SI KWELI CHADEMA yapiga marufuku ambao hawana elimu ya kidato cha sita na kuendelea kugombea serikali za mitaa na uchaguzi mkuu

SI KWELI CHADEMA yapiga marufuku ambao hawana elimu ya kidato cha sita na kuendelea kugombea serikali za mitaa na uchaguzi mkuu

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao

Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji.

Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi

barua chadema.jpg
 
Tunachokijua
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mchakato wa kidemokrasia ambapo wananchi hupiga kura kila baada ya miaka mitano kuwachagua viongozi wa ngazi za mitaa kama vile Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, na Wajumbe wa Serikali za Mitaa.

Kumekuwa na barua inayosambaa mitandaoni ikidaiwa kuwa ni ya CHADEMA ambayo ikionekana kuandikwa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na mambo ya nje CHADEMA, John Mrema, Barua hiyo inaeleza kuwa CHADEMA wametoa kanuni mpya ambayo inaeleza mtu anayeruhusiwa kugombea uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 ni yule mwenye Elimu ya kuanzia kidato cha Sita huku barua hiyo ikiwataka Wananchi kuzingatia kanuni hiyo.

Je, Ukweli wa barua hiyo ni upi?
JamiiCheck Imefatilia taarifa zilizotolewa kwenye barua hiyo na kubaini kuwa hazina Ukweli wowote, aidha barua hiyo haijawahi kutolewa na CHADEMA kupitia kurasa zao Rasmi za mitandao ya kijamii wala kwenye vyombo rasmi vya taarifa vya CHADEMA.

Vilevile, barua hiyo haijawahi kuchapishwa kwenye akaunti za John Mrema ingawa ndiye aliyedaiwa kusaini Barua hiyo, Aidha, John Mrema amechapisha taarifa ya kanusho kupitia kaunti yake ya mtandao wa X na kueleza kuwa taarifa hiyo ni ya uzushi na kuwataka watu kuipuuza.

Siku za hivi karibuni viongozi mbalimbali wa CHADEMA wamekuwa wakizungumzia kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa, ila hawajawahi kueleza kuhusu mabadiliko ya kanuni inayowataka watu wanaotaka kugombea wawe na Elimu kuanzia kidato cha Sita na kueendela, ila wamekuwa wakisisitiza watu kwenda kujiandikisha kwa ajili ya zoezi la kupiga kura na kujiandaa kwa uchaguzi ikiwemo kujiandaa kuchagua viongozi na kuchaguliwa kuwa kiongozi na si kueleza mabadiliko ya kanuni kama barua ile ilivyoeleza.
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao

Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji.

Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi
View attachment 3120101
Ndugu zangu Chadema hapa mmejiandalia sanda wenyewe. Hivi hamkufikiria kwamba mtapoteza wanachama wengi kwa kigezo hiki??
 
Tuanzie huku chini, wapewe vijana wenye elimu tupande tuone labda kutabadilika. Naunga mkono hoja ya Chadema.
Hoja haina mashiko kistratejia. Mnaenda kupoteza mapema sana...
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kwani hakuna wazee waliomaliza form six au wenye degree? Tatizo ukisikia form six unadhani ni Hawa wa sasa
Kama hii taarifa ni ya kweli nadhani ni uamuzi mbaya. Siyo kwamba sijui umuhimu wa elimu au elimu haina umuhimu kwenye uongozi wa sasa, ila uamuzi umekuwa wa ghafla mno na umetoka juu. I mean jambo kama hili inatakiwa ifanywe research kwanza, wapiga kura na wananchi kwa ujumla waulizwe maoni yao baada ya hapo ndiyo uamuzi ufanyike. Vinginevyo, kama huu uamuzi ni matokeo ya utafiti uliofanywa basi hakuna shida. NB: wanasiasa wetu wamezoea sana amri za kutoka juu kwenda chini na nyingi hufanyika bila wananchi kushirikishwa.
 
Shida watawapata kweli? Maana huku mtaani changamoto kwakweli vijana wengi wa Elimu hiyo hawajitoi sana kwenye mambo ya kijamii kwanini hata wasingeweka kidato Cha nne Kwa serikali za mitaa maana CCM bado tunaruhusu darasa la pili
 
Kuliko kuchukua mtu wa darasa la sababu kuwa mwenyekiti WA Kijiji au mtaa Karne ya 21, Bora wasiwe na viongozi uongozi.
Naunga hoja mkono 100%
Je walimu walio ishia form four na kwenda chuo cha ualimu nao hwana sifa. Nafikiri kunahitajika maelezo zaidi.
 
Hoja haina mashiko kistratejia. Mnaenda kupoteza mapema sana...
Tunaenda kupoteza nini? Wakati unajibu ukumbuke Mm ni mpiga kura si mwanasiasa na sio chawa hivyo sifungwi na upande wowote.
 
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao

Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji.

Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi
View attachment 3120101
Fake hawa watu wanao tengeneza barua za chama fake inabidi wakamatwe.
 
Kwa maeneo ya mjini ni sawa ila huko vijijini Kazulamimba au Mahande wanaokubalika utakuta hata kuandika jina shida
Wewe unaiamini hiyo barua? Kwa akili ya kawaida tu, CHADEMA wanaweza kufanya hivyo?
FAKE! FAKE! FAKE! FAKE!
Na nina imani hiyo barua kaiandika Makala! Maanake akili zake huyooo……..

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Kuliko kuchukua mtu wa darasa la sababu kuwa mwenyekiti WA Kijiji au mtaa Karne ya 21, Bora wasiwe na viongozi uongozi.
Naunga hoja mkono 100%
Mimi CCM naungana na wewe

Serikalini sasa hivi hawaajiri darasa la saba hata kuendesha mkokoteni

Hayo mambo yaende hadi kwa wagombea ubunge,udiwani na serikali za mitaa viwango vipande jamani

Hivi karne hii kweli mtu anataka darasa la saba awe kiongozi wa mtaa ,kitongoji au kijiji au mbunge enzi hizi za shule za sekondari kila kata nchi nzima hapana

Darasa la saba waanze kuwa phased out viwango vya elimu vimepanda kwenye hata kata
 
Kama hii taarifa ni ya kweli nadhani ni uamuzi mbaya. Siyo kwamba sijui umuhimu wa elimu au elimu haina umuhimu kwenye uongozi wa sasa, ila uamuzi umekuwa wa ghafla mno na umetoka juu. I mean jambo kama hili inatakiwa ifanywe research kwanza, wapiga kura na wananchi kwa ujumla waulizwe maoni yao baada ya hapo ndiyo uamuzi ufanyike. Vinginevyo, kama huu uamuzi ni matokeo ya utafiti uliofanywa basi hakuna shida. NB: wanasiasa wetu wamezoea sana amri za kutoka juu kwenda chini na nyingi hufanyika bila wananchi kushirikishwa.
Kwanza ni kinyume na Katiba na Kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
 
Back
Top Bottom