SI KWELI CHADEMA yapiga marufuku ambao hawana elimu ya kidato cha sita na kuendelea kugombea serikali za mitaa na uchaguzi mkuu

SI KWELI CHADEMA yapiga marufuku ambao hawana elimu ya kidato cha sita na kuendelea kugombea serikali za mitaa na uchaguzi mkuu

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao

Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji.

Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi

barua chadema.jpg
 
Tunachokijua
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mchakato wa kidemokrasia ambapo wananchi hupiga kura kila baada ya miaka mitano kuwachagua viongozi wa ngazi za mitaa kama vile Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, na Wajumbe wa Serikali za Mitaa.

Kumekuwa na barua inayosambaa mitandaoni ikidaiwa kuwa ni ya CHADEMA ambayo ikionekana kuandikwa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na mambo ya nje CHADEMA, John Mrema, Barua hiyo inaeleza kuwa CHADEMA wametoa kanuni mpya ambayo inaeleza mtu anayeruhusiwa kugombea uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 ni yule mwenye Elimu ya kuanzia kidato cha Sita huku barua hiyo ikiwataka Wananchi kuzingatia kanuni hiyo.

Je, Ukweli wa barua hiyo ni upi?
JamiiCheck Imefatilia taarifa zilizotolewa kwenye barua hiyo na kubaini kuwa hazina Ukweli wowote, aidha barua hiyo haijawahi kutolewa na CHADEMA kupitia kurasa zao Rasmi za mitandao ya kijamii wala kwenye vyombo rasmi vya taarifa vya CHADEMA.

Vilevile, barua hiyo haijawahi kuchapishwa kwenye akaunti za John Mrema ingawa ndiye aliyedaiwa kusaini Barua hiyo, Aidha, John Mrema amechapisha taarifa ya kanusho kupitia kaunti yake ya mtandao wa X na kueleza kuwa taarifa hiyo ni ya uzushi na kuwataka watu kuipuuza.

Siku za hivi karibuni viongozi mbalimbali wa CHADEMA wamekuwa wakizungumzia kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa, ila hawajawahi kueleza kuhusu mabadiliko ya kanuni inayowataka watu wanaotaka kugombea wawe na Elimu kuanzia kidato cha Sita na kueendela, ila wamekuwa wakisisitiza watu kwenda kujiandikisha kwa ajili ya zoezi la kupiga kura na kujiandaa kwa uchaguzi ikiwemo kujiandaa kuchagua viongozi na kuchaguliwa kuwa kiongozi na si kueleza mabadiliko ya kanuni kama barua ile ilivyoeleza.
Wewe unaiamini hiyo barua? Kwa akili ya kawaida tu, CHADEMA wanaweza kufanya hivyo?
FAKE! FAKE! FAKE! FAKE!
Na nina imani hiyo barua kaiandika Makala! Maanake akili zake huyooo……..

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Kumbe una imani tu, weka counter evidence kuthibitisha ni feki
 
Elimu inakupa uwezo wa kupambanua mambo ,mwanasiasa mwenye elimu anakuwa bora.
 
UPDATe: Apparently kuna ripoti kwamba hii ni fake news.

But the abstract question raised is interesting nevertheless.

××××××××××××××××××××××××××××××
Mimi huwa sipendi siasa za majitaka, kuchafuana vyama, nk.

Na sijui ajenda yako, na sijui kama wewe ni sehemu ya vita hizi za vyama, na sitaki kuwa sehemu ya vita hizi za vyama.

Ila, ninasimamia kanuni za msingi.

Nikitaka kusema kuwa hili sharti, kwa kifupi, linavunja haki za kikatiba za wananchi kuhomnea uongozi, kwa sababu haki hizi za kikatiba hazina masharti ya kielimu zaidi ya kujua kusoma na kuandika.

Lakini, nikajiuliza zaidi.

Kama katiba haina kigezo cha usomi rasmi ili kugombea viti vya serikaki za mitaa, mtu yeyote anayejua kusoma na kuandika anaweza kugombea, halafu CHADEMA ikaweka kigezo cha kielimu cha Kidato cha Sita, je, hapo CHADEMA inakuwa imevunja haki za kikatiba za wanachama kwa kuweka kigezo hicho?

Au kigezo hicho hakivunji haki ya kikatiba kwa sababu wanachama wa CHADEMA wanaweza kujiunga na vyama vingine kugombea nafasi hizo hizo, si lazima wagombee wakiwa CHADEMA.

Hilo sharti ni sawa na sharti la kukubali itikadi nyingine tu za CHADEMA?
Sharti la kujua kusoma na kuandika ni sharti ambalo ni 'minimum'. Kupata elimu zaidi ni bora kuliko kubaki na elimu ndogo, hasa katika mazingira ya ulimwengu wa sasa ambao ni rapidly revolving. Kama chama kikiweka sharti la wagombea wake kuwa na elimu kuanzia kidato cha SITA, sioni inakuwaje ni kuvunja Katiba, wakati Katiba haijaweka ukomo wa kupata elimu kwamba ni marufuku mtu kuwa na elimu zaidi ya kusoma na kuandika. Shida ni kwamba mbona sharti hili limekuja abruptly hivyo kama linatokea kwenye vyanzo sahihi vya chama? Nadhani linaweza kuwa tangazo "fake".
 
Hiyo itakuwa ni CHADEMA ya kuchongwa katika ofisi za Lumumba.
 
Kuna vitu havihitaji katiba kubadilshwa ni chama husika kimya kimya kinateua mgombea msomi aliyesoma form six kimya kimya bila kumwambia huyo wa darasa la saba au form four kuwa tumekukataa sababu huna cheti cha form six

Sio kila kitu lazima kisubiri katiba mpya

Kwa hili Chadema wako sahihi kama mchungaji Mtikila alibadilisha mambo mengi kwa katiba hii hiip

Hilo halihitaji katiba kubadilishwa vyama vyenyewe vyaweza tuletea wagombea wasomi sio hao darasa la saba sababu wao ndio waidhinishaji nani agombee

Hakuna haja hata ya kubadili katiba kwenye hili vyama vya siasa vijiongeze iwe CCM au upinzani

Sio kila kitu kinahitaji katiba ya nchi ibadilishwe hata kama inasomeka darasa la saba aweza gombea serikali ya mtaa ,udiwani nk
Kama wanavyofanya CCM kwenye Urais??
 
Kwa nafasi ya mwenyekiti wa mtaa na wajumbe wa mtaa na vijiji Mara nyingi sio rahisi umpate mwenye Elimu ya Six achilia mbali form four.

Hasa vijijini .

Hii taarifa itakuwa sio rasmi. Ebu tusubiri tuone.
Pamoja na shule zote hizi za kata upatikanaji wa form four kuongoza vijiji na mitaa bado ni changamoto??
 
Sharti la kujua kusoma na kuandika ni sharti ambalo ni 'minimum'. Kupata elimu zaidi ni bora kuliko kubaki na elimu ndogo, hasa katika mazingira ya ulimwengu wa sasa ambao ni rapidly revolving. Kama chama kikiweka sharti la wagombea wake kuwa na elimu kuanzia kidato cha SITA, sioni inakuwaje ni kuvunja Katiba, wakati Katiba haijaweka ukomo wa kupata elimu kwamba ni marufuku mtu kuwa na elimu zaidi ya kusoma na kuandika. Shida ni kwamba mbona sharti hili limekuja abruptly hivyo kama linatokea kwenye vyanzo sahihi vya chama? Nadhani linaweza kuwa tangazo "fake".
Mkuu,

Katiba ikisema haki ya kupiga kura ni ya kila Mtanzania aliyefikisha miaka 18 na mwenye akili timamu, halafu Tume ya uchaguzi ikazidisha vigezo na kusema mpiga kura ni lazima awe kamaliza form six, hapo Tume ya Uchaguzi imevunja katiba au haijavunja katiba?
 
Chadema imewapiga marufuku maelfu ya watanzania ambao wana elimu ya msingi na kidato cha nne wasigombee uongozi wowote katila chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Chama hicho, japo kimewanyima haki ya kugombea, kinatarajia kwenda kuwaomba kura ili kuwatumia kisiasa kwa faida yao

Ni nadra sana kukutana na mjumbe wa serikali ya mtaa au kitongoji mwenye elimu ya kidato cha sita, achilia mbali mwenyekiti wa mtaa na wa kijiji.

Sasa ni zamu ya watanzania hao kuwaadhibu chadema kwa dhambi hii ya ubaguzi
View attachment 3120101
CHAWA mnahangaika sana na CHADEMA ambayo mlisema imekufa, sioni mkisema kuhusu ACT na CUF.
 
Yaani utokee ugomvi wa wana ndoa mtaani mtu aupeleke kwa kijana ambaye hata hajaoa, na muda wote kalewa visungura. Mwenyekiti wa mtaa ni mzee wa busara wa eneo hilo
UVCCM ndio wanataka hivyo.
 
Mkuu,

Katiba ikisema haki ya kupiga kura ni ya kila Mtanzania aliyefikisha miaka 18 na mwenye akili timamu, halafu Tume ya uchaguzi ikazidisha vigezo na kusema mpiga kura ni lazima awe kamaliza form six, hapo Tume ya Uchaguzi imevunja katiba au haijavunja katiba?
Kwani Tume ndiyo iliyoweka hilo sharti? Mimi nimeongelea katika muktadha wa ilani ya chama kwa sababu kusema kiongozi awe na elimu ya kidato cha SITA hakujaondoa sharti la kujua kusoma na kuandika, na wala si kuwanyima Watanzania haki ya kupiga kura. After all, nilitoka maoni haya ni hypothetical sense, kwa sababu hili tangazo kinaonekana tu jamiiforums na sijaliona katika vyanzo vingine vya chama kama mtandao wa X na Facebook au kwenye taarifa ya habari, na pia kwa nini limekuja abruptly hivyo wakati Chadema wameshaanza chaguzi za ndani ya chama bila sharti hili jipya? Hivyo, inawezekana ni tangazo la kupika (fake news).
 
Kwani Tume ndiyo iliyoweka hilo sharti? Mimi nimeongelea katika muktadha wa ilani ya chama kwa sababu kusema kiongozi awe na elimu ya kidato cha SITA hakujaondoa sharti la kujua kusoma na kuandika, na wala si kuwanyima Watanzania haki ya kupiga kura. After all, nilitoka maoni haya ni hypothetical sense, kwa sababu hili tangazo kinaonekana tu jamiiforums na sijaliona katika vyanzo vingine vya chama kama mtandao wa X na Facebook au kwenye taarifa ya habari, na pia kwa nini limekuja abruptly hivyo wakati Chadema wameshaanza chaguzi za ndani ya chama bila sharti hili jipya? Hivyo, inawezekana ni tangazo la kupika (fake news).
Ni hivi,

Kimantiki, levels za elimu Tanzania ziko hivi.

Kuanzia chini kwenda juu.

1. Kujua kusoma na kuandika. Kigezo hiki hakihitaji usome shule yoyote, ufaulu mtihani wowote, uwe na cheti chochote.

2. Darasa la saba. Kigezo hiki kinataka umalize shule ya msingi na uwe na cheti cha kumaliza darasa la saba.

3. Form Four. Ditto.

4. Form Six. Ditto.

5. Vyuo vya elimu ya juu kwa ngazi zake.Stashahada mpaka shahada zote mpaka shahada ya uzamivu


Kwa hiyo, ukisikia kigwzo cha kazi fulani ni kujua kusoma na kuandika, maana yake hapo hata cheti cha darasa la saba hakihitajiki.

Sasa, ikiwa katiba inamruhusu mtu anayejua kusoma na kuandika tu kugombea uenyekiti wa kijiji, nradi awe anajua kusoma na kuandika tu, CHADEMA ikiweka kigezo cha ziada cha kumaliza form six hapi haitawanyima wananchi haki yao ya kikatiba inayosema hawahitaji kumaliza form six, hawahitaji kumaliza form four, hawahitaji kunakiza darasa la saba, wanahitaji kujua kusoma na kuandika tu?

Sharti likiwa minimum maana yake mtu akitimiza sharti hilo tu anaruhusiwa. Mfano, minimum age of voting is 18 years. Maana yake mtu aliye na umri wa zaidi ya miaka 18 anaruhusiwa kupiga kura, lakini wa chini ya miaka 18 haruhusiwi.

Sasa ukisema sharti la kusoma na kuandika ni minimum, halafu ukaweka sharti lingine minimum la form six, hapo umeondoa minimum kutoka kujua kusoma na kuandika umeipandisha mpaka kuwa form six.

Huoni kwamba watu wanaojua kusoma na kuandika lakini hawajafija form six umewaengua katika kutafuta uongozi hapo? Na kama katiba ya nchi inawaruhusu kugombea uongozi, huoni kiwa hiki kigezo kinavunja katiba ya nchi?
 
Mkuu,

Katiba ikisema haki ya kupiga kura ni ya kila Mtanzania aliyefikisha miaka 18 na mwenye akili timamu, halafu Tume ya uchaguzi ikazidisha vigezo na kusema mpiga kura ni lazima awe kamaliza form six, hapo Tume ya Uchaguzi imevunja katiba au haijavunja katiba?
Kiongozi, for the sake of mjadala (ingawa nahisi tangazo ni fake) soma Ibara ya 30(2)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, halafu urudi tujadili vizuri zaidi. Hii ibara ina'restrict' haki zote zilizotolewa kwenye Katiba. Si unajua the Bill of Rights kwenye Katiba yetu "is not entrenched?" Anyway, cheki kwanza, halafu uone je Tume ikisema hivyo, itakuwa imekosea/imevunja Katiba?
 
Back
Top Bottom