Pre GE2025 CHADEMA peke yake haiwezi kamwe kuitoa CCM madarakani...

Pre GE2025 CHADEMA peke yake haiwezi kamwe kuitoa CCM madarakani...

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Upo sahihi
TZ hakuna vyama vya upinzani, wanasiasa wa upinzani wote ni mamluki wa ccm ktk kisiasa
Unaupimaje umamluki wao.

Yaani kama CHADEMA ingekuwa ni mamluki wa CCM, inakuwaje CCM inatumia nguvu kubwa sana kupambana na CHADEMA na tena kwa kutumia nguvu za dola...??
 
1000 digits umeandika hoja yenye kina kirefu Sana...

Kuhusu pesa kwa asilimia mia Moja (100%) nakuunga mkono. Hakuna siasa bila pesa. Harakati ni pesa.

Kuna mahali kama chama kuna ulegevu wa kuweka uratibishaji wa ukusanyaji na utumiaji wa fedha ndani ya chama.

Kanuni ya fedha ya chama haijulikani kama ipo ama haipo...

Ni kweli kabisa kuna tatizo kubwa sana kwa Waafrika kwenye uaminifu wa Fedha.

Yaani Taasisi yenye wanachama mil. 5 bado inategemea ruzuku ni kosa kubwa sana.
Hebu fikiri patokee Kanisa moja lenye waumini mi.5 . halafu ina mhamasishaji kama Dr. Gwajima. au Geo Dave nadhani lingekua na pesa nyingi kama Serikali ya China.
Watu wanahitaji hamasa na kuona mambo yakifanyika.

Huwezi kuwa na mawakala wa serikali za mitaa bila kuwa na pesa. Lazima wasimamizi wawe na uhakika wa kuweka bando kwenye simu, kula chakula ,kupata posho , na ofisi za chama ziwepo ambazo zinaweza kuuza hata kofia za Chama na tshrt na kutoa kadi za uanachama lakini pia kuhakikisha wenyeviti wa serikali za mitaa na vijiji wanapata mikopo ya Chama kuendesha shughuli zao za kiuchumi. Ni lazima vijana waone tofauti ya CCM na Chadema kwa vitendo. CCM wenyeviti wengi ni wazee hawahitaji tena kufanya biashara zaidi ya kupewa kanga na na tisheti na kofia na kusema CCM hoyee. Lakini Chadema ilikua na nafasi kubwa ya kutumia ushawishi na kukusanya pesa kwa wanachama na kisha kuwawezesha wanachama wake kukopa hata kwa kuzizungusha kama zaka kwa waislam na kuhakikisha wanajenga ofisi na kuweka Takwimu ya Wanachama wake na kuweza kuwaita na hata kukutana ofisini kupanga mikakati ya kisiasa na kiuchumi kuanzia kule vijijini.

Tunategemea kuona ushindani mkubwa kwenye chaguzi hizi ndani ya chadema kuanzia Mwenyekiti Taifa mpaka kwenye ngazi ya msingi kule chini.

Kuna watu wanadhani kumshindanisha Mbowe ni usaliti au ni kutaka kuua chama . Hapana ni namba bora ya kupima sera na malengo na maono mapana ya Mwenyekiti.

Demokrasia sio lazima Mbowe ashindwe bali ni uhuru wa wanachama kuchagua na kuchaguliwa kwa uhuru na haki na uwazi.
Tusimnyime Mbowe haki yake ya kukitumikia chama na watanzania wapenda mabadiliko lakini ni lazima kampeni zifanyike kwa haki, watu washindanishwe kwa haki ,wacharurane kwa uwazi , maovu yao yafichuliwe kama yapo ili wananchi wajue mbivu na mbichi.
 
Tunategemea kuona ushindani mkubwa kwenye chaguzi hizi ndani ya chadema kuanzia Mwenyekiti Taifa mpaka kwenye ngazi ya msingi kule chini.
Kuna baadhi ya watu hili la Mwenyekiti Mbowe kupingwa wanaona ni usaliti.
Kuna watu wanadhani kumshindanisha Mbowe ni usaliti au ni kutaka kuua chama
Hili nalo ni kama tunazuia demokrasia kukua ndani ya Chama.
Demokrasia sio lazima Mbowe ashindwe bali ni uhuru wa wanachama kuchagua na kuchaguliwa kwa uhuru na haki na uwazi.
Kweli kabisa.
 
Kabisa... Lakini angalau kati ya watu 10 basi watu 9 wawe na ajira rasmi.

Hapa bongo kati ya watu kumi ni watu watatu tu ndiyo wapo kwenye ajira rasmi. Hapo changanya ajira rasmi na isiyo rasmi
Hebu fafanua kidogo mataifa yalio endelea huko duniani walio kwenye ajira rasmi na wasio kwenye ajira rasmi uwiano wao ukoje halafu turudi kujadili hapa kwetu nipo hapo chini ya mfenesi natoa matope kwenye mabuti!
 
Hebu fafanua kidogo mataifa yalio endelea huko duniani walio kwenye ajira rasmi na wasio kwenye ajira rasmi uwiano wao ukoje halafu turudi kujadili hapa kwetu nipo hapo chini ya mfenesi natoa matope kwenye mabuti!
Marekani ni 4%

Uingereza ni 4%

Russia ni 5.1%

China ni 5%

Kwenye watu 100 ni kati ya watu 4 mpaka 5 ndiyo hawana ajira rasmi.
 
Kabisa... Lakini angalau kati ya watu 10 basi watu 9 wawe na ajira rasmi.

Hapa bongo kati ya watu kumi ni watu watatu tu ndiyo wapo kwenye ajira rasmi. Hapo changanya ajira rasmi na isiyo rasmi

Tatizo ni watunga sera wasomi wakubwa kabisa lakini wabinafsi kama akina Dr. Mwigulu na Kitilia Mkumbo ambao walipaswa kuwa wanaharakati na sio watunga sera na wasimamizi wa wizara.

Hii nchi ndani ya miaka mitano inawezekana kabisa kuwa na uchumi mkubwa kuliko Kenya endapo tu tutawakataa watawala wapenda starehe na wabinafsi kama waliopo madarakani. Waziri anasimdikizwa bungeni na msafara wa magari ya kifahari kwenda kusoma bajeti iliyojaa pesa za mikopo na ahadi na misaada.

Yale magari aliyokua nayo kwenye msafara yakiuzwa yote ni zaidi ya bil. 1.5 . Ambapo zunaweza kununua Ambulace za Hospitali za aina ya Toyota Hiace zaidi ya 40.
Zinauwezo wa kujenga vyoo vya mashimo vya mil.10 zaidi ya vyoo 150.

Kupanga ni kuchagua. Rasilimali zipo watu ni wengi sana ndio maana matajiri kama akina MO ,Bakhresa,GSM ,Lake Oil ,Taifa Gas wanapaa kiuchumi kwa sababu population ni kubwa sana kwa sasa na kodi inaongezeka kwa sababu hata kwenye mafuta kadi inakusanywa sana mana Bajaji na pikikipi tu achilia mbali magari yameongezeka sana kwa miaka hii tofauti na wakati wa Nyerere,mwinyi,mkapa ,JK na JPM . Sasa inakuaje tuendelee kupiga Kopo ulaya kwa safari za kila siku na misafara mikubwa.

Wanaongeza posho za Mwenge , posho za vikao,posho za semina ,wanaongeza makongamano , magari ya kifahari na anasa za kila aina halafu wanasema pesa za ndani hazitoshi eti zinaishia kwenye mishahara ya wafanyakazi.

Lengo ni kuhalalisha wizi wao na matumizi yao mabaya huku wakiwachonganisha wafanyakazi na wananchi wasio na ajira rasmi serikalini. Yaani wananchi wannchi waamini kuwa Kodi ya Wananchi mil.65 inalizwa na mishahara ya wafanyakazi wasiofika laki 6.

Kumbe kodi zote zinaishia kwenye kundi dogo la Watawala ,mabalozi,Majaji,mawaziri,wabunge , wakurugenzi, makatibu wakuu wa wizara maRC na maDC na wakuu wengine wizarani. Ambao idadi yao haifiki hata efu tano.
Huku walimu ,mapolisi ,wanajeshi, majeshi ya magereza, uhamiaji na wakuzima moto wote wakiwa na mishahara duni isiyolingana na posho tu ya kununulia mapazia na meza kila mwaka ya hilo kundi dogo nililolitaja .

Wapinzani wafungueni macho sasa wafanyakazi kuwa Serikali ya CCM inawachonganisha na wananchi ndio maana kwa sasa vijana waliokosa ajira hawana hasira na CCM na serikali yake bali wana hasira na wafanyakazi wa umma kwa sababu kuwa wanalipwa mamilioni ya pesa na kumaliza kodi zao mpaka seriali inakopa . Imefikia mahali mpaka wamadai kuwa wafanyakazi wastaafu na miaka 40 ili wengine waajiriwe. Bila kujua kuwa wafanyakazi karibu wote mishahra yao haifiki laki 6 kwa mwezi na hawana pesa ya usafiri ,kodi ya nyumba , pesa ya maji ,pesa ya umeme,chakula wakiwa kazini wanajinulia na maji ya kunywa ,mavazi n.k.
Ukipiga mahesabu mishahara yao inaishia kwenye eneo na mazingira ya kazi hivyo kuwalazimu kukopa ili waweze kusomesha watoto na kutunza familia na kujenga. Sasa wakistafu na miaka 40 itakuaje mana wengine watakua hawajaoa wala kuolewa na kuzaa.
Yote ni kwa sababu Serikali inatumia kodi kwa mambo ya anasa na kuteua na kutengua na kulipana fadhili za madara na safari za ulaya na Uarabuni kumwagilia moyo mana maisha yenyewe ni haya na watanzania wamelala.
 
Umenena vyema,

CHADEMA inategemea CCM kuitoa CCM madarakani.

Sijui kama nimeeleweka🤔

Mkapa aliwahi kusema kuwa hakuna nchi Duniani ambayo Chama Tawala kinasaidia wapinzani wake ili waingie madarakani bali ni wapinzani wanatakiwa wafanye jitahada wenyewe na sio kutegemea waliopo madarakani wawaonee huruma.

Lisu namuelewa sana.

Kuna watu wanasema oooh ,Mwenda zake alizuia mikutano ,oooh ,alikua dikteta nk. Lakini sasa mama amaruhusu Mikutano na siasa zifanyike na maandamano. Lakini wanashindwa kuelewa kuwa Hakuna sheria iliyokua inakataza mikutano ya hadhara bali ni maelekezo tu ya mdomoni kama vitisho tu kutishia nyau.

Kama Kenya walikishinda chama cha KANU kwenye mazingira magumu kuliko yale ya JPM tena pakiwa na Ukabila mkubwa sana. ambapo karibu idara zote Zilishikiliwa na Wakikuyu ,wakamba na Wakalenjii.

Katiba yao ilikua ni ya Kibabe kuliko ya Tanzania mana ilikua ni lazima kufauata nyayo za Rais Moi ili uishi.
Leo Tanzania tuna CCM nyepesi sana iliyogawanyika vipoande na kuungwa na pesa na madaraka tu.

CCM ya sasa inaogopa kishindo hata cha Walemavu wa miguu Kama wale Washami waliokimbia kishindo cha watu wenye ukoma .
 
CCM wataondoka madarakani kwa mtutu wa bunduki. Hizi hizi bunduki na majeshi wanayotumia kukandamiza upinzani na kuiba kura ndiyo hizo hizo zitakuja kuwageukia. Kwa vile hawataki kuondoka kwa amani kupitia kura basi wataondoka kwa shari na uwagaji wa damu.
Wewe ndo una hoja halisia.
Hakuna kitu sipendi kusikia kama kura na maandamano!
Kuna wakat nahisi hata Chadema wanafanya sarakasi wapate kula.
Mengine yanawapata kama tu collateral damage.
Mana huwezi kutumia fomula ile ile miaka yoote na hupat matokeo na dalili za matokeo na bado ukatuaminisha unamaanisha!
Tusikie Plan B.
 
Mkapa aliwahi kusema kuwa hakuna nchi Duniani ambayo Chama Tawala kinasaidia wapinzani wake ili waingie madarakani bali ni wapinzani wanatakiwa wafanye jitahada wenyewe na sio kutegemea waliopo madarakani wawaonee huruma.

Lisu namuelewa sana.

Kuna watu wanasema oooh ,Mwenda zake alizuia mikutano ,oooh ,alikua dikteta nk. Lakini sasa mama amaruhusu Mikutano na siasa zifanyike na maandamano. Lakini wanashindwa kuelewa kuwa Hakuna sheria iliyokua inakataza mikutano ya hadhara bali ni maelekezo tu ya mdomoni kama vitisho tu kutishia nyau.

Kama Kenya walikishinda chama cha KANU kwenye mazingira magumu kuliko yale ya JPM tena pakiwa na Ukabila mkubwa sana. ambapo karibu idara zote Zilishikiliwa na Wakikuyu ,wakamba na Wakalenjii.

Katiba yao ilikua ni ya Kibabe kuliko ya Tanzania mana ilikua ni lazima kufauata nyayo za Rais Moi ili uishi.
Leo Tanzania tuna CCM nyepesi sana iliyogawanyika vipoande na kuungwa na pesa na madaraka tu.

CCM ya sasa inaogopa kishindo hata cha Walemavu wa miguu Kama wale Washami waliokimbia kishindo cha watu wenye ukoma .
KANU iliuwawa na watu Toka ndani ya KANU!!

CCM itakuwa hivyo hivyo 2025 endapo watalazimisha huyo aliyepo kugombea 🔥
 
KANU ilikuwa na watu Toka ndani ya KANU!!

CCM itakuwa hivyo hivyo 2025🔥
KANU ilikuwa na watu toka ndani ya KANU... Unamaanisha nini!?

Ni kama umeandika jambo lenye mkanganyiko hivi.
 
KANU ilikuwa na watu toka ndani ya KANU... Unamaanisha nini!?

Ni kama umeandika jambo lenye mkanganyiko hivi.
Iliuwawa na watu Toka ndani ya KANU!!

Ni KANUNI, kuwa msaliti Huwa hatoki nje, Bali ndani, jikoni.

Paka wawekee chakula kingi uwezavyo katika sahani, ila kuparuana lazima.
 
KANU ilikuwa na watu Toka ndani ya KANU!!

CCM itakuwa hivyo hivyo 2025🔥

Tatizoni kuwa Watanganyika jambo la kijinga linasambaa haraka kuliko jambo la akili na maarifa.
Kuna jambo limeshajengeka kwenye akili za watu kuwa wale wanaohamia upinzani ni wasaliti na mamluki wanaotumwa na CCM.

Tena wanakuambia kabisa kuwa wale ni wasaliti wametumwa na CCM msiwapokee wametumwa kuhujumu Chama . Ujinga mtupu. Wakati huo huo CCM inawakaribisha na kuwapa madaraka wale wanaotoka upinzani!

Hali hii inawafanya wale wanotoka CCM na kujiunga na upinzani kuishi maisha ya shida sana ndani ya Chama na kutengwa sana na kukejeliwa kwenye mitandoa hasa pale wanapojaribu kugombea nafasi za uongozi kama haki yao ya kuomba ridhaa kwa ajili ya kukijenga chama ili waweze kuzidi kuwavuta wengine . Badala yake wanakejeliwa na kuitwa wasaliti ,mamluki wa CCM n.k ,hatimaye kujiona wapweke sana hivyo kuamua kurudi CCM. Kule wakirudi CCM kama kawaida yake inawapokea kwa vingi'ora na mbwembwe kubwa ili tu kuhakikisha watu wengi wanaona ni bora wafie ndani ya CCM kwani heshima zao ndani ya Chadema zinadhiliwa na hata wakifa hawazikwi kwa heshima inayostahili badala yake watu wanaona ni bora wazike Mbwa kwa heshma kwa sababu tu ni mbwa wa wanaedhani kuwa ni mwenzao kutokana na kuwa ni lini alianza nao harakati.

Bado upinzani haujajua kuwa Lengo la watanzania ni kuwa na Katiba mpya inayoweka maslahi ya umma mbele na sio vyama na kuwafanya watanzania wote kuwa huru kisiasa ,kijamii na kiuchumi.

Mfano kwa sasa ni wazi kuwa kuna Watu ndani ya CCM wanapaswa kuwa Wapinzani nje ya CCM halikadhalika kuna Wapinzani hasa Chadema wanapaswa kuwa kwenda CCM mana nia zao na fikra zao zinafanana sana na za kina Bashe na Mwigulu. Ni watu kwenye majukwaa wanajinadi kama watetezi wa wanyonge lakini wamejaa tamaa kubwa sana ya fedha na mali. Hawa wanaonekana kila baada ya uchaguzi wanarudi CCM au wanaanzisha chokochoko ili wapate uteuzi.
Mfano Mtu kama Mpina , hata wale Covid 19 ni majembe sana. Hata ukiwasikiliza bungeni . Wakirudi Chadema wakubaliwe kwa sababu walitumia demokrasia na uhuru tunaoutaka kufika walipofika.
Walitumia mwanaya na ubovu wa katiba kuingia bungeni kinyume na katiba ya chama chao na katiba ya nchi lakini wamejipatia kazi kutokana na nguvu ya Serikali na Ikulu na nguvu ya Bunge na mahakama lakini pia wamecheza na akili ya siasa kuwa kuna haki fulani zimekiukwa ndani ya chama chao wakapata loop hole japo ni kweli kuwa baadhi yao hawaipendi CCM na hawana chembe ya falsafa za CCM. Wakirudi kukipigania chama chao ili kuingia CCM basi wapokelewe. Lengo ni kuitoa CCM na kuisambaratisha kwanza kisha kuleta katiba mpya itakayomfanya mtanzania yeyote kuwa huru kufanya kazi ya siasa ,au biashara au kazi nyingine ya umma bila kuingiliwa na CCM kama ilivyo sasa.

Huku kuwabagua na kuwapa majina mabaya wale wanaotoka vyama vingine kuja Chadema imewafanya mpaka wapinzani wengine kuona kuwa kwenda chadema ni hatari zaidi kuliko kurudi CCM. Mfano Zito Kabwe na wengi ndani ya Chama chake wapo tayari kuungana na CCM kuliko Chadema kwa sababu wanatulanwa na kudhalilishwa zaidi na wanachadema kuliko wanaCCM . Hii sio maana ya Demokrasia. Huu ni uhuni unaotakiwa kupingwa sana.
Hili linatakiwa liachwe mara moja ili Chadema kiwa chama chenye Nia hakisi ya kuongoza dola. Mnaweza msiwateue au kuwapa nafasi ndani ya chama lakini mnaweza kuwatumia k2a heshma kubwa kwenye kampeni bila kuwakejeli au kuwatukana kwenye mitando. Kukaa kimya wakati mwingine ni hekima kubwa.

Hivi mtu kama Dr. Slaa ni mtu wa kupuuza na kumwita msaliti na mamluki wakati tangu akiwa CCM mpaka sasa amesimamia msimamo wake wa kupinga kuuzwa kwa rasilimali za umma na ufisadi ndio maana alikataa kumuunga mkono Lowasa . Na ule ulikua ni msimamo usio na unafiki na akaondoka nchini bila kuhamia CCM kwa imani yake kubwa aliyokua nayo ndani ya chama chake akaona ni bora akae pembeni kuliko kushika silaha na kuigeuzia Chadema kwenye Kampeni. Alitumia hekima Kubwa sana.

Dr.Slaa anapaswa kuenziwa ndani ya Chadema na sio kutukanwa.

Mambo ya kutukana wale wanaopingana kwa hoja yalifanyika wakati huo wa chama kimoja na sio sasa. Kwa sasa mnatakiwa muweke mdahalo mjenge hoja juu ya umoja wetu ,sera zetu za uchumi na maendeleo ,vita dhidi ya ufisadi n.k.

CCM hawana cha kutuambia tena mana wamezuia mitandoa na vyombo vyote vya habari ili waseme wao lakini wamekosa cha kusema na hawaamniki tena. Sasa kwenye kampeni watatumia nini tena kutuhadaa au wataahidi kipi ambacho hawajawahi kukiahidi?

Mpaka sasa Rais peke yake kuelekea 2025 ametumia mabilioni ya pesa kununua pikipiki kuhofia upinzani. Yaani CCM wana hofu kuliko wapinzani. Hata Lisu hajawahi kusema kuwa atagombea tangu ameanza maandamano . Nimemfuatilia sana . Kwa maana hiyo Lisu bado hajaanza kampeni kwa mujibu wa sheria . Samia alishaanza kabla ya muda wake hivyo kikanuni hawezi kupitishwa na tume labda wabadili kanuni. Hana sifa ndani ya CCM na pia kwenye tume ya uchaguzi hana sifa mana alianza kampeni kabla ya wakati.
Anapaswa kuenguliwa mapema ili kuondoa aibu kubwa kwa taifa kuweka mgombea asiyefuata kanuni.

Kwa hiyo kama wapinzani wapo siriasi kuiondoa CCM madarakani ni lazima wawashawishi wale wanaoona kuwa wanaendana nao kimisimamo toka ndani ya CCM , ACT , CUF na NCCR mageuzi ili washinde uchaguzi. CCM ikishindwa itasambaratika mana hakuna atakayeweza kubaki kwenye chama bila kuwa na uteuzi. Wasomi wote wataikimbia CCM . Harakati za CCM ndani ya vyuo itakoma ,Watoto wadogo wanaoitwa Chipukizi watakoma na kurudi kusoma mana sheria hairuhusu watoto chini ya miaka 18 kuijihusisha na siasa.

Wafanyabiashara wa madawa na magendo na wakwepa kodi watakimbia . Ugaidi utapotea mana pesa wanazopokea toka nje zitahojiwa kuwa zinakwenda wapi !! Siasa za udini ,ukabila zitaondoka na kubaki siasa za hoja na ushawishi wa sera. Jeshi litajiimarisha katika sayansi na teknolojia badala ya Siasa. Polisi watafanya kazi zao kwa amani na kwa wepesi kwasababu watakua hawana mashinikizo ya kisiasa. Adui wa polisi watakua ni wahalifu na sio wanasiasa.
Nchi itakua na furaha kuu.
 
Tatizoni kuwa Watanganyika jambo la kijinga linasambaa haraka kuliko jambo la akili na maarifa.
Kuna jambo limeshajengeka kwenye akili za watu kuwa wale wanaohamia upinzani ni wasaliti na mamluki wanaotumwa na CCM.

Tena wanakuambia kabisa kuwa wale ni wasaliti wametumwa na CCM msiwapokee wametumwa kuhujumu Chama . Ujinga mtupu. Wakati huo huo CCM inawakaribisha na kuwapa madaraka wale wanaotoka upinzani!

Hali hii inawafanya wale wanotoka CCM na kujiunga na upinzani kuishi maisha ya shida sana ndani ya Chama na kutengwa sana na kukejeliwa kwenye mitandoa hasa pale wanapojaribu kugombea nafasi za uongozi kama haki yao ya kuomba ridhaa kwa ajili ya kukijenga chama ili waweze kuzidi kuwavuta wengine . Badala yake wanakejeliwa na kuitwa wasaliti ,mamluki wa CCM n.k ,hatimaye kujiona wapweke sana hivyo kuamua kurudi CCM. Kule wakirudi CCM kama kawaida yake inawapokea kwa vingi'ora na mbwembwe kubwa ili tu kuhakikisha watu wengi wanaona ni bora wafie ndani ya CCM kwani heshima zao ndani ya Chadema zinadhiliwa na hata wakifa hawazikwi kwa heshima inayostahili badala yake watu wanaona ni bora wazike Mbwa kwa heshma kwa sababu tu ni mbwa wa wanaedhani kuwa ni mwenzao kutokana na kuwa ni lini alianza nao harakati.

Bado upinzani haujajua kuwa Lengo la watanzania ni kuwa na Katiba mpya inayoweka maslahi ya umma mbele na sio vyama na kuwafanya watanzania wote kuwa huru kisiasa ,kijamii na kiuchumi.

Mfano kwa sasa ni wazi kuwa kuna Watu ndani ya CCM wanapaswa kuwa Wapinzani nje ya CCM halikadhalika kuna Wapinzani hasa Chadema wanapaswa kuwa kwenda CCM mana nia zao na fikra zao zinafanana sana na za kina Bashe na Mwigulu. Ni watu kwenye majukwaa wanajinadi kama watetezi wa wanyonge lakini wamejaa tamaa kubwa sana ya fedha na mali. Hawa wanaonekana kila baada ya uchaguzi wanarudi CCM au wanaanzisha chokochoko ili wapate uteuzi.
Mfano Mtu kama Mpina , hata wale Covid 19 ni majembe sana. Hata ukiwasikiliza bungeni . Wakirudi Chadema wakubaliwe kwa sababu walitumia demokrasia na uhuru tunaoutaka kufika walipofika.
Walitumia mwanaya na ubovu wa katiba kuingia bungeni kinyume na katiba ya chama chao na katiba ya nchi lakini wamejipatia kazi kutokana na nguvu ya Serikali na Ikulu na nguvu ya Bunge na mahakama lakini pia wamecheza na akili ya siasa kuwa kuna haki fulani zimekiukwa ndani ya chama chao wakapata loop hole japo ni kweli kuwa baadhi yao hawaipendi CCM na hawana chembe ya falsafa za CCM. Wakirudi kukipigania chama chao ili kuingia CCM basi wapokelewe. Lengo ni kuitoa CCM na kuisambaratisha kwanza kisha kuleta katiba mpya itakayomfanya mtanzania yeyote kuwa huru kufanya kazi ya siasa ,au biashara au kazi nyingine ya umma bila kuingiliwa na CCM kama ilivyo sasa.

Huku kuwabagua na kuwapa majina mabaya wale wanaotoka vyama vingine kuja Chadema imewafanya mpaka wapinzani wengine kuona kuwa kwenda chadema ni hatari zaidi kuliko kurudi CCM. Mfano Zito Kabwe na wengi ndani ya Chama chake wapo tayari kuungana na CCM kuliko Chadema kwa sababu wanatulanwa na kudhalilishwa zaidi na wanachadema kuliko wanaCCM . Hii sio maana ya Demokrasia. Huu ni uhuni unaotakiwa kupingwa sana.
Hili linatakiwa liachwe mara moja ili Chadema kiwa chama chenye Nia hakisi ya kuongoza dola. Mnaweza msiwateue au kuwapa nafasi ndani ya chama lakini mnaweza kuwatumia k2a heshma kubwa kwenye kampeni bila kuwakejeli au kuwatukana kwenye mitando. Kukaa kimya wakati mwingine ni hekima kubwa.

Hivi mtu kama Dr. Slaa ni mtu wa kupuuza na kumwita msaliti na mamluki wakati tangu akiwa CCM mpaka sasa amesimamia msimamo wake wa kupinga kuuzwa kwa rasilimali za umma na ufisadi ndio maana alikataa kumuunga mkono Lowasa . Na ule ulikua ni msimamo usio na unafiki na akaondoka nchini bila kuhamia CCM kwa imani yake kubwa aliyokua nayo ndani ya chama chake akaona ni bora akae pembeni kuliko kushika silaha na kuigeuzia Chadema kwenye Kampeni. Alitumia hekima Kubwa sana.

Dr.Slaa anapaswa kuenziwa ndani ya Chadema na sio kutukanwa.

Mambo ya kutukana wale wanaopingana kwa hoja yalifanyika wakati huo wa chama kimoja na sio sasa. Kwa sasa mnatakiwa muweke mdahalo mjenge hoja juu ya umoja wetu ,sera zetu za uchumi na maendeleo ,vita dhidi ya ufisadi n.k.

CCM hawana cha kutuambia tena mana wamezuia mitandoa na vyombo vyote vya habari ili waseme wao lakini wamekosa cha kusema na hawaamniki tena. Sasa kwenye kampeni watatumia nini tena kutuhadaa au wataahidi kipi ambacho hawajawahi kukiahidi?

Mpaka sasa Rais peke yake kuelekea 2025 ametumia mabilioni ya pesa kununua pikipiki kuhofia upinzani. Yaani CCM wana hofu kuliko wapinzani. Hata Lisu hajawahi kusema kuwa atagombea tangu ameanza maandamano . Nimemfuatilia sana . Kwa maana hiyo Lisu bado hajaanza kampeni kwa mujibu wa sheria . Samia alishaanza kabla ya muda wake hivyo kikanuni hawezi kupitishwa na tume labda wabadili kanuni. Hana sifa ndani ya CCM na pia kwenye tume ya uchaguzi hana sifa mana alianza kampeni kabla ya wakati.
Anapaswa kuenguliwa mapema ili kuondoa aibu kubwa kwa taifa kuweka mgombea asiyefuata kanuni.

Kwa hiyo kama wapinzani wapo siriasi kuiondoa CCM madarakani ni lazima wawashawishi wale wanaoona kuwa wanaendana nao kimisimamo toka ndani ya CCM , ACT , CUF na NCCR mageuzi ili washinde uchaguzi. CCM ikishindwa itasambaratika mana hakuna atakayeweza kubaki kwenye chama bila kuwa na uteuzi. Wasomi wote wataikimbia CCM . Harakati za CCM ndani ya vyuo itakoma ,Watoto wadogo wanaoitwa Chipukizi watakoma na kurudi kusoma mana sheria hairuhusu watoto chini ya miaka 18 kuijihusisha na siasa.

Wafanyabiashara wa madawa na magendo na wakwepa kodi watakimbia . Ugaidi utapotea mana pesa wanazopokea toka nje zitahojiwa kuwa zinakwenda wapi !! Siasa za udini ,ukabila zitaondoka na kubaki siasa za hoja na ushawishi wa sera. Jeshi litajiimarisha katika sayansi na teknolojia badala ya Siasa. Polisi watafanya kazi zao kwa amani na kwa wepesi kwasababu watakua hawana mashinikizo ya kisiasa. Adui wa polisi watakua ni wahalifu na sio wanasiasa.
Nchi itakua na furaha kuu.
Hii comment ingetafutiwa heading, ikaboreshwa kidogo,

Ingefaa kuwa thread inayojitegemea.
 
Kwanza hakuna mjadala kuwa CCM inatakiwa kutolewa madarakani kwa njia yoyote ile.

Pia hakuna mjadala kuwa mpaka sasa hakuna jinsi nyingine ya kuwa na chama kingine nje ya CHADEMA cha kupambana na CCM.

Ni ukweli kwamba CHADEMA ni chama bora cha siasa kuliko vyama vyote vya siasa nchini CCM ikiwemo.

Baada ya CHADEMA kwa ubora, inafuatia CCM na vyama vingine kama vile ACT na vinginevyo viko kwenye fungu (bundle) moja.

Lakini kuitoa CCM madarakani pamoja na udhaifu wake,inataka jamii ya watanzania kwa uhalaiki wake ( amassed) kujua nini kifanyike ili kuitoa CCM madarakani.

Kuishutumu CCM kwa uovu wake ni jambo la zamani kwa sasa. Kati ya watanzania 100 watanzania 60 wanaujua uovu wa CCM kwa undani sana.

Hakuna asiyejua kuwa CCM ndiyo inaifilisi nchi hii. Watanzania wote wanajua maisha yao yanaharibiwa na CCM kuwepo madarakani.

Lakini asilimia tisini (90%) ya watanzania hawapo tayari kushiriki kwenye harakati za kuitoa CCM madarakani.

Watanzania wengi wanadhani kazi ya kuitoa CCM madarakani ni ya CHADEMA peke yao.

Kila siku wanalaumiwa ni kwa nini hawaitoi CCM madarakani. Cha kushangaza watu wengi wanaogopa kuiudhi CCM.

Huwezi kuta wafanyakazi Serikalini, wafanyabiashara, wakulima na watu wa kawaida wakipambana hadharani na CCM.

Kwa mazingira haya huwezi tarajia CHADEMA peke yao kuitoa CCM madarakani.

Kutegemea CHADEMA peke yake kuitoa CCM madarakani, ni kutarajia muujiza.
kwasabubu tu unaichukia CCM kibinafsi, ndio wananchi wakuunge mkono kuing'oa CCM mamlakani 🤣

kwanza watastaajabu sana watakaposkia hoja yako, lakini pia watakushangaa mno, kisha watakuonea huruma na halafu watakupuuza na kusikitika sana, na kukonclude kwamba kijana wao is no more mentally and saikolojikali fit, tatizo la afya ya akili linaweza kua limechukua mkondo wake kwa kijana 🐒

itoshe tu kusema ni zaidi ya asilimia 90% ya wananchi na waTanzania wana Imani kubwa sana, matumaini na mapendo ya dhati na CCM, kuliko chama kingine chochote nchini, na hata vyama vyote wakiungana bado hataifikia kiwango cha kuing"oa CCM mamlakani....

kwanza hawaelewani, hawaaminiani, kila moja ana uchu wa fedha na madaraka, hawapendani, ni maadui miongoni mwao, wanataamaa na mioyo ya kusalitiana n.k

na kwahivyo basi hakuna uwezekano miongoni, kwanza wa kuungana kama wapinzani wenye sauti na uelekeo moja, lakini pili hakuna uwezekano wa kuidhoofisha CCM bali kuimarisha zaidi mamlakani na tatu, hakuna kabisa uwezekano wa kuiondoa CCM mamlakani sasa, lakini pia wakati ujao....🐒

Kidumu Chama Cha Mapinduzi 🐒
 
Back
Top Bottom