CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Mambo yote ya uchaguzi na ubunge yanaratibiwa na NEC, NEC ndiyo inapeleka majina Bungeni. Hivyo Chadema wanapaswa kuiandikia NEC, kuwa imewavua uanachama hao wasaliti 19, na imeupokea uteuzi viti maalum na kupeleka list rasmi ya wabunge wao 19.
Barua ya Chadema kwa NEC, Spika anakuwa cc. only.
P
 
H
He is deef and blinded,under the so called uteuzi.not only him they are many who have tried to undermine CDM for the sake of uteuzi.and by doing so they think CDM will perish NEVER.the like are kafulila,mwampamba,katambi,silinde,lijuakali,shonza etc etc.after all when wemasepetu was member of CDM Makonda said he is selling ngada.after turning back,he was declared clean.cheap politics like those belongs to fools,and won't make the country prosper further
 
NEC ni ya Nani??kwa nini hakuna NEC huru??Kama hujui ni ya ccm
 
Siku hizi Paschal hunaga issue
 
Hahaha Pascal Chadema ni chama kinachojitegemea ki maamuzi hawategemei ushauri wa ccm kutoa maamuzi.

Wameshatoa maamuzi hakuna kurudi nyuma.

Nyie ccm mnamatatizo sana, hamuongelei mzizi wa tatizo mnaongelea ubunge wa covid-19.

Tatizo sio Chadema kuwafukuza covid-19 uanachama, tatizo ni CCM KUVURUGA UCHAGUZI MKUU WA October 28, 2020.
Chadema haipingi covid-19 wasiwe wabunge inakataa kukubali matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita.

Nasema na kurudia Chadema imeshafanya maamuzi hizi ni kelele tu hamna hoja.

Ongeleeni uchaguzi mkuu ambao ndio mzizi wa tatizo sio kuongelea Chadema na covid-19.
 
Poti bana....
 
Hapa tu pamenitosha kuona uwezo wako mdogo wa akili, kumbe upo kwa ajili ya kusaidia tu pale unapoona mtu anataka kuanguka? how about the rest? Vipi kama kapitia njia sahihi?Upo tayari kupongeza? kama sivyo basi wewe ni hewa
 
Yanoi haya mengine haoni kama ya shida kwa taifa, mpaka mtu anatka mahabusu bila hata jaji kujua leo hayo hayaoni ati anaishauri chdema,
 
Mkuu Mayalla aka Njaa, kwani hujachoka tu kuandika!? Ulazima wa wao ccm kulazimisha hayo majina unatoka wapi!? Wanataka nini hasa!? Au ushindi walioupata haujawatosha!?
 
Hakuna kitu hatari kama kukosa akili wakati unazeeka na watu wanategemea unavyozeeka ndiyo hekima na busara vinachukua nafasi yake lakini mwenzetu ndiyo anazidi kuwa mjinga haswa.
 
Chadema ikifa ndiyo furaha ya CCM,why worry?
Binafsi sipo tayari kubadili mamlaka kuu ya nchi kirahisi tu na sikutegemea kama TL angeweza kumshinda JPM lakini kinachokera ni haya marosoroso kibao katika awamu hii.
Paskali Mayala haya yaliyotokea hayajawahi kutokea na tumerudi nyuma.
CCM imeshinda na itaendelea kushinda lakini kama yalivyo maji upinzani/maoni tofauti huwezi kuyazuia na hili limeonekana wazi (miaka mitano ya CCM kufanya siasa peke yake tulitegemea Chadema mikutano yao ikose watu.Waanchi kuwachangia wafungwa wa Chadema millioni nayo ni ishara tosha).Kuliko CCM kuzuia kwa nguvu zote ni vizuri ikavilea hivi vyama ili hata siku wakitolewa madarakani angalau wawe na nafuu ya maisha.
Nilitegemea baada ya kushinda diplomacy ingetumika kuwavuta wapinzani na kulegeza baadhi ya mambo lakini tunachoshuhudia ni vijembe na vitisho.Hu
 
Hahaha sasa kama Chadema hawajawahi kupeleka jina lolote NEC, wao NEC walipata wapi majina hayo kuyapeleka kwa spika?!

Walijua ni batili ndio maana mwanasheria mkuu wa serikali alisema wabunge 19 ni halali na wasibugudhiwe na Chadema, alijua wamefanya ubatili, na spika akatokea TBC na kusema atawalinda wabunge 19 wa viti maalum kwa nguvu zote.

Matamshi ya AG na Spika tayari yalitosha kukuonyesheni nyie kwamba hili limetengenezwa kuhalalisha haram, yaani uchaguzi wa October 28, 2020.

Mnazunguka na maandishi marefu na mengi lakini mnaukimbia ukweli kwamba tatizo ni ccm waliohalibu uchaguzi mkuu na kupelekea Chadema kukataa matokeo na uhalali wake.

Badala yake ccm mmegeuka kuwa washauri wa chadema wakubali uovu au la....!
 
Mkuu Pascal.

Nafahamu kuwa “wengi wetu tupo vizuri kwenye kugawa kile ambacho hatuna yaani ushauri mzuri”(Napoleon Hill).

Hata hivyo niwie radhi nami nikushauri kidogo.

Punguza intellectual arrogance bro. Nyuzi zako nyingi hasa za siasa za vyama zinarindima na hiyo kitu kiasi cha kumpiku the late BWM(R I P).

On a hindsight, hii inaweza kuwa imekupotezea na itaendelea kukupotezea fursa nyingi achilia mbali kuwafanya watu waku ‘ antagonize’ na kuku ‘snub’ kila inapotokea nafasi ya kufanya hivyo.

Na hali hii mkuu ni kwa pande zote mbili: wale ambao unajinasibisha kuwaunga mkono na hawa wengine ambao unapingana nao.

Wote hawakukubali!

Otherwise sitasema zaidi juu ya uzi wako ambao naona uko driven zaidi na hio hali niliyoitaja kuliko nia ya kweli ya kuwasaidia wapinzani wako wa siasa au kulinufaisha taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…