Pre GE2025 CHADEMA: Tuna Wanachama milioni 17 Nchi nzima!

Pre GE2025 CHADEMA: Tuna Wanachama milioni 17 Nchi nzima!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Uko sahihi kabisa Mkuu.
Kuandaa tamasha kubwa, sio Chini ya milioni 180 hadi 300

Lakini watu wameandaa hayo matamasha zaidi ya 6 Mwaka huu pekee.

Haijulikani mtoa hela (financiers) ni nani, ila yanaandaliwa Kila kukicha
 
Pamoja na hoja yako, lakini mnapokuwa mmejitokeza wengi kupiga Kura, mathalani Wanachama wote hao 17milioni, hata kama wakiiba lakini hakutakosekana Kura zaidi ya milioni 8 hadi 10 hapo

Ndiyo maana nasisitiza, watu kujitokeza wengi wakati wa zoezi la kupiga kura
Mbona Umetumia Nafsi ya Pili wingi Sheikh??
Mimi si Mmoja wa Nafsi ya Pili wingi
 
Pamoja na hayo Mkuu, hata kama wangeiba hizo kura, lakini wangejitokeza hao Wanachama milioni 17 hamna hamna hapo wangepata Kura kama milioni 10 hivi tukichukulia kura milioni 7 zimeibwa


Hoja yangu ni kwamba Idara ya Uenezi haifanyi kazi zake kiufanisi
Washasema mara nyingi kuwa kura zinazotangazwa hazina uhusiano wowote na kura zilizopigwa. Yaani, matokeo ya kura wanakuwa nayo tayari kabla ya siku ya kupiga kura!
 
Washasema mara nyingi kuwa kura zinazotangazwa hazina uhusiano wowote na kura zilizopigwa. Yaani, matokeo ya kura wanakuwa nayo tayari kabla ya siku ya kupiga kura!
Hii ni hatari sasa 🙌
 
Kwahio CHADEMA ina registered voters zaidi ya CCM na ni chama cha Tisa kwa wanachama wengi duniani ?

Basi waende wikipedia wakarekebishe Data sababu huko hawamo kabisa...

 
Chama kikuu Cha Upinzani nchini Chadema limesema Katika leja yake kina Jumla ya Wanachama milioni 17

Source: East Africa Radio
Hiyo milioni saba (7) pekee wakiwa ni wananchama kwelikweli, wakiamua chama chao kisiendelee kuonewa nchi nzima inatosha kabisa kuondoa upuuzi wote wanao fanyiwa na CCM.

Na bado kutakuwa na akiba ya milioni 10; na wengi wengine wasiokuwa wanachama wasio kubali uchafu wa CCM.

Tatizo la CHADEMA (viongozi) ni kutojuwa kuwapanga tu wana chama wao.
 
Hiyo milioni saba (7) pekee wakiwa ni wananchama kwelikweli, wakiamua chama chao kisiendelee kuonewa nchi nzima inatosha kabisa kuondoa upuuzi wote wanao fanyiwa na CCM.

Na bado kutakuwa na akiba ya milioni 10; na wengi wengine wasiokuwa wanachama wasio kubali uchafu wa CCM.

Tatizo la CHADEMA (viongozi) ni kutojuwa kuwapanga tu wana chama wao.
Wewe umeamini hizo takwimu? 🐼😂
 
Inawezekana kweli wanao Wanachama 17 Milioni kama walivyosema kupitia Database waliyonayo

Ila hoja yangu ni kwamba hiyo Idara ya Uenezi imelala, haifanyi kazi yake ipasavyo
Siyo "idara ya uenezi" pekee. Huu ni udhaifu mkubwa wa uongozi wa chama.
Raslimali muhimu ya chama chochote ni wana chama wake. Sasa kama chama hakiwezi kuitumia ipasavyo raslimali hiyo kutakuwepo tofauti gani kati ya wafugaji wa kimasai wenye mifugo mia na zaidi, wakati wanashindwa hata kuwapeleka watoto shule kwa kukosa ada!

Chama kina mtaji mkubwa, lakini hakijui namna ya kuutumia mtaji huo!
 
Wajitahidi kufikia 30m tu - kazi itakuwa imekwisha.
 
CDM waacheni CCM wawabishie, yaani kukimbiza mwizi ni kimya kimya !! style ya kwetu Buguruni.
 
Kama Chama kina Wanachama 17 Milioni, wakati huo CCM ikipata ushindi wa Kura milioni 12 plus ina maana hakukufanyika uhamasishaji wa kutosha Kuwavutia wapiga Kura kujitokeza Kwa wingi kwenda kupiga Kura.

Hilo kosa lisijirudie Mwaka 2025
Sasa sijui sisi tunao wahimiza CHADEMA wafanye kazi kwa niaba yetu kutusaidia kuondoa uovu huu chini ya CCM, tuyaseme vipi, na mara ngapi haya tunayo washauri ili wapate kuyafanya!

Haya yote unayo yaandika humu mkuu 'Grahams'; wengine tulianza takribani miaka mitano iliyo pita kuwahimiza CHADEMA wajipange na kuwa tayari kwa hii 2025. Tumeshauri njia mbalimbali za kukifanya chama kuwa hai, tokea huko mitaani; kila ngazi hadi makao makuu ya chama..., ilikuwa ni kazi ya kuwaiga tu hao hao CCM kimuundo; lakini naona CHADEMA wao walitumia muda wao kivingine.

Sasa tupo hapa, pamoja na kwamba Magufuli hayupo kufanya yaliyo fanyika 2019/2020; lakini Samia yupo, ambaye yeye kaamua kutumia njia ya pesa, badala ya maguvu. Matokeo yatakuwa ni yale yale.
 
Sasa sijui sisi tunao wahimiza CHADEMA wafanye kazi kwa niaba yetu kutusaidia kuondoa uovu huu chini ya CCM, tuyaseme vipi, na mara ngapi haya tunayo washauri ili wapate kuyafanya!

Haya yote unayo yaandika humu mkuu 'Grahams'; wengine tulianza takribani miaka mitano iliyo pita kuwahimiza CHADEMA wajipange na kuwa tayari kwa hii 2025. Tumeshauri njia mbalimbali za kukifanya chama kuwa hai, tokea huko mitaani; kila ngazi hadi makao makuu ya chama..., ilikuwa ni kazi ya kuwaiga tu hao hao CCM kimuundo; lakini naona CHADEMA wao walitumia muda wao kivingine.

Sasa tupo hapa, pamoja na kwamba Magufuli hayupo kufanya yaliyo fanyika 2019/2020; lakini Samia yupo, ambaye yeye kaamua kutumia njia ya pesa, badala ya maguvu. Matokeo yatakuwa ni yale yale.
Kuna wakati linakuwa sikio la kufa...

Wasipojipanga kuenenda na wakati yatawakuta ya NCCR ya 1995

Siasa inahitaji mabadiriko na kuendana na wakati, ndiyo maana CCM inaajiri hadi wataalamu wa nje ili kuwapa uzoefu.

Mwaka Jana mwishoni na Mwaka huu kabla ya Mwezi July, CCM iliwapeleka Makada wao Nchi ya China kwenda kujifunza lakini pia hata pale Lumumba kwenye Chuo chao cha Makada.

Wanasema kama unaishi Mwaka 2024 Kwa slogan za Mwaka 1992 huwezi kutoboa

Chadema must change
 
Siyo "idara ya uenezi" pekee. Huu ni udhaifu mkubwa wa uongozi wa chama.
Raslimali muhimu ya chama chochote ni wana chama wake. Sasa kama chama hakiwezi kuitumia ipasavyo raslimali hiyo kutakuwepo tofauti gani kati ya wafugaji wa kimasai wenye mifugo mia na zaidi, wakati wanashindwa hata kuwapeleka watoto shule kwa kukosa ada!

Chama kina mtaji mkubwa, lakini hakijui namna ya kuutumia mtaji huo!
Wasipoangalia Chama kitadumaa

Wanashindwa nini kuajiri wataalamu Washauri kwaajili ya kuwapika Viongozi wao na Chama Kwa ujumla.

Chadema kinapokea Ruzuku zaidi ya milioni 100 Kwa Mwezi, wastani wa bilioni 1.2 Kwa Mwaka.

Unashindwa nini kuajiri Consultant firm Kwa kuwalipa maybe 50M kuwapika Viongozi wao Wakuu na wale wa Mikoa na Wilaya??
 
Back
Top Bottom