Chadema kuwaburuza Mahakamani OCD wa Kigoma na Dodoma kwa tuhuma za Wizi

Chadema kuwaburuza Mahakamani OCD wa Kigoma na Dodoma kwa tuhuma za Wizi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Watashitakiwa kwa Majina yao binafsi kama wanavyoshitakiwa vibaka wengine, hii ni baada ya kuamuru na kushiriki wizi wa nyaraka za Chadema waziwazi bila kificho chochote.

OCD wa Dodoma ameonekana wazi akishiriki kuvunja ofisi ya Kanda ya kati na kuiba nyaraka kadhaa pamoja na pesa Taslimu, huku OCD wa Kigoma akituhumiwa kuvunja kijiwe cha Chadema na kuiba mlingoti wa bendera na bendera yenyewe ambavyo vyote ni Mali ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Tayari Mawakili wa Chadema wameelekezwa kufungua mashitaka hayo ifikapo Jumatatu saa 2 asubuhi.

Polisi_Kigoma_wamevunja_kijiwe_chetu_kwa_gari,_pia_Polisi_wamevunja_ofisi_ya_Kanda_ya_Kati_na_...jpg

Taarifa hii Muhimu imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Mh Benson alipokuwa anaongea na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za Chama hicho Kinondoni , pamoja na hayo pia Mh Kigaila amehoji IGP anakotoa mamlaka ya kukamata Wafuasi wa Chadema wanaohudhuria Kesi ya Mbowe Mahakamani, ambapo amemtaka IGP Sirro kuonyesha Kifungu chochote cha Katiba ya Nchi kinachokataza wananchi kuhudhuria kesi Mahakamani kabla hajafunguliwa Mashitaka ya kusababisha fujo isiyo na tija yoyote, kwake binafsi , kwa familia yake wala kwa nchi Jumatatu asubuhi.
 
1628331313579.png
ha ha ha...!!!
Hii picha inanikumbusha mbali na inaeleza mengi!

Katibu wa Tawi: "nakubabatiza kwa jiwe, kwa jina la Chama"(ameshika nyaraka)
Mwenyekiti wa Tawi: Laanakum we chadema, huku akirusha jie(kavaa barghashia)
Mwenyekiti Kamati ya ulinzi: ngoja nimwue kabisa na hili jiwe(kabeba fatuma)
Mjumbe wa Tawi: eeeehh jama.... jama... jama .....mtamwua(kavaa Tshirt nyekundu na meno kuna mapengo ya kutosha)
Chalii wa chadema: tumeyakwepa sana hayo madongo kiongozi!
 
Mkuu mimi nadhani kama Wafuasi wa chadema wangeenda kusikiliza kesi mahakamani yasingetokea yale. Ilivyoonekana wafuasi wale walienda kutoa/ kushinikiza mahakama ifuate mawazo yao jambo ambalo kwa utaratibu si sahihi.
 
Mkuu mimi nadhani kama Wafuasi wa chadema wangeenda kusikiliza kesi mahakamani yasingetokea yale. Ilivyoonekana wafuasi wale walienda kutoa/ kushinikiza mahakama ifuate mawazo yao jambo ambalo kwa utaratibu si sahihi.
Mabango hayajawahi kuwa shinikizo , kumbuka kwamba IGP alianza kukataza watu kwenda mahakamani kabla hata ya siku ya kesi , hapo alimaanisha nini , ni shinikizo lipi aliloliona ?
 
Watashitakiwa kwa Majina yao binafsi kama wanavyoshitakiwa vibaka wengine , hii ni baada ya kuamuru na kushiriki wizi wa nyaraka za Chadema waziwazi bila kificho chochote .

OCD wa Dodoma ameonekana wazi akishiriki kuvunja ofisi ya Kanda ya kati na kuiba nyaraka kadhaa pamoja na pesa Taslimu , huku OCD wa Kigoma akituhumiwa kuvunja kijiwe cha Chadema na kuiba mlingoti wa bendera na bendera yenyewe ambavyo vyote ni Mali ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tayari Mawakili wa Chadema wameelekezwa kufungua mashitaka hayo ifikapo Jumatatu saa 2 asubuhi .

View attachment 1883821

Taarifa hii Muhimu imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Mh Benson alipokuwa anaongea na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za Chama hicho Kinondoni , pamoja na hayo pia Mh Kigaila amehoji IGP anakotoa mamlaka ya kukamata Wafuasi wa Chadema wanaohudhuria Kesi ya Mbowe Mahakamani , ambapo amemtaka IGP Sirro kuonyesha Kifungu chochote cha Katiba ya Nchi kinachokataza wananchi kuhudhuria kesi Mahakamani kabla hajafunguliwa Mashitaka ya kusababisha fujo isiyo na tija yoyote , kwake binafsi , kwa familia yake wala kwa nchi Jumatatu asubuhi .

View attachment 1883822
Sasa viongozi wa CHADEMA wanaanza kupata akili na ufahamu sahihi wa namna ya kushughulikia matatizo yao dhidi aidha ya Serikali au watendaji mmoja mmoja at individual levels, BADALA YA KUFANYA MAANDAMO nchi nzima! Huo ndio mkondo sahihi, hongereni sana.
 
Mahakama za CCM siku hizi zinatenda haki?..

Kama vipi tufungie kesi dhidi ya wale Covid 19 pia kupitia wanasheria wetu nguli aka wasomi..
 
TBCCMM NA CHANNEL TEN WALIKUWEPO?
Habari zao naziamini sana.
 
Mahakama za CCM siku hizi zinatenda haki?..

Kama vipi tufungie kesi dhidi ya wale Covid 19 pia kupitia wanasheria wetu nguli aka wasomi..
Msikate tamaa hata kabla hamjaanza utaratibu wa kufungua hizo kesi. Nendeni tu, mtajua hayo yote huko mbele kwa mbele! COVID 19 hamuwawezi, wana kula hiyo mihela ya Ubunge na wakubwa wenu.
 
1. Hiyo mahakama ina lipwa na CHAMA GANI??

2. Hao OCD wanalipwa na CHAMA GANI...?

acheni kupoteza muda na resource zenu
IMG-20210806-WA0048.jpg


Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Safi sana.Tatizo Mahakama na mifumo yote sio ya kuaminika, but hatua hii itawatia adabu japo kidogo.

Naamini CCTV camera zinamuhusu.
CHADEMA WANASHINDWA KUFUNGA HATA CCTV ZA Elfu 60. Mfano siku wale wahuni wamempiga Mbowe getini kwake Dodoma hata CCTV hamna?

CCTV zitatumika hadi mahakama ya the Hague. Ni muhimu sana. Tena fungeni zile HD.
 
Back
Top Bottom