Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Status
Not open for further replies.
(1) Rachel au Regia wamelalamika? Hapana. Wameelewa na kukubaliana na maamuzi ya chama chao. Tuwaunge mkono basi.

(2) Lengo ni kuleta mabadiliko Tanzania mwaka huu. Wananchi wamechoshwa sana na utawala wa miaka 49 wa TANU na CCM. Wengi hapa tunamkubali Slaa aongoze hayo mapambano. Mbona wengine mnatafuta namna ya kutugawa tena? Tuungane ili kushinda kwa sasa, na tukubali maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA.

(3) Watanzania wataunda Katiba Mpya ya Tanzania na hata ya CHADEMA, baada ya kuing'oa CCM.

(4) Wale wanaoutumia muda wao hapa kuikosoa CHADEMA kwa namna ya kutaka kuiongezea nguvu wanafanya vyema. Wale wanotaka kuidhoofisha wanapigania CCM ibaki madarakani.

(5) Nadhani CCM wanapata ahueni wanopoona namna akina MMKJ wanavyojitahidi kupooza nguvu ya CHADEMA.

Nikiwa mwanachama hai wa Chadema siamini mawazo ya mwanachama au mwananchi yana nia ya kuua Chama. Mtazamo na maoni ya mtu yeyote hayana nia ya kuua chama. Maswali au mshangao hauna nia ya kuua chama.

Chama cha siasa kinajiiua chenyewe kwa matendo, sera, maadili na mwendesho wake. naichukia CCM kwasababu ya umangimeza, imekataa kusikia kilio cha wananchi na kero zake kwa kukumbatia chama zaidi ya sera na kanuni zake.

Nikiwa mmoja wa wanaCHADEMA napenda kukosolewa kuulizwa na kuhojiwa kwani hii yote kwa Chama watu na viongozi makini ndiyo misingi ya kufanya sahihi. Sera ya zidumu fikira sahihi imekufa haipo na haitakuja. Yeyote mwenye mawazo, yanayofanana na yasiyofanana anakaribishwa kwani wote wanatoa changamoto kujenga chama imara na chenye misingi bora kwa wanachama na wananchi.

kama kunamakosa ni haki ya wanachama wananchi kuuliza, kuhoji na kutaka maelezo bila ya vitisho kwamba kila mwenye hoja tofauti anawalakini. Hiki ni chama cha siasa sio kampuni. Naungana na wote wenye mawazo chanya na wale wenye mawazo hasi kwa manufaa ya chama. CCM inakufa kwa sababu kilaanayewakosoa anaonekana adui na kutupwa kuzimu, sitaki chama changu kirithi huu upupu.
 
Hakuna kikao kingine cha juu cha kutengua au kuhoji maamuzi hayo ya wananchi.

Hii itasababisha umakini katika kura za awali na wananchi wenyewe kujua wasitegemee kugombolewa mbele ya safari na wagombea watajua kabisa kuwa ukicheza vibaya ni pingu (siyo kamati ya maadili) na ukishindwa umeshinda hakuna kubebwa.

Jamani hii ndiyo demokrasia. Demokrasia ni pamoja kuacha makosa yatokee na wananchi wakosee, na wagombea wakosee. Demokrasia siyo lazima mtu tunayemtaka ashinde bali mchakato utoe uwezekano wa mtu tunayemtaka kushinda kushindwa. Demokrasia inayombeba fulani siyo demokrasia ni idumughasia.

Wewe unafurahisha sana maoni yako ndio maana CCJ haipo ,Lengo la Chama ni kushika dola
 
Ni furaha iliyoje unapoona kuwa jambo ambalo ligekuwa ni mgogoro linatatuliwa kwa amani na upendo. Hongera sana Viongozi wa Chadema kwa kutatua haya mambo kwa busara kubwa na amani.

Sasa mwendo mdundo kwenda kuchukua jimbo la Segerea. Hatuwezi kusema mengi ila kwa kifupi ni kwamba maelezo ya Chama yamejitosheleza na yalikuwabaliwa na kila mhusika!

orv0ub.jpg
 
I am just interested to know what kind of healing to the nation if you take a middle finger that has been there and replace it with a thumb from another animal...

... kulikuwa na sababu nzuri tu za kufanya hivyo siewezi kuziweka hapa kwa sababu ya kumwaga kuku wengi kwenye mtama kidogo!

... Demokrasia inayombeba fulani siyo demokrasia ni idumughasia.

Duuuh... hizi quotes ni za kukumbuka!! 🙂
 
CHADEMA, Hii mada ni kwa faida yenu kuliko vinginevyo, inabidi mfikirie mara mbili; Kuna watu tumeamua kuchukua Likizo maalum ili Uchaguzi utukute TZ angalau tumpatie Kura Yetu Dr. Slaa; sasa nyinyi mnaanza Mambo ya Ki-CCM: Mnatukatisha tamaa. Kuhusu swala la 'potential' Just imagine; huu ni mfano tu anyway!!! Mbowe sasahivi anakubali kuwa Dr. Slaa ni Potential ndani ya Chadema kwa nafasi ya Urais, imagine Jimboni kwa Mbowe patokee tatizo wakati wa uchaguzi, tarehe iahirishwe, na wakati uchaguzi unarudiwa Dr Slaa awe amepoteza nafasi ya Urais, kisha wanachama waseme Dr. Slaa ni potential kuliko Mbowe, kwa hiyo mbowe kaa pembeni umpishe Dr. Salaa agombee ubunge, ..... Hapo utaona moto wake.. Mweeee!!!

1.majimbon ya vijijini wana vote mtu wa kabila lao na majimbo ya mjini wana vote mtu yeyote mfano wako hau-apply katika hili.....
2.kama mbowe amempisha kwenye urais ambao ni kiti cha juu kabisa kwa nini wewe unadhani atashindwa kumpisha kwenye ubunge. mbona mbowe aliachia jimbo lake mwaka 2005 na kugombea urais, je unadhani mbowe alikuwa hajui kama chadema hakijakua vya kutosha na haitashinda urais 2005, bali alifanya hivyo kwa ajili ya kukuza chama.
3. kutokana na sababu ya pili utaona mbowe ameshaachia kiti cha ubunge na urais kwa ajili ya chama, na hii ni dhairi kwamba kama ikitokea tena mara ya pili na kwa faida ya chama basi mbowe ataachiaaaaaaa.
NB mbowe keshafanya hayo ambayo unasema hawezi kuyafanyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
1.majimbon ya vijijini wana vote mtu wa kabila lao na majimbo ya mjini wana vote mtu yeyote mfano wako hau-apply katika hili.....
2.kama mbowe amempisha kwenye urais ambao ni kiti cha juu kabisa kwa nini wewe unadhani atashindwa kumpisha kwenye ubunge. mbona mbowe aliachia jimbo lake mwaka 2005 na kugombea urais, je unadhani mbowe alikuwa hajui kama chadema hakijakua vya kutosha na haitashinda urais 2005, bali alifanya hivyo kwa ajili ya kukuza chama.
3. kutokana na sababu ya pili utaona mbowe ameshaachia kiti cha ubunge na urais kwa ajili ya chama, na hii ni dhairi kwamba kama ikitokea tena mara ya pili na kwa faida ya chama basi mbowe ataachiaaaaaaa.
NB mbowe keshafanya hayo ambayo unasema hawezi kuyafanyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Hekima tupu!
 
Hongera Rachel, Hongera Mpendazoe na hongera uongozi wa chadema kwa kumaliza suala hili kiutu uzima hiyo ni Demokrasia iliyochangamana na Hekima...!
 
1.majimbon ya vijijini wana vote mtu wa kabila lao na majimbo ya mjini wana vote mtu yeyote mfano wako hau-apply katika hili.....
2.kama mbowe amempisha kwenye urais ambao ni kiti cha juu kabisa kwa nini wewe unadhani atashindwa kumpisha kwenye ubunge. mbona mbowe aliachia jimbo lake mwaka 2005 na kugombea urais, je unadhani mbowe alikuwa hajui kama chadema hakijakua vya kutosha na haitashinda urais 2005, bali alifanya hivyo kwa ajili ya kukuza chama.
3. kutokana na sababu ya pili utaona mbowe ameshaachia kiti cha ubunge na urais kwa ajili ya chama, na hii ni dhairi kwamba kama ikitokea tena mara ya pili na kwa faida ya chama basi mbowe ataachiaaaaaaa.
NB mbowe keshafanya hayo ambayo unasema hawezi kuyafanyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Mkuu Semilong,

Napata shida kidogo kwenye editing, kwa hiyo samahani kwa atakayekwazwa na message isiyo na paragraph

1. Unasema wavijijijini wanachagua mtu wa kabila lao!!!! sipendi kuamini hivyo, hata kama utakuwa na mifano katika hili, bado nitasema hizo ni fikra tunazopigania kuachana nazo, mi naamini Dr. Slaa anaweza kwenda Kigoma akagombea na kupata Ubunge, hicho unachoamini sio 'good practice' katika siasa zinazolenga kuwakomboa wananchi kutoka katika lindi la umaskini na ukandamizaji. ... Bila kujali ni kijijini ama mji mtu achaguliwe kutokana na Uwezo wake wa kiutendaji na si kabila lake

2. I will live to see it..., hata hivyo nisingependa mfano huo uje kutokea, kwa kuwa natazamia Dr. Slaa apite, akakae pale magogoni na kuendeleza mapambano yake vizuri. Mbowe kutoka Ubunge kwenda kugombea Urais ni wazi kabisa Urais ni zaidi ya Ubunge, Uraisi ni taasisi, kwa hiyo hata wanaoshindwa Uraisi kama wako makini mimi huwa bado nawaheshimu na naamini wanaweza watumikia wananchi hata wakiwa nje ya Bunge.

3. Nafasi ya kugombea Urais si ya Mwenyekiti pekee, ni ya mwanachama yeyote yule, kwa hiyo si kwamba ni Matakwa ya Mbowe kuachia, wanachadema kwa ujumla wao ndio wameona nani anafaa kwa wakati huu; Utaratibu unaowasumbua CCM ulianzia somewhere... kwa faida ya Chama, sasa una-backfire. Tuko pamoja Anyway!
 
Nawapongeza CHADEMA kwa kufikia solution. Naamnini busara ndiyo zimewafikisha hapo. Nawatakia kila la kheri, tupo pamoja.
 
Mkuu Semilong,

Napata shida kidogo kwenye editing, kwa hiyo samahani kwa atakayekwazwa na message isiyo na paragraph

1. Unasema wavijijijini wanachagua mtu wa kabila lao!!!! sipendi kuamini hivyo, hata kama utakuwa na mifano katika hili, bado nitasema hizo ni fikra tunazopigania kuachana nazo, mi naamini Dr. Slaa anaweza kwenda Kigoma akagombea na kupata Ubunge, hicho unachoamini sio 'good practice' katika siasa zinazolenga kuwakomboa wananchi kutoka katika lindi la umaskini na ukandamizaji. ... Bila kujali ni kijijini ama mji mtu achaguliwe kutokana na Uwezo wake wa kiutendaji na si kabila lake

2. I will live to see it..., hata hivyo nisingependa mfano huo uje kutokea, kwa kuwa natazamia Dr. Slaa apite, akakae pale magogoni na kuendeleza mapambano yake vizuri. Mbowe kutoka Ubunge kwenda kugombea Urais ni wazi kabisa Urais ni zaidi ya Ubunge, Uraisi ni taasisi, kwa hiyo hata wanaoshindwa Uraisi kama wako makini mimi huwa bado nawaheshimu na naamini wanaweza watumikia wananchi hata wakiwa nje ya Bunge.

3. Nafasi ya kugombea Urais si ya Mwenyekiti pekee, ni ya mwanachama yeyote yule, kwa hiyo si kwamba ni Matakwa ya Mbowe kuachia, wanachadema kwa ujumla wao ndio wameona nani anafaa kwa wakati huu; Utaratibu unaowasumbua CCM ulianzia somewhere... kwa faida ya Chama, sasa una-backfire. Tuko pamoja Anyway!

kuna text book na reality
text book - ni kwamba mtu yeyote anaweza kugombea kwenye kijiji chochote TZ bila kubaguliwa

reality - ni kwamba mjini watu wamechanganyika, mmakonde anaishi kawe kwa hiyo anajua matatizo ya kawe na akigombea anawakilisha wananchi wa kawe ambao wametoka mikoa mbalimbali. vijijini watu hawajachanganyika kwa hiyo mtu mwingine wa nje anaonaka yeye ni outsider ambaye hawezi kuwa loyal na jimbo, ni kama vile kumpa mkenya nchi na wakati waTZ wapo.

ili watu wa vijijini waweze kuvote mtu yeyote inahitajika movement kubwa sana ya watu ambayo itaua makabila, kitu ambacho sio leo au kesho kitatokea
 
Haya muhusika wa kwanza huyo
Mkuu wangu sijui kama una maana ya kuwa mimi ndio mhusika au kuna mtu mwingine.

Mimi nachokisemea ni ubishi uliopo hapa, nimebakia kuutazama tu kwa macho na kusoma hoja zenu kwani sina la kuzungumza. Hii haina maana sina imani na maamuzi yaliyofanywa. Binafsi sielewi lolote linalohusiana na mbinu za Chadema. Mimi ni mwanachama tu kama wanachama wengine sina hata nafasi ya kubeba box la kura.
Ila nachoweza kusema hapa ni kwamba hii habari ya kuwaengua dada yetu GenderSensitive kidogo imenishtua na hakika ningefurahi kama ningemwona yeye mwenyewe akikabidhi kiti chake kwa furaha ya vita hii.
Na mwisho ikumbukwe tu kwamba siku zote nimekuwa nikisema kwamba safari hii vita ya Chadema ni kumwondoa CCM by all means necessary na vigumu sana kwa nyie msokuwa wanachama kuelewa dhamira hii. Watu huenda vitani wakapoteza maisha ili wengine wawe huru na sijasikia mtu akilaani kitendo cha kuwapeleka watu mbele ya vita hali wengineo wakichukua madaraka kirahisi. Kwa hivyo Chadema wana kila haki, hila ya kutumia mbinu za iana yoyote ile ili mradi dhamira yao ikamilike.

Kifupi, inatakiwa watu tufahamu kwamba wananchi wamechoka na CCM.. Watu kama nyie ambao mmeombwa na Chadema kujiunga hata kabla ya uchaguzi mkakataa au kupinga kujiunga nao, Chadema haikuwaita majina yoyote na wala hadi leo mnapochangia humu hatuwezi kuwaiteni majina kama Wasaliti au watu waliokimbia vita yetu na CCM kwa visingizio. Tunapokea lawama zenu, tunajifunza zaidi kutoka kwenu pamoja na kwamba hatukufurahia kabisa kutuachia vita hii sisi wenyewe hali uwezekano mkubwa wa ushindi ulikuwepo.

Sasa sielewi kama keho wewe mkuu wangu ukitaka kujiunga na Chadema unafikiri itakuwa busara Chadema wakijiuliza kwanza kwanini wewe hukujiunga nao kabla ya uchaguzi huu?.. maanake inawezekana pia wewe kama raia unategemea kuona kama CCM itashinda ili mipango yako iweze kwenda vizuri ndani ya uongozi wa CCM ndio maana huweiz kujiunga na Chadema wasiokuwa na uhakika! - Who knoews?
 
ka"nzi" kanadokeza kuwa suala la Regia nalo limepatiwa usuluhishi wa kiutu "uzima" na "muafaka". Na shukrani kubwa zinatolewa kwa wale mliochangia mada hii na imewatia moyo wakuu kuwa kweli kuna watu wanaitakia mema Chadema na wanafuatilia mambo yake kwa karibu ili kisije kufanana na CCM.
 
ka"nzi" kanadokeza kuwa suala la Regia nalo limepatiwa usuluhishi wa kiutu "uzima" na "muafaka". Na shukrani kubwa zinatolewa kwa wale mliochangia mada hii na imewatia moyo wakuu kuwa kweli kuna watu wanaitakia mema Chadema na wanafuatilia mambo yake kwa karibu ili kisije kufanana na CCM.

Exactly my objection.

Now nimeongea sana kuhusu weakness za Regia hapa, kwa hiyo kama namtetea simtetei kwa basis ya kwamba ni mgombea anayefaa na yuko strong.Lakini at least Regia wanamjua, ni mtu wa chama chao, kafanya kazi miaka mingi, ana loyalty kwa chama, na kama kuna matatizo ya exposure anaweza kufundishwa -I hope anafundishika-. Lakini hawa mamluki mapandikizi wa kuja kutokea siku moja kabla ya primaries wanaweza hata kuwa ma spy wa CCM hawa, vyama inabidi viwe makini nao sana, na kama kweli wanataka kufanya kazi za chama wapewe muda kujionyesha mpaka 2015.

CHADEMA kukubali mamluki hawa ni kukubali kwamba wako desperate, hawana principles na wanajali kushinda kwa njia yoyote bila kujali wana sacrifice nini katika ushindi wao.
 
ka"nzi" kanadokeza kuwa suala la Regia nalo limepatiwa usuluhishi wa kiutu "uzima" na "muafaka". Na shukrani kubwa zinatolewa kwa wale mliochangia mada hii na imewatia moyo wakuu kuwa kweli kuna watu wanaitakia mema Chadema na wanafuatilia mambo yake kwa karibu ili kisije kufanana na CCM.

Sasa wajifunze kutumia common sense zao na si kusubiri hadi watu wa JF wawakemee. Wakija kuchukua madaraka ya nchi sitaki wawe wanasubiri kusikia akina NN wanasemaje huko JF.

Wawe tayari kufanya maamuzi mazito na magumu na si kusikilizia upepo unavuma wapi kwanza halafu ndio wanaamua.

Na kutofautiana na CCM ni kazi ndogo sana. Sijui wao walikuwa wanafikiria nini tu.
 
Mkuu wangu sijui kama una maana ya kuwa mimi ndio mhusika au kuna mtu mwingine.

Mimi nachokisemea ni ubishi uliopo hapa, nimebakia kuutazama tu kwa macho na kusoma hoja zenu kwani sina la kuzungumza. Hii haina maana sina imani na maamuzi yaliyofanywa. Binafsi sielewi lolote linalohusiana na mbinu za Chadema. Mimi ni mwanachama tu kama wanachama wengine sina hata nafasi ya kubeba box la kura.
Ila nachoweza kusema hapa ni kwamba hii habari ya kuwaengua dada yetu GenderSensitive kidogo imenishtua na hakika ningefurahi kama ningemwona yeye mwenyewe akikabidhi kiti chake kwa furaha ya vita hii.
Na mwisho ikumbukwe tu kwamba siku zote nimekuwa nikisema kwamba safari hii vita ya Chadema ni kumwondoa CCM by all means necessary na vigumu sana kwa nyie msokuwa wanachama kuelewa dhamira hii. Watu huenda vitani wakapoteza maisha ili wengine wawe huru na sijasikia mtu akilaani kitendo cha kuwapeleka watu mbele ya vita hali wengineo wakichukua madaraka kirahisi. Kwa hivyo Chadema wana kila haki, hila ya kutumia mbinu za iana yoyote ile ili mradi dhamira yao ikamilike.

Kifupi, inatakiwa watu tufahamu kwamba wananchi wamechoka na CCM.. Watu kama nyie ambao mmeombwa na Chadema kujiunga hata kabla ya uchaguzi mkakataa au kupinga kujiunga nao, Chadema haikuwaita majina yoyote na wala hadi leo mnapochangia humu hatuwezi kuwaiteni majina kama Wasaliti au watu waliokimbia vita yetu na CCM kwa visingizio. Tunapokea lawama zenu, tunajifunza zaidi kutoka kwenu pamoja na kwamba hatukufurahia kabisa kutuachia vita hii sisi wenyewe hali uwezekano mkubwa wa ushindi ulikuwepo.

Sasa sielewi kama keho wewe mkuu wangu ukitaka kujiunga na Chadema unafikiri itakuwa busara Chadema wakijiuliza kwanza kwanini wewe hukujiunga nao kabla ya uchaguzi huu?.. maanake inawezekana pia wewe kama raia unategemea kuona kama CCM itashinda ili mipango yako iweze kwenda vizuri ndani ya uongozi wa CCM ndio maana huweiz kujiunga na Chadema wasiokuwa na uhakika! - Who knoews?

No Mkandara nilikuwa nasema yaani muhusika ktk walioenguliwa ,akajitokeza kwa furaha inaonekana yuko side ya chama na wako pale kushinda.
Sijakulenga wewe no ,sorry for not be specific .
 
Nami niweke wazo langu kuhusu hii ishu ya "uanachama" wa Chadema. Mkandara na Kiranga wameizungumzia kwa namna ambayo imeniachia mawazo.

Watachaguliwa viongozi wengi toka Chadema na watu ambao sio wananchama wa Chadema. Yaani kuna wananchama na wafuasi. Kwa sasa, wafuasi wa Chadema ni wengi sana kuliko wananchama wake, na ndio wanaipa nguvu.

Kutokana na ukweli wa kuishi nje ya nchi, wengi wetu hapa ni wafuasi wa Chadema, na sio wanachama. Wako tayari kuwa wanachama lakini hawawezi. Kama kungekuwa na uwezekano wa kuitumia Chadema misaada ya kifedha bila kuvunja sheria, wengi tungefanya hivyo. Wiki mbili hivi zilizopita nilituma ujumbe Dar wanisaidie kufikisha mchango wa kifedha kwa Chadema. Lakini sijui kama hilo liliwezekana maana hata ile thread ya michango siioni tena. Imekwenda wapi?

Kiranga anaongelea hatari za mamluki. Ila ni vema kabisa Chadema kuwapokea wale wanaoamua kuitema CCM wakati huu. Yaani kuwe na mpasuko ndani ya CCM na Chadema isifurahie kuwapokea? In politics, there are only permanent interests. There are no permanent loyalties.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom