Uchaguzi 2020 CHADEMA: Jeshi la polisi limeomba majina ya wagombea wetu

Uchaguzi 2020 CHADEMA: Jeshi la polisi limeomba majina ya wagombea wetu

Polis wanafanya mambo kienyeji sana, wao walipaswa kuonesha sababu ya kuomba majina hayo, polis wanafanya kazi kienyeji sana...
 
Tulishawazoea kwa kulalamika! Umesema hujui sababu badala ya kwenda kuwauliza sababu tayari eti unasema UNAMTAKA IGP .... Who are you?? Mnaanza kuleta sababu za kushindwa! Kama Polisi wanataka kuwajua wagombea wenu ili waimarishe ulinzi kwenye maeneo yao. Kila wakati kuwaza negativity tuuuu!!

Mkuu nnaona umeamua kulitukana Jeshi lenu la Policeccm kuwa halijui Majukumu yake..
 
Siasa siyo mchezo mchafu sema watu wanapofanya siasa ndiyo wachafu.

Na siasa ikijaa watu wachafu inakuwa haina lengo la kuleta mabadiliko yoyote kwa wananchi zaidi ya kuiba Mali za umma tu
Na kiongozi muongo, anayetekeleza kwa hila yale asemayo, hupata laana ya milele.
 
Tuisome sheria ya uchaguzi kabla ya kuanza kulaumu.watia Mia wote na wagombea wanaitaji kulindwa hivyo wanapotaka kuwstambua ni kuwapatia ulinzi kwenye hiki kipindi kigumu ambacho kila mtu anaamini anaweza kuwa mbunge hivyo aina mpya ya uhalifu wa watiania kufanyiana njama mbaya waweza kuibuka
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Taarifa kwa Umma

Jeshi la Polisi maeneo mbalimbali ya nchi yetu limepeleka barua kwa viongozi wetu ngazi za Wilaya wakiwataka kuwapelekea Majina ya Wagombea wetu ndani ya Chama wa nafasi ya Ubunge.

Barua hizo ambazo zimesainiwa na Wakuu wa Polisi wa Wilaya hazitaji sababu za kuhitaji Majina ya Wagombea wetu wala kuelezea Nia na misingi ya kisheria ya kutaka kupelekewa Majina hayo.

Kwa hatua za sasa tumewaelekeza viongozi wetu nchi nzima kuwa wasipeleke Majina hayo hadi hapo Polisi watakapotoa sababu na misingi ya kisheria za kuhitaji Majina ya watia Nia na Wagombea wa Chama chetu.

Pili tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi awachukulie hatua mara moja wakuu wa polisi wa Wilaya ambao wameandika barua hizo huku wakijua kuwa hawana mamlaka ya kisheria ya kuingilia michakato ya uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya siasa.

Aidha tunamtaka IGP atengue barua hizo na aliongoze Jeshi la Polisi Kwa mujibu wa sheria na weledi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwezi Octoba.

Mwisho tunaendelea kufuatilia kwa karibu hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na Jeshi la Polisi dhidi ya watia nia na wagombea wetu maeneo mbalimbali nchini kama vile kuwakamata, kuwalaza mahabusu na wengine wanatakiwa kusalimisha magari yao binafsi Polisi bila kuelezea sababu za hatua hiyo.

Tunalitaka Jeshi la Polisi litimize wajibu wake kwa mujibu wa sheria za nchi yetu na liache Mara moja tabia ya kukandamiza Chama chetu kwa kushusha bendera za Chama chetu kama ilivyofanyika kule Same,Mkoani Kilimanjaro.

John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

Limetolewa Leo Alhamisi 16 Julai,2020.

View attachment 1508520
Kazi imeanza tayari
 
Tume ya uchaguzi imeagizwa polisi kuchukua majina ya wagombea wa chadema
 
Tuisome sheria ya uchaguzi kabla ya kuanza kulaumu.watia Mia wote na wagombea wanaitaji kulindwa hivyo wanapotaka kuwstambua ni kuwapatia ulinzi kwenye hiki kipindi kigumu ambacho kila mtu anaamini anaweza kuwa mbunge hivyo aina mpya ya uhalifu wa watiania kufanyiana njama mbaya waweza kuibuka
Lisu kutwa anaomba ulinzi,.lakini hao policeccm wamekaa kimya,.sasa from no where wanaomba majina ya watia nia wa cdm, wamjibu kwanza lisu barua zake alizowatumia.
 
Hivi Chadema ni wa kuandika barua ya hivi kweli asee? Au ni mkakati wa kuichafua chadame ionekane kutoa tuhuma za ovyo?

Na kama ni kweli hii ni ya Chadema mbona hawakuweka ushahidi wa hizo barua za polisi zinazolalamikiwa hapa?

Wasipo ziweka hizo barua tutaamini kuwa hizo ni propaganda tu kama ilivyokuwa kwenye tukio la kupigwa na kuvunjwa kwa KUB huku watu wakitamka "tumetumwa kukuvunja mkuu na unamsumbua Rais".
Barua zipo Tele wosap... Sema mambo yakiwa ovyo hawakawii kusema FAKE
 
Wanatafuta bao LA mkono kama uchaguzi wa Serikali za mitaa.. CCM wanasema wanakubalika hofu yote hii ya nini??

Kwa hasira nilizonazo nitampigia yoyote atakayepitishwa na CDM eneo langu,

Jamani tupigeni kura regardles of the outcome...
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)

Taarifa kwa Umma

Jeshi la Polisi maeneo mbalimbali ya nchi yetu limepeleka barua kwa viongozi wetu ngazi za Wilaya wakiwataka kuwapelekea Majina ya Wagombea wetu ndani ya Chama wa nafasi ya Ubunge.

Barua hizo ambazo zimesainiwa na Wakuu wa Polisi wa Wilaya hazitaji sababu za kuhitaji Majina ya Wagombea wetu wala kuelezea Nia na misingi ya kisheria ya kutaka kupelekewa Majina hayo.

Kwa hatua za sasa tumewaelekeza viongozi wetu nchi nzima kuwa wasipeleke Majina hayo hadi hapo Polisi watakapotoa sababu na misingi ya kisheria za kuhitaji Majina ya watia Nia na Wagombea wa Chama chetu.

Pili tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi awachukulie hatua mara moja wakuu wa polisi wa Wilaya ambao wameandika barua hizo huku wakijua kuwa hawana mamlaka ya kisheria ya kuingilia michakato ya uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya siasa.

Aidha tunamtaka IGP atengue barua hizo na aliongoze Jeshi la Polisi Kwa mujibu wa sheria na weledi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwezi Octoba.

Mwisho tunaendelea kufuatilia kwa karibu hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na Jeshi la Polisi dhidi ya watia nia na wagombea wetu maeneo mbalimbali nchini kama vile kuwakamata, kuwalaza mahabusu na wengine wanatakiwa kusalimisha magari yao binafsi Polisi bila kuelezea sababu za hatua hiyo.

Tunalitaka Jeshi la Polisi litimize wajibu wake kwa mujibu wa sheria za nchi yetu na liache Mara moja tabia ya kukandamiza Chama chetu kwa kushusha bendera za Chama chetu kama ilivyofanyika kule Same,Mkoani Kilimanjaro.

John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

Limetolewa Leo Alhamisi 16 Julai,2020.

View attachment 1508520
Kwa waandishi wa habari mnapelela list ya majina yote, lakini kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hamtaki....yaani kati ya zero strategy hii imefunga mwaka.
 
Inaweza kuwa linataka kutoa ulinzi wa wagombea!
Nchi hii ilipaswa iwe na katiba inayoeleza kila kitu, haya mambo ya kuamka unatunga mhmm.
 
CHADEMA chama langu chapisheni T-shirt zenye jina la Lissu na muuze kwa bei ya kawaida mtatengeneza Ukwasi wa kutosha na itakuwa ni bonge la kampeni.

Hawa polisi tumewalegezea sana tunakaa nao huku kitaa wamefuga hadi kuku yaani siku wakilinukisha tunaanza na mayai yanayoatamiwa baadae mabeki tatu wao then tunaendelea nao
 
Back
Top Bottom