CHADEMA yaanza kutumia mbinu za kisasa kudai Tume Huru ya Uchaguzi. Kalamu na Mask zenye maneno "TUME HURU" zaanza kusambazwa mitaani


Narudia tena, hujui kuandika kwa usahihi, hata kwenye uzi huu mbali ya kuandika upuuzi, bado una tatizo la kuandika kwa usahihi. Hakuna neno badara, bali neno sahihi ni badala. Hakuna kitu kiitwacho mawakiri, bali neno sahihi ni mawakili. Hivi unaona shida gani kurudi shule wakati elimu ni bure?
 
tatizo kubwa lipo zaidi ndani ya chama chetu (CCM) ambacho kwa sasa kinahemea ndani ya mbeleko ya mapolisi.

mbeleko ikichanika tu, CCM yetu kwishnei kama ilivyokuwa kwa KANU (Kenya) na/au UNIP (Zambia)!!
 
Sasa kama unakubali kuna watanzania wako vijijini huko hawajui maana ya tume huru, huoni kama wakisoma hiyo kalamu ndio utakuwa mwanzo wao wa kitaka kujua hiyo tume huru ni kitu gani? na wakishapewa elimu ndio utakuwa mwanzo wa kuwaamsha na wao waanze kuitaka hiyo tume?

Haya mambo yanahitaji uwezo mpana kidogo wa kufikiria, siku zote ukiona watu wazima na akili zao wamefanya jambo jiulize mara mbili kwanini wamefanya hivi, usikimbilie kupinga tu, hiyo ni njia rahisi na itawafikia wengi kwa muda mfupi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ibara ya 74(7) imeweka wazi kuwa tume itakuwa chombo huru na kitafanya kazi bila kuingiliwa,na kwa mujibu wa sheria.
 

Huyu jamaa ni homeboy wa JIWE...!
Hawa jamaa Wana matatizo ya LUGHA iwe Kiswahili au English...ndo maana Magufuli mwaka huu anatimiza miaka 5 Ikulu lakini hajakanyaga Ulaya.. Tatizo lugha.

Wewe msikilize Jiwe akiongea Kiswahili chake ni very poor kimechanganyika na sijui Kisukuma au Kizirankende na huku anajiita Daktari msomi...!!Sijui Thesis yake aliandikiwa na Nani...Ni shiida!
 
Sawa, nmepata kalamu..imeandikwa... Tume huru TZ ...then what next???
 
Ibara ya 74(7) imeweka wazi kuwa tume itakuwa chombo huru na kitafanya kazi bila kuingiliwa,na kwa mujibu wa sheria.

Kwa Magufuli katiba kwake ni kama novel. Tume ingekuwa huru tusingeona ikiamrishwa kushiriki kunajisi box la kura. Tume hii sio huru fullstop.
 
Ibara ya 74(7) imeweka wazi kuwa tume itakuwa chombo huru na kitafanya kazi bila kuingiliwa,na kwa mujibu wa sheria.
Now niambie, itafanyaje kazi bila kuingiliwa wakati mwenyekiti wa hiyo tume anateuliwa na Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama tawala kinachoshindana na vyama pinzani kwenye chaguzi?

Unaona huyo mwenyekiti wa tume atakuwa fair?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuteuliwa ndio hofy
Kwani ukiteuliwa ndio unatakiwa upindishe sheria? Na hao mawakala wenu kuanzia kituo hadi taifa huwa wanapindisha sheria?
 
Muda sio mrefu mwokozi Wa ccm mambosasa ataingilia kati kuzipiga marufuku...

Huyu goalkeeper Mambosasa aendelee na huo ujinga wake wa kutumika na Maficcm ya Lumumba Kama Toilet paper......Kuna siku atamkumbuka Marehemu Al-Bashir wa Sudan..!!! Hii dunia inaendelea kuzunguka kwenye muhimili wake.... ikawa asubuhi ikawa jioni siku ya kwanza....then....mwisho unakuja..!!!
 
Kwahyo hapo shda ni katiba ya tanzania inayompa raisi mamlaka au ni raisi wa nchi ndo anashda??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu tufafanuliwe huo muundo wa tumefanya huru...fafanueni kuhusu composition yake ...na uteuzi wa tume hiyo inayoitwa huru...pia mfafanue kwanini tume ya Sasa mnaona siyo huru...haitoshi tu kusema tume huru ...fafanua zaidi ili watu waelewe....
Tumekwishafanya mengi na tumeweka mifano mingi mno kuhusu uozo wa Tume iliyopo na tunashukuru kwamba karibu kila mwananchi ameelewa , kuhusu muundo wa Tume huru rejea Katiba ya Warioba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…