Too low for you, yaani hata wewe unadhani Ritz wa JF ndio Ridhiwani Kikwete!? Ridhiwani akeshe hapa JF kwa shida gani na mipesa aliyotuibia kwa mgongo wa Baba yake atatumbuwa saa ngapi?
Ritz wa JF ni majobless wa Lumumba ambao wanaishi kwa ujira wa buku sabasaba na ndio maana muda wote wapo online hapa JF maana ni sehemu ya ajira yao.
Ritz peopleeeeeeeeeeeeeeeeesssssssssssssssssssssToo low for you, teh teh teh, hii lugha ni mtihani, wakati mwingine ni bora ujikite kwenye kiswahili chako au kihaya.
Chadema walikuwa wamejipanga kuhusu muundo huu toka kwenye ilani yao ya uchaguzi ya 2010, copy and paste ya CCM ndiyo tatizo tulilonalo; nachoshukuru mimi ni JK kumchagua mzee Warioba, kawaida Mkurya ukimkabidhi madaraka utakoma. hongera zangu za moyoni zimfikie mzee wangu Warioba.....simamia haki za nchi hii kwa miaka mingine 100, okoa kizazi kijacho sisi wa sasa washatugeuza vitumbua.
Mbona hawajasema chochote kuhusu mualiko wa Mbowe Ikulu.
Chadema waweka msimamo serikali tatu, mabomu Arusha
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imekutana kwa dharura kujadili muundo wa serikali tatu na hatma ya Muungano wa Tanganyika na Zanziba, na leo chama hicho kinatarajia kutoa taarifa rasmi ya msimamo wake.
Halikadhalika, suala la Tume huru ya uchaguzi limejadiliwa kwa kina na wajumbe hao huku wengi wakiwa na hofu kuwa kulingana na ilivyopendekezwa kwenye rasimu hakuna uwezekano wa Tanzania kuwa na tume huru kama ilivyo nchini Kenya.
Hayo yalisemwa jana na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohamed,wakati akizungumza na NIPASHE kuhusu yaliyojiri kwenye mkutano huo wa dharura. Alisema Chadema itatoa msimamo wake leo mbele ya waandishi wa habari ili Watanzania waweze kujua kwa uwazi kuhusu masuala ambayo yameonekana kuwa mapya.
Katiba mpya
Alisema kikao hicho kilianza Julai 06, mwaka huu, na suala kubwa lilikuwa ni kujadili kipengele kwa kipengele rasimu ya Katiba, na wajumbe wengi walizungumzia kinagaubaga suala la serikali tatu na hatima ya Muungano.Wajumbe wengi wameonekana kulizungumzia kwa kina suala la Muungano, suala la serikali tatu ilikuwa ni moja ya mapendekezo ya Chadema kwa Tume, muundo wake ndio tunaujadili kwa kina, alisema.
Tume huru ya Uchaguzi
Mohamed alisema suala la tume huru ya uchaguzi limechukua nafasi kubwa katika kikao hicho na huku wajumbe wengi wakionyesha hofu iwapo kutakuwa na Tume huru itakayotenda haki wakati wa chaguzi.
Katiba ya Tanganyika
Alisema msimamo wa Chadema ni kutaka ipatikane Katiba inayotengeneza viongozi na si watawala.Alibainisha kuwa suala lingine ni kuanza mchakato wa uundaji Katiba ya Tanganyika kwa kuwa Zanzibar tayari kuna Katiba na itakapokamilika ya Muungano ni wazi kuwa Tanganyika itashindwa kuendesha shughuli zake.
Shambulio la Bomu Arusha
Aidha, Mwenyekiti huyo, alisema kikao hicho pia kilijadili hali ya kisiasa nchini ikiwamo tukio la kulipuliwa kwa bomu katika kampeni za Chadema mkoani Arusha na uchaguzi katika kata 26 nchini.Tukio la shambulio la bomu lilitokea mwezi Juni, mwaka huu, na kuua watu watatu, akiwamo kiongozi wa Chadema, na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi wa udiwani katika kata ya Kaloleni.
Hili ni tamko la 43 la Chadema toka mwaka huu uanze.
vipi, walionyesha na ule mkanda/video ya kujilipua kwa bomu arusha?
ha ha ha, CDM ni chama makini.....kwa hili watanielewa tu.Umeshavunja sheria ya cdm kwa kumsifia JK.
Tatizo mnawasemaji wengi sana, angalia hii orodha.
1. Mwita Maranya,
2. Mohamedi Mtoi,
3. Yericko Nyerere,
4. Molemo,
5. Mungi,
6. Crashwise,
7. Matola,
Source!?
Hao makamanda kazi yao si ya kitoto.Ni wapi walijiita wasemaji?
ule mkanda anaodai wa mauaji aliutoa? au alikuwa anajifariji.Haikuwa Ajenda kwa Sababu sio issue kwa CHADEMA.
PS
Akina Wassira, Lukuvi Full Kununa that day Ikulu, Vp hawajalianzisha tu ndani ya CC Yenu
Hiyo ID saa hizi ameingia mtu mwingine ndio amempokea shift, ukita kuamini maneno yangu angalia latest started thread yake utajuwa hawa ni watu zaidi ya mmoja na uandishi wao ni tofauti.Hao makamanda kazi yao si ya kitoto.Ni wapi walijiita wasemaji?
Unadhihirisha ujuha wako kwa kuandika comments tatu mfululizo umeshindwa kuziweka pamoja? au unataka uonekane umepost nyingi? ufala mwingine bana!hicho kilikuwa kikao cha kugawana ruzuku
Mkuu, hilo nalo unalikataa? muda mwingine tukubali tu kwamba CDM mnachemka kwa mambo madogo madogo.
Kamanda Mwita Maranya alikuwa kinara wa kuwahadaa wanaJF na guests wanao peruzi humu kuwa Mbowe amepata mwaliko kutoka state department.
Hapo hapo kaja Dr Slaa na kusema mwaliko wa Mbowe umetokea Ikulu kupitia bungeni mpaka kwa ofisi ya KUB.
Wakaja wadaku wakuu nchini, Tanzania Daima, nao wana lao kuwa Mbowe alipata mwaliko kama mwenyekiti wa CHADEMA na maana hiyo CHADEMA ilipata mwaliko rasmi.
Kamanda Saanane hili ni bora mkubali kuwa CDM mmefanya blunder. Huku Mnyika na Makene hawajulikani walipo.