Pre GE2025 CHADEMA kuongea na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya Chama Februari 1

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
31 January 2024
Dodoma, Tanzania

MKUTANO WA KUMI NA NNE WA BUNGE WAENDELEA KUFANYIKA BUNGENI JIJINI DODOMA​


Mkutano wa Kumi na Nne wa Bunge la Kumi na Mbili ulianza kufanyika siku ya Jumanne tarehe 30 Januari, 2024 Bungeni Jijini Dodoma na unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 16 Februari, 2024.

Mkutano huu umeongezewa wiki moja kutokana uzito wa majukumu yaliyopangwa ikiwemo uzito wa Miswada itakayoshughulikiwa.

Miswada hiyo ambayo tayari imeanza kujadiliwa Bungeni ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2023 na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi wa Mwaka 2023.

Miswada mingine ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Vyama vya Siasa wa Mwaka 2023 na Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.5) wa Mwaka 2023.

Vilevile katika Mkutano huu wa Bunge Kamati za Kudumu za Bunge zitawasilisha taarifa za shughuli zilizotekelezwa na Kamati kwa mwaka 2023.

Aidha, wastani wa Maswali 250 ya kawaida na Maswali 24 ya Papo kwa Papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge.

Source: Tovuti ya Bunge
 
Maandamano aruhusu Rais Samia! mbona unampa ukubwa asiokuwa nao?
Samia na washauri wake wajanja sana: maandamano wamefanya nyumbu faida za maandamano hayo zote zimemuendea yeye utafikiri ndo aliyeyaratibu. Nyumbu waliishia kupakaa vumbi kwenye kope za macho tu na kutoka jasho jasho linalonuka kwenye kwapa zao.
 
Eti kinachoungwa mkono na wananchi wengi zaidi. Thibitisha uweke na idadi. Huu ni ubwabwajaji kama ubwabwajaji mwingine wa chadema
 
Tunasubiri Mwongozo
 
Samia na washauri wake wajanja sana: maandamano wamefanya nyumbu faida za maandamano hayo zote zimemuendea yeye utafikiri ndo aliyeyaratibu. Nyumbu waliishia kupakaa vumbi kwenye kope za macho tu na kutoka jasho jasho linalonuka kwenye kwapa zao.
Uliumia ukiwa wapi Mkuu?
 
Uliumia ukiwa wapi Mkuu?
Mkuu, kwa hakika niliumia nkiwa kwenye maandamano ya nyumbu wa mbowe huku nikila vumbi na kutoka jasho la kwapa kwa hasira baada ya kupigwa 3 kwa sifuri kiulaiiini na mama Samia, The Mother of Modern Tanzania.
 
Mkuu, kwa hakika niliumia nkiwa kwenye maandamano ya nyumbu wa mbowe huku nikila vumbi na kutoka jasho la kwapa kwa hasira baada ya kupigwa 3 kwa sifuri kiulaiiini na mama Samia, The Mother of Modern Tanzania.
Roho mbaya inakutia umaskini dogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…