CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika


Mkuu hapo umenena .. people are projecting their expectations onto Ukawa .. huyo mgombea hata hajagusia katiba mpya and they are dreaming kuwa viongozi hawa wakiingia watabadili sheria. Inasikitisha kuwa safari ya matumaini is just that hope without basis or foundation. .
 

Kuungana na kuwa chama kimoja chenye nguvu ni jambo jema, lakini tusisahau kujiuliza swali la msingi sana je hiki kitu kinawezekana? Na kama hakiwezekani je hawa wapinzani wafanye nini? Je waendelea kila chama kivyake au wajaribu kama wanavyojaribu katika Ukawa ingawaje kuna nguvu kubwa inayotumika usiku na mchana kuwavuruga?
 
Mag3:

Wewe kweli umeichoka CCM. Hivi walikupeleka JKT wakati ule wa zamani?
Mkuu Zakumi,
Kuichoka tu CCM bila kuwa na silaha zinazokidhi mapambano kihoja ni kupoteza muda!

Ni sawa na watu wanaosema kila siku wanamchukia kiumbe anayeitwa shetani anayerubuni watu duniani wakati hawafanyi hata jitihada za kupambana ili kumshinda huyu shetani na hata wakifanya jitihada, silaha wanazotumia ni hafifu ambazo hazikidhi mazingira ya ushindi!
 
Muungano wa NARC ulioiondoa KANU 2002 ulikufa wakati wa uchaguzi uliofuata 2007 na Kibaki akagombea kupitia PNU. Lakini NARC walikuwa wamefanikisha jambo moja nalo ni kuing'oa KANU madarakani na mpaka leo hii KANU imekufa na kusahaulika! Wenzetu wamepitia kipindi kigumu cha mpito lakini tazama leo wako wapi....
Pengine mabadiliko tunayotayaka hayatakuja katika njia iliyonyooka na tutapitia kipindi cha mpito kitakachokuwa na misukosuko. Inawezekana UKAWA isiwe na maisha marefu itakaposhinda uchaguzi lakini lengo kuu la kuing'oa CCM litakuwa limetimia. Tutapita kwenye kipindi cha mpito chenye dhoruba lakini mwisho wa siku naamini tutatoka hapo tukiwa imara tayari kwa kuvuka hatua nyingine.
 

..lakini ukawa si unajulikana kwamba ni umoja wa katiba mpya, katiba ya Mzee Warioba?

..mpaka pale mgombea wa ukawa atakapokuja na msimamo mwingine basi there is a basis for us kuamini kwamba atasimamia matakwa ya katiba ya vyama vinavyounda ukawa.

..kama ambavyo kuna uwezekano wa ukawa kusambaratika huko mbele ya safari, uko uwezekano pia wa umoja huo kudumu na kutoa mchango mkubwa kwa mageuzi ambayo tumekuwa tukiyalilia kwa muda mrefu.

..binafsi nimeona niwape nafasi hawa ukawa tuone watafanya nini. naamini hata wakiboronga itakuwa rahisi kuwatimua.

..nina HOFU kubwa sana na hatma ya wapenda mageuzi nchi hii, ikiwa CCM ya Nape Nnauye, Paul Makonda, Ridhiwani Kikwete, January Makamba,.. itachukua madaraka.

cc Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mag3, Alinda
 

Nilimsikiliza vizuri mgombea wa Ukawa kwenye speech yake Kunduchi, hakuna mahali alisema kilichomfanya akaachana na CCM ni katiba au hata ufisadi. Amehama Chama kwa sababu moja tu - jina lake lilikatwa! Lowassa hajasema ameondoka CCM kwa sababu hawana sera nzuri, au kwasababu yeye anataka Serikali tatu. Hajasema hayo. Na hata hansard za Bunge Maalum la Katiba inaonesha aliunga mkono serikali mbili.

Kwa kifupi, kuna maswali mengi sana juu ya hii 'fast track exercise' ya kumpata mgombea wa UKAWA. Najua Mbowe na Lissu wamekazana kusema kuwa wanapambana na mfumo. Lakini hawataki kusema 'mfumo' unajengwa na nani? Na je, mgombea wao anahusika kwa namna yeyote katika kujenga mfumo wanaoupinga?
 

Nimeisoma vizuri katiba ya Marekani na hakuna kipengele chochote kinachotaja Republican au Democrat party. Wamarekani wameunda vyama hivi na vingine vya siasa kutokana na vipengele vya katiba vinavyowapa watu uhuru wa kukusanyika na kutowa mawazo. Hivyo misingi ya demokrasia sio kuwa na vyama vya kisiasa. Vyama vya siasa vimekuja baadaye sana kukusanya watu wenye mawazo yanayofanana (Itikadi) na vilevile kuwapa watu majukwaa ya kutoa mawazo.

Kwa Tanzania na nchi nyingine za kiAfrika, misingi ya kuunda demokrasia hatuifati. Na baadaye tunataka watu waunde vyama vya kisiasa na baadaye walazimishane kuwa na mawazo ya kufanana. Hii demokrasia ni ya kupotezeana wakati tu. Mawazo ya Lowassa ni kuwa rais. Hii sio itikadi na mwenye nia ya kujenga demokrasia hii sio njia ya kwenda. Itakuwa njia pale mawazo yake yapotasaidia kuleta matukio ya kihistoria yatakayobadilisha mwelekeo wa nchi. Kwa maana nyingine mipango ya Lowassa ni bahati nasibu kwa CDM na Taifa.
 

Mag3;

Ujio wa Lowassa ni bahati nasibu. Lakini game changer watabakia kuwa wananchi wanaopiga kura. Siku ya uchaguzi wakitoka kwa wingi na kuchagua CDM/UKAWA kwa sababu Lowasa yupo CDM, watakuwa wamefanya mabadiliko ya kihistoria. Au baada ya matokeo kutangazwa wakahamua kuleta misimamo ya kubadilisha matokeo, watakuwa wamefanya mapinduzi.

Kutegemea ujasiri wa viongozi wa CCM wanaojiunga CDM kuleta mabadiliko ni kutojipenda. Mwezi wa saba nilikuwa Segerea. Makongoro Mahanga na wapambe wake walikuwa anatembea kwenye mabaa kutafuta kura. Kama angeshinda kura za maoni ubovu wa CCM asingeuona. Je ni ujasiri gani atauleta CDM?
 



Mwanakijiji na Alinda:

Timing ni kitu muhimu katika siasa. Katika moja ya hotuba zake baada ya uchaguzi wa mwaka 2010, JK alisema hatuwezi kubadili kanuni za mchezo wakati mchezo umeanza. Alikuwa na maana kanuni mpya (katiba) itapatikana kabla ya uchaguzi wa 2015.

Kama kungekuwa na uwezekano, UKAWA ungekuwa na juhudi moja kubwa. Timing ya katiba mpya kwenye uchaguzi wa 2015. Wapinzani wasingeshiriki kwenye uchaguzi wa aina yoyote mpaka katiba mpya ipatikane. Kwa maoni yangu naona wanatumia nguvu nyingi sana kutaka kushinda uchaguzi huu na baadaye kubadilisha kanuni wakiwa washindi. Kwa kushiriki kwao, inawalazimu kuyamezea mambo yasio sameheka.
 

Je angezungumza mambo uliyotaja, si angelikalia tawi?



 

..wale hilo lisikupe shida.

..Dr.Mwakyembe amepata PhD yake kwa thesis ambayo inatetea muungano wa serikali 3.

..lakini kwasababu yuko kwenye CCM basi kwenye bunge la katiba akatetea serikali 2.

..Dr.Asha-Rose Migiro alikuwa mjumbe wa Tume ya Jaji Kisanga ambayo ilipendekeza serikali 3.

..lakini kwenye bunge la katiba Dr.Migiro akabadilika na kutetea serikali 2.

..mimi nadhani hansard haina maana hapa. kitu cha msingi ni Lowassa amejiunga na chama ambacho sera yake ni serikali 3.

cc MBEBA MAONO KAJA
 
Last edited by a moderator:

..ccm wangeweza kuendelea na uchaguzi na vyama vya kina Dovutwa, Mziray, na Hamad Rashid.

..nyinyi mnacheza na CCM nyinyi. hakuna mabadiliko yatafanyika bila CCM kupokonywa ikulu na bunge.
 
..ccm wangeweza kuendelea na uchaguzi na vyama vya kina Dovutwa, Mziray, na Hamad Rashid.

..nyinyi mnacheza na CCM nyinyi. hakuna mabadiliko yatafanyika bila CCM kupokonywa ikulu na bunge.

Vyama vidogo kama hivyo ni vya kuvifanyia utemi. Mnaviambia tu mkishiriki tu, tunachoma nyumba zenu moto.
 
JokaKuu, wapo watu kama mwenzangu Mzee Mwanakijiji ambao wameamua kuangalia kila tendo kwa jicho hasi mradi mhusika katika ufanikishaji wake ni mtu asiyekubalika machoni pao. Wanaamini kwamba motisha inayomsukuma mtu huyo ni maslahi binafsi na hawatoi nafasi kabisa kwa mtu kama huyo kufanikisha mabadiliko bila kutanguliza ubinafsi. They dont trust that person to willingly put the needs or wishes of others before their own...Because of this, Mzee Mwanakijiji has turned into a very predictable cynic.


Sasa hapa hata sikuelewi mzee mwenzangu; tuchukulie mfano...unapanga kusafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma kwa gari ndogo halafu unaanza kujiuliza maswali; je gari likiharibikia njiani, Je tukipata ajali, je daraja likisombwa na maji na maswali kama hayo. Je maswali kama haya yanaweza kweli yakakufanya usite na badala yake uhairishe safari yako? Mzee mwenzangu sema tu lilipolo moyoni...huna imani na upinzani.

Wakati wa kutoa manifesto bado, wakati wa kutoa ilani bado, wakati wa kujinadi bado, lakini wewe tayari unaihukumu UKAWA. Haulazimishwi kuipigia kura UKAWA lakini kwa nini usisubiri uonje chakula kilicho jikoni kabla ya kutoa hukumu, kwa nini hungoji kampeni zianze na ukiona maswali yako hayajibiwi uwanyime kura? Safari hii natumaini midahalo itakuwepo, sidhani kama wapo watakaoweka mpira kwapani kama safari iliyopita.

Cynic - who advocates the doctrines that virtue is the only good, that the essence of virtue is self-control, and that surrender to any external influence is beneath human dignity.
 
Vyama vidogo kama hivyo ni vya kuvifanyia utemi. Mnaviambia tu mkishiriki tu, tunachoma nyumba zenu moto.
Zakumi, ndio maana nasema wengi wenu hamuijui CCM and what it is capable of. Je umesahau Bunge Maalum La Katiba? Kususa kwa wapinzani kulisaidia nini, si waliendelea tu kama vile hakuna upinzani! Take note: ni hivyo vyama vidogo ndivyo viliwapa CCM uhalali. Mbona nyumba zao hazikuchomwa?
 

Mag3, mzee mwenzangu naona wengi wanachukulia UKAWA kama chama cha siasa. UKAWA haiwezi kuja na manifesto yao, hawana ilani yao na hawana chombo chochote cha kuweza kutoa ahadi zozote. Kimsingi, UKAWA haishiriki uchagui huu na haiwezi kuunda serikali kwa sababu kitu hicho hakipo, in actuality. Hivyo, tuzungumzie vyama hapa, ni kweli tusubiri ilani na ahadi za CDM kwa mgombea wake wa Urais. Lakini hili halizuii kutaka kujua misimamo ya msingi (core values) za mgombea. Mgombea wa Urais hawezi kuja na kusubiri ilani tu ndio tujue anataka kufanya nini; ni vizuri tujue yeye mwenyewe anataka kufanya nini ili tuone mambo hayo yakiwemo ndani ya Ilani. Vinginevyo, Ilani itakuwa na mambo x na kumbe yeye anataka kufanya mambo y. Akifanya mambo y ambayo hakutuambia atafanya tutamuulizaje? Au hata kumshabikia tutamshabikiaje.

Binafsi ninakaribia kwenye fensi fulani hivi ambayo labda naweza kujikuta pragmatically naunga mkono harakati hizi. Lakini nikijua matokeo yake yanatabirika. Kwamba, naweza kusema "tuitoe tu CCM, regardless what happens next" ukichukulia mfano wa Kenya chini ya NARC ambao mmoja ametukumbushia hapo. Kwamba, labda tusifikirie mabadiliko mazuri miaka mitano ijayo labda mabadiliko ya kweli kabisa yatakuja 2020 baada ya kuitoa CCM kwanza.
 
Mkuu JokaKuu,
Hoja yako ni nini hapa?

Hii mifano ya wana CCM unayoitoa niya watu ambao walikataliwa na vikao vya CCM kuteuliwa kuwa wagombea Urais wa Tanzania, inawezekana moja ya kikwazo ni kuwa vigeugeu katika misimamo muhimu ya kitaifa.

Kwa sasa tunaongelea Rais wa Tanzania ambaye madaraka yake ndani ya Katiba yalishawahi kusemwa na Mwl. Nyerere yanaweza kumfanya kuwa dikteta kama ana hulka za kidikteta.

Katiba ya Tanzania (1977) kwa jinsi ilivyo mbovu, inahitaji Rais anayeaminika na ambaye siyo mtovu wa uadilifu.

Kwa maelezo ya Mzee Butiku, Lowassa ni mtetezi mkuu wa Serikali mbili kwa sababu ya madaraka na nguvu zitokanazo na Rais wa Tanzania katika serikali mbili. Ieleweke kuwa, Lowassa hakuingia CHADEMA kwa sababu amevutiwa na Sera za CHADEMA bali ameingia CHADEMA kwa sababu jina lake limekatwa na wazee wa CCM na kwa sababu hiyo, ndiyo maana alipoingia CHADEMA hakutaka kuwa wanachama wa kawaida bali alitaka kuwa mgombea Urais.

Mabere Marando ametueleza, CHADEMA walianza maongezi na Lowassa ya kuhusu kuhamia CHADEMA kabla hata ya vikao vya CCM vya kuteuwa wagombea Urais havijaanza.


Kitu kingine ninachokiona kwa sasa, Hata kama Lowassa atashinda Urais, kitu ambacho mpaka sasa sina uhakika, naamini hawezi kuachia nguvu na madaraka yatokanayo na serikali mbili ili awe Rais wa Tanzania katika serikali tatu. Ninaamini Rasimu ya Warioba ambayo imetoa masharti ya kipindi cha mpito kwa miaka minne ataiweka kabatini mpaka baada ya uchaguzi wa pili ili kuhakikisha anamaliza kipindi chake cha pili kwa mujibu wa Katiba akiwa Rais katika serikali mbili, kwa maana hii, Serikali tatu tutaziona mwaka 2025.
 


..OK.

..lakini hilo pia litakuwa ni swali zuri sana la kumhoji wakati wa kampeni. serikali 2 au 3?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…