Uchaguzi 2020 CHADEMA kutikisa Dar kwa siku tatu, Uchaguzi Mgombea Urais Tanzania na Zanzibar

Uchaguzi 2020 CHADEMA kutikisa Dar kwa siku tatu, Uchaguzi Mgombea Urais Tanzania na Zanzibar

Je lissu atamuunga mkono Membe?
Je Membe atamuunga mkono Lissu?
Kama hawataungana si watagawana kura?
Je itakuwa live?
Membe hana madhala yeyote,hata akigombea Membe hawezi kupata hata kura elfu hamsini,sisi huku mitaani hatumjui labda kama zitapigwa za mitandaoni.
 
Ninajua hapa tunazubaishwa tu, ila wenye Kufuatilia mambo Kiundani tumeshajua kuwa Tundu Antipasi Lissu ndiyo atakuwa CHADEMA Flag Bearer.
 
Kama tittle inavyosemeka ndugu wadau, naanza kwa kutangaza interests kwanza kwamba mimi si shabiki wa chama chochote cha siasa sijawai na natarajia kuwa sitakuwa shabiki in shaa Allaah.


Turudi katika mada yetu, kesho 02/08/2020 mchakato wa kumpata mgombea kupitia chedema utaanza huku makada watatu wakiwania nafasi hiyo.

1.Tundu Antipas Mghwai Lissu

2.Lazaro samwel Nyalandu

3.Rosemary Majinge


Katika wagombea hao watatu nampaka nafasi ya Moja kwa moja Rosemary majinge kuwa mgombea mwenza yaani makamu wa Rais kwa sababu zifuatazo.

i.Rosemary aliwekwa kimkakati juu ya gender balance hivyo hafikiriwi kupata nafasi ya moja kwa moja ya kugombea urais wa JMT.

ii.Wajumbe wa chadema hawamjui Rosemary kwa sababu si mtu wa majukwaani na siyo mwanamke wa prukushani na vuruamai.

ktk nafasi ya urais yoyote anaweza kupita utategemea wajumbe wameamkaje siku ya jumanne.
 
Hapa ndipo tunaukumbuka umuhimu wa Makonda kuwa RC wa Dar, wajumbe wote hawa wangepitishiwa bahasha za khaki wampitishe yeyote bali Tundu Lissu kwa maslahi mapana ya Chama cha Kijani.
 
Naimani Kamati Kuu italeta mgombea mwenye sifa, mwenye uwezo wa kusimamia mambo, anayeelewa mahitaji halisi ya wananchi. asiyekubali kuyumbishwa, anayefahamika kwa wapiga kura, aliye na historia ambayo wengi watatamani kuisikia.
 
Kila LA heri chadema, ushauri. Uwazi ukatawale, haki ikatendeke.wagombea wakahesabu kura wenyewe.pia waombe vyombo vya habari virushe live...
 
Naona vipofu mmeshikana mikono alafu mnashaurana anza kuruka wewe
 
Sasa ni Rasmi.

Chama kikuu Cha upinzani nchini Chadema kitaanza vikao vyake kwa siku 3 mfululizo kuanzia Jumapili tarehe 2 mpaka Jumanne tarehe 4 katika ukumbi maarufu nchini wa Mlimani City.

Kikao Cha Kamati Kuu kitafanyika kesho Jumapili huku Baraza Kuu likiwa siku ya Jumatatu na Mkutano Mkuu utakuwa siku ya Jumanne.

Agenda Kuu ya vikao hivi ni kuchambua na hatimaye kupiga kura kumpitisha Rasmi mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema.

Tayari wajumbe wa vikao hivi wameshaanza kuwasili jijini Dar es Salaam wakiwa na shauku kubwa ya kutimiza takwa la kikatiba.

Mchuano mkali kwenye nafasi ya Urais ni Kati ya mafahali wawili Lazaro Nyalandu Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kanda ya Kati na Mjumbe wa Kamati Kuu akipambana na Tundu Lissu Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa na mwanasiasa mashuhuri zaidi kwa Afrika.

Ikumbukwe Chadema ilitikisa nchi siku ya Jumanne wiki hii wakati maelfu kwa maelfu ya watu walipojaa majiani kumlaki Tundu Lissu aliyerejea matibabuni huku kukiwa na maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea nchini kumsindikiza mwanasiasa huyo makao makuu ya Chama huku umati huu ukiimba 'Rais' Rais' Rais' kote alikopita ambapo Barabara ilifungwa kwa masaa manne kumsindikiza shujaa huyo.

Sisi wa Molemo Media Kama Sikuzote Tunatarajia kuwaletea matangazo ya moja kwa moja wasomaji wetu wa Jamii Forums ili Dunia kuweza kujua kinachoendelea ndani ya vikao hivyo muhimu.Tuna Imani hatukuwahi kuwaangusha wafuatiliaji wetu.

Wagombea wa CHADEMA ni;

Wakili Simba Neo

Lazaro Nyalandu

Tundu Lissu

Dk.Maryrose Majinge

Wakili Gaspar Mwanalyela

Isaya Mwita

Mchungaji Leonard Manyama
Mbona kama umeshaweka wazi Tundu ndie umtakaye?
 
Kwa mjibu wa katiba ya nchi, kama mgombea urais atatoka Tanzania bara lazima mgombea mwenza atoke Tanzania visiwani and vice versa. Hivyo Rosemary hana sifa hiyo ya kuwa mgombea mwenza.

Hayo majina matatu yapange kulingana na mapendekezo ya kura za wajumbe ambazo Lazaro Nyarandu aliwaacha kwa mbali hao wengine. La sivyo tutakuelewa vingine. Kura za wajumbe lazima ziheshimiwe kama zilivyoheshimiwa zile za CCM kwa kuwang'oa vigogo kama Makonda, Mwakyembe, Mwamri, Lugora, Wasira, Nyerere watatu nk. Wajumbe wa chadema nao walishang'oa vigogo kama Tundu Lissu nk. Hiyo ndiyo demokrasia. Mkienda nje ya hapo chadema itapasuka vipande viwili, kitu ambacho ccm inakisubiri kwa hamu.
 
Kama tittle inavyosemeka ndugu wadau, naanza kwa kutangaza interests kwanza kwamba mimi si shabiki wa chama chochote cha siasa sijawai na natarajia kuwa sitakuwa shabiki in shaa Allaah.


Turudi katika mada yetu, kesho 02/08/2020 mchakato wa kumpata mgombea kupitia chedema utaanza huku makada watatu wakiwania nafasi hiyo.

1.Tundu Antipas Mghwai Lissu

2.Lazaro samwel Nyalandu

3.Rosemary Majinge


Katika wagombea hao watatu nampaka nafasi ya Moja kwa moja Rosemary majinge kuwa mgombea mwenza yaani makamu wa Rais kwa sababu zifuatazo.

i.Rosemary aliwekwa kimkakati juu ya gender balance hivyo hafikiriwi kupata nafasi ya moja kwa moja ya kugombea urais wa JMT.

ii.Wajumbe wa chadema hawamjui Rosemary kwa sababu si mtu wa majukwaani na siyo mwanamke wa prukushani na vuruamai.

ktk nafasi ya urais yoyote anaweza kupita utategemea wajumbe wameamkaje siku ya jumanne.
Wewe akili huna,mgombea akitoka bara mgombea mwenza lazima atoke Zanzibar,kati ya hao watatu hakuna mzanzibar,huo ugombea mwenza huyo Catherine ataupataje?
 
Kwa mjibu wa katiba ya nchi, kama mgombea urais atatoka Tanzania bara lazima mgombea mwenza atoke Tanzania visiwani and vice versa. Hivyo Rosemary hana sifa hiyo ya kuwa mgombea mwenza.

Hayo majina matatu yapange kulingana na mapendekezo ya kura za wajumbe ambazo Lazaro Nyarandu aliwaacha kwa mbali hao wengine. La sivyo tutakuelewa vingine. Kura za wajumbe lazima ziheshimiwe kama zilivyoheshimiwa zile za CCM kwa kuwang'oa vigogo kama Makonda, Mwakyembe, Mwamri, Lugora, Wasira nk.
Fomu ya urais ilichapishwa moja tu.
 
Back
Top Bottom