CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Zakumi, ndio maana nasema wengi wenu hamuijui CCM and what it is capable of. Je umesahau Bunge Maalum La Katiba? Kususa kwa wapinzani kulisaidia nini, si waliendelea tu kama vile hakuna upinzani! Take note: ni hivyo vyama vidogo ndivyo viliwapa CCM uhalali. Mbona nyumba zao hazikuchomwa?

Kwa upande wangu nasema uwezo mkubwa walionao CCM ni kuwa wapo kwenye serikali na kuakikisha kuwa ruzuku na posho zinakuwa ni sehemu ya distractions za upinzani.

Kwa heshima ya kufanya jambo la kihistoria kwa nchi yangu, ningeweza kuwa mbunge wa bunge la katiba bila malipo yoyote. Najua ungeweza kufanya hivyo pia. Na wachangiaji wengi wa ukumbi huu wangeweza kufanya hivyo pia.

Lakini kwa sababu bunge la katiba lilikuwa sehemu ya watu kutengeneza pesa, nchi imepata kile CCM ilichotaka.
 
Mkuu Zakumi,
Kuichoka tu CCM bila kuwa na silaha zinazokidhi mapambano kihoja ni kupoteza muda!

Ni sawa na watu wanaosema kila siku wanamchukia kiumbe anayeitwa shetani anayerubuni watu duniani wakati hawafanyi hata jitihada za kupambana ili kumshinda huyu shetani na hata wakifanya jitihada, silaha wanazotumia ni hafifu ambazo hazikidhi mazingira ya ushindi!

Moja ya kitu nilichopima nilipokuwa Tanzania ni mawazo ya wananchi. Kwenye TVs na vyombo vya habari, watu walikuwa wanalalamika kuhusu rushwa. Rushwa imezidi. Rushwa imefanya vile. Lakini sikusikia watu wakijaribu kuunganisha utawala wa kisiasa na rushwa.

Swali langu likawa je akitokea kiongozi wa CCM ambaye ataonyesha nia ya kupambana na rushwa, nini itakuwa hatima ya vyama vya upinzani? Kwa maoni yangu akitokea kiongozi kama huyo, CDM inaweza kurudi kuwa chama cha wabunge watatu na CUF ikabakia Pemba tu.

Na kama CDM atashinda na kumpata mtu ambaye anaweza kusimamia masuala ya rushwa, inawezekana hiyo ikawa safari ya kifo cha CCM.

Hivyo kwa maoni yangu binafsi hivi vyama vya kisiasa ni personalities. Na katika kila ngazi sio vyama ndivyo vinavyopambana bali personalities. Hivyo hakuna mapambano ya kihoja. Labda katika miji mikubwa.
 
Mkuu,
Kwa sentensi hii, nadhani kwa sasa tunaongea lugha moja!

Mkuu umefanya vyema kutuweka wote ukurasa moja na kuondokana na ushabiki. Prof Lipumba kagusia suala ambalo si la kubeza .. la dhumuni kuu la Ukawa. Haikuwa kuing'oa CCM bali kuleta katiba mpya. Hii ni FACT.
Sasa baada ya kutoka BMK, umoja huu uliendelezwa na tuliambiwa lengo lake bado lilikuwa kupatikana kwa katiba mpya ya wananchi
Kwa "expedited process" waliotumia kum-nominate Lowassa na sababu walizotoa, na kukiri kuwa walianza mazungumzo na Lowassa zamani inatupa wasiwasi kuwa lengo halikuwa hili la katiba. Bora wangetuambia process hii waliitumia kumpata Jaji Warioba! Lakini siyo Lowassa ambaye ni 'open secret' alikuwa nyuma ya juhudi zote za ku-sabotage process ya kupita kwa rasimu ya Warioba. Ushahidi upo ukiangalia waliokuwa mstari wa mbele kuipiga vita rasimu ya Warioba ni Chenge (mastermind), Serukamba, Ole Sendeka na wakapata msaada kutoka CCM in general. Lowassa alikuwa kinara wa kupinga rasimu ya Warioba akijua fika kuwa atagombea mwaka huu na alitaka kugombea chini ya mazingira yaleyale kwa ticket ya CCM.
Kuhama kwake haikutokana na kuwa "aliokoka" and he suddenly saw the Light. . Hapana! Motive yake ni ileile - Power!
 
Moja ya kitu nilichopima nilipokuwa Tanzania ni mawazo ya wananchi. Kwenye TVs na vyombo vya habari, watu walikuwa wanalalamika kuhusu rushwa. Rushwa imezidi. Rushwa imefanya vile. Lakini sikusikia watu wakijaribu kuunganisha utawala wa kisiasa na rushwa.

Swali langu likawa je akitokea kiongozi wa CCM ambaye ataonyesha nia ya kupambana na rushwa, nini itakuwa hatima ya vyama vya upinzani? Kwa maoni yangu akitokea kiongozi kama huyo, CDM inaweza kurudi kuwa chama cha wabunge watatu na CUF ikabakia Pemba tu.

Na kama CDM atashinda na kumpata mtu ambaye anaweza kusimamia masuala ya rushwa, inawezekana hiyo ikawa safari ya kifo cha CCM.

Hivyo kwa maoni yangu binafsi hivi vyama vya kisiasa ni personalities. Na katika kila ngazi sio vyama ndivyo vinavyopambana bali personalities. Hivyo hakuna mapambano ya kihoja. Labda katika miji mikubwa.

Mkuu umenena .. watanzania wamechoka na rushwa na disregard to the rule of law.
Mfano ikitokea hili likawa addressed na CCM, tutashangaa kuona jinsi watu watakavyoridhika na hata kuwa tayari kuishi na chama kimoja kwa miaka 20
Kudhani kuwa suala ni mfumo na kuweka epitome of what people really are tired of (rushwa na ufisadi) ni poor judgement! Na waliomtumia Lowassa kama symbol of corruption ni Chadema. Hawana uwezo ndani ya miezi 3 kumsafisha na kutushawishi. Hiyo ni
1. Underestimating voters' judgement
2. Overestimating their ability and influence on general population
Kabla ya kufanya maamuzi sidhani kama walifanya SWOT analysis makini.
 
Mkuu umefanya vyema kutuweka wote ukurasa moja na kuondokana na ushabiki. Prof Lipumba kagusia suala ambalo si la kubeza .. la dhumuni kuu la Ukawa. Haikuwa kuing'oa CCM bali kuleta katiba mpya. Hii ni FACT.
Sasa baada ya kutoka BMK, umoja huu uliendelezwa na tuliambiwa lengo lake bado lilikuwa kupatikana kwa katiba mpya ya wananchi
Kwa "expedited process" waliotumia kum-nominate Lowassa na sababu walizotoa, na kukiri kuwa walianza mazungumzo na Lowassa zamani inatupa wasiwasi kuwa lengo halikuwa hili la katiba. Bora wangetuambia process hii waliitumia kumpata Jaji Warioba! Lakini siyo Lowassa ambaye ni 'open secret' alikuwa nyuma ya juhudi zote za ku-sabotage process ya kupita kwa rasimu ya Warioba. Ushahidi upo ukiangalia waliokuwa mstari wa mbele kuipiga vita rasimu ya Warioba ni Chenge (mastermind), Serukamba, Ole Sendeka na wakapata msaada kutoka CCM in general. Lowassa alikuwa kinara wa kupinga rasimu ya Warioba akijua fika kuwa atagombea mwaka huu na alitaka kugombea chini ya mazingira yaleyale kwa ticket ya CCM.
Kuhama kwake haikutokana na kuwa "aliokoka" and he suddenly saw the Light. . Hapana! Motive yake ni ileile - Power!



Sina kumbukumbu kama Lowassa aliwahi ongea chochote kuhusu katiba mpya/au serikali 2 3.. Kama kuna mtu mwenye andishi lake tunaomba aliweke hapa ili tufahamu nini msimamo wake kuhusu swala zima la katiba mpya..
 
Mkuu umenena .. watanzania wamechoka na rushwa na disregard to the rule of law.
Mfano ikitokea hili likawa addressed na CCM, tutashangaa kuona jinsi watu watakavyoridhika na hata kuwa tayari kuishi na chama kimoja kwa miaka 20
Kudhani kuwa suala ni mfumo na kuweka epitome of what people really are tired of (rushwa na ufisadi) ni poor judgement! Na waliomtumia Lowassa kama symbol of corruption ni Chadema. Hawana uwezo ndani ya miezi 3 kumsafisha na kutushawishi. Hiyo ni
1. Underestimating voters' judgement
2. Overestimating their ability and influence on general population
Kabla ya kufanya maamuzi sidhani kama walifanya SWOT analysis makini.


Simtetei Lowassa kuhsu swala la rushwa ila nina swali.. Zaidi ya Richmond je kuna tuhuma nyingine kumhusu huyu mh. hata katika swala zima la rushwa?

Maana nimekuwa nikisika kuwa Lowassa ni mla rushwa lakini hatuambiwi ni vipi,lini, na wapi..

Tusije anza meza bila kuhoji propoganda za CCM juu ya rushwa na Lowassa.
 
Simtetei Lowassa kuhsu swala la rushwa ila nina swali.. Zaidi ya Richmond je kuna tuhuma nyingine kumhusu huyu mh. hata katika swala zima la rushwa?

Maana nimekuwa nikisika kuwa Lowassa ni mla rushwa lakini hatuambiwi ni vipi,lini, na wapi..

Tusije anza meza bila kuhoji propoganda za CCM juu ya rushwa na Lowassa.

Hapana si kumtetea kuuliza na ni swali zuri sana .. labda nikupe mwanga kidogo ndani ya muda. Lakini kwa kifupi ana ardhi nyingi sana alizojilimbikizia akiwa Waziri wa ardhi na mifugo na pia amehusika ktk dili nyingi za 10% ktk manunuzi mbalimbali.
File lake na familia yake ni kubwa na lipo humu ni kulitafuta .. nitakutupia link nikilipata.
Ila najua fika kuwa faili lipo CCM na litaanza kutumika muda si mrefu
 
Hapana si kumtetea kuuliza na ni swali zuri sana .. labda nikupe mwanga kidogo ndani ya muda. Lakini kwa kifupi ana ardhi nyingi sana alizojilimbikizia akiwa Waziri wa ardhi na mifugo na pia amehusika ktk dili nyingi za 10% ktk manunuzi mbalimbali.
File lake na familia yake ni kubwa na lipo humu ni kulitafuta .. nitakutupia link nikilipata.
Ila najua fika kuwa faili lipo CCM na litaanza kutumika muda si mrefu

Dili alizopiga huyu mheshimiwa ni kubwa mno ukilinganisha na zile walizopiga wana CCM wengine waliobaki ndani kama Mzee wa Vijisenti a.k.a NYOKA WA MAKENGEZA na wengineo?
 
..lakini ukawa si unajulikana kwamba ni umoja wa katiba mpya, katiba ya Mzee Warioba?

..mpaka pale mgombea wa ukawa atakapokuja na msimamo mwingine basi there is a basis for us kuamini kwamba atasimamia matakwa ya katiba ya vyama vinavyounda ukawa.

..kama ambavyo kuna uwezekano wa ukawa kusambaratika huko mbele ya safari, uko uwezekano pia wa umoja huo kudumu na kutoa mchango mkubwa kwa mageuzi ambayo tumekuwa tukiyalilia kwa muda mrefu.

..binafsi nimeona niwape nafasi hawa ukawa tuone watafanya nini. naamini hata wakiboronga itakuwa rahisi kuwatimua.

..nina HOFU kubwa sana na hatma ya wapenda mageuzi nchi hii, ikiwa CCM ya Nape Nnauye, Paul Makonda, Ridhiwani Kikwete, January Makamba,.. itachukua madaraka.

cc Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mag3, Alinda

Yaani hivi sasa tunajaribu kutathmini RISK ipi ni bora kuichukua...
i)Kuiamini UKAWA kuchukua nchi pamoja na kutokuwa na hakika ya jinsi watakavyoendesha mambo mbele ya safari
AU
ii)Kuwapa fursa nyingine CCM kuendelea kutawala pamoja na madudu yote yaliyotokea na kuwaamini kuwa sasa wamekuwa wasafi baada ya Lowassa kuondoka.
 
Sina kumbukumbu kama Lowassa aliwahi ongea chochote kuhusu katiba mpya/au serikali 2 3.. Kama kuna mtu mwenye andishi lake tunaomba aliweke hapa ili tufahamu nini msimamo wake kuhusu swala zima la katiba mpya..
Kama kuna mtu moja ndani ya CCM alikuwa non-commital kwenye swala la Katiba pendekezwa ni Edward Lowassa lakini kwa watu ambao wako tayari kumvika taji la mfalme wa mafisadi Tanzania dai kama hilo lilitegemewa. Edward Lowassa alianza hata kuzikosoa sera za CCM kabla ya hapo lakini kama walivyosema wahenga, give a dog a bad name then hang him. Je Lowassa ndio mbuzi wa kafara katika kukitakasa chama cha mafisadi, CCM?

Lowassa hajawahi kuwa top leader nchi hii, kila wakati amekuwepo mtu mkubwa zaidi juu yake aliyeapa kwa msahafu kuilinda na kuitetea katiba ya nchi hii. Toka mwaka 2008 alipojiuzulu Uwaziri Mkuu na kukaa nje ya serikali, ufisadi umezidi kusitawi na kufikia kiwango cha kutisha. Ni baada ya kuwa nje ya serikali ndio kwa mara ya kwanza tukashuhudia serikali dhaifu ikikiri hadharani kuwa wapo wahalifu wenye nguvu wasiokamatika.

Wako watu kama Chenge wameita dola milioni moja kwenye account zao nje ya nchi vijisenti, wameshtakiwa kwa kuua na wamekuwa ndio washauri wakuu wa mikataba ya kifisadi awamu hadi awamu lakini wanaendelea kuaminika na kupewa heshima ya kutuandikia katiba mpya. Hivi sasa anagombea ubunge na kashinda kwa kura nyingi katika kura kura ya maoni lakini Edward Lowassa hapewi hata benefit of doubt anapokanusha tuhuma.

Tunaye Kiongozi Mkuu wa nchi, kahusishwa na kila kashfa tuliloingia tangu akiwa ni Waziri wa Nishati hadi alipochaguliwa kuiongoza nchi mwaka 2005 kwa njia ya wizi lakini bado anapewa benefit of doubt. Amewahi kuvunja katiba ya nchi aliyoapa kulinda na kuitetea alipoamua kuwasamehe wezi na kuwaomba warudishe walochoiba lakini bado anapewa benefit of doubt licha ya kwamba kwa wenzetu wastaarabu, the buck stops with the President.

Hivi sasa tunaye mgombea mteule wa Uraisi ambaye ripoti zipo zikimhusisha na kashfa ya upotevu wa mabilioni ya pesa iliyotokana na kodi za wanachi lakini anapewa benefit of doubt. Amehusishwa na kashfa ya uuzwaji wa nyumba za serikali kiasi kwamba Mawaziri wanakosa makazi huku nyumba ambazo wangekaa zimegawiwa kiholela kwa washikaji wasiohusika, lakini maadam yuko CCM, anapewa benefit of doubt na kutakaswa kuwa ni msafi.

Edward Lowassa mwenyewe, kwa kuhamia upinzani, ni kama amewafia mafisadi wote wa nchi hii na kuchukua dhambi zao na sasa ni wasafi waking'ara kama theluji. Maadam ameamua kujitetea akiwa nje ya CCM, yeye pamoja dhambi zote ndani ya serikali ya CCM, anatakiwa afungwe ndani ya sanduku na kutupwa baharini. Baada ya hapo ufisadi utabaki ni historia katika taifa hili, na Watanzania tutaishi raha mstarehe milele na milele!

Kwamba binadamu yeyote anaweza kutakasika isipokuwa moja anayeitwa Edward Lowassa? Kwamba dhambi zote zinasameheka isipokuwa za Edward Lowassa? Kwamba ufisadi wote sasa umehamia Chadema na kuiacha CCM ikiwa safi? Kwamba...are you kidding me? Kwa nini hatuko tayari kumpa benefit of doubt huyu mtu moja kama tumeweza kuwapa maelfu kwa maelfu mafisadi walio ndani ya CCM? Hii chuki inasababishwa na nini?
 
Yaani hivi sasa tunajaribu kutathmini RISK ipi ni bora kuichukua...
i)Kuiamini UKAWA kuchukua nchi pamoja na kutokuwa na hakika ya jinsi watakavyoendesha mambo mbele ya safari
AU
ii)Kuwapa fursa nyingine CCM kuendelea kutawala pamoja na madudu yote yaliyotokea na kuwaamini kuwa sasa wamekuwa wasafi baada ya Lowassa kuondoka.

..hivyo ndivyo demokrasia ilivyo.

..kwa chama tawala unakuwa unajua rekodi na mwenendo wake. Hivyo ukiamua kukichagua u r basically voting for more of the same.

..kwa upande wa upinzani inategemewa watabadili mwelekeo kulinganisha na nini chama tawala wamekuwa wakifanya. Unachagua ukitegemea watatekeleza kwa kiasi kikubwa mambo ambayo wamekuwa wakiyapigia kelele.

..kwa hiyo uchaguzi wowote ule ni RISK au KAMARI. Wakati mwingine wagombea hutoa ahadi halafu wakashindwa kuzitekeleza. Unakumbuka "maisha bora kwa kila Mtanzania"??
 
i)Kuiamini UKAWA kuchukua nchi pamoja na kutokuwa na hakika ya jinsi watakavyoendesha mambo mbele ya safari
Kwanza je tuna hakika ya jinsi CCM watakavyoendesha mambo mbele ya safari? Pili, hatuna sababu ya kutoiamini UKAWA kwani tulipofika tunahitaji mabadiliko na hayo mabadiliko yataletwa tu na timu mpya...ni uenda wazimu kuwategemea waliotufikisha hapo ndio watutoe!
ii)Kuwapa fursa nyingine CCM kuendelea kutawala pamoja na madudu yote yaliyotokea na kuwaamini kuwa sasa wamekuwa wasafi baada ya Lowassa kuondoka.
Tuna sababu chungu nzima ya kutowapa fursa nyingine CCM na kwa ufahamisho Lowassa alijiuzulu miaka saba iliyopita! CCM wamepewa fursa chungu nzima toka tupate uhuru and what have they got to show for it? It is corruption, corruption and more corruption...no more please!
 
Kama kuna mtu moja ndani ya CCM alikuwa non-commital kwenye swala la Katiba pendekezwa ni Edward Lowassa lakini kwa watu ambao wako tayari kumvika taji la mfalme wa mafisadi Tanzania dai kama hilo lilitegemewa. Edward Lowassa alianza hata kuzikosoa sera za CCM kabla ya hapo lakini kama walivyosema wahenga, give a dog a bad name then hang him. Je Lowassa ndio mbuzi wa kafara katika kukitakasa chama cha mafisadi, CCM?

Lowassa hajawahi kuwa top leader nchi hii, kila wakati amekuwepo mtu mkubwa zaidi juu yake aliyeapa kwa msahafu kuilinda na kuitetea katiba ya nchi hii. Toka mwaka 2008 alipojiuzulu Uwaziri Mkuu na kukaa nje ya serikali, ufisadi umezidi kusitawi na kufikia kiwango cha kutisha. Ni baada ya kuwa nje ya serikali ndio kwa mara ya kwanza tukashuhudia serikali dhaifu ikikiri hadharani kuwa wapo wahalifu wenye nguvu wasiokamatika.

Wako watu kama Chenge wameita dola milioni moja kwenye account zao nje ya nchi vijisenti, wameshtakiwa kwa kuua na wamekuwa ndio washauri wakuu wa mikataba ya kifisadi awamu hadi awamu lakini wanaendelea kuaminika na kupewa heshima ya kutuandikia katiba mpya. Hivi sasa anagombea ubunge na kashinda kwa kura nyingi katika kura kura ya maoni lakini Edward Lowassa hapewi hata benefit of doubt anapokanusha tuhuma.

Tunaye Kiongozi Mkuu wa nchi, kahusishwa na kila kashfa tuliloingia tangu akiwa ni Waziri wa Nishati hadi alipochaguliwa kuiongoza nchi mwaka 2005 kwa njia ya wizi lakini bado anapewa benefit of doubt. Amewahi kuvunja katiba ya nchi aliyoapa kulinda na kuitetea alipoamua kuwasamehe wezi na kuwaomba warudishe walochoiba lakini bado anapewa benefit of doubt licha ya kwamba kwa wenzetu wastaarabu, the buck stops with the President.

Hivi sasa tunaye mgombea mteule wa Uraisi ambaye ripoti zipo zikimhusisha na kashfa ya upotevu wa mabilioni ya pesa iliyotokana na kodi za wanachi lakini anapewa benefit of doubt. Amehusishwa na kashfa ya uuzwaji wa nyumba za serikali kiasi kwamba Mawaziri wanakosa makazi huku nyumba ambazo wangekaa zimegawiwa kiholela kwa washikaji wasiohusika, lakini maadam yuko CCM, anapewa benefit of doubt na kutakaswa kuwa ni msafi.

Edward Lowassa mwenyewe, kwa kuhamia upinzani, ni kama amewafia mafisadi wote wa nchi hii na kuchukua dhambi zao na sasa ni wasafi waking'ara kama theluji. Maadam ameamua kujitetea akiwa nje ya CCM, yeye pamoja dhambi zote ndani ya serikali ya CCM, anatakiwa afungwe ndani ya sanduku na kutupwa baharini. Baada ya hapo ufisadi utabaki ni historia katika taifa hili, na Watanzania tutaishi raha mstarehe milele na milele!

Kwamba binadamu yeyote anaweza kutakasika isipokuwa moja anayeitwa Edward Lowassa? Kwamba dhambi zote zinasameheka isipokuwa za Edward Lowassa? Kwamba ufisadi wote sasa umehamia Chadema na kuiacha CCM ikiwa safi? Kwamba...are you kidding me? Kwa nini hatuko tayari kumpa benefit of doubt huyu mtu moja kama tumeweza kuwapa maelfu kwa maelfu mafisadi walio ndani ya CCM? Hii chuki inasababishwa na nini?
You have never failed to disappoint me.
First paragraph yako nilidhani imebeba maelezo yote hayo kwa ufupi. Like, non-commitance kuibeba thesis statement.
Lowassa ni muumini wa serikali mbili, unalijua hilo. Hizo aya zinazofuata ni maelezo mengi yasiyoakisi majibu ya swali lililoulizwa. Yes kuna mafisadi CCM,sasa hiyo inahusikaje na swali lililoulizwa??

Unatumia a lot of energy na upo on a defensive mode .... Hiyo inanipa faraja kubwa.
 
You have never failed to disappoint me.
First paragraph yako nilidhani imebeba maelezo yote hayo kwa ufupi. Like, non-commitance kuibeba thesis statement.
Lowassa ni muumini wa serikali mbili, unalijua hilo. Hizo aya zinazofuata ni maelezo mengi yasiyoakisi majibu ya swali lililoulizwa. Yes kuna mafisadi CCM,sasa hiyo inahusikaje na swali lililoulizwa??

Unatumia a lot of energy na upo on a defensive mode .... Hiyo inanipa faraja kubwa.


Karibu sana Mkuu Kobello...of course you had to step in (I was beginning to wonder what happened to you) I do hope you are recuperating well from the shock treatment! Defensive mode? That could be the understatement of the year! Am actually having and displaying heightened senses caused by genes that have until now remained dormant thanks to the great peril and situation we are facing as a country.

It calls for the utmost concentration and ability to dominate opponents or in simple terms, I am in attack mode and you should be wary. 50+ years is a long time by any standard...actually it is a lifetime. The only obstacle standing in our way in our quest for change is a door and if we cant open it with the key we have we have but one alternative, use any tool to available to break it and you can take that to the bank! Ballyhoo!
 
Kobello,

..lowassa ni muumini wa serikali 2 lakini sasa ni mwanachama wa cdm ambayo sera yake ni serikali 3.

..kuna uwezekano lowassa akabadilika, au akaibadilisha cdm.

..lakini suala la uumini wa serikali 2 vs 3 lipo zaidi kwa wana-ccm. Labda tunaweza kujufunza kwa mifano iliyoko ccm.

..balozi amina salum aliongoza tume iliyotoa mapendekezo ya muungano wa serikali 3. Dr
Asha migiro alikuwa mjumbe wa tume ya jaji kisanga iliyopendekeza serikali 3. Dr.mwakyembe aliandika thesis ya phD kutetea serikali 3. Lakini wote hao leo ni waumini wa serikali 2.

..maswali ya msingi ni haya: does lowassa care enough about serikali 2 kiasi cha kupelekea kujaribu kuibadilisha cdm? Je, ana uwezo wa kihoja ktk kutekeleza azma hiyo? Je, ana watu wa kutosha ndani ya cdm watakaomuunga mkono kubadilisha msimamo kwenda serikali 3? Nini future ya ukawa ikiwa cdm itabadilika na kuunga mkono serikali 2?

Cc Mag3, Nguruvi3, Mwalimu
 
Last edited by a moderator:
Kobello,

..lowassa ni muumini wa serikali 2 lakini sasa ni mwanachama wa cdm ambayo sera yake ni serikali 3.

..kuna uwezekano lowassa akabadilika, au akaibadilisha cdm.

..lakini suala la uumini wa serikali 2 vs 3 lipo zaidi kwa wana-ccm. Labda tunaweza kujufunza kwa mifano iliyoko ccm.

..balozi amina salum aliongoza tume iliyotoa mapendekezo ya muungano wa serikali 3. Dr
Asha migiro alikuwa mjumbe wa tume ya jaji kisanga iliyopendekeza serikali 3. Dr.mwakyembe aliandika thesis ya phD kutetea serikali 3. Lakini wote hao leo ni waumini wa serikali 2.

..maswali ya msingi ni haya: does lowassa care enough about serikali 2 kiasi cha kupelekea kujaribu kuibadilisha cdm? Je, ana uwezo wa kihoja ktk kutekeleza azma hiyo? Je, ana watu wa kutosha ndani ya cdm watakaomuunga mkono kubadilisha msimamo kwenda serikali 3? Nini future ya ukawa ikiwa cdm itabadilika na kuunga mkono serikali 2?

Cc Mag3, Nguruvi3, Mwalimu
Suala kubwa mkuu ni principles ambazo CDM inasimamia kama zina-reflex matakwa ya watanzania kwa ujumla.
Sera ya majimbo imepigwa chini na watanzania kwa ujumla, hiyo ni Sera ya uongozi inayopendekezwa na CDM.Hata UKAWA haisimamii Sera ya majimbo kwa sababu haipo kwenye katiba mpya. Je, CDM wapo tayari kukibali failure hiyo?
Pili, serikali tatu ni Sera ya UKAWA kwa ujumla, lakini serikali tatu zipi? Confederate kama wanavyotaka CUF ambapo Zanzibar itakuwa ma kiti cjake UN au Federal kama ilivyopendekezwa na tume?
Wagombea wa UKAWA hawaakisi msimamo wa CDM na hatujui kama wamebadilisha msimamo mpaka watakaposema. Kwa hoyo mpaka sasa tunachojua ni kuwa hawaamini mifumo ilivyopendekezwa na tume ya katiba.
Sasa, in principle kuna mahusiano gani kati ya wagombea hao na UKAWA?
 
Last edited by a moderator:
Kobello,

..lowassa ni muumini wa serikali 2 lakini sasa ni mwanachama wa cdm ambayo sera yake ni serikali 3.

..kuna uwezekano lowassa akabadilika, au akaibadilisha cdm.

..lakini suala la uumini wa serikali 2 vs 3 lipo zaidi kwa wana-ccm. Labda tunaweza kujufunza kwa mifano iliyoko ccm.

..balozi amina salum aliongoza tume iliyotoa mapendekezo ya muungano wa serikali 3. Dr
Asha migiro alikuwa mjumbe wa tume ya jaji kisanga iliyopendekeza serikali 3. Dr.mwakyembe aliandika thesis ya phD kutetea serikali 3. Lakini wote hao leo ni waumini wa serikali 2.

..maswali ya msingi ni haya: does lowassa care enough about serikali 2 kiasi cha kupelekea kujaribu kuibadilisha cdm? Je, ana uwezo wa kihoja ktk kutekeleza azma hiyo? Je, ana watu wa kutosha ndani ya cdm watakaomuunga mkono kubadilisha msimamo kwenda serikali 3? Nini future ya ukawa ikiwa cdm itabadilika na kuunga mkono serikali 2?

Cc Mag3, Nguruvi3, Mwalimu
Hapo ndipo nawashangaa wasiomtaka Lowassa, hawampi nafasi yoyote kwamba anaweza akarekebisha/akabadili msimamo wake kulingana na muda, wakati na mahala. Kwao Lowassa ni dude lililo tofauti kabisa na wanadamu wengine na kwamba yanayowezekana kwa wengine hayawezekani kwa Lowassa! In short they are not ready to judge him the same way they would do unto other humans including themselves!

Lowassa kasema mambo matatu, nayo ni;

  1. CCM si baba wala mama.
  2. CCM si ile aliyojiunga nayo na kumlea kwani imepoteza lengo, dira na mwelekeo.
  3. CCM haina tena uwezo, dhamira wala uhalali wa kutufikisha kwenye matumaini.
Haya ni maneno mazito na yanaonesha jinsi alivyokuwa disillusioned ndani ya chama hiki. Akaomba kuijunga na Chadema na wao wakakubali kumpokea. Sasa wanatokea watu wanadai mara kainunua Chadema, mara kahonga bilioni 10 kwa Mh. Mbowe, mara kawakatia kitu kidogo akina Tundu Lissu na upuuzi kama huo while there is absolutely no evidence...halafu wapo watu humu eti wanaamini!

Nachoka na Watanzania...
 
Karibu sana Mkuu Kobello...of course you had to step in (I was beginning to wonder what happened to you) I do hope you are recuperating well from the shock treatment! Defensive mode? That could be the understatement of the year! Am actually having and displaying heightened senses caused by genes that have until now remained dormant thanks to the great peril and situation we are facing as a country.

It calls for the utmost concentration and ability to dominate opponents or in simple terms, I am in attack mode and you should be wary. 50+ years is a long time by any standard...actually it is a lifetime. The only obstacle standing in our way in our quest for change is a door and if we cant open it with the key we have we have but one alternative, use any tool to available to break it and you can take that to the bank! Ballyhoo!
If you were talking about policies, character and giving us statistical analysis, then may be I'd give you that so-called "genetically motivated excitement".
But, my brother, I know for a fact that you don't believe in what you are saying.Somehow you horizontally inherited the " dirty genes" from your "acquired" leader and they are as dominant as a female hyena on heat.
Please stop lying to yourself.
 
Hili la serikali 2 ni la kuangalia kwa mtazamo mpana

Upo ushahidi , wabunge wa CCM katika bunge maalum waligawanyika. Waliitwa na kupewa msimamo, jambo lilozaa Ukawa

Rais Kikwete,aliwaambia CCM wajiandae na mabadiliko ya serikali 2 kwenda 3. Hii ilikuwa ni baada ya rasimu ya kwanza

Jaji Warioba ni muumini wa serikali 2. Hata hivyo, alisema ameshawishika kuunga mkono serikali 3 kutokana na mabadiliko ya hali ya kisiasa nchini na duniani na kwamba jambo hilo haliepukiki

Ni mbadiliko ya dunia anayosema Warioba ndiyo yaliyomlazimuNyerere kukubali uwepo wa mfumo wa vyama vingi, jambo alilolikataa miaka 30 kabla ya kutokea kwake

Asha Rose alikuwa mjumbe wa tume ya Kisanga iliyopendekeza serikali 3.
Kwa maneno mengine anaamini katika serikali 3. Ni Asha huyo ndiye aliyegawa nakala za katiba yao pendekezwa iliyokufa akiwa anaamini 3 nakutekeleza serikali 2

Da'Amina naye ni kama Asha. Mkuu JokaKuu kaeleza hapo juu

Hivyo, kumsema Lowassa na kufumbia macho wengine ni double standard and unfair

That said and done, haiondoi ukweli kua anapotaka kubeba dhamana kubwa ni vema akaeleweka.

Ni katika kuondoa mashaka kama alivyouliza Alinda hapo juu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom