Uchaguzi 2020 CHADEMA, ACT Wazalendo vyapigwa marufuku kunadi wagombea wasio wa vyama vyao. Waambiwa kufanya hivyo ni kuwachanganya Wananchi

Uchaguzi 2020 CHADEMA, ACT Wazalendo vyapigwa marufuku kunadi wagombea wasio wa vyama vyao. Waambiwa kufanya hivyo ni kuwachanganya Wananchi

Siasa haitaki hasira.
Ni kama Mchezo wa riadha,wote mnakimbia mbio zilezile,lakini waweza kumkabidhi mwenzio kijiti amalize mbio!hauwezi kuuliza kwa nini,hakumaliza mbio wewe mwenyewe!
Hapa naona ni timu mbili zipo katika kinyang'anyiro,mwingine anaushawishi na Taasisi za Serikali na vyombo vya dola na mwingine hana fursa ya kushawishi wala kuvisimamia vyombo vya dola na taasisi za Serikali.!!
Hizi ni mbio aidha ukimbie mwenyewe hadi mwisho wa kamba au umpe kijiti mwingine mwenye pumzi ili afike mwisho(finishing line).
 
Watanzania hatuna misimamo katika maisha yetu. Yaani kazi za serikali pia zimekuwa za kujikomba kwa Jiwe. Siyo kwa merit tena. Yaani kila mtu yuko busy ili aonekane anamzidi mwezie kujikomba. Kwa kweli tunahitaji katiba mpya kuondokana na hali hii.
 
Sasa wananchi wanachanganywa vipi wakati wanajua hii ni ACT na hii ni CHADEMA. Kwanini wana wasiwasi na hivyo vyama, kwani vipi mbona TLP ya Mrema na UDP ya Cheyo mbona walimsupport John Magufuli? Haya mambo ya kijinga yanashusha status ya nchi yetu kwa ujinga wa CCM. Tangu lini CCM na huyo msajili wanawaonea huruma wananchi wa Tanzania???
Mrema na Cheyo hawajasimamisha mgombea URAIS hivyo watampigia moja kwa moja MAGUFULI kwa sababu hawatamkuta mgombea URAIS wa TLP au wa UDP.
 
walikuwa wanaruhusiwa kukutana na wanachi? tuwe na kumbukumbu
Hao walishafuata sheria inavyosema! Unajua Chadema wanafeli sehemu nyingi sana. Kwa mfano mwaka jana wakati wa kuboresha daftari la wapigakura CCM ilikuwq inahamasisha wanachama wao kwenda kuboresha na kujiandikisha wakati Chadema walikuwa wanawakataza wanachama wao wasishiriki wakitegemea kuwa kutakuwa na Katiba mpya na kwamba hawatashiriki uchaguzi bila Katiba mpya.

Sasa uchaguzi umekuja tena hawakumbuki Katiba mpya. Wakishindwa watalalamika kuwa wameibiwa wakati hawakuwaandaa wanachama na washabiki wao!! Chadema ni shidaaa!!
 
Mbona jana yule kiongozi wa Tume alikua anamnadi mgombea fulani je sio kutuchanganya huko?
 
Sasa si asubiri aone kama wananchi aka wapiga kura watachaganya madesa.
Labda itawachanganya wale watoto wa shule wanaofika kwenye kampeni za CCM badala ya kukaa darasani na kusoma.
 
Wakuu mkistaajabu ya tume ya uchaguzi basi jiandae kuona ya msajili.

Jana kumbe Sisty kuwahi kote huko na boda boda pale makao makuu ya Chadema ni kupeleka barua ya katazo kuwa kuwanadi wagombea wa nje ya vyama vyao ni kukiuka maadili ya uchaguzi hivyo wamepigwa marufuku.

Yani hii ofisi ya msajili imekuja na kituko cha aina yake!



===
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Sisty Nyahoza ahudhuria kipindi cha Clouds360 kinachoendeshwa na Clouds Media na kuongea masuala mbalimbali wakati huu nchi ikiwa inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.

Aidha, katika mahojiano hayo, Sisty aliulizwa kuhusu masuala mbalimbali ikiwamo suala zima la Vyama vya Siasa kuungana na kushirikiana katika uchaguzi.

Akitoa ufafanuzi wa kina kuhusu suala hili Mh. Sisty Nyahoza alisema “Vyama pekee vimewahi kuungana ni ASP na TANU viliungana ikawa CCM. Kilichofanyika 2015 kwa jina la UKAWA ule ni ushirikiano kwamba wote mnabakia mna status ya kisheria kama chama cha siasa halafu mnashirikiana kwenye shughuli za kisiasa”

Ameongeza kuwa "Kisiasa kuna ushirikiano wa aina mbili, wa kwanza ni Coalition mnashirikiana kwa malengo ya kushinda uchaguzi. Halafu kuna Alliance mnashirikiana katika mambo yanayojitokeza tu katika siasa halafu kila mmoja anaendelea na shughuli zake, Coalition imewekewa masharti”

“Ni vyema haya mambo ya ushirikiano vile vyama vinataka kushirikiana viingie mkataba wakubaliane sera zetu zitakuwa zipi, tutawekaje wagombea, tutaundaje Serikali, tutagawanaje vipi ruzuku. Baada ya hayo makubaliano wayalete kwa msajili wa vyama vya siasa”

“Waliokuwa wameshasema wanaunga mkono wa chama kingine wanachopaswa wanatakiwa wabakie kama walivyobakia baada ya uteuzi wa Wagombea, baada ya uteuzi wa wagombea Urais Agosti 25 hawawezi kuteua tena mgombea Urais”

Aidha akiweka bayana kuhusu ushirikiano unaofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo na ACT Wazalendo Sisty Nyahoza amesema “Wao (CHADEMA, ACT) hawapaswi kwenda hadharani na kumsapoti mgombea yule kwa sababu ukiwa unamnadi mgombea wa chama kingine na wewe una chama na sera zako, wananchi hawajui baada ya uchaguzi mtaunda Serikali moja au utatekeleza ya kwako. Mnawachanganya wananchi”-
Naomba kuuliza Swali: kwa hivyo tumewaafikiana kwamba miaka 5 ya kwanza ya bwana magufuki , maisha ya wananchi hayajaboreshwa? Kwani alivyoomba Kura 2015, si alisema maisha ya wananchi yataboreshwa na tutakuwa Ulaya? Kama kashindwa awamu ya kwanza, kwanini apewe awamu ya pili?
 
Mrema hawajasimamisha mgombea wa URAIS kwa hiyo hategemei kuunda serikali.
Kwahio wakati wa Kampeni mgombea hawezi kuona kwamba hii kazi siiwezi/siitaki au fulani anaweza kuifanya vema kuliko mimi kwahio tumpe yeye...., kipi bora niendelee kuwaambia wananchi wanichague mimi wakati sitaki au niwaambie nani anafaa kuliko mimi?
 
Vyama vyote vyenye wagombea uraisi vinavyoacha kunadi wagombea wao na kunadi mgombea wa nyumba ya jirani

Mmebaki kuscreen shot post za watu na kuwawekea watu ambacho hawajaongea. Hiki ulichokiedit na kuniquote mimi, ni mimi ndio niliyesema? Mods huu mchezo wa kuedit post za watu na kuelekeza kwa watu wengine, unazidi kushika kasi hapa jukwaani, chukueni hatua.
 
Kwahio wakati wa Kampeni mgombea hawezi kuona kwamba hii kazi siiwezi/siitaki au fulani anaweza kuifanya vema kuliko mimi kwahio tumpe yeye...., kipi bora niendelee kuwaambia wananchi wanichague mimi wakati sitaki au niwaambie nani anafaa kuliko mimi?
Waliokuchagua ugombee kuanzia kamati kuu,halmashauri kuu na mkutano mkuu ina maana wote walikuwa akili hawana walipokuteua? Wewe uliyeteuliwa ndio una akili kubwa!??
 
Hata akinadiwa Nani Bora kuliko kumnadi mtu wa nje. Sheria za kipuuzi kweli
 
Wakuu mkistaajabu ya tume ya uchaguzi basi jiandae kuona ya msajili.

Jana kumbe Sisty kuwahi kote huko na boda boda pale makao makuu ya Chadema ni kupeleka barua ya katazo kuwa kuwanadi wagombea wa nje ya vyama vyao ni kukiuka maadili ya uchaguzi hivyo wamepigwa marufuku.

Yani hii ofisi ya msajili imekuja na kituko cha aina yake!



===
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Sisty Nyahoza ahudhuria kipindi cha Clouds360 kinachoendeshwa na Clouds Media na kuongea masuala mbalimbali wakati huu nchi ikiwa inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.

Aidha, katika mahojiano hayo, Sisty aliulizwa kuhusu masuala mbalimbali ikiwamo suala zima la Vyama vya Siasa kuungana na kushirikiana katika uchaguzi.

Akitoa ufafanuzi wa kina kuhusu suala hili Mh. Sisty Nyahoza alisema “Vyama pekee vimewahi kuungana ni ASP na TANU viliungana ikawa CCM. Kilichofanyika 2015 kwa jina la UKAWA ule ni ushirikiano kwamba wote mnabakia mna status ya kisheria kama chama cha siasa halafu mnashirikiana kwenye shughuli za kisiasa”

Ameongeza kuwa "Kisiasa kuna ushirikiano wa aina mbili, wa kwanza ni Coalition mnashirikiana kwa malengo ya kushinda uchaguzi. Halafu kuna Alliance mnashirikiana katika mambo yanayojitokeza tu katika siasa halafu kila mmoja anaendelea na shughuli zake, Coalition imewekewa masharti”

“Ni vyema haya mambo ya ushirikiano vile vyama vinataka kushirikiana viingie mkataba wakubaliane sera zetu zitakuwa zipi, tutawekaje wagombea, tutaundaje Serikali, tutagawanaje vipi ruzuku. Baada ya hayo makubaliano wayalete kwa msajili wa vyama vya siasa”

“Waliokuwa wameshasema wanaunga mkono wa chama kingine wanachopaswa wanatakiwa wabakie kama walivyobakia baada ya uteuzi wa Wagombea, baada ya uteuzi wa wagombea Urais Agosti 25 hawawezi kuteua tena mgombea Urais”

Aidha akiweka bayana kuhusu ushirikiano unaofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo na ACT Wazalendo Sisty Nyahoza amesema “Wao (CHADEMA, ACT) hawapaswi kwenda hadharani na kumsapoti mgombea yule kwa sababu ukiwa unamnadi mgombea wa chama kingine na wewe una chama na sera zako, wananchi hawajui baada ya uchaguzi mtaunda Serikali moja au utatekeleza ya kwako. Mnawachanganya wananchi”-

Uchaguzi uliopita TLP ilikuwa na mgombea wa Urais wa Tanzania lakini Mwenyekiti wao Mrema alitangaza kumuunga mkono Magufuli na alifanya hivyo.
NEC His Master's Voice.
 
Waliokuchagua ugombee kuanzia kamati kuu,halmashauri kuu na mkutano mkuu ina maana wote walikuwa akili hawana walipokuteua? Wewe uliyeteuliwa ndio una akili kubwa!??
Kwani wananchi wana akili ndogo ?, si wataamua wanachokiona siku ya siku...., yeye mgombea na Chama kinaona fulani anafaa iweje NEC ndio ilazimishe mtu apigiwe kura wakati yeye mwenyewe anaona vinginevyo?
 
Hao walishafuata sheria inavyosema! Unajua Chadema wanafeli sehemu nyingi sana. Kwa mfano mwaka jana wakati wa kuboresha daftari la wapigakura CCM ilikuwq inahamasisha wanachama wao kwenda kuboresha na kujiandikisha wakati Chadema walikuwa wanawakataza wanachama wao wasishiriki wakitegemea kuwa kutakuwa na Katiba mpya na kwamba hawatashiriki uchaguzi bila Katiba mpya.

Sasa uchaguzi umekuja tena hawakumbuki Katiba mpya. Wakishindwa watalalamika kuwa wameibiwa wakati hawakuwaandaa wanachama na washabiki wao!! Chadema ni shidaaa!!
Mrema alishafuata sheria ipi?
Mimi si mwana siasa
Tafadhali nijibu kutaalamu
 
Back
Top Bottom