Uchaguzi 2020 Chadema imekosa ajenda za msingi ya kupambana na chama tawala!

Uchaguzi 2020 Chadema imekosa ajenda za msingi ya kupambana na chama tawala!

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Inashangaza sana na inatia huruma, dunia nzima ipo katika wimbi zito la kupambana na ugonjwa wa Covid-19. Ugonjwa ambao umeua watu zaidi ya laki moja dunia nzima.

Wanasiasa na wafuasi wa Chadema wanakesha mitandaoni kuiombea vibaya nchi yao ipate maambukizi ili chama tawala kionekane kilishindwa kuchukua hatua. Je huu ni uungwana?

Wanadiriki kupost picha ya maiti ikichukuliwa na wahudumu wa afya kuonyesha sasa mlipuko upo katika hali mbaya. Lakini hata kama ni kweli walipaswa kupost na kutoa maelezo ambayo sio ya kufitinisha kwamba hatua stahiki hazichukuliwi.

Hawajiulizi swali moja kubwa kwamba ugonjwa huu haubagui na watu ambao wako katika hatari ya kuupata ni watu wasio na uwezo.

Mimi binafsi nilitarajia wawe pamoja na serikali kuonyesha mshikamano katika kupambana na hili janga. Lakini wao siku nzima ni kuombea mabaya tu hasa wanaombea idadi ya reported cases ziwe nyingi. Na hii itawsaidia nini?

Mimi nilidhani wao kwa miaka hii mitano ya serikali ya CCM chini ya Rais Magufuli wangepambanua nini ameshindwa kutekeleza katika ilani yake ya Chama ili ndio ziwe ajenda za kumkabili kisiasa,lakini sio kumuombea mabaya ili Covid -19 iuwe watanzania wengi ili waanze kumzodoa.

Labda sababu jamaa amepiga kazi tena ambazo zinaonekana kwa macho ndio maana wamekosa ajenda za kumkabili, zaidi ya maneno ya kitoto kama amejificha Chato kukwepa Covid -19.

Walianza na kisingizio cha zuio la kisiasa eti limewaporomosha kisiasa. Lakini yeye alizuia ile mikutano ambayo for publick interest ingezuia watu wasijengewe Mabarabara,zahanati na vituo vya afya,Mradi kama JNHHP, madaraja kama wami na busisi to kigongo n.k.

Na zuio hili alilifanya kwa mujibu wa wa katiba kama ibara ya 30(1) ya katiba ya JMT inavyo ainisha. Na ndio maana kuna mdau aliwaambia kama kama hili zuio ni udikteta basi nendeni HC mkaweke petition,wote walifyata mkia.

Na bahati nzuri aliruhusu siasa kwenye majimbo ili wasimwingilie na afanye maendeleo kwa manufaa ya umma.

Leo hii wamebakiza kuombea mabaya kwa nchi yao,na kuibua kilio cha tume huru wakati miaka yote ipo huru na wanashinda ubunge na madiwani. Inasikitisha sana kuwa na Chama cha namna hii.
 
Nakubaliana na wewe hili la Covid 19 wanavyolifurahia, wanasahau kuwa wanakata tawi walilolikalia.

Binafsi naona serikali kwa nafasi yake imejitahidi sana wanaotaka total lockdown wajue na hali ya uchumi wa Dunia ulivyo na vipato vya watu hasa maskini,kitu muhimu ni kuendelea kutoa elimu namna ya kujikinga.

Baadhi ya nchi dunia ya kwanza huko tayari wanataka kuruhusu baadhi ya shughuli ziendelee hii ina maanisha wameshaona athari ya kiuchumi.

Ushauri wangu tuisupport serikali katika janga hili ili kwa pamoja tuvuke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ndicho kilichopo kazini mkuu.

chadema sijui wataambia nini watu october[emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ndivyo wewe unahangaikia nini? Kazi nzuri aliyoifanya ambapo kila mtu hatoisahau ukiwepo wewe ni suala la utekaji na kuwapoteza watu wasio na hatia. Pamoja na mashambulizi ya risasi mchana kweupe kwa baadhi ya wanasiasa akiwemo Mh Lissu.

Suala la corona msiligeuze. Rejea matamko ya RC Makonda. Bila kumsahau aliyesema ni kaugojwa tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
chagu wa malunde, Kwa mara ya mwisho ninachokumbuka, ni kuwa mkuu pamoja uongozi mzima hawautambui uwepo wa Chadema nchini. Amefanya mashauriano na vyama anavyodhani ndivyo vya upinzani, akakitenga Chadema.

Sasa sioni ni kwa nini muendelee kuhangaika na chama au jumuia msioitambua !!. Shaurianeni na vile mlivyovitambua akina Cuf ya Lipumba, Nccr ya Mbatia nk. Kwa mtazamo wa Ccm ni kuwa Chadema hakipo , hangaikeni na vile vilivyopo.

Kuhusu COVID 19, ni kuwa kuna mambo yameamuliwa kisiasa na hii italeta shida. Unafunga mashule na vyiuo lakini unaruhusu mikusanyiko sokoni, makanisani, misikitini , vituo vya mabasi nk. Hapo umefanya nini ?!.

Wapinzani walishauri kabla hatujawa na ugonjwa na wagonjwa. Kusimamishwa kwa usafiri wa anga, hasa kutoka mataifa yalioathirika zaidi. Lakini walipokea majibu ya kejeli mengine kutoka kwa msemaji wa chama eti "Corona ni kama wapinzani (Chadema) eti watapamba na nayo kama wanavyopambana na chadema". Mwingine eti hatuwezi kuzuia watalii sasa leo wako wapi ?!.

Usikimbilie kuwalaumu Chadema, tatizo limo humo humo mwenu kwa sababu hawahitati ushauri toka upande wa pili.

Odhis *
 
Odhiambo cairo,
Ishu sio kutoa ushauri, ishu ni kufurahia taifa lako lipate matatizo hasa la janga kama hili, jambo ambalo sio zuri. Kuhusu kutoitwa ikulu hilo ni suala lingine maana kutoitwa ikulu sio kwamba hawatambui ila labda amepima ninyi niwa aina gani.Maana huwa kuna wapinzani na wapingaji. Labda ameshagundua nyie ni wapingaji na hamuwezi kukaa meza moja mkajadili sasa awaite ili iweje?

Pia unadhani hata kama tungesimamisha usafiri wa anga huu ugonjwa usingepenya? Maana kuna ndugu zako wanatoka Kenya sasa hivi wanapita njia za panya badara ya kupita border ya sirari,hujui kama hao nao wanaweza kuuleta na huu ugonjwa unaweza kukaa na mtu kuanzia siku ya kwanza mpaka ya kumi na nne.

Huu sio wakati wa kuleta Chuki ati kisa kuna mtu aliwaita nyie corona virus. Trump aliwadhihaki China lakini wachina wamewasaidia wamarekani huu ndio uungwana.
Kwa hiyo mnapaswa muonyeshe ukomavu wa kisiasa.

N.b. Mimi sio mwana CCM ila nazungumzia ukweli wa mambo.
 
Mulokozijr12,
Dhambi zenu ndiyo zinaleta majanga kabisa..Hivi kwa akili yako unaweza kutueleza kwa ukweli kua hao wapinzani wetu wanashangilia ili janga? Hivi wao kutoa mawazo yao kama lockdown ina maana wana support kuwepo ili janga?

Kenya, S.Africa, Uganda, Botswana, Rwanda, England, Spain wameweka lockdown je,CHADEMA ndiyo wamewashauri hivi?

Kwa upumbavu wa hivi unastahili kujifunza jinsi ya kufanya siasa wala siyo upuuzi kama huu...nyie ndiyo mlimpigia makofi na vigelegele Pole Pole alipowaita CHADEMA NI COVID-19
 
Back
Top Bottom