Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo kufanya maandamano ya amani Nov 2, 2020 kupinga kuvurugwa kwa Uchaguzi Mkuu

Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo kufanya maandamano ya amani Nov 2, 2020 kupinga kuvurugwa kwa Uchaguzi Mkuu

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
631
Reaction score
1,577
CHADEMA na ACT Wazalendo tunautangazia umma na wanaopinga kuvurugwa kwa Uchaguzi Mkuu kushiriki Maandamano ya Amani kesho Jumatatu ya Tarehe 2/11/20. Madhumuni ya Maandamano ni kudai kurudiwa Uchaguzi Mkuu chini ya Tume Huru ya Uchaguzi.

Maandamano yataanzia sehemu 2, kundi moja litaanzia Buguruni Sheli kuchukua barabara ya Uhuru mpaka Kariakoo, Msimbazi Road mpaka fire, Morogoro road, Bibi Titi mpaka Ofisi za Tume.

Kundi lingine litaanza Ubungo Bus Terminal kuchukua Morogoro road mpaka fire kisha Bibi Titi kuelekea Ofisi ya Tume.

Wajumbe wa Kamati Kuu mnaopenda kushiriki maandamano tafadhali mtachagua kati ya maeneo hayo. Maandamano yanaanza saa mbili kamili asubuhi kuelekea Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Ukumbi wa Mwalimu JK Nyerere Conference Center. Viongozi Wakuu wataongoza Maandamano hayo.

 
Safi sana, bado hasira za kushindwa vibaya zipo lkn kila siku zinavyozidi kwenda ndivyo zinavyozidi kupungua, hata matusi yanazidi kupungua siyo kama siku kwanza hapa JF, rhetoric zimebadilika kuelekea kukubali hali kama ilivyo, time heals all wounds wanasema Wazungu, hivyo wataandamana kesho, kesho kutwa ikifika Ijumaa wamechoka, mwishowe watakubaliana na hali na maisha kurudia kawaida, ...
 
Polisi wanahaha nchi nzima. Lakini maandamano yako palepale!

IMG_20201101_201326_195.jpg
 
Ndugu yangu posho za ubunge ufaidi na familia yako, baada ya kukosa uniingize mimi barabarani nikale mkong'oto wa Polisi . Chukua familia yako itangulize mbele. Mimi najua uchaguzi umeisha kifuatacho ni kuchapa kazi.
 
TAARIFA MUHIMU SANA!!!

Watanzania tuishio nje ya nchi (TANZANIA DIASPORA) tumeanza kuandamana kupinga UCHAFUZI uliofanyika juzi hapo nyumbani Tanzania!

Hawa ni ndugu zetu kutoka Ulaya ya Kaskazini (Sweden 🇸🇪, Norway 🇳🇴 na Denmark 🇩🇰) ambao tayari wameanza maandamano yao nje ya Ubalozi wetu uliopo Stockholm, Sweden...

Watanzania tuishio nchini hapa Ufaransa 🇫🇷 tunaandaa maandamano hayo kesho Jumatatu, November 2, 2020 nje ya Ubalozi wa Tanzania 🇹🇿 nchini Ufaransa 🇫🇷.

Maandamano yataanza saa 2 asubuhi na kumalizika saa 6 mchana!

Baada ya maandamano, WAZANZIBARI tuishio nchini hapa, kwa kuongozwa na Balozi wetu (BABU MZANZIBARI), tutazindua Ubalozi wetu (Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar nchini Ufaransa)... Ofisi za Ubalozi wetu zipo mitaa ya TROCADÉRO, karibu sana na mnara wa EIFFEL...

Kwa niaba ya Wazanzibari wote waishio nchini hapa Ufaransa, mimi, BABU MZANZIBARI, Balozi wa Zanzibar nchini Ufaransa, natumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zetu Watanzania waishio nchini hapa, katika uzinduzi wa Ubalozi wetu!

Usafiri, kula, kunywa ni kwa gharama yangu mwenyewe!...

Kwa kauli moja, tumekubaliana kuwa hatuitambui serikali haramu ya John Pombe Joseph Magufuli! Hatuitambui serikali haramu ya Hussein Ali Hassan Mwinyi!

Rais wa Zanzibar tunayemtambua ni Maalim Seif Sharif Hamad aliyechaguliwa na wananchi wa Zanzibar!... Na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunayemtambua ni Tundu Antipas Lissu, aliyechaguliwa na Watanzania!...

Mungu ibariki Zanzibar yenye mamlaka kamili, Mungu ibariki Tanzania!... 🙏🏾

👉🏾👉🏾👉🏾 Sambaza ujumbe huu umfikie kila Mtanzania mpenda haki!...👍🏾
 
Mmeandaa watu wa kuyaanzisha au ni yoyote atakae wahi kufika?

Nadhani kesho sio mbali Ila sioni Hilo likifanikiwa hata kwa asilimia 5.

Msifanye haya mambo kwa hasira zenu binafsi, mmeshajua watu mtaani wanataka Nini Maana ni lazima nao wawe na mawazo na hasira Kama zenu ndo mtawaona Ila Kama mnafanya hivi kutokana na maamuzi ya ndani mtafeli Sanaa.

Huku nilipo watu wamelalamika juzi na Jana ila leo wameshayaacha na siasa wanaendelea na shughuli zao hakuna hata Ile amsha Kama ya kipindi Cha mange
 
Back
Top Bottom