CHADEMA mnatuchanganya. Tunataka Katiba inayosimamia haki na sio Katiba Mpya. Kamwe Katiba hiyo haiwezi kutengenezwa na Wanasiasa

CHADEMA mnatuchanganya. Tunataka Katiba inayosimamia haki na sio Katiba Mpya. Kamwe Katiba hiyo haiwezi kutengenezwa na Wanasiasa

Kati ya vitu CCM walivyoweza ni kufanya brainwashing kwa watu.

Taifa likiwa na watu wasiotambua haki zao vizuri na waoga ni rahisi sana kufanya spinning.

Watoto wamekuzwa kuaminishwa mzungu ni adui

Watoto wanaaminishwa mchango wa kuanzia TAA,TANU mpaka CCM ndio ulichangia nchi kupata uhuru huku wakiaminishwa hakuna chama bora zaidi ya CCM.

Je, kipindi kile watu wote walikua TANU?

Kwa jibu jepesi ni kuwa watu walitaka uhuru hata wale wasokua na vyama ila ubabe wa kuungishwa TANU ndio ulionekana kama ndio chama cha kikombozi ila mzungu angeweza kutoka bila hata kuwa TANU.

Historia hii hii ndio imefanyiwa janja janja za Washirika wa CCM mtu kama Okello hatambuliki kwa usahihi.
 
Ubarikiwe ndugu mtoa mada kwa kuanzisha mjadala wenye afya kwenye taifa letu kwa wakati muafaka. Najua huu mjadala utachafuliwa na wanachama wenye mahaba na vyama vyao kwa matusi dhidi ya watu watakaotoa mawazo yatakayokinzana na utashi wao huku wakijinasibu kuwa wapiganiaji wa demokrasia na uhuru wa kutoa maoni.
 
Ndio maana hayati JPM hakucheka na HAO JAMAA.

JPM alikuwa na maono ni kweli vyama vingi vya UPINZANI BARANI AFRIKA viko kwa ajili ya kuchelewesha tu MAENDELEO, viko kuchochea UHASAMA UTENGANO, VURUGU.

Vyama vingi vya Afrika viko kuona kila SERIKALI iliyoko madarakani INASHINDWA NA KUANGUKA hata Kama INAFANYA VYEMA....ni siasa mahsusi za "domokrasia" zilizoasisiwa KULETA SINTOFAHAMU HUMU AFRIKA.

Nitapingwa sana kwa kusema hayo ila ukichunguza utamaizi kuwa kuna ukweli angalau 51%.

#MamaSSHAnaupiga MWINGI
Tungekuwa na katiba sahihi inayodhibiti maamuzi mabovu ya Rais, kuna uwezekano mkubwa kuwa JPM angekuwa hai leo hii. Asingepuuza Covid-19 kama alivyofanya na yeye binafsi angechukua tahadhari zote kuhakikisha hivyo virusi havimsogelei.

Mapambio ya sifa za unafiki kama haya ndiyo yamemtowesha kabla ya wakati wake. Kama alivyoshindwa yeye, hakuna anayeweza kuangamiza upinzani nchini na duniani. Msijidanganye.
 
Sijapinga swala la kupiga kelele. Kwanza wapiganie haki zilizopo kikatiba na wakapokonywa Kama mikutano ya hadhara, Uhuru wa habari na Sheria kandamizi. Wakipata haki hiyo waende wakahubiri na kufundisha watu maana na mabadiliko ya Katiba Tena kwa namna ya kutafuta suluhu ya kisiasa na sio kwa vitisho na kushindana. Na mwisho m chakato wa uundwaji Katiba usitawaliwe na wanasiasa

Katiba ndio msingi wa sheria zote. Katiba hii inampa absolute powers Rais wa JMT. Ushahidi wa hatari yake tumeushuhudia kupitia matendo ya JPM alivyotupilia mbali sheria mbalimbali na kukiuka mifumo iliyowekwa kisheria ili kukidhi matakwa yake binafsi.

Huwezi kupigania haki zilizopo kikatiba kabla hujarekebisha vifungu kinzani kama vile vinavyowezesha madaraka ya Rais kuchezea haki hizo kwa kadiri “anavyojisikia”. Rais kudai kuwa baadhi ya maamuzi muhimu kwa taifa yatategemea “ameamkaje siku hiyo” si kitu cha kusherehekewa. Katiba inayomuwezesha Rais wakati wowote anapojisikia kupiga marufuku shughuli na mikutano ya kisiasa ambayo ipo kikatiba na kisheria!

Tunazidi kushuhudia Rais wa sasa Mama SSH akisahihisha makosa mengi ya JPM yaliyoathiri watu binafsi na uchumi wa Taifa kwa ujumla yaliyotendwa kutokana na mikingamo ya katiba.

Katiba yetu imejaa controversies na contradictions kibao kiasi kwamba Rais anaweza kufanya chochote; kukubali chochote au kukataa chochote kinacholetwa kwake na watu au taasisi husika bila kuwajibika kisheria.

Hivyo ni fallacy (dhana potofu) kuwaambia wapinzani “wapiganie haki za kikatiba” kwanza kabla hawajadai marekebisho ya Katiba hiyo.
 
Shida huwa hamsomi hoja vizuri. Mnakimbilia kwenye ushabiki.

Kwa mchakato upi tunaweza kupata Katiba inayofaa? Ule ule wa Jk?! Ule ule uliojaa wanasiasa.

Lazma ngeuze azma yenu kutokea kwenye Katiba mpya na kwenda kwenye tume na chaguzi huru na chaguzi za haki la Katiba likianza Sasa litatuletea Katiba isiyofaaa.

Mkuu cdm watadai katiba mpya, ww na hao wenzako daini katiba ya haki maana hakuna anayewazuia.
 
Elewa hoja. Sijawabeza wanasiasa ata kidogo kwenye kumsukuma Hilo. Ila nachopinga NI wanasiasa kiutawala mchakato wake mzima. Kwanza hawataafikiana na Pili watajadili maswala ya kiuchaguzi tu na kuacha maeneo mengi nyeti. Wawepo Ila wasitawale mchakato
Kama hayo makundi mengine hayawezi hata kutetea maslahi yao ndio wataweza kuandika hiyo katiba? Ukiachia wanasiasa hasa wa upinzani, hao unaowasema wataandika katiba ya haki, ni lini uliwahi kuwasikia wakiogelea katiba hata isiyo ya haki?
 
Kitu wapinzani wanachofeli ni kuongozwa na hasira na ushindani na kupigania maslahi binafsi ya kisiasa hivyo kukosa logic na plan nzuri kufanikisha mipango yao.

Jakaya Kikwete alianzisha mchakato wa Katiba mpya Ila mchakato mzima katika mazingira hayo ulitawaliwa na wanasiasa. Bunge lilijaa wanasiasa na kwa maamuzi yao lingeleta katiba mbovu Tena iliyoegemea kuibeba CCM kwani walikuwa wengi na wenye nguvu ya maamuzi. Wangekuja na katiba mpya lkn isiyofaa. Jk alijua akaitupilia mbali mwishoni.

Sasa mnavyoomba tuimalizie mchakato mnataka tuimalizie kwa staili hiyo hiyo?!

Je, mnataka katiba mpya au katiba nzuri?

Mi nadhani kwa busara CHADEMA ombeni tume huru na chaguzi za haki. Piganieni mabadiliko hayo ya Sheria na katiba Ila swala la katiba liacheni. Waacheni watu wasio wanasiasa watuundie katiba.

*Katiba itakayowasimamia na kuwawajibisha wanasiasa pia. Katiba hiyo wanasiasa hawawezi kuiunda.

*Katiba itakayojibu kila kitu na kuondoa mizengwe kwenye kila sekta kuanzia kilimo, biashara, Viwanda, madini na Mikataba yote isiyo ya kiusalama Kama madini na manunuzi, ubia, hesabu za taasisii na mashirika ya umma kuwa wazi kwa umma wakati wote.

*Katiba itakayomlazimisha mbunge kabla ya kwenda bungeni kwenye kikao chochote akae vikao vyenye maandishi angalau vitatu na wadau wote katika Jimbo lake na kuikusanya mawazo na Kisha kuyafikisha bungeni au serikalini na sio Sasa wabunge kwenda kuzungumza mawazo binafsi na marafiki zao wachache wanaokunywa nao bia vijiweni.

Bunge jipya la katiba lisizidi 10% ya wanasiasa. Waingie wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, bunge lijae wataalamu kwa 30% mfano walimu, madaktari, wanasheria na wachumi. Na wanaoshiriki kwenye bunge Hilo wakubali kutokugombea au kuteuliwa nafasi yoyote ya kisiasa au za kiuteuzi kwa miaka kumi ili kuondoa bunge Hilo Hilo kuja kugeuka chombo Cha utawala Mara baada ya kuunda katiba.

Bunge lililopita na mchakato mzima wa Katiba ndio uliowaibua akina polepole na Kabudi. Watu watashindwa kutoa mawazo kwa Uhuru wakitarajia hisani za watawala

Na nawaomba wimbo isiwe katiba mpya Bali tunataka katiba yenye kulinda haki. Na katiba yenye kutenda haki kamwe haiwezi kuletwa na wanasiasa. Kila sehemu wanasiasa huvutana tu kutafuta msindi. Kwenye katiba lazima kila mtu awe msindi.
Unataka wachukue copy ya bible labda
 
Kama hayo makundi mengine hayawezi hata kutetea maslahi yao ndio wataweza kuandika hiyo katiba? Ukiachia wanasiasa hasa wa upinzani, hao unaowasema wataandika katiba ya haki, ni lini uliwahi kuwasikia wakiogelea katiba hata isiyo ya haki?
Hoja yangu wao wapiganie Uhuru wa kufanya siasa kwanza. Kupitia Uhuru huo watoe elimu ya Katiba kwenye jamii Tena wakiwa watulivu Kama motivation speaker. Waweke mazingira ya kupatikana Katiba ya haki. Nachosema hapa Katiba ikitungwa na wanasiasa itakuwa mbovu Sana na CCM watapanga wanachotaka kwani kwenye siasa wao ndio Wana nguvu ya maamuzi.
 
Hoja yangu wao wapiganie Uhuru wa kufanya siasa kwanza. Kupitia Uhuru huo watoe elimu ya Katiba kwenye jamii Tena wakiwa watulivu Kama motivation speaker. Waweke mazingira ya kupatikana Katiba ya haki. Nachosema hapa Katiba ikitungwa na wanasiasa itakuwa mbovu Sana na CCM watapanga wanachotaka kwani kwenye siasa wao ndio Wana nguvu ya maamuzi.

Hiyo katiba mpya ambayo mtaandika nyie ya haki isiyo na wanasiasa mmefikia wapi hadi sasa? Au mtaanza lini mchakato wake? Au umekuja kupambaza watu kwa faida ya ccm Boss?
 
Katiba
Kitu wapinzani wanachofeli ni kuongozwa na hasira na ushindani na kupigania maslahi binafsi ya kisiasa hivyo kukosa logic na plan nzuri kufanikisha mipango yao.

Jakaya Kikwete alianzisha mchakato wa Katiba mpya Ila mchakato mzima katika mazingira hayo ulitawaliwa na wanasiasa. Bunge lilijaa wanasiasa na kwa maamuzi yao lingeleta katiba mbovu Tena iliyoegemea kuibeba CCM kwani walikuwa wengi na wenye nguvu ya maamuzi. Wangekuja na katiba mpya lkn isiyofaa. Jk alijua akaitupilia mbali mwishoni.

Sasa mnavyoomba tuimalizie mchakato mnataka tuimalizie kwa staili hiyo hiyo?!

Je, mnataka katiba mpya au katiba nzuri?

Mi nadhani kwa busara CHADEMA ombeni tume huru na chaguzi za haki. Piganieni mabadiliko hayo ya Sheria na katiba Ila swala la katiba liacheni. Waacheni watu wasio wanasiasa watuundie katiba.

*Katiba itakayowasimamia na kuwawajibisha wanasiasa pia. Katiba hiyo wanasiasa hawawezi kuiunda.

*Katiba itakayojibu kila kitu na kuondoa mizengwe kwenye kila sekta kuanzia kilimo, biashara, Viwanda, madini na Mikataba yote isiyo ya kiusalama Kama madini na manunuzi, ubia, hesabu za taasisii na mashirika ya umma kuwa wazi kwa umma wakati wote.

*Katiba itakayomlazimisha mbunge kabla ya kwenda bungeni kwenye kikao chochote akae vikao vyenye maandishi angalau vitatu na wadau wote katika Jimbo lake na kuikusanya mawazo na Kisha kuyafikisha bungeni au serikalini na sio Sasa wabunge kwenda kuzungumza mawazo binafsi na marafiki zao wachache wanaokunywa nao bia vijiweni.

Bunge jipya la katiba lisizidi 10% ya wanasiasa. Waingie wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, bunge lijae wataalamu kwa 30% mfano walimu, madaktari, wanasheria na wachumi. Na wanaoshiriki kwenye bunge Hilo wakubali kutokugombea au kuteuliwa nafasi yoyote ya kisiasa au za kiuteuzi kwa miaka kumi ili kuondoa bunge Hilo Hilo kuja kugeuka chombo Cha utawala Mara baada ya kuunda katiba.

Bunge lililopita na mchakato mzima wa Katiba ndio uliowaibua akina polepole na Kabudi. Watu watashindwa kutoa mawazo kwa Uhuru wakitarajia hisani za watawala

Na nawaomba wimbo isiwe katiba mpya Bali tunataka katiba yenye kulinda haki. Na katiba yenye kutenda haki kamwe haiwezi kuletwa na wanasiasa. Kila sehemu wanasiasa huvutana tu kutafuta msindi. Kwenye katiba lazima kila mtu awe msindi.
Katiba mpya ianzie kwenye vyama vya siasa
 
Hayo ya Tume huru, katiba mpya na bunge live wanayasemea wapi ???

Muda huu watumie kupigania haki zilizopo kikatiba Ila zimezimwa. Kama kuwepo wabunge waliovuliwa uanachama, kuzuiwa mikutano ya kisiasa na Uhuru wa habari. Watumie fursa hiyo kuweka ELIMU ya Katiba ili mchakato ukianza upya uwe na Afya
 
Kudai Chadema wanakuchanganya kwenye hili ni kutokuwatendea haki.

Katiba inahitajika na wananchi ambao ndiyo watakayoiandika. Kumbuka katiba iliyopo iliandikwa na nani na kwenye mazingira gani?

Chadema hawajahitaji wanasiasa kuandika katiba bali wanataka mchakato wa katiba mpya kurejelewa.

Chadema kusukuma mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya uliosimama tangia 2015 tatizo liko wapi hapo? Labda kama wanakuchanganya kea kuuhitaji mchakato huu kurejelewa?

Kama wao wanakuchanganya kwa kutaka mchakato kurejelewa labda wewe ulipendelea nani basi waweke msukumo kwenye kulirejelea hili?
Nimesema kwenye kulejea mchakato slogan iwe Katiba inayolinda haki. Na tukiulejea Katiba mpya Sasa itatawaliwa na siasa na CCM wataiunda yote na Wale mnaowaita Covid 19 kwani ndio wapo bungeni na watageuka kuwa bunge la Katiba.
 
Katiba ndio msingi wa sheria zote. Katiba hii inampa absolute powers Rais wa JMT. Ushahidi wa hatari yake tumeushuhudia kupitia matendo ya JPM alivyotupilia mbali sheria mbalimbali na kukiuka mifumo iliyowekwa kisheria ili kukidhi matakwa yake binafsi.

Huwezi kupigania haki zilizopo kikatiba kabla hujarekebisha vifungu kinzani kama vile vinavyowezesha madaraka ya Rais kuchezea haki hizo kwa kadiri “anavyojisikia”. Rais kudai kuwa baadhi ya maamuzi muhimu kwa taifa yatategemea “ameamkaje siku hiyo” si kitu cha kusherehekewa. Katiba inayomuwezesha Rais wakati wowote anapojisikia kupiga marufuku shughuli na mikutano ya kisiasa ambayo ipo kikatiba na kisheria!

Tunazidi kushuhudia Rais wa sasa Mama SSH akisahihisha makosa mengi ya JPM yaliyoathiri watu binafsi na uchumi wa Taifa kwa ujumla yaliyotendwa kutokana na mikingamo ya katiba.

Katiba yetu imejaa controversies na contradictions kibao kiasi kwamba Rais anaweza kufanya chochote; kukubali chochote au kukataa chochote kinacholetwa kwake na watu au taasisi husika bila kuwajibika kisheria.

Hivyo ni fallacy (dhana potofu) kuwaambia wapinzani “wapiganie haki za kikatiba” kwanza kabla hawajadai marekebisho ya Katiba hiyo.
Katiba NI kitu kikubwa Sana. Sio Cha kwenda nacho haraka wakati tupo kwenye hasira na makovu kibao. Kwenye uadui mkubwa wa kisiasa na siasa za visasi. Mchakato huo ukianza Sasa hautaleta Katiba Bali wachumia tumbo na watafuta fursa. Lazma tuwe na mazingira ya Maridhiano. Kusiwe na uadui mkubwa Kati ya wapinzani na utawala.
Sasa ukianza mchakato chadema watataka tubadili kila kitu huku CCM wengi wakitaka Katiba itakayowalinda wasitoke madarakani milele.

Tutawaleta akina makonda, Polepole na Kabudi wapya.
 
Nimesema kwenye kulejea mchakato slogan iwe Katiba inayolinda haki. Na tukiulejea Katiba mpya Sasa itatawaliwa na siasa na CCM wataiunda yote na Wale mnaowaita Covid 19 kwani ndio wapo bungeni na watageuka kuwa bunge la Katiba.

Tuko pamoja mkuu.

La msingi tukubaliane katiba ni kipaumbele.

Kusukuma mbele busara hii kueleweka nani anafanya?

Schedules and modalities those are details to follow.

Kupatikana busara ndipo ngoma ilipo sasa. Au Chadema awe sawa na ban-yan mbaya kiatu chake dawa?

Au siyo mkuu?
 
Kitu wapinzani wanachofeli ni kuongozwa na hasira na ushindani na kupigania maslahi binafsi ya kisiasa hivyo kukosa logic na plan nzuri kufanikisha mipango yao.

Jakaya Kikwete alianzisha mchakato wa Katiba mpya Ila mchakato mzima katika mazingira hayo ulitawaliwa na wanasiasa. Bunge lilijaa wanasiasa na kwa maamuzi yao lingeleta katiba mbovu Tena iliyoegemea kuibeba CCM kwani walikuwa wengi na wenye nguvu ya maamuzi. Wangekuja na katiba mpya lkn isiyofaa. Jk alijua akaitupilia mbali mwishoni.

Sasa mnavyoomba tuimalizie mchakato mnataka tuimalizie kwa staili hiyo hiyo?!

Je, mnataka katiba mpya au katiba nzuri?

Mi nadhani kwa busara CHADEMA ombeni tume huru na chaguzi za haki. Piganieni mabadiliko hayo ya Sheria na katiba Ila swala la katiba liacheni. Waacheni watu wasio wanasiasa watuundie katiba.

*Katiba itakayowasimamia na kuwawajibisha wanasiasa pia. Katiba hiyo wanasiasa hawawezi kuiunda.

*Katiba itakayojibu kila kitu na kuondoa mizengwe kwenye kila sekta kuanzia kilimo, biashara, Viwanda, madini na Mikataba yote isiyo ya kiusalama Kama madini na manunuzi, ubia, hesabu za taasisii na mashirika ya umma kuwa wazi kwa umma wakati wote.

*Katiba itakayomlazimisha mbunge kabla ya kwenda bungeni kwenye kikao chochote akae vikao vyenye maandishi angalau vitatu na wadau wote katika Jimbo lake na kuikusanya mawazo na Kisha kuyafikisha bungeni au serikalini na sio Sasa wabunge kwenda kuzungumza mawazo binafsi na marafiki zao wachache wanaokunywa nao bia vijiweni.

Bunge jipya la katiba lisizidi 10% ya wanasiasa. Waingie wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, bunge lijae wataalamu kwa 30% mfano walimu, madaktari, wanasheria na wachumi. Na wanaoshiriki kwenye bunge Hilo wakubali kutokugombea au kuteuliwa nafasi yoyote ya kisiasa au za kiuteuzi kwa miaka kumi ili kuondoa bunge Hilo Hilo kuja kugeuka chombo Cha utawala Mara baada ya kuunda katiba.

Bunge lililopita na mchakato mzima wa Katiba ndio uliowaibua akina polepole na Kabudi. Watu watashindwa kutoa mawazo kwa Uhuru wakitarajia hisani za watawala

Na nawaomba wimbo isiwe katiba mpya Bali tunataka katiba yenye kulinda haki. Na katiba yenye kutenda haki kamwe haiwezi kuletwa na wanasiasa. Kila sehemu wanasiasa huvutana tu kutafuta msindi. Kwenye katiba lazima kila mtu awe msindi.
Naunga mkono hoja,wanasiasa wa chama chochote wakae mbali kabisaaa maana ni vigeugeu kabisaaaa.
Leo LOWASA FISADI,KESHO WANATAKA USHAHIDI.
LEO SETH NA ESCROW MAFISADI,KESHO WAACHIWE.
LEO NYALANDU ANABEBA TWIGA,KESHO NI MGOMBEA WETU NA MJUMBE KAMATI KUU
 
Katiba

Katiba mpya ianzie kwenye vyama vya siasa
Katiba nzuri sio NI kwa manufaa ya wananchi na sio wanasiasa. Na maswala ya kisiasa ndio ganayofanya swala la Katiba kuonekana kuwa ipo kwa manufaa ya kisiasa tu. Ndio maana tunakosa maridhiano
 
Katiba Ni waraka wa kisiasa, pia katiba Ni waraka wa kisheria.Unawezaje kuwaweka wanasiasa pembeni..
 
JPM alikua anawapeleka kwenye total extinction...kingebaki kama chama kilichosajiliwa tu basi kama kilivyo JAHAZI ASILIA ... Chadema ni Chama cha wahuni na ni kama kikundi cha kigaidi wao ni waumini wa vurugu , matusi , hawana hoja zinazoeleweka wanazidiwa hadi na ACT WAZALENDO ...
 
NI kweli kabisa, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Back
Top Bottom