisiasa na si kufanya uamuzi wa jazba na kuwaumiza wengi. "Chadema inawaumiza wapiga kura wake bila ya wao kuwa na makosa na hii si sahihi.

Wanajaribu kuonesha mambo ambayo si sawa kwa kumkataa Rais aliyechaguliwa kwa kufuata taratibu zote za kikatiba, wameonesha kukosa adabu na busara, siwaungi mkono kwa hilo," alisisitiza Tendwa.

Katika hatua nyingine, Mrema alisema hatasita kuwazomea Chadema kwa kukurupuka, watakaporejea bungeni siku na wakati watakapoona mambo nje ya Bunge yamewashinda.

Mrema alisema, alikuwa miongoni mwa waliowazomea wakati wakitoka bungeni na atakuwa wa kwanza kuwazomea watakaporejea kwa sababu kufanya hivyo kutathibitisha unafiki wao katika siasa.

"Kumkataa Rais halali hakuna tofauti sana na uhaini, sasa wenzetu hawa inabidi waangalie madhara yake kwa chama chao na wapiga kura wao," alisema.

Mrema aliongeza kuwa kwa walichokifanya Chadema, wanastahili adhabu ya Bunge kwa sababu wanachochea chuki miongoni mwa watu dhidi ya Serikali iliyoko madarakani, kutokana na ukweli kuwa inaongozwa na Rais wanayemkataa.

"Waliapa hawa na hiyo ina maana kuwa wanamkubali Rais, sasa ina maana gani kuingia bungeni na kutoka kwa dharau?

Inabidi Chadema waelewe kuwa Rais ni wa wote na kama wana yao, basi wafute taratibu zinazostahili ili kuyawasilisha na si ‘nataka sitaki' zao za kugoma wakati Bunge wanalihitaji."

Kituo cha Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (Cegodeta), kimesema kitendo cha Chadema kutomtambua Kikwete, ni sawa na uasi unaoweza kusababisha uvunjifu wa amani na hatimaye machafuko na kinajiandaa kuifikisha mahakamani.

Taarifa ya Kituo hicho iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wake, Thomas Ngawaiya, iliitaka Chadema kuacha mara moja msimamo wake huo kwa kisingizio cha matokeo ‘kuchakachuliwa'.

"Cegodeta haiamini kwamba matokeo ya kura za urais yalichakachuliwa, kwa sababu Chadema walikuwa na mawakala kwenye kila kituo, kila kata na kila jimbo … mawakala wa vyama vya upinzani walikuwa wengi kwa ujumla wao, kuliko wa chama tawala," ilisema taarifa.

Ilikiri kuwa zilikuwapo kasoro ndogondogo katika takwimu za baadhi ya majimbo ambazo zilirekebishwa kama vile kurudiwa kwa uchaguzi katika baadhi ya majimbo, lakini hata hivyo, hizo zingeweza kubadilisha matokeo yaliyompa ushindi Kikwete.

"Chadema iache kudanganya wananchi. Inashangaza kwamba kati ya vyama saba vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi wa urais ni Chadema peke yake, ndiyo inayokataa kutambua matokeo, pengine inafanya hivyo kuridhisha wafadhili wao wa nje walioifadhili wakati wa kampeni," iliongeza.

Ilisema kutomtambua Rais ni kosa la jinai hasa baada ya wabunge wa Chadema kuapa kutii na kuiheshimu Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

"Kutii Katiba ya nchi ni pamoja na kumtambua Rais aliyechaguliwa kwa mujibu wa Katiba," ilisema.

Taarifa hiyo ilisema kwa kuwa Rais ni sehemu ya Bunge kitendo cha wabunge hao kususia huku wakipokea mishahara na posho ambayo ni jasho la wananchi, ni makosa na ni sawa na utapeli wa kisiasa.

Cegodeta imeipa Chadema mwezi mmoja kubadili msimamo wake huo vinginevyo itaifikisha mahakamani kwa kuvunja Katiba ya nchi.

Nayo CCM imesema tamko la Chadema kutotambua matokeo ya urais ni la uasi, na uhaini dhidi ya demokrasia na utawala wa nchi.


"Hii ni dalili kwamba Chadema wamechoshwa na amani iliyopo nchini; na sasa wanaandaa mazingira ya vurugu," ilisema katika tamko lake lililosainiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, John Chiligati.


Iliitaka Chadema kutambua, kwamba uchaguzi ulishuhudiwa na waangalizi wa ndani na nje ya nchi na wote wakatoa taarifa kwamba ulikuwa huru na wa haki.


Ilisema ni muhimu Chadema ielewe, kwamba kwa mujibu wa Sheria na Katiba ya nchi, matokeo ya Rais yakishatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi hayawezi kuhojiwa na Mahakama au chombo chochote.


"Hivyo katika hatua hii matakwa ya Katiba yametimizwa na Rais yupo madarakani kwa mujibu wa Katiba.


Nia yao wanataka tuache kazi ya kushughulikia maendeleo ya wananchi ili tuingie katika mgogoro wa kikatiba utakaodumu muda mrefu na kuiingiza nchi katika misuguano na mzozo wa kisiasa na kuchelewesha maendeleo ya wananchi," CCM ilisema.


Iliongeza kuwa Chadema iliacha jukumu la msingi na la lazima la kuhamasisha watu kujitokeza kupiga kura, na badala yake ikawa bingwa wa kuhamasisha wafuasi wake kufanya fujo, vitisho na vurugu kulikosababisha watu kuogopa kujitokeza kupiga kura.


CCM ilisema Chadema wanataka kumridhisha na kumfariji Dk. Willibrod Slaa baada ya kushindwa katika uchaguzi. "Ni vema wamtafutie shughuli ya kufanya kuliko kutumia mbinu ya kukataa matokeo.


Kuhusu wabunge na madiwani wa Chadema, CCM ilishangaa kuona wanaendelea na kazi wakati hawatambui matokeo ya Rais, na hawamtambui Rais na Serikali yake na kusema huo ni unafiki wa hali ya juu.


"Vipi wanajiandaa kuunda Serikali kivuli wakati Serikali yenyewe kwa maoni yao haipo? Unapataje kivuli wakati kitu cha kutoa kivuli hakipo?" ilihoji.


"Tunawashauri wajiondoe bungeni haraka, vinginevyo wajiandae kuondolewa kwa Azimio la Bunge, hadi watakapogundua kwamba Rais yupo na Serikali ipo," ilisema taarifa.


Ilisema Chadema wanadhihirisha uongo wao kwa kuwa kila chama kilijaza Fomu Na. 21A, 21B na 21C kwa ajili ya matokeo ya urais, ubunge na udiwani.


Jambo la ajabu wanakataa matokeo ya Fomu Na. 21A na kukubali Fomu Na. 21B na 21C ambazo zinawahusu wabunge na madiwani.


"Tunawashauri viongozi wa Chadema, kwamba uchag
uzi umekwisha, sasa tuache malumbano na misuguano ya kisiasa na tuanze kazi kwa pamoja ya kujenga nchi yetu," ilisema taarifa

Chanzo: Habari Leo
 
KIKWETE KUZINDUA MAANDALIZI YA UCHAGUZI 2015 DODOMA INAWAHUSU NINI CHADEMA???

Hivi jamaa, naona kweli watu mnaweza kuendelea kusikiliza hutuba kutoka kwa chanzo kimoja lakini mkatofautiana namna ambavyo kila mmoja wenu kaelewa. Ndg Kikwete alienda Dodoma kufanya mambo mawili tu: (1) KUZINDUA harakati za CCM kuktwaa tena madaraka mwaka 2015 ndio mtu anatarajia Chama kilichodai kudhulumiwa kikae kikisikiliza, au ndio kusema????


Pili, hutuba iliotolewa bungeni (2) ilidhihirisha kejeli kuhusu swala nyeti UDINI huku tukisikia kukemea mbegu hiyo waliopandikiza wenyewe huku tukikumbuka vema kwamba ni JANA YAKE TU ambapo mtoa mada alionyesha VIPAUMBELE vyake viliko kwa kufanya uteuzi wa awali WABUNGE VITI MAALUM (nafasi 10) kwa kuteua watatu mfululizo kwa msingi unaosaliti kabisa MAUDHUI yote hapo juu. Kama haitoshi, pia JANA YAKE hiyo hiyo MSAIDIZI wake Mkuu Ndg Bilal KUTOA AHADI nzito zenye upendeleo wa kidini kwa kikundi kimoja juu ya nyinginezo huku (3) tukiarajia wakati wowote Tanzania yangu isiyokua na DINI yake rasmi kuvishwa kanzu Jipya OIC. Ndio kilichokua kikipakaziwa UDINI kilitarajiwa kiendelee kusikiliza bungeni kweli??

Hi kweli hadi hapo, kulikua na haja gani Wabunge wa chama cha CHADEMA ambacho hadi sasa KINADAI KUPORWA ushindi wake kubakia kwenye viti kumsikiliza MTUHUMIWA wao ambaye UJUMBE WAKE KUU ilikua ni KUTANGAZIA WA-CCM wenzake Kwamba MAANDALIZI YA UCHAGUZI WA MWAKA WA 2015 ndio amekuja kuuzindua pale bungeni????
 
kama Mbunge wa CCM hajui kirefu cha SADC je Chiligati ataweza kuzichambua sheria na kugundua kuwa Chadema wamebugi?
Hana jipya MEMKWA huyo
 
Huko ni kutapatapa tu kisheria hakuna impact yoyote kwa wabunge wa CHADEMA, CCM hawakutarajia hizo reaction against uchakachuaji wa kura halali za wananchi!!!. Na wanatakiwa waelewe kwamba vita sio CHADEMA tu against CCM na NEC yao, bali wananchi wote wenye kuitakia mema Tanzania na mafisadi wa CCM
 
kwa nini chadema haikupata wabunge zaidi ya 100. Wabunge kiduchu kilele nyingi. Hawana adabu. Dhara kubwa. Eti wanatambua serikali lakini si matokeo. Kwa nini walitoka badala ya kueleza hoja yao kwa njia nyingine. Badala ya kuchezea chombo kikubwa kama bunge. Wachochezi wakubwa . Chadema has a devil sipirit.

Mtenda akitendewa hujihisi kaonewa, Wahenga walisema. Wakati Kikwete, Makame, Kinana na Usalama wa Taifa wanaiba kura hiyo kwako ilikuwa ni safi kabisa. Kitendo cha Chadema kupinga wizi huo kinakuuma sana na kukufanya uropoke na kuwaita waliodhulumiwa kuwa wana mashetani? Je si ni kweli kwamba wezi na wakiukaji matakwa ya wananchi kuwa wao wanaongozwa na Belzebuli. Unakumbuka anayempa kinga Kikwete ni nani? Nadhani Sheikh Yahya alitueleza kuwa atamuongezea ulinzi na Kikwete hajawahi kukana wala kuukataa ulinzi huo.
 
- Well, kwa maoni yangu Mh. Chiligati, amekosea sana maana sasa hapa anacheza ngoma ya mtego waliotegewa CCM, I mean kwa vitisho vyake hivi anakubali kwamba wabunge 46 tu wanaweza kutishia bunge zima lenye wabunge karibu 350 ambao pia wamechaguliwa na wananchi bila ya matatizo yoyote! Anaonekana kukerwa na kitendo hicho cha wabunge 46 tu kutoka nje, masikini ya Mungu haelewi kwamba hii ndio Demokrasia at work na ni kawaida sana, haelewi kwamba reaction yake itaishia kuwafanya waliotoka nje kuamini kwamba wamefanikiwa lengo lao la kututisha taifa zima wakati ukweli ni kwamba walichokifanya ni kitu kidogo sana ambacho kama yeye kweli ni pro-propagandist kama cheo chake ndani ya CCM kinavyotakiwa kuwa alitakiwa ku-play it down kwamba wala hakuwaona wabunge hao wakitoka kumbe walitoka?

- Ndio maana hili taifa itatuchukua muda mrefu sana kusonga mbele, yaani wabunge wakitoka tu kwenye hotuba ya rais, basi ni kuwatishia kuwafukuza, sasa ukiwafukuza umetatua nini hasa? Mh. Chiligati ana nafasi gani katika katiba ya Jamhuri hii mpaka kufikia kutishia kuwafukuza wabunge waliochaguliwa na wananchi kisa tu wamefanya kitu kidogo sana cha kususia kusikiliza hotuba ya Rais?

- Tulisema jana kwamba response za CCM ndio zitaamua ukubwa na udogo wa hii ishu, kwa mwendo huu CCM tayari wanaanza kuonyesha wasi wasi fulani ambao utaishia kumfanya mwananchi yoyote mwerevu aaanze kuwa na wasi wasi kwamba vitisho kama hivi kwa ishu ndogo sana ya wabunge kutoka nje wakati wa hotuba ya Rais wanajaribu kuficha nini? I mean hukuiba kura wala U-Rais, sasa kwanini unaanza kuwatishia wanaokusingizia kuiba, badala ya kuwa-ignore na kuendelea kutawala kama mujibu wa katiba ya Jamhuri unavyosema?

- Wabunge 46 tu waliotumwa na wananchi kuwawakilisha bungeni kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri, wameamua kususia hotuba ya Rais halafu kiongozi wa upande wa pili unawatishia kuwafukuza, badala ya kuendelea na kazi muhimu za taifa na wabunge wengine? Hivi hili taifa tumelogwa na nani hasa?


William.
 
- Well, kwa maoni yangu Mh. Chiligati, amekosea sana maana sasa hapa anacheza ngoma ya mtego waliotegewa CCM, I mean kwa vitisho vyake hivi anakubali kwamba wabunge 46 tu wanaweza kutishia bunge zima lenye wabunge karibu 350 ambao pia wamechaguliwa na wananchi bila ya matatizo yoyote! Anaonekana kukerwa na kitendo hicho cha wabunge 46 tu kutoka nje, masikini ya Mungu haelewi kwamba hii ndio Demokrasia at work na ni kawaida sana, haelewi kwamba reaction yake itaishia kuwafanya waliotoka nje kuamini kwamba wamefanikiwa lengo lao la kututisha taifa zima wakati ukweli ni kwamba walichokifanya ni kitu kidogo sana ambacho kama yeye kweli ni pro-propagandist kama cheo chake ndani ya CCM kinavyotakiwa kuwa alitakiwa ku-play it down kwamba wala hakuwaona wabunge hao wakitoka kumbe walitoka?

- Ndio maana hili taifa itatuchukua muda mrefu sana kusonga mbele, yaani wabunge wakitoka tu kwenye hotuba ya rais, basi ni kuwatishia kuwafukuza, sasa ukiwafukuza umetatua nini hasa? Mh. Chiligati ana nafasi gani katika katiba ya Jamhuri hii mpaka kufikia kutishia kuwafukuza wabunge waliochaguliwa na wananchi kisa tu wamefanya kitu kidogo sana cha kususia kusikiliza hotuba ya Rais?

- Tulisema jana kwamba response za CCM ndio zitaamua ukubwa na udogo wa hii ishu, kwa mwendo huu CCM tayari wanaanza kuonyesha wasi wasi fulani ambao utaishia kumfanya mwananchi yoyote mwerevu aaanze kuwa na wasi wasi kwamba vitisho kama hivi kwa ishu ndogo sana ya wabunge kutoka nje wakati wa hotuba ya Rais wanajaribu kuficha nini? I mean hukuiba kura wala U-Rais, sasa kwanini unaanza kuwatishia wanaokusingizia kuiba, badala ya kuwa-ignore na kuendelea kutawala kama mujibu wa katiba ya Jamhuri unavyosema?

- Wabunge 46 tu waliotumwa na wananchi kuwawakilisha bungeni kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri, wameamua kususia hotuba ya Rais halafu kiongozi wa upande wa pili unawatishia kuwafukuza, badala ya kuendelea na kazi muhimu za taifa na wabunge wengine? Hivi hili taifa tumelogwa na nani hasa?


William.

Well said William. Huyu mzee nadhani ana matatizo na kama CCM wakimuachia tuu hivihivi anaweza kuwaweka pabaya sana. Chadema wameshatuma message yao tena ya nguvu sana. Sasa CCM wanatapatapa wasijue la kufanya. Eti walisema kutoka kwa wabunge wa Chadema hakutaathiri chochote ! Hayo ya kuwafukuza yametokana na nini sasa? .......Wamekula ya Mbuzi sasa wameota mapembe (FM-Academia)
 
Hamna kitu kama hicho hakiwezekani kabisa, mmbunge ni mwakilishi wa wananchi waliemchagua. Maana yake atuwezi fanya democray ya ancient Greece leo where by all qaulified citizens gathered na ku-participate in direct democracy. Mambo hayo leo unaweza fanya kwenye maamuzi ya shule whereby parents and teachers can have a say.

Leo ni kitu ambacho hakiwezekani kitaifa kutokana na uwingi wa watu na time consumption ndipo hapo anapokuja mmbunge. Kazi yake Mmbunge ni kuzungumza kwa niaba ya watu waliomchagua kwa sababu atuwezi fanya direct democracy.

Na mmbunge anapita kwa namna ya democrasia wananchi waliopewa kuitumia dunia ya leo. Representative democracy inaanza mgombea anapotoa nia ya kuwania kiti, unafuata mchujo mwishowe uchaguzi mkuu kote uko anapitishwa kupitia mfumo wa 'kura' hili aweze shinda nafasi ya kuwasimamia. Kwa kuwa leo atuwezi fanya mambo through direct democracy. Kwa maana hiyo mmbunge ni sauti ya jimbo.

Sasa wao watamfukuza vipi mtu ambae kachaguliwa na watu, na wakifanya hivyo maana yake hawazitambui sauti za watu waliomchagua. Huu sasa ndio utakuwa u-monarchy na si demokrasia tena na ukiukaji mkubwa wa democracy. Hawa watu wamekaa juu sana kiasi kwamba hawaelewi mabosi wao halisi ni sisi wananchi na sisi ndio tuna amua. Na wabunge ni sehemu ya maamuzi yetu, ni kitu ambacho hawawezi fanya kisheria na wala amna sheria hiyo. Unless kama kuna maadili mengine yamevunjwa lakini kutoka nnje ya bunge kwa ajili ya protest is part of that democracy kwakuwa wao wameona jambo fulani si sawa katika demokrasia yetu, sasa hilo si kosa la kumfukuza mtu anaedai haki kupitia demokrasia. Vinginevyo ni kutowatambua maelfu ya wapiga kura.
 
Mheshimwa William! Heshima sana Mkuu.
Sasa utakubaliana na mimi kuwa SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA. CCM imepoteza kabisa confidency mbele ya umma kwa kuendekeza viongozi wabovu kama huyo Mzee aliyeita waandishi wa habari akasema Bashe sio raia wa Tanzania na kisha akaingia mitini, leo anataka kuwafukuza Wabunge, yeye amekuwa Spika??? Hata Spika hawezi ila mpaka pale sababu za Kanuni na sheria zitakaporuhusu kufanya hivyo
CCM ina kila dalili za kuanguka na wale tunaoipenda tutabaki midomo wazi. EL amemshauri Mh. Pinda achunguze ni kwa nini vijana wana hasira na CCM, inawezakana EL ameliona hili na anajua madhara yake kwa siku za Usoni, lakini hao wengine hapo wanataka kumpendeza rais hata ikibidi kufuta vumbi la viatu watafanya lakini they don't want to face the reality.
Amini usiamini madudu yanayoendelea yanazidi kuizamisha ccm na itazimi ingawa si kwa mapenzi yetu
 
Waziri huazimishwa madaraka na Raisi (halali) hivyo akipendezewa anaweza kuyapokonya.

Kwa upande mwingine, Mbunge hukabidhiwa madaraka na wananchi na mwenye kuweza kumpokonya ni huyo mpiga kura. Sasa basi, pindi Chiligati anaposema uwezekano wa CCM kuwafukuza kazi wabunge wa CHADEMA huyu bwana KAFUNIKA SIRI KUBWA MNO ambayo nashangaa wengi hatujaiona kabisaaaaaa!!!!

Keputeni anasema hivi kwa mujibu wa katiba ya CCM wabunge huchaguliwa taasisi hiyo hiyo inayoitwa CCM hivyo kuifanya CCM kupata baraka za kuweza kuwapokonya tu. Jamani mazoa mabaya sana sana kiasi kwamba wakati mwingine hawafanya WANGA kuanza kutimka mbio mchana mchana uchi wa mnyama kadhania kwamba ni usiku BADO GIZA imetanda. Mzee Chili, Tanzania kumekucha wote tumeamka ni kweupe hapa ndugu .... !!!!
 
CCM wafanye hivyo haraka waonje nguvu ya umma itakayowahukumu kwa uhaini walioufanya. CCM wasidhani ukimya wa watanzania ni udhaifu kwani watanzania walioibiwa kura zao wapo tayari kuidai haki yao iliyoporwa muda wowote watakaporuhusiwa kufanya hivyo. Kejeli kama za Kikwete, Chiligati na wengineo zinaweza tu kuchochea hasira za wananchi waliodhulumiwa na si kugandamiza utashi wao. CCM wanajua walichofanya safari hii mpaka umma kulalamika kiasi hiki. Wasimwage petroli kwenye moto unaofukuta ili wasijeungua kwa mwako wake.
 
Bogus are u CHADEMA who act like college students.Plus ur leader who need to go to anger management,he is a manipulater and tribalism .All for his personal selfishness.
 
Wapiganaji,
Hamna haja ya kuhofu. Hizo ni porojo za ccm ili wajisafishe na aibu iliyowakumba pale bungeni kwani hawakuizoea kabisa. Kwa ccm iliyozoea kupigiwa makofi hata ikivurunda, tukio la chadema kususia hotuba ya bosi wao mbele ya viongozi wote wa nchi (bara na visiwani) na wageni waalikwa, limewaaibisha na kuwauma sana. Jk amepata damage isiyo ya kawaida. Hata wananchi mitaani wanazungumza kwamba kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kubeza tukio hilo na akabaki na amani. Sasa wanachofanya ni kujibaraguza kwa mbele ya jamii kwa kuandaa eti tamko la ccm na vyama vingine ili angalau kurejesha heshima.

Mimi binafsi ninawashauri ccm. Wamepigwa bao. Watulie, watafakari namna watakavyotekeleza ahadi walizowatolea wananchi. Wakiendelea kupambana na chama makini kama chadema watapoteza muda wao na mbaya zaidi wataendelea kukijengea umaarufu na wao kwa upande wa pili wataendelea kudidimia. Mimi nimekwishawatahadharisha huko nyuma kuwa ccm wasijidanganye wakadhani chadema ni chama cha uswahilini kama kafu. Chadema ni chama makini, kimesheheni wasomi, wanaharakati na wakongwe waliobobea katika masuala mbalimbali ya uendeshaji wa nchi. Kila wanalofanya hawakurupuki tu, kama inavyofanya ccm na vyama vingine. Katika kosa mtakalofanya kisiasa ni kuwaondoa bungeni wabunge wa chadema. Sijui serikali ya ccm itamwongoza nani. Miaka mitano ijayo itakuwa jehanamu yenu, labda viongozi wa serikali wasifanye ziara mikoa na majimbo yote iliyowakataa ccm. Vinginevyo, historia itaandikwa.
 
Back
Top Bottom