Elections 2015 CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!

Bila kusahau Ikulu itajaa wachaga na watu wa kaskazin tu.Yaan mungu atuepushe mbali na hiki chama kuchukua Dola.
 
Naomba kujua chama ambacho kimeacha mlango wazi kwa mwanachama kukishitaki mahakamani?naamini hakuna chama kinahitaji kupoteza muda na wanachama wake mahakamani badala ya kwenda ku-preach sera na malengo kwa wananchi.
 
Mleta mada ameleta mada ya kijinga.

CHADEMA haiwezi kuleta udikteta kwani tayari tunaishi kwenye udikteta unaosimamiwa na CCM.

Unajaribu kuwatisha watu ambao hawatishiki tena.

Kama ni kupigwa mabomu ya machozi, CHADEMA wanaongoza.

Kama ni kubambikiwa kesi lukuki, hata za kuitwa magaidi, CHADEMA wanaongoza.

Kama ni kupigwa na polisi na wapenzi na wanachama wao kuuwawa pia, CHADEMA wanaongoza.

Niseme nini tena ili juha kama huyu mleta mada aache kuleta mada za kipumbavu?

Ni Watanzania gani hao mnaodhani wanadanganyika na tisha-toto hizi za kijinga?
Moderator na Invisible tafadhali muwe mnatuepusha na wazushi kama hawa, wanaotaka kupotosha ukweli, kwamba nchi imefika pabaya, na udikteta huu umeletwa rasmi na CCM.

Uthibitisho ni Sheria ya Makosa ya Mtandao ambayo inakiuka Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayothibitisha haki ya Uhuru wa Maoni, Kujieleza, Kutafuta na Kusambaza taarifa muhimu kwa jamii.

Sasa bloggers nao watafunga mdomo?
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi, hili swali niliwahi kuliuliza kule nyuma, ila kilichotokea katika mchakato mzima wa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema, ndio muendelezo wa huu udikiteta niliuozungumzia hapa, na sasa ni dhahiri Chadema inakwenda kuchukua nchi October kupitia Lowassa, hivyo sasa for sure Tanzania tunakwenda kuongozwa na chama cha kidikteta, na kiukweli Lowassa ni kiongozi dikteta wa ukweli, ila pia nakubaliana na hii hoja yangu kuwa Tanzania kwa hapa tulipofikia, tunahitaji chama cha kidikteta na rais dikteta kama Lowassa ambaye atakuwa ni benevolent dictator kufanya mambo yaende.

Ingekuwa kama huu udikiteta wa viongozi wa Chadema, isingewezekana kwa mwanachama mpya anapokelewa leo, kesho anakwenda kuchukua fomu za urais ambazo zilipaswa kutolewa na Katibu Mkuu wa chama, lakini kufuatia Lowassa kukaribishwa kidikiteta, Katibu Mkuu nae akaamua kuleta udikiteta wake kugoma kutoa fomu, Mwenyekiti dikteta akautumia udikiteta wake, kupoka majukumu ya Katibu Mkuu, na kutoa fomu yeye!, Katibu Mkuu atake asitake!, anune asinune!, asuse asisuse!, fomu zikatolewa!.

Kiukweli mwanzo niliukasirikia udikiteta huu kwa jinsi ulivyoshughulikia suala la Zitto nikiamini alionewa!, lakini leo nimefarijika baada ya kujiridhisha kuwa kumbe huu udikiteta wa Chadema, ni msumeno unakata kote kote, kama upanga wa makali kuwili!, unao opatare bila ubaguzi, kama upanga huu au msumeno huu, ulimkata Zitto na kuishia kujitimkia zake, sasa umemkumba Katibu Mkuu ambaye ameamua kununa na kususa, then huu ni udikiteta wa haki bin haki, hauna double standards, yaani uamuzi wa kupiga mapanga shwa... Zitto alipoleta za kuleta, akapigwa panga shwa... Mwamba Lowassa alipopiga hodi Chadema, kuna watu wakataka kugoma kumfungulia mlango eti tuu kwa vile yuko kwenye listi ya mafisadi wa Chadema, ule ule udikiteta ukasaidia, mlango ukafunguliwa kinguvu, Lowassa akaruhusiwa kuingia, na sasa ndio mgombea wa Chadema na UKAWA!, maadamu nyie mliko Chadema unaujua udikiteta huu, dawa iliyobakia sio kususa, ni ama mjinyamazie tuu na kuendelea na utekelezaji wa majukumu yenu ya kila siku, au tumieni haki yenu ya kidemokrasia ya fungasheni na ondokeni!.

Japo maamuzi ya kidikiteta sometimes sio mazuri, lakini kiukweli kwenye hili la Lawassa, udikiteta huu ni mzuri, kwa sababu ndio utakaisaidia Chadema kuingia ikulu.

Tena namsisitizia Rais Lowassa akifika tuu Magogoni,

  1. Kazi ya kwanza ni kuipurura CCM malizo zake zote ilizozikwapua kwa umma wa Watanzania na kujimilikisha, hivyo CCM itabaki landless, penniless na poweless hivyp kujifia zake natural death!.
  2. Kazi ya pili, ni kuzirudisha zile nyumba zote za umma viongozi wa CCM walizijigawia wakisimamiwa na Fisadi John Pombe Magufuli ambaye alizigawa hadi kwa vimada wake!.
  3. Kazi ya tatu ni kuwapandisha kizimbani mafisadi wote, wakiwemo wa EPA, na wale mafisadi wawili waliokuwa wapangaji wa ile nyumba nyeupe!.
  4. Fisadi wa kwanza kwa kufanya biashara ikulu ile kinga ya kutokushitakiwa inahusu kutokushitakiwa kwa kutekeleza majukumu ya urais, kwa vile kufanya biashara ikulu sii miongoni mwa makumu ya urais, then kinga ile haihusiki na wanashitakika!.
  5. Wa pili ni kwa kupageuza pale 'patakatifu' petu kugeuka ni pango la walanguzi!, tena hadi kesi ya tule tujizawadi twa suti 3 za Seville itatinga mahakamani,
  6. Nyingine nyingi zitafuatia...

Na kwa jinsi baadhi ya watu walivyomtesa rais wetu huyu, akiingia kuna watu sijui watakomaje!.

Pasco
 
Nafanya rejea kuhusu muktadha wa udikiteta ndani ya nchi ambao Chadema inauspicious kelele kupitia UKUTA na Udikiteta halisi uliomo ndani ya Chadema, jee tuishauri Chadema kuondoa kwanza boriti kwenye jicho lake ndipo lifuate kibanzi kwenye jicho la mwenzie? !.

Au mkuki ni kwa nguruwe tuu?!.

Nashauri katika utekelezaji wa kuuvunja huu UKUTA Mkuu nje, Chadema pia ivunje vile vikuta vyake vidogo vya ndani by practising what you preach! .
Jumapili Njema.
Pasco
 
Hapo ndo unafiki wa pasco unapoaanza mtu akisimamia katiba mnasema dikitetor akishidwa kusimamia mnaanza ooh hakuna uwajibikaji.
je mnataka wafanye nini?
Mkuu JME, hapa nazingatia sana ulichosema kuhusu mtu akisimamia katiba kuhusu dhana ya udikiteta! .

Pasco
 
Bandiko hili linazungumzia faida za udikiteta.

Pasco
 
Mkuu Kijakazi, naomba kuutumia ujumbe wako huu kuhusu udikiteta uwafikie wana UKUTA! .

Pasco
 
Mkuu the boss 23, kumbe taifa letu linahitaji viongozi wenye elements za udikiteta, waambie hawa jamaa zetu ili hitaji ili lieleweke kwao.

Pasco
 
Mkuu 50Thebe, ni kweli CCM wanaongoza kidikteta! .

Pasco
 
Nadhani chadema pamoja na kuwa kilishakufa kinapaswa kifutwe kwa sababu kinakiuka kaitiba ya JMT
 
Pasco kumbe ulishalidadisi hili kitambo, shikamoo blaza
 
bw pasco tanzania inahitaji kiongozi dikteta ili kurudisha misingi ya azimio la arusha​,
Mkuu Prince asante kwa taarifa hii kuhusu hitaji la kiongozi dikiteta na ni kweli dikiteta John Pombe Joseph Magufuli anarudisha misingi ya Azimio la Arusha, hivyo tuungane wote kuwashangaa wana UKUTA? !.
Pasco
 
Pasco, unaweza kuwa na hoja ya maana, lakini kwa maoni yangu, naona unaiwasilisha vibaya; na au kwa nia mahususi kwako binafsi, yenye lengo maalum ambalo haliwezi kutusaidia sana kama taifa, bali kuwaondoa watu katika hoja ya msingi-kwamba katika muktadha huu wewe Pasco wa JF unaweza kuwa unafanya "spinning". Wewe mwenyewe unafahamu kwamba Chadema kama chama cha siasa kisheria na kikatiba inayo haki ya kujiwekea utaratibu wake maalum kwa wanachama wake.

Pasco, wewe unafahamu kwamba kujiunga na chama au kikundi chochote ni sawa na kuingia mkataba, na kwenye mkataba huwa kuna kipengele kinachoeleza ni wapi au ni namna gani mtashughulikia mgongano au kutoelewana iwapo itatokea hivyo. Suala la kuzuia mwanachama kukimbilia kortini na badala yake kusisitiza kumaliza suala hilo ndani ya vikao vya chama haiwezi kuwa udikiteta hata kidogo kiasi cha wewe kuanza kuvuruga maoni ya wanaopinga kuzuia mikutano ya kisiasa ambayo imeruhusiwa na katiba ya nchi.
 
Mkuu 50Thebe, ni kweli CCM wanaongoza kidikteta! .

Pasco

Mkuu Pasco

Heshima kwako.

Mbona unaninukuu namna hii? Mchango wangu ule ulikuwa kwenye context nyingine ambayo napata ukakasi ikiwa naweza kurudia kuandika content ile ile kwa context ya sasa.

Pengine niseme hivi: takribani miezi 12 sasa tumeshuhudia mabadiliko makubwa sana kupindukia kwenye siasa zetu hususani kwenye eneo la ideology za vyama hivi (ingawa haipo wazi sana). Kwa mfano, waliolaani ufisadi kiasi cha kuombea tupate raisi dikteta sasa wanalaani udikteta. Waliotuhumiwa kwa ufisadi sasa wameunda chombo (mahakama ya mafisadi - wahujumu wa uchumi). Bila shaka wataunda chombo maalumu kitakachochunguza namna uhujumu uchumi unavyofanyika badala ya polisi na PCCB. Hivyo kuna contrast kubwa sana ya maisha ya siasa zetu toka mara ya mwisho nilipotupia maoni yangu haya.

Kwa muhtasari huu na swali lako kwamba: CCM inatawaliwa kidikteta ama lah? Maoni yangu ni kwamba CCM haitawaliwi kidikteta. Tunachoshuhudia ni usimamizi wa sheria, kanuni na taratibu zikiwamo 'presidential decree' ndio zinatumiwa na serikali ya CCM. Wakati mwingine najiuliza ikiwa Mh Raisi Magufuli anatumia katiba tofauti na ile iliyotumika wakati wa muhula wa Mh Raisi Kikwete.

Nihitimishe kwamba: CCM hawaongozi nnchi kidikteta. Bali safari hii wameonesha kusimamia sheria, kanuni na taratibu kwa umadhubuti zaidi. Na pale miongozo hii inakwama tayari wametuonesha kwamba wanaweza kutumia 'presidential decree' ili kupata matokeo.

Nawasilisha.
 
Mkuu MwanaHaki hapa umesema kweli kuhusu serikali ya kidikteta japo wakati ukiandika haya ilitarajiwa Chadema ndio washinde na kuendesha udikiteta huu, maadam CCM ndio iliyoshinda na kuuendesha udikiteta ule ule ambao Chadema ingeuendesha, kuna ugumu gani Chadema kumsupport Dikiteta Mzalendo John Pombe Joseph Magufuli? .

Pasco
 
Mkuu Pasco, u dikteta sio jambo la kusifiwa likitoka chama chochote. Nafikiri JPM sio Dikteta , nadhani ameona nchi haina nidhamu ya kazi na wanasiasa pia hawana nidhamu ya sheria wala kazi. Nashauri Raisi ajikite kuwatumikia wananchi ila pia awaruhusu wanasiasa wafanye siasa maana ni kazi yao na sheria zinawaruhusu. Ukitaka mtu àheshimu sheria lazima wewe pia uwe mfano wa kwanza wa kuheshimu sheria. Nafikiri Rais wetu ataliona hili jambo kwa mwanga ulio bora maana anachofanya kwa watanzania ni chema ila aache wengine nao watimize wajibu wao
 
Nadhani chadema pamoja na kuwa kilishakufa kinapaswa kifutwe kwa sababu kinakiuka kaitiba ya JMT


kufutwa ndo suluhisho la kutatua suala la
udikteta? hivi kama na wewe ndo umetoa
mchango ktk post hii tuna safar ndefu sana
ktk elimu yetu kilikufa chadema magufuli
kura milion 8 chadema wanafuata milion
kura milion 6 halafu kilikufa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…