CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

CHADEMA iko kwenye mioyo ya watu haiko kwenye pesa mkuu.
Hizo ni enzi za real politics, kujiunga na chama fulani ni imani, na mapenzi ya dhati ya moyoni. Enzi hizo fedha ilikuwa sii msingi, ni matokeo. Sasa ni tofauti, fedha ndio kila kitu!. Chadema ilishindwa kuendesha kikao cha Baraza Kuu kutokana na ukata, ingekuwa ni mapenzi ya dhati ya moyoni, wajumbe wa Baraza Kuu wangejitolea!. Mpaka Mama alipookoa jahazi ndipo Baraza Kuu likakutana!. Siasa za sasa pesa ndio kila kitu!.

Mimi ni Pro Nyerere, nimegombea CCM, sikutoa hata senti moja, nikapata kura 1.

Nilimshauri Magufuli kufuta ruzuku kwa vyama vya siasa Ruzuku kwa vyama vya Siasa: Mnaonaje tumshauri Rais Magufuli aifutilie mbali ruzuku hii? Ni ufisadi
Na sasa nimemshauri Samia kufuta ruzuku Pascal Mayalla: Vyama vya siasa visipewe ruzuku, viongozi wake wajitolee


View: https://youtu.be/kpOuytUa4O4?si=JO1joEa6GuP3pFAUP
 
Hahaha unadhani ccm inapata wapi pesa? CCM ruzuku yao kubwa sana kuliko vyama vyote. Pia wanapewa na nchi rafiki au vyama rafiki kama CCP, na Vingine duniani.

Ili hivi vyama viweze kuwepo ruzuku lazima iwepo, vyama vile vya kiukombozi pia vilikuwa vinapata pesa kutoka nchi rafiki. Na mpaka sasa kila chama kina marafiki ndani na nje, ila Chadema walizuiliwa kupokea pesa moja kwa moja, ikatengenezwa kwamba pesa za Chadema kutoka nje zipitie serikali kuu, na mtoaji aseme ni za nini ili chama kisizitumie kwa kazi tofauti. Lakini hii ilikuwa kwa chadema na CUF(enzi hizo).
 
Aisee,Mungu aliamua ugomvi.
 
Nimeliona andiko hili japo sijalisoma its contents lakini hii ni habari njema kwa Chadema View attachment 3064986 kwasababu itawaepushia karma ya machozi, jasho na damu ya makamanda hawa.

Hiki ambacho Chadema inakwenda kukifanya sasa, mimi niliwashauri kitambo CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Hata baada ya Chadema kushinda kesi mahakamani kuwa wametimuliwa kihalali, bado tuliwashauri Chadema
Ushauri wa bure: CHADEMA iachane na issue ya Wabunge wake 19, iwasamehe waendelee na Ubunge wao. Kwa muda uliobakia kuwatengua hakuna maslahi yoyote!
Na hili la kuwasamehe likija kutokea, mimi ni miongoni mwa tutakao farijika sana kwasababu tulishauri, tukapuuzwa, ila ushauri wetu unatekelezwa step by step Siasa za Kijungu Jiko, Penye Uzia, Penyeza Rupia!. Hakuna Mkate Mgumu Mbele ya Chai!, Hata Uwe Mgumu Vipi, Mbele ya Chai/Rupia, Lazima Utalainika!

Wawasamehe tuu yaishe!.
P
 
Wanabodi,
Sijitapi ila japo kuna watu we are nobodies, lakini tuna kauli umba!, tukisema jambo linatokea. Mimi ni mmoja wa watu hawa wenye kauli umba "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia

Kwenye bandiko hili nilisema mambo mawili.
1. Makamanda hawa 19 wataendelea na ubunge wao full term!. Hili limetokea makamanda hawa 19 wanaendelea kupeta!.
2. Karma itawatandika Chadema kwenda 6ft under, hili la pili sasa ndio linakwenda kutokea iwapo kesho Mwenyekiti Mbowe, atashupaza shingo kung'ang'ania kutetea kiti chake!.

Tusubirie hiyo kesho, mimi nikiwa miongoni mwa tutakao kuwepo nyumbani kwa Mwenyekiti Mbowe kumsikilikiza ana akiiunganisha nyumba yake kwa kukubali matokeo, kuwa miaka 20 inatosha, ama akiibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe!.

Tusubirie hiyo kesho.
Mungu Mbariki Mwenyekiti Mbowe kuuona ukweli!.
Mungu ibariki Chadema.
Mungu ibariki Tanzania.

P.
 
Karma itawatandika Chadema kwenda 6ft under, hili la pili sasa ndio linakwenda kutokea iwapo kesho Mwenyekiti Mbowe, atashupaza shingo kung'ang'ania kutetea kiti chake!.
Hii karma umekuwa ukiitamka dhidi ya Chadema kwa muda mrefu sana ina maana chama hiki tu ndio hukosea? chama chako Ccm au vyama vingine havikosei?

Au ni mbinu ya kuhalalisha wanavyotendewa na watawala kwa kivuli cha karma?
 
Mhuu huu ni mtazamo wako mzuri, ameshaamua anagombea na amini mimi CDM haitakuwa kwani kushindwa kwa sanduku la kura sii ugomvi uamuzi wa wana CDM. Uchaguzi wa CDM unaakisi struggle za kidini na kisiasa kwani nahisi hata serikali na ccm might have interest in it, they prefer lesser evil.
 
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…